Kama Dr. Slaa anakuwa Rais na CHADEMA inaachiwa nchi leo....

Mkeshaji

JF-Expert Member
Jan 7, 2011
4,262
1,416
Wakuu salaam,
Nimejaribu kutafakari mwenendo mzima wa taifa letu na matukio kadhaa ambayo yamelikumba taifa letu kufikia sasa na hasa haya ya hivi karibuni bado nabaki na maswali lukuki kichwani bila majibu.

Ukianzia mgomo wa madaktari, mgogoro wa posho za wabunge, "kufilisika kwa serikali", kupanda kwa kasi kwa gharama za maisha......., ni wazi kuwa tuna tatizo kubwa sana ambalo kiujumla tunaweza kusema ni Tatizo la Uongozi".

Kama hivyo ndivyo, na tunajua kuwa serikali iliyopo madarakani ni serikali ya ccm, hapana shaka kuwa chama hiki kimeshindwa kutuongoza na kutufikisha kwenye "Tanzania tunayoitamani".

Kama wote tunakubaliana kuwa serikali ya ccm imeshindwa kutuongoza, ni wazi kuwa tunahitaji chama/watu mbadala wa kututoa katika matatizo haya na kutupeleka kwenye mafanikio tunayoyaota.
Wengi wanaweza kusema chama hicho ni CHADEMA na kiongozi mkuu wa kuliendesha gurudumu hilo ni Mh. Dr. Wilbroad Slaa kipenzi cha Watanzania.

Changamoto inabaki kuwa:
Je kama Dr. Slaa anakuwa Rais na CHADEMA inaachiwa nchi kuanzia leo, kitu gani wanaweza kukifanya ambacho kitasaidia kutatua matatizo lukuki ya Watanzania na kuwapa matumaini mapya katika kipindi hiki kifupi hadi kufikia 2015?

Kumbuka, mabadiliko hayo ni lazima yaonekane waziwazi na wananchi kama ilivyo rahisi kuyaona matatizo sasa.
 
1. Jambo la kwanza kabisa ni kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wale wote waliohusika na kashfa ya Radar, EPA, Richmond, IPTL, meremeta, kiwira, TRL na nyinginezo ndani ya kipindi cha siku mia moja.

2. Kuhakikisha mchakato wa katiba mpya unakwenda kwa spidi inayotakiwa na sio kusua sua kama JK

3. Kuhakikisha Watanganyika wanarudishiwa nchi yao ili waondokane na kutawaliwa na kisiwa.

4. Kuhakikisha kunakuwa na sera nzuri za uwekezaji ili kuondokana na wageni kupora ardhi ya wazawa. Wazawa wanaweza kuingia ubia na wawekezaji na sio kuwafukuza na kujitwalia ardhi yao.

5. Kukuza viwanda vya ndani ili kuongeza uzalishaji na usafirishaji wa bidhaa nje ya nchi. Hii inawezekana kwa kuvipatia motisha viwanda vya ndani ikiwa ni pamoja na kupunguza gharama za umeme nk.

6. Yapo mengi
 
1. Jambo la kwanza kabisa ni kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wale wote waliohusika na kashfa ya Radar, EPA, Richmond, IPTL, meremeta, kiwira, TRL na nyinginezo ndani ya kipindi cha siku mia moja.

2. Kuhakikisha mchakato wa katiba mpya unakwenda kwa spidi inayotakiwa na sio kusua sua kama JK

3. Kuhakikisha Watanganyika wanarudishiwa nchi yao ili waondokane na kutawaliwa na kisiwa.

4. Kuhakikisha kunakuwa na sera nzuri za uwekezaji ili kuondokana na wageni kupora ardhi ya wazawa. Wazawa wanaweza kuingia ubia na wawekezaji na sio kuwafukuza na kujitwalia ardhi yao.

5. Kukuza viwanda vya ndani ili kuongeza uzalishaji na usafirishaji wa bidhaa nje ya nchi. Hii inawezekana kwa kuvipatia motisha viwanda vya ndani ikiwa ni pamoja na kupunguza gharama za umeme nk.

6. Yapo mengi
Wakati unachangia kumbuka kuwa serikali haina hata senti tano. Ndo unaachiwa nchi katika hali hiyo.
 
Wakati unachangia kumbuka kuwa serikali haina hata senti tano. Ndo unaachiwa nchi katika hali hiyo.

