Mbunge wa CCM
JF-Expert Member
- Nov 13, 2009
- 475
- 22
Waungwana nimepata kisa hiki kwenye gazati la habari leo na nimeguswa na maoni ya mmoja wa wasomaji wa gazeti hilo. Hebu jisomee na wewe:
Habari yenyewe
WALIMU wawili mkoani Singida wanatuhumiwa kumbaka na kumpa ujauzito mwanafunzi mwenye umri wa miaka 17 anayesoma kidato cha tatu katika shule ya sekondari ya Mtinko.
Walimu hao katika Halmashauri ya Wilaya ya Singida akiwemo wa shule ya msingi wanatarajiwa kupandishwa kizimbani leo kujibu mashitaka yanayowakabili.
Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa na Hakimu Chiganga Tengwa wa Mahakama ya Hakimu Mkazi mjini hapa, na Mwendesha Mashitaka, atakuwa Mkaguzi wa Polisi, Nasoro Shekevi.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida,Celina Kaluba,amewataja walimu hao kuwa ni Deogratius Donald (23) wa Shule ya Sekondari Mtinko na William Mwidunda (2 wa Shule ya Msingi Mtinko.
Kamanda Kaluba amesema, ujauzito wa mwanafunzi huyo hivi sasa umefikisha umri wa miezi minne.
Kaluba amesema,walimu hao wanatuhumiwa kumbaka mwanafunzi huyo kwa nyakati tofauti na kumpa ujauzito. Watuhumiwa hao wanaishi katika nyumba moja ya kupanga kijijini Mtinko.
Inadaiwa kuwa Donald ndiye aliyekuwa akimfundisha masomo ya ziada (tuisheni) mwanafunzi huyo kwenye nyumba anayoishi na kwamba, mara baada ya kumaliza kumfundisha, alikuwa akimbaka msichana huyo.
Kwa mujibu wa Sheria ya Makosa ya Kujamiana nchini, msichana yeyote mwenye umri wa chini ya miaka 18, hata kama akiridhia kufanya tendo la kujamiiana, mwanamume anayefanya naye tendo hilo anafanya kosa la kubaka.
Habari zaidi zinadai kuwa wakati Donald akiwa kwenye majukumu mengine, alikuwa akimpa rafiki yake Mwidunda jukumu la kumfundisha mwanafunzi huyo.
Kwa mujibu wa Kamanda Kaluba, Desemba 14, baba mzazi wa msichana huyo, Abdallah Omari, alitoa taarifa katika Kituo Kidogo cha Polisi Mtinko kuhusu mwanawe kupewa ujauzito
Maoni ya msomaji
Walimu siku zote nikuonewa tu! hivi nilini mwalimu yeye atapata haki hata kulindwa katika jamii? mzazi huyu alishindwa kumlipa mwalimu huyu hela yake ya tuition na baada ya kumdai sasa imekuwa kesi ya kubaka. binti huyu kapewa ujauzito na wanafunzi wenzake sasa ni walimu kulaumiwa. Watanzania umefika wakti tutambue kazi anayoifanya mwalimu katka jamii na kuiheshimu. we cannot blame teacher for evrything they do it is uncouth and very discouraging. Angekuwa afisa mwingine yeyote habari hizi yawezekana zi singetolewa kwa uzito huu.
Tafakari
1.
Majuzi tulimsikia Sophia samba aisema kuwa mh. Sendeka ana kesi inayofanana nah ii lakini kahifadhiwa kwa sababu anazozijua samba na wenzie. Hivi hawa walimu wangekuwa saizi ya mh. Sendeka wangefikishwa mahakamani?
2.
Kuna ukweli gani kwenye maoni ya msomaji kuwa walimu kila siku ni wa kuonewa tu? Na eti wamesingiziwa baada ya mzazi kushindwa kulipia tuition?
3.
