Kama Haki ya Zanzibar haikupatikana, ni dhahiri dunia imebariki uonevu wa CCM

KISHADA

JF-Expert Member
Oct 18, 2012
2,224
3,290
Yamesemwa mengi, yamefanyika mengi na yanaendelea kufanyika mengi mabaya dhidi ya haki za Zanzibar kuanzia haki za kwenye Muungano, haki za kisiasa, kiraia, kiuchuimi n.k. Watu wamekosoa na kufanya jitihada nyingi za kistaarabu kwa kufuata mifumo ya kisiasa, kidiplomasia na kidemokrasia.

Kabla ya 2015 kulifanywa jitihada nyingi kuinusuru Zanzibar kurejea kwenye mitafaruku na kikomo ilikuwa ni kuundwa kwa GNU baaDA YA KATIBA KUFANYIWA UKARABATI. Hata hivyo hali hio haikuwafurahisha wale WATESI WA ZANZIBAR na mawakala wao ambao kwa kuzingatia tu maslahi yao basi ndani ya miaka mitano mgogoro ukarudishwa kupitia ZEC na JECHA baada ya kufuta matokeo halali ya uchaguzi wa 2015.

Hii si bahati mbaya maana wote wanaohusika walijitokeza. Kwanza jamuhuri ya Muungano iliruhusu kutumika vyombo vyake kulinda wavunja taratibu na tulisikia kauli zote za vitisho zilivyotolewa. Tulishuihudia mizinga na maderaya ya JMT yakipita mitaani na tulishuhudia HAKIKISHO LA RAIS MAGUFULI kwa Dr Shein baada ya kufanyika ubatili ule wa uchaguzi wa Marudio. Hapa JMT haiwezi kukwepa Lawama na ushiriki wake kuhusu kupora HAKI YA WAZANZIBARI.

Kwa upande wa dunia kuna masuali bado. Jitihada za wazi hazijaonekana isipokuwa tulipata kauli za awali za kusema uchaguzi wa 2015 ulikuwa huru na haki na kutaka mshindi halali atangazwe (USA), Aidha Jumuiya za kikanda za kusimamia uchaguzi na zile za ndani zote zilikubali kuwa uchaguzi ulikwenda sawa. Jumuiya kama UNDP, EU, SADC, EA nk. zote zilisifu uchaguzi ule.

Baada ya kufutwa uchaguzi mzigo uliwaelemea CUF na Maalim Seif wao( Masikini mzee wa watu), kwa kuhangaika kuwatuliza wafuasi na kuanza safari ndefu yenye uchovu. Lengo ni kutaka HAKI ITENDEKE na kunusuru uvunjifu wa amani.
Ushiriki wa Jumuiya za Kimataifa za wazi umeoneshwa na Liberal International (LI) ambapo waliahidi kulibeba suala hilo na hatujuwi limeishia wapi kwa sasa baada ya suala hilo kufikishwa Umoja wa Mataifa.

MASUALI YANAENDELEA.

Hivi jumuiya ya kimataifa hawajuwi ulaghai na ushiriki wa CCM katika kuvuruga Haki ile ya 2015? na nini nafasi yao ?

Ikiwa kabla ya 2015 dunia ilishiriki kuleta utatuzi wa mgogoro wa Zanzibar hadi kuzaliwa miafaka kadhaa mpaka ulipofika wa kikatiba mwaka 2009 hivi huu wa 2015 hauwahusu na wameiwacha mkono Zanzibar na kuiwacha CCM ifanye itakavyo?

MTAZAMO.

Kwa mtazamo wangu Dunia inajuwa kinachoendelea Zanzibar, Tanzania na Afrika kwa jumla. Vipi ushiriki wao hilo ni suala lengine. Lakini ikumbukwe kwamba Tanzania ina DENI LA KIMATAIFA KUHUSU HAKI NA DEMOKRASIA ZANZIBAR KUTOKANA NA UCHAGUZI WA 2015. Kwa maana hio SULUHU haijapatikana na DUNIA vile vile ina DENI kwa Zanzibar kuhusu HAKI , DEMOKRASIA na HESHIMA. Hili la uchaguzi wa 2015 Dunia haiwezi kukwepa wajibu wake, ndio nikasema ikiwa haki haitapatikana ni Dhahiri imebariki uonevu wa CCM.

