Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,059
- 22,755
Kwa nini serikali inadai chenji ya rada ? Kumbe chenji inayodaiwa ni ya CCM na si taifa. Kwa nini kamati ya CCM haikutumwa Uingereza kufuatilia hizo chenji na badala yake ikatumwa kamati ya bunge ? Je ndani ya katiba yetu ni kipengele kipi kinaipa CCM hizi nguvu za kutuhumu, kushitaki, kuendesha kesi na kutoa hukumu nje ya vyombo husika ?Nape said:Uamuzi wa kumchukulia hatua Chenge ulichukuliwa na kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa. Uamuzi ulichukuliwa na kikao halali cha chama kuwawajibisha watuhumiwa wa masuala ya ufisadi, wakiwamo watuhumiwa wa rada.
Yawezekana ni kweli na ndio sababu wahalifu hawana wasiwasi wakiwa ndani ya CCM, nani atathubutu kuwachukulia hatua za kisheria ? Ndio maana vyombo vyote vya dola vinafanya kazi kwa maagizo ya viongozi wa CCM hasa jeshi la polisi, usalama wa taifa na mwaka jana likatumika hadi JWTZ. Tumeshuhudia polisi wakiwaua raia na hakuna hatua zinachukuliwa kwa sababu wanatekeleza maagizo ya vikao halali vya CCM. Kumbe tume ya uchaguzi na msajili wa vyama mahakama ni kweli vinaipendelea CCM !Nape said:Chama ni chombo cha juu kuliko Serikali, hivyo uamuzi uliofanywa kwenye kikao halali, utaendelea kusimama hata kama Serikali itaendelea kumsafisha Chenge.
Mbona siku zote CCM inavikoromea vyama na hasa Chadema kutoa ushahidi wa ufisadi wa viongozi wa CCM kuanzia Mwenyekiti wake kama ile Orodha ya Mafisadi ya Mwebeyanga mwaka 2007 ? Je vipi wale watuhumiwa wa KAGODA, Meremeta, Kiwira, Dowans, Tangold, Richmond n.k.Nape said:Yawezekana wenyewe Serikali