Nchi hii ina mopesa kocho kocho, kama wakituachia nchi bila pesa.

1. tutachukua magari yote ya gharama ya wizara na mawaziri kisha piga bei ( bei ya faster faster)
2. Funga account zote za CCM kwa kuwa pesa na vitega uchumi vya CCM ni mali ya watanzania wote not CCM pekee.
3. Funga accounts zote za vigogo wa CCM na serikali yake.
4. Punguza mishahara mikubwa ya mabosi wa TANAPA, TANESCO, BOT nk.
5. weka kodi yenye kueleweka mwenye madini ( Tanzanite, gold, diamond n.k ) punguza kodi ya mafuta.
6. Weka kodi ya kueleweka kwenye mbuga zote za wanyama, weka wasimamizi wenye uchungu na nchi yetu.

should i say more? dont we have enough on that, all this will be done in 3 month, YES WE CAN
 
CDM watawapigia magoti ma Don wa ufisadi ili serikali iendeshwe vizuri...
kama hilo ni kweli, mbona serikali hii iliyopo madarakani tayari inafanya hivyo lakini mambo ndo yanazidi kuwa worst..?
 
Haya mambo yanahitaji seriousness tu!! Kama Mogadishu, Bagdadi, Kabul na Islamabad wanaserikali inayokusanya kodi na kulipa wafanyakazi wake. Sioni kama Dar Es Salam ni tatizo!!
 
Haya mambo yanahitaji seriousness tu!! Kama Mogadishu, Bagdadi, Kabul na Islamabad wanaserikali inayokusanya kodi na kulipa wafanyakazi wake. Sioni kama Dar Es Salam ni tatizo!!
Nimeshasema chadema watapokea nchi wakiwa na zero balance at hazina, still nchi itakuwa na madeni kibao...na hapo bado matatizo yakiwemo hayo ya madaktari.....na mengineyo yatakuwa yana-exist...
How are they going to run a govt with zero balance?
How are they going to fulfill people's expectations?

Kumbuka watakuwepo wale wa akina "Ngoja tuone sasa"
 
Mkuu nchi hii ni tajiri sana. Hebu angalia mkakati

1) Serikali lazima iwe ndogo wizara zitapunguzwa(manaibu, wakuu wa wilaya, mikoa wote watatolewa).
2) Rasilimali watu,maji (maziwa, bahari, mito, Samaki (ziwa victoria), madini (dhahabu, almasi, chuma,Tanzanite). Mrahaba wa madini 3% utatolewa na kubadilishwa kuwa 50% shareholding ( kama Botswana). Biashara holela hatuitaki, we want win win situation.
3) Utawala wa sheria. Wezi lazima waeleweshwe kuwa hawatavumiliwa hata kidogo.
4) Watendaji wasiochukua maamuzi hawatavumiliwa.
 
Nimeshasema chadema watapokea nchi wakiwa na zero balance at hazina, still nchi itakuwa na madeni kibao...na hapo bado matatizo yakiwemo hayo ya madaktari.....na mengineyo yatakuwa yana-exist...
How are they going to run a govt with zero balance?
How are they going to fulfill people's expectations?

Kumbuka watakuwepo wale wa akina "Ngoja tuone sasa"

Mkuu nchi hii ina rasilimali nyingi sana. Rasilimali ya kwanza ni Watu akiwemo wewe, Dr. Slaa na mimi hatuwezi kuanza na zero balance.
 
Mkuu nchi hii ni tajiri sana. Hebu angalia mkakati

1) Serikali lazima iwe ndogo wizara zitapunguzwa(manaibu, wakuu wa wilaya, mikoa wote watatolewa).
2) Rasilimali watu,maji (maziwa, bahari, mito, Samaki (ziwa victoria), madini (dhahabu, almasi, chuma,Tanzanite). Mrahaba wa madini 3% utatolewa na kubadilishwa kuwa 50% shareholding ( kama Botswana). Biashara holela hatuitaki, we want win win situation.
3) Utawala wa sheria. Wezi lazima waeleweshwe kuwa hawatavumiliwa hata kidogo.
4) Watendaji wasiochukua maamuzi hawatavumiliwa.

Ukiacha hiyo namba nne, hayo mengine yote yanahitaji pesa ambayo kwa sasa haipo serikalini.
Halafu hiyo inaonekana ni mipango ya muda mrefu, mingine inahitaji negotiations za muda mrefu.