Jee dunia imebariki hilo tusubiri tufike huo mwaka 2020 tuone nini kitafuata au kabla ya hapo nini kitajiri.

Akili ya kichambuzi haikubali, LAZIMA KUNA KITU KINAENDELEA NA NAFIKIRI KADIRI MUDA UNAVYOKWENDA TUTAPATA JAWABU.

KUWEPO AU KUTOKUWEPO MGOGORO ?
Hili limekuwa ni suali linachagiza wasomi na wanasiasa. Kwa nini useme Zanzibar hakuna mgogoro au kwa sababu kuko kimya na watu hawauani? Kule kuna mgogoro mkubwa na nadhani dunia inalielewa hilo. Kama hawaelewi basi lazima wana ajenda ya SIRI NA CCM kuhusu Zanzibar. Kwani migogoro ya aina hii imetatuliwa vipi nchi nyengine zikiwemo za Afrika. Mifano hai ni kule IVORY COAST na karibuni hivi kule MALI.

Kwa mara nyengine tunataka kuona ubeberu ulivyo linapokuja suala la maslahi yake. Hili la Zanzibar ni kufeli kwa Dhana YA DEMOKRASIA Duniani na ni kufeli kwa Vyombo vya Kidunia KUSIMAMIA HAKI ZA WACHACHE.

Muda utasema

I love Tanzania, I love Zanzibar




Kishada.
 
Ikiwa kabla ya 2015 dunia ilishiriki kuleta utatuzi wa mgogoro wa Zanzibar hadi kuzaliwa miafaka kadhaa mpaka ulipofika wa kikatiba mwaka 2009 hivi huu wa 2015 hauwahusu na wameiwacha mkono Zanzibar na kuiwacha CCM ifanye itakavyo?

Acha tuone
 
Zanzibar kuna mgogoro mkubwa uliofunikwa mkeka wa uchaguzi wa marudio wa 2016. Kuendelea kwa serikali iliyopo ya Dr Shein ni kubariki ZEC/ CCM kufuta chaguzi zote zijazo (Already made a reference) na kuanzia hapo ule Msemo wa rais Magufuli unatimia ... " CCM ITATAWALA MILELE"

Sasa katika hali hio ile investment kubwa ya demokrasia ndio imezikwa rasmi na sasa kuanzia hapo mabeberu watalazimika kuleta Ajenda nyengine. na sio hii ya demokrasia tena.
 
Waliobariki Muungano hawawezi ruhusu uvunjike ,,,, itakuchukua miaka mingi kuwaelewa wazungu
 
Wa Zanzibari Wanafiki Sana Acha wanyooshwe

Alijitokeza Mtu Tena akiwa ndani ya Mamlaka ya Rais aka take risk ya kuwakabili Watanganyika lakin ilipofika Dodoma wote wakaungana Na Watanganyika akabaki peke yake Na Walinzi wake Na Madereva

Nasema Acha wanyooswe
 
Wa Zanzibari Wanafiki Sana Acha wanyooshwe

Alijitokeza Mtu Tena akiwa ndani ya Mamlaka ya Rais aka take risk ya kuwakabili Watanganyika lakin ilipofika Dodoma wote wakaungana Na Watanganyika akabaki peke yake Na Walinzi wake Na Madereva

Nasema Acha wanyooswe

Mkuu zungumzia muktadha wa mada. Wewe unaonaje
 
Ikifia hatua hio, ndio tunazidi kuamini kuwa jumuiya ya kimataifa ni wanafiki sana na hapo ndipo itatoa mwanya wa kuamini zile consipirancy za upendeleo ama wa kiuchumi, kiitikadi na kiimani. CCM walifanya too much.
 