Hii sheria inayowamulika wanaume tu na kutosema chochote kwa upande wa msichana hata kama aliridhia kufanya ngono, inatufaa kweli? Si ubaguzi?
Leteni maoni yenu.
Source: http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=5025
Habari yenyewe
WALIMU wawili mkoani Singida wanatuhumiwa kumbaka na kumpa ujauzito mwanafunzi mwenye umri wa miaka 17 anayesoma kidato cha tatu katika shule ya sekondari ya Mtinko.
Walimu hao katika Halmashauri ya Wilaya ya Singida akiwemo wa shule ya msingi wanatarajiwa kupandishwa kizimbani leo kujibu mashitaka yanayowakabili.
Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa na Hakimu Chiganga Tengwa wa Mahakama ya Hakimu Mkazi mjini hapa, na Mwendesha Mashitaka, atakuwa Mkaguzi wa Polisi, Nasoro Shekevi.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida,Celina Kaluba,amewataja walimu hao kuwa ni Deogratius Donald (23) wa Shule ya Sekondari Mtinko na William Mwidunda (2 wa Shule ya Msingi Mtinko.
Kamanda Kaluba amesema, ujauzito wa mwanafunzi huyo hivi sasa umefikisha umri wa miezi minne.
Kaluba amesema,walimu hao wanatuhumiwa kumbaka mwanafunzi huyo kwa nyakati tofauti na kumpa ujauzito. Watuhumiwa hao wanaishi katika nyumba moja ya kupanga kijijini Mtinko.
Inadaiwa kuwa Donald ndiye aliyekuwa akimfundisha masomo ya ziada (tuisheni) mwanafunzi huyo kwenye nyumba anayoishi na kwamba, mara baada ya kumaliza kumfundisha, alikuwa akimbaka msichana huyo.
Kwa mujibu wa Sheria ya Makosa ya Kujamiana nchini, msichana yeyote mwenye umri wa chini ya miaka 18, hata kama akiridhia kufanya tendo la kujamiiana, mwanamume anayefanya naye tendo hilo anafanya kosa la kubaka.
Habari zaidi zinadai kuwa wakati Donald akiwa kwenye majukumu mengine, alikuwa akimpa rafiki yake Mwidunda jukumu la kumfundisha mwanafunzi huyo.
Kwa mujibu wa Kamanda Kaluba, Desemba 14, baba mzazi wa msichana huyo, Abdallah Omari, alitoa taarifa katika Kituo Kidogo cha Polisi Mtinko kuhusu mwanawe kupewa ujauzito
Maoni ya msomaji
Walimu siku zote nikuonewa tu! hivi nilini mwalimu yeye atapata haki hata kulindwa katika jamii? mzazi huyu alishindwa kumlipa mwalimu huyu hela yake ya tuition na baada ya kumdai sasa imekuwa kesi ya kubaka. binti huyu kapewa ujauzito na wanafunzi wenzake sasa ni walimu kulaumiwa. Watanzania umefika wakti tutambue kazi anayoifanya mwalimu katka jamii na kuiheshimu. we cannot blame teacher for evrything they do it is uncouth and very discouraging. Angekuwa afisa mwingine yeyote habari hizi yawezekana zi singetolewa kwa uzito huu.
Tafakari
1.
Majuzi tulimsikia Sophia samba aisema kuwa mh. Sendeka ana kesi inayofanana nah ii lakini kahifadhiwa kwa sababu anazozijua samba na wenzie. Hivi hawa walimu wangekuwa saizi ya mh. Sendeka wangefikishwa mahakamani?
2.
Kuna ukweli gani kwenye maoni ya msomaji kuwa walimu kila siku ni wa kuonewa tu? Na eti wamesingiziwa baada ya mzazi kushindwa kulipia tuition?
3.
Hii sheria inayowamulika wanaume tu na kutosema chochote kwa upande wa msichana hata kama aliridhia kufanya ngono, inatufaa kweli? Si ubaguzi?
Leteni maoni yenu.
Source: http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=5025