Nataka mipango itakayoleta immediate changes say mwaka mmoja watu waone mabadiliko.
Kumbuka hapa siongelei mabadiliko ya figure, sijui inflation imeshuka kutoka ....hadi...hapana, nazungumzia mabadiliko ambayo kila mwananchi ataya-feel....yanayomgusa mwananchi directly na akayaona hata bila kuambiwa.
 
1. Jambo la kwanza kabisa ni kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wale wote waliohusika na kashfa ya Radar, EPA, Richmond, IPTL, meremeta, kiwira, TRL na nyinginezo ndani ya kipindi cha siku mia moja.

2. Kuhakikisha mchakato wa katiba mpya unakwenda kwa spidi inayotakiwa na sio kusua sua kama JK

3. Kuhakikisha Watanganyika wanarudishiwa nchi yao ili waondokane na kutawaliwa na kisiwa.

4. Kuhakikisha kunakuwa na sera nzuri za uwekezaji ili kuondokana na wageni kupora ardhi ya wazawa. Wazawa wanaweza kuingia ubia na wawekezaji na sio kuwafukuza na kujitwalia ardhi yao.

5. Kukuza viwanda vya ndani ili kuongeza uzalishaji na usafirishaji wa bidhaa nje ya nchi. Hii inawezekana kwa kuvipatia motisha viwanda vya ndani ikiwa ni pamoja na kupunguza gharama za umeme nk.

6. Yapo mengi

hujakosea
 
Nimeshasema chadema watapokea nchi wakiwa na zero balance at hazina, still nchi itakuwa na madeni kibao...na hapo bado matatizo yakiwemo hayo ya madaktari.....na mengineyo yatakuwa yana-exist...
How are they going to run a govt with zero balance?
How are they going to fulfill people's expectations?

Kumbuka watakuwepo wale wa akina "Ngoja tuone sasa"

CDM watakua kama Obama basi nia nzuri lakini hamna vitendea kazi na kwa hiyo kero na lawama zitaendelea...nafikiri hata kukopa sasa hatuwezi tena hizi IMF,WB ambazo ni short term solution ila long term financial and economic slavery....kazi kweli kweli hii nchi
 
padri slaa hawezi kuwa rais
kwanza ana historia ya usaliti
1.alilisaliti kanisa katoliki
lililomsomesha na kumpa hiyo
PHD fake.kwa kuliibia hela mpka
akafukuzwa
2.alilikisaliti chama kilichomlea
kwa tamaa ya madaraka ccm na
kukimbilia chama cha edwn mtei
cdm
3.amemsaliti mke wake wa
kwanza rose kamili.kisa tamaa
HATA AKIPATA NCHI ATATUSALITI
HUYU KWA KUWA NDIO TABIA YAKE
 
Kuna wachangiaji wengi hapa JF ambao wanatoa kupaumbele kikubwa sana kwa historia ya Dr. Slaa binafsi. Hasa kuacha kwake upadri, kumpa talaka mke wake wa kwanza na kumchukua Josephine bila kuzingatia taratibu zinazokubalika.

Kwetu sisi wanaharakati tunaotaka mabadiliko ya kweli na uhuru wa kweli, tunaona hizi ni dosari ndogo tu, ambazo hazituzuii kumwona Dr Slaa ndiye kiongozi wa kitaifa atayeweza kutekeleza sera na madhumuni ya CHADEMA kama yalivyoainishwa miaka hii ya karibuni. Dr Slaa ni msomi aliyebobea hata kimataifa; ni m'bunifu na mchapa kazi makini. Dr Slaa ni mzalendo wa hali ya juu anayeona uchungu na mali ya umma inayofujwa au kuibwa; na ana huruma kwa wanyonge wa Tz wanaozidi kutaabika. Dr Slaa ni jasiri, kwa maana kwamba hasiti na haogopi kusema analoamini kuwa ni la kweli. Dr Slaa sio mkatili.

Sifa hizi za Dr Slaa zinajiongeza kwa yeye kuwa na uwezo wa kufanya kazi na watu wa kada zote; bila kujali wana vyeo au elimu ya kiwango gani. Naamini kwamba Chadema kimebahatika kumpata kiongozi wa aina hii; na anaweza kukabidhiwa usukani wa gari la taifa litakalotuondoa katika adha zinazozidi kuongezeka kila kukicha.

