Kama hawa ndiyo wanafunzi wa leo basi walimu kazi ipo

Jana katika kazi zangu za ujenzi wa taifa nilikuwa mjini Babati katika shule ya sekondari x. Miongoni mwa changamoto zinazowakabili walimu kwa sasa ni utovu wa nidhamu kutoka kwa wanafunzi wao.

Hebu fikiria mwanaJF mwenzangu hivi inakuwaje mwanafunzi anapata ujasiri wa kuiba baiskeli ya mwalimu wake!

Yule mwalimu aliyeibiwa baiskeli alituelezea kwa hisia mno jinsi alivyojibana hadi kupata baiskeli yake ambayo hakudumu nayo hata siku 2 mwanafunzi akaiotea.

Muhimu ni sisi wazazi au walezi kuwasaidia walimu katika kuwaform watoto wetu kimaadili ili kuwamotisha walimu kuwasaidie wanetu ktk masomo yao.

Ni kweli pia kwamba hata walimu wa zama hizi wana changamoto zao kimaadili lakini sisi kama wazazi au walezi tutimize wajibu wetu ktk malezi ili tuwe na kizazi bora kimaadili.

Naomba kuwasilisha


Huyo mwanafunzi ni mwizi na ndiyo tabia yake. Akifanikiwa kuendelea na masomo akafika Chuo Kikuu akapata kazi yoyote ile, iwe ya Serikali, sekta binafsi, Mahakama, Mbunge au mwanasiasa mwingine basi lazima, kwa nafasi yoyote atakayoipata, ataiba tu na atakuwa fisadi mkubwa. Tusidhani ufisadi unakuja tu ghafla kwa mtu, la hasha, chembechembe zake ziko kwenye damu na huonekana toka mapema kama hivyo.
 
Jana katika kazi zangu za ujenzi wa taifa nilikuwa mjini Babati katika shule ya sekondari x. Miongoni mwa changamoto zinazowakabili walimu kwa sasa ni utovu wa nidhamu kutoka kwa wanafunzi wao.

Hebu fikiria mwanaJF mwenzangu hivi inakuwaje mwanafunzi anapata ujasiri wa kuiba baiskeli ya mwalimu wake!

Yule mwalimu aliyeibiwa baiskeli alituelezea kwa hisia mno jinsi alivyojibana hadi kupata baiskeli yake ambayo hakudumu nayo hata siku 2 mwanafunzi akaiotea.

Muhimu ni sisi wazazi au walezi kuwasaidia walimu katika kuwaform watoto wetu kimaadili ili kuwamotisha walimu kuwasaidie wanetu ktk masomo yao.

Ni kweli pia kwamba hata walimu wa zama hizi wana changamoto zao kimaadili lakini sisi kama wazazi au walezi tutimize wajibu wetu ktk malezi ili tuwe na kizazi bora kimaadili.

Naomba kuwasilisha
Mbona hata wanafunzi wa zamani walikuwa wakorofi tena kuliko wa sasa..
Angalia rate ya migomo sasa hivi na zamani ipi ni kubwa..

Tatizo la wazee wanataka kutuaminisha kwamba wao walikuwa perfect..
Mngekuwa pefect basi tungezaliwa na kukuta TZ iko kama US au UK ... lkn mbona pamoja na nidhamu yenu ndio kwanza tunaibiwa na Wakina Chenge n.k au na wazee kama wakina chenge ni kizazi cha sasa hivi??
 
Bora huyo kaiba baiskeli! Kuna walioba Mtihani shuleni na sasa ni Viongozi wetu!
 
Nunua gari kaa na funguo ofisini wabaki kujitizima kwenye kioo, hizi nyingine lawama tu
 
Dah nimecheka sanaaa, nikakumbuka tukiwa f6 wanafunzi walivyochoma banda la kuku la Mwl, Mwl aliumia sana.
 
Jana katika kazi zangu za ujenzi wa taifa nilikuwa mjini Babati katika shule ya sekondari x. Miongoni mwa changamoto zinazowakabili walimu kwa sasa ni utovu wa nidhamu kutoka kwa wanafunzi wao.

Hebu fikiria mwanaJF mwenzangu hivi inakuwaje mwanafunzi anapata ujasiri wa kuiba baiskeli ya mwalimu wake!

Yule mwalimu aliyeibiwa baiskeli alituelezea kwa hisia mno jinsi alivyojibana hadi kupata baiskeli yake ambayo hakudumu nayo hata siku 2 mwanafunzi akaiotea.

Muhimu ni sisi wazazi au walezi kuwasaidia walimu katika kuwaform watoto wetu kimaadili ili kuwamotisha walimu kuwasaidie wanetu ktk masomo yao.

Ni kweli pia kwamba hata walimu wa zama hizi wana changamoto zao kimaadili lakini sisi kama wazazi au walezi tutimize wajibu wetu ktk malezi ili tuwe na kizazi bora kimaadili.

Naomba kuwasilisha
Mkuu mbona umekuja kunisema huku tena?
 
Huu uzi unanifikkirisha na kunichekesha sana..kwa mfano, umeelewa nini hapa "Yule mwalimu aliyeibiwa baiskeli alituelezea kwa hisia mno jinsi alivyojibana hadi kupata baiskeli yake ambayo hakudumu nayo hata siku 2 mwanafunzi akaiotea"
Mleta mada katumia utaakamu kufikisha ujumbe mpana kwa maneno machache
 
Back
Top Bottom