Wazungu ni washenzi tu wala si wa kuwategemea kwa lolote kwenye crusade ya ukombozi wetu.

mfano mwengine ni hii issue ya Lissu.... wanaifahamu kabisa undani wake lakini utasikia sijui mara oh EU wamesaidia nini sijui, France wamewekeza kitu gani wapi sijui, Britain wamesaini mkataba gani uko. nyambaf kabisa!!

wenzetu Wakenya washafanya yao miaka ile na sasa kule ni watu kuheshimiana kwa kwenda mbele.
Watanzania tukiendelea kusubiri kudra za Wazungu tutasubiri hadi kiama!!
 
Wazungu ni washenzi tu wala si wa kuwategemea kwa lolote kwenye crusade ya ukombozi wetu.

mfano mwengine ni hii issue ya Lissu.... wanaifahamu kabisa undani wake lakini utasikia sijui mara oh EU wamesaidia nini sijui, France wamewekeza kitu gani wapi sijui, Britain wamesaini mkataba gani uko. nyambaf kabisa!!

wenzetu Wakenya washafanya yao miaka ile na sasa kule ni watu kuheshimiana kwa kwenda mbele.
Watanzania tukiendelea kusubiri kudra za Wazungu tutasubiri hadi kiama!!
Wazungu ni washenzi tu wala si wa kuwategemea kwa lolote kwenye crusade ya ukombozi wetu.

mfano mwengine ni hii issue ya Lissu.... wanaifahamu kabisa undani wake lakini utasikia sijui mara oh EU wamesaidia nini sijui, France wamewekeza kitu gani wapi sijui, Britain wamesaini mkataba gani uko. nyambaf kabisa!!

wenzetu Wakenya washafanya yao miaka ile na sasa kule ni watu kuheshimiana kwa kwenda mbele.
Watanzania tukiendelea kusubiri kudra za Wazungu tutasubiri hadi kiama!!
Kuna watu wanatuharibia nchi kwa kuendekeza ubinafsi wao na watoto wao.Ni afadhali wangefuta vyama vingi ili tujuwe kuwa hupaswi kupewa madaraka ikiwa hukuchaguliwa kupitia vyama.
 
Yamesemwa mengi, yamefanyika mengi na yanaendelea kufanyika mengi mabaya dhidi ya haki za Zanzibar kuanzia haki za kwenye Muungano, haki za kisiasa, kiraia, kiuchuimi n.k. Watu wamekosoa na kufanya jitihada nyingi za kistaarabu kwa kufuata mifumo ya kisiasa, kidiplomasia na kidemokrasia.

Kabla ya 2015 kulifanywa jitihada nyingi kuinusuru Zanzibar kurejea kwenye mitafaruku na kikomo ilikuwa ni kuundwa kwa GNU baaDA YA KATIBA KUFANYIWA UKARABATI. Hata hivyo hali hio haikuwafurahisha wale WATESI WA ZANZIBAR na mawakala wao ambao kwa kuzingatia tu maslahi yao basi ndani ya miaka mitano mgogoro ukarudishwa kupitia ZEC na JECHA baada ya kufuta matokeo halali ya uchaguzi wa 2015.

Hii si bahati mbaya maana wote wanaohusika walijitokeza. Kwanza jamuhuri ya Muungano iliruhusu kutumika vyombo vyake kulinda wavunja taratibu na tulisikia kauli zote za vitisho zilivyotolewa. Tulishuihudia mizinga na maderaya ya JMT yakipita mitaani na tulishuhudia HAKIKISHO LA RAIS MAGUFULI kwa Dr Shein baada ya kufanyika ubatili ule wa uchaguzi wa Marudio. Hapa JMT haiwezi kukwepa Lawama na ushiriki wake kuhusu kupora HAKI YA WAZANZIBARI.