Kilasara Mamremi
 
Wakuu salaam,
Nimejaribu kutafakari mwenendo mzima wa taifa letu na matukio kadhaa ambayo yamelikumba taifa letu kufikia sasa na hasa haya ya hivi karibuni bado nabaki na maswali lukuki kichwani bila majibu.

Ukianzia mgomo wa madaktari, mgogoro wa posho za wabunge, "kufilisika kwa serikali", kupanda kwa kasi kwa gharama za maisha......., ni wazi kuwa tuna tatizo kubwa sana ambalo kiujumla tunaweza kusema ni Tatizo la Uongozi".

Kama hivyo ndivyo, na tunajua kuwa serikali iliyopo madarakani ni serikali ya ccm, hapana shaka kuwa chama hiki kimeshindwa kutuongoza na kutufikisha kwenye "Tanzania tunayoitamani".

Kama wote tunakubaliana kuwa serikali ya ccm imeshindwa kutuongoza, ni wazi kuwa tunahitaji chama/watu mbadala wa kututoa katika matatizo haya na kutupeleka kwenye mafanikio tunayoyaota.
Wengi wanaweza kusema chama hicho ni CHADEMA na kiongozi mkuu wa kuliendesha gurudumu hilo ni Mh. Dr. Wilbroad Slaa kipenzi cha Watanzania.

Changamoto inabaki kuwa:
Je kama Dr. Slaa anakuwa Rais na CHADEMA inaachiwa nchi kuanzia leo, kitu gani wanaweza kukifanya ambacho kitasaidia kutatua matatizo lukuki ya Watanzania na kuwapa matumaini mapya katika kipindi hiki kifupi hadi kufikia 2015?

Kumbuka, mabadiliko hayo ni lazima yaonekane waziwazi na wananchi kama ilivyo rahisi kuyaona matatizo sasa.

Slaa akiwa rais wa nchi gani; unaota au? aandae mabomu yake feki ya kulipua 2015 - na 2020.
 
Kuna wachangiaji wengi hapa JF ambao wanatoa kupaumbele kikubwa sana kwa historia ya Dr. Slaa binafsi. Hasa kuacha kwake upadri, kumpa talaka mke wake wa kwanza na kumchukua Josephine bila kuzingatia taratibu zinazokubalika.

Kwetu sisi wanaharakati tunaotaka mabadiliko ya kweli na uhuru wa kweli, tunaona hizi ni dosari ndogo tu, ambazo hazituzuii kumwona Dr Slaa ndiye kiongozi wa kitaifa atayeweza kutekeleza sera na madhumuni ya CHADEMA kama yalivyoainishwa miaka hii ya karibuni. Dr Slaa ni msomi aliyebobea hata kimataifa; ni m'bunifu na mchapa kazi makini. Dr Slaa ni mzalendo wa hali ya juu anayeona uchungu na mali ya umma inayofujwa au kuibwa; na ana huruma kwa wanyonge wa Tz wanaozidi kutaabika. Dr Slaa ni jasiri, kwa maana kwamba hasiti na haogopi kusema analoamini kuwa ni la kweli. Dr Slaa sio mkatili.

Sifa hizi za Dr Slaa zinajiongeza kwa yeye kuwa na uwezo wa kufanya kazi na watu wa kada zote; bila kujali wana vyeo au elimu ya kiwango gani. Naamini kwamba Chadema kimebahatika kumpata kiongozi wa aina hii; na anaweza kukabidhiwa usukani wa gari la taifa litakalotuondoa katika adha zinazozidi kuongezeka kila kukicha.

Kilasara Mamremi

Arusha/ Moshi
 
Tatizo kubwa ambalo mimi naliona ni unafiki wa watendaji wa serikali.Wao wanaitaka serikali kwa maana ya masilahi wanayopata lakini mioyo yao iko cdm.Ndiyo maana leo hii barua ya siri kutoka ikulu inafika kwanza cdm kabla ya alitumiwa hiyo barua hajaipata.
 
Tatizo kubwa ambalo mimi naliona ni unafiki wa watendaji wa serikali.Wao wanaitaka serikali kwa maana ya masilahi wanayopata lakini mioyo yao iko cdm.Ndiyo maana leo hii barua ya siri kutoka ikulu inafika kwanza cdm kabla ya alitumiwa hiyo barua hajaipata.
katika harakati za kumkomboa mtanzania, ni jambo jema hilo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom