Kama hatujui kilichomo katika mkataba wa ujenzi wa Bwawa la Umeme huko mto Rufiji, tuna uhakika gani bei ya umeme itakuwa nafuu?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,011
144,371
Japo ni kweli kuwa umeme unaotokana na maji huwa ni wa bei nafuu kulinganisha na umeme unaotokana na vyanzo vingine kama vile mafuta, gesi, nuclear, n.k , lakini je,si kweli kuwa mkataba wa ujenzi wa chanzo husika cha umeme unaweza kufanya bei ya umeme kuwa kubwa kuliko inavyotarajiwa?

Kwa mfano, kama mkataba una kipengele kinachosema kiasi fulani cha fedha zitazotokana na mauzo ya umeme zitatumika kumlipa mjenzi/mkandarasi wa mradi, mkataba wa aina hii hauwezi kufanya bei kuwa kubwa kuliko inavyostahili?

Au kama mradi umejengwa na mkandarasi kwa gharama zake (awe amechukua mkopo au vinginevyo) huku akijilipa kwa kutumia sehemu ya fedha za mauzo ya umeme, hapa bei ya umeme haiwezi kuwa kubwa kuliko inavyotarajiwa?

Kwasababu ya kujiuliza ni mengi na kwakuwa hatujui kilichomo katika mkataba, ni bora tu tukawa walpole kuliko kuwa washangiliaji.

Tukumbuke ya gesi ya Mtwara na hatima yake kwa Watanzania na Taifa kwa ujumla.
 
Sisi tunamuamini Rais Magufuli kila anachochosema Kwasababu ni mcha Mungu na wala hajatumwa na Wazungu kuja kuharibu Nchi km yule mgombea

Umeme utakuwa sawa na bwerere, tunamuomba Rais Magufuli awe makini na Chadema wasije wakabomoa bwawa
Mungu anataniwa sana siku hizi? Hata waigizao huonekana ni wapenzi wa Mungu? God loves ever, kills never.
 
Si bwawa la umeme tu mi sielewi hata hii mikataba mipya kibao tunayoingia na hawa mabeberu wa madini..hata sielewi kwa nini inafichwa fichwa wakati madini ni mali ya Watanzania?
 
Mungu anataniwa sana siku hizi? Hata waigizao huonekana ni wapenzi wa Mungu? God loves ever, kills never.
Hasira za Chadema kukataliwa usilete kwangu
20200912_081929.jpg
 
Hicho kipengele cha mkandarasi kujilipa mwenyewe kutokana na mauzo ya umeme wewe na Lissu mmekitoa wapi? Maana mpaka sasa hivi mkandarasi ameshalipwa na serikali certificate saba zaidi ya tril 2. Acheni kupumbaza watu.
 
Sisi tunamuamini Rais Magufuli kila anachochosema Kwasababu ni mcha Mungu na wala hajatumwa na Wazungu kuja kuharibu Nchi km yule mgombea

Umeme utakuwa sawa na bwerere, tunamuomba Rais Magufuli awe makini na Chadema wasije wakabomoa bwawa
Naona toka juzi bashiru aliposema sema kwamba mjibu hoja za mitandano,nakuona ni mwendo waa kuharisha tu.
 
Mwambie huyo mgombea wa Chadema aache uongo. Atapata aibu kubwa sana mwaka huu. Naweka ushahidi hapa chini kuonyesha malipo yanafanyika kwa awamu na sio kwamba mkandarasi atalipwa kutokana na mauzo ya umeme. Acheni siasa za uongo
 

Attachments

  • Screenshot_20200912-162102.png
    Screenshot_20200912-162102.png
    54.2 KB · Views: 2
Hicho kipengele cha mkandarasi kujilipa mwenyewe kutokana na mauzo ya umeme wewe na Lissu mmekitoa wapi? Maana mpaka sasa hivi mkandarasi ameshalipwa na serikali certificate saba zaidi ya tril 2. Acheni kupumbaza watu.
Umeelewa kilichoandikwa?Acha kukurupuka!
 
Mwambie huyo mgombea wa Chadema aache uongo. Atapata aibu kubwa sana mwaka huu.
Naweka ushahidi hapa chini kuonyesha malipo yanafanyika kwa awamu na sio kwamba mkandarasi atalipwa kutokana na mauzo ya umeme. Acheni siasa za uongo
Miaka yote niliyoshuhudia kampeni za chadema, mwaka huu wana hali ngumu sana. Nahofia wasije kutoana macho mwakani wakigawana ruzuku kiduchu.
 
Sisi tunamuamini Rais Magufuli kila anachochosema Kwasababu ni mcha Mungu
na wala hajatumwa na Wazungu kuja kuharibu Nchi km yule mgombea

Umeme utakuwa sawa na bwerere, tunamuomba Rais Magufuli awe makini na Chadema wasije wakabomoa bwawa
Kwahiyo nchi iendeshwe kwa imani na si sheria sio? Kama anaweza kununua jogoo kwa Tsh laki moja atashindwa vipi kusaini mkataba mbovu ukizingatia hata lugha ya mkataba haijui?

Kama anaaminika kwanini afanye siri mambo muhimu ya nchi? Huoni akitoka yeye wewe ndio utakuwa muovu namba mbili?
 
Back
Top Bottom