Kwa upande wa dunia kuna masuali bado. Jitihada za wazi hazijaonekana isipokuwa tulipata kauli za awali za kusema uchaguzi wa 2015 ulikuwa huru na haki na kutaka mshindi halali atangazwe (USA), Aidha Jumuiya za kikanda za kusimamia uchaguzi na zile za ndani zote zilikubali kuwa uchaguzi ulikwenda sawa. Jumuiya kama UNDP, EU, SADC, EA nk. zote zilisifu uchaguzi ule.

Baada ya kufutwa uchaguzi mzigo uliwaelemea CUF na Maalim Seif wao( Masikini mzee wa watu), kwa kuhangaika kuwatuliza wafuasi na kuanza safari ndefu yenye uchovu. Lengo ni kutaka HAKI ITENDEKE na kunusuru uvunjifu wa amani.
Ushiriki wa Jumuiya za Kimataifa za wazi umeoneshwa na Liberal International (LI) ambapo waliahidi kulibeba suala hilo na hatujuwi limeishia wapi kwa sasa baada ya suala hilo kufikishwa Umoja wa Mataifa.

MASUALI YANAENDELEA.

Hivi jumuiya ya kimataifa hawajuwi ulaghai na ushiriki wa CCM katika kuvuruga Haki ile ya 2015? na nini nafasi yao ?

Ikiwa kabla ya 2015 dunia ilishiriki kuleta utatuzi wa mgogoro wa Zanzibar hadi kuzaliwa miafaka kadhaa mpaka ulipofika wa kikatiba mwaka 2009 hivi huu wa 2015 hauwahusu na wameiwacha mkono Zanzibar na kuiwacha CCM ifanye itakavyo?

MTAZAMO.

Kwa mtazamo wangu Dunia inajuwa kinachoendelea Zanzibar, Tanzania na Afrika kwa jumla. Vipi ushiriki wao hilo ni suala lengine. Lakini ikumbukwe kwamba Tanzania ina DENI LA KIMATAIFA KUHUSU HAKI NA DEMOKRASIA ZANZIBAR KUTOKANA NA UCHAGUZI WA 2015. Kwa maana hio SULUHU haijapatikana na DUNIA vile vile ina DENI kwa Zanzibar kuhusu HAKI , DEMOKRASIA na HESHIMA. Hili la uchaguzi wa 2015 Dunia haiwezi kukwepa wajibu wake, ndio nikasema ikiwa haki haitapatikana ni Dhahiri imebariki uonevu wa CCM.

Jee dunia imebariki hilo tusubiri tufike huo mwaka 2020 tuone nini kitafuata au kabla ya hapo nini kitajiri.

Akili ya kichambuzi haikubali, LAZIMA KUNA KITU KINAENDELEA NA NAFIKIRI KADIRI MUDA UNAVYOKWENDA TUTAPATA JAWABU.

KUWEPO AU KUTOKUWEPO MGOGORO ?
Hili limekuwa ni suali linachagiza wasomi na wanasiasa. Kwa nini useme Zanzibar hakuna mgogoro au kwa sababu kuko kimya na watu hawauani? Kule kuna mgogoro mkubwa na nadhani dunia inalielewa hilo. Kama hawaelewi basi lazima wana ajenda ya SIRI NA CCM kuhusu Zanzibar. Kwani migogoro ya aina hii imetatuliwa vipi nchi nyengine zikiwemo za Afrika. Mifano hai ni kule IVORY COAST na karibuni hivi kule MALI.

Kwa mara nyengine tunataka kuona ubeberu ulivyo linapokuja suala la maslahi yake. Hili la Zanzibar ni kufeli kwa Dhana YA DEMOKRASIA Duniani na ni kufeli kwa Vyombo vya Kidunia KUSIMAMIA HAKI ZA WACHACHE.

Muda utasema

I love Tanzania, I love Zanzibar




Kishada.
Inaonekana kama vile unaamini haki ya mtu mmoja ndiyo haki ya wa zanzibar? Fafanua tujue mkuu.
 
Back
Top Bottom