Kama faini huongezeka usipolipa ndani ya siku 7 kwa shillingi 7,500/- kwanini umkamate mtu anapochelewa kulipa?

kluger

JF-Expert Member
Jun 16, 2016
2,093
1,894
Wakuu salaam kwenu,

Naomba kuuliza kuna kero moja imeniaharibia kabisa siku yangu leo.

Mdogo wangu katumia gari yangu kwenda kanisani, bahati mbaya week mbili zilizopita niliwahi kamatwa kwa kosa la speed iliyozidi kiwango cha 50 nikiwa safarini mkoani.

Sikufanikiwa kulipa na fine hizo zimeongezeka mara dufu.

Leo wamemkamata na kumpeleka kituoni kwa kosa langu.

Nichojiuliza kama fine hizi usipolipa ndani ya siku saba zinaongezeka kwa shillings 7,500/- kwa nini umkamate mtu anapochelewa kulipa?? Maana ya hiyo elfu 7 mia 5 ni nni??

Huu ni uonevu, hawa traffic imefika mahali wanatengeneza uhasama mkubwa na raia, najua wapo viongozi wao watasoma humu, tunawafikishia tu salamu, kuweni na hekima katika kusimamia sheria na si kukomoana.

Siku njema.
 
Wakuu salaam kwenu,

Naomba kuuliza kuna kero moja imeniaharibia kabisa siku yangu leo.

Mdogo wangu katumia gari yangu kwenda kanisani, bahati mbaya week mbili zilizopita niliwahi kamatwa kwa kosa la speed iliyozidi kiwango cha 50 nikiwa safarini mkoani.

Sikufanikiwa kulipa na fine hizo zimeongezeka mara dufu.

Leo wamemkamata na kumpeleka kituoni kwa kosa langu.

Nichojiuliza kama fine hizi usipolipa ndani ya siku saba zinaongezeka kwa shillings 7,500/- kwa nini umkamate mtu anapochelewa kulipa?? Maana ya hiyo elfu 7 mia 5 ni nni??

Huu ni uonevu, hawa traffic imefika mahali wanatengeneza uhasama mkubwa na raia, najua wapo viongozi wao watasoma humu, tunawafikishia tu salamu, kuweni na hekima katika kusimamia sheria na si kukomoana.

Siku njema.
lipa faini, tsh 7500 imewekwa ni km adhabu ya kuchelewesha kulipa yani ni adhabu ndogo, ukionekana kukaidi hata hiyo adhabu ndogo wana upgrade adhabu. usitegemee kwakua unaongezewa 7500 ndo ikawa halali ya kulipa siku utakayojisikia.
 
Sishabikii hicho kilichofanyika na hao askari!
Naomba kukumbshia hiki;
It take very short time to comply but very long time and difficulties/involving for not complying 🏻🏻!
 
Tuelimishane Wenye kujua, baada ya fine,unapewa Siku saba kulipa kisha baada ya Siku 7 ongezeko la 7,500; Swali kanuni ama sheria tozo inasema nini?
 
7500 ni ndogo sana kwa mtu mmoja lkn kama mpo watu kama ww elf 10000 inakuwa ni pesa nyingi sn. Ww nenda kalipe hela acha kulalamika wakati ww ndie uliyeanza kuvunja sheria
 
Hiyo fine huwa inaongezeka kwa kiasi kikubwa kwa kila siku Kama sijakosea kiasi Kwamba inashangaza na kuumiza sana!
Wala siyo kweli kuwa inaongezeka Tsh 7,500/- bali inaongezeka kwa kila Siku hadi itakapolipwa n.k
 
Hahaaaaaa mimi tulizua ugomvi mpaka magari yalipark ilikuwa high road ila jamaa wanachezea sana zile torch,7500 inaongezeka kama usipolipa ndani ya muda husika pole hakuna namna
 
Hahaaaaaa mimi tulizua ugomvi mpaka magari yalipark ilikuwa high road ila jamaa wanachezea sana zile torch,7500 inaongezeka kama usipolipa ndani ya muda husika pole hakuna namna

Inaongezeka mara moja tu?
Nazani inaongezeka kwa kila Siku ndo maana huwa ndani ya muda mfupi inakuwa kubwa mara dufu
 
Utii wa sheria bila shuruti unasaidia kuepukana na mengi sana ikiwemo usifumbufu unaoweza kuepukika!
 
Jana kunako taarifa ya Habari niliona madereva wa Magari ya Serikali wakilalamika eti kuna sheria mbili zinakinzana kati ya Ile ya usalama barabarani na sheria ya umma namba 101
Hebu mliowaelewa malalamiko yao anzisheni Uzi tupate kujadili na kuona Kama wanaweza kuwa hoja ya msingi au hapana!
 
Inaongezeka kwa kila siku mpaka inadouble baada ya kupita siku saba,kwahiyo kama ulitakiwa kulipa elfu thelathini itapanda mpaka elfu sitini na kukomea hapo
 
Gari yangu inadaiwa pia elfu sitini,nitalipa siku thamani ya elfu sitini ya wakati huo itakapokuwa sawa na elfu thelathini ya wakati naandikiwa faini
 
Back
Top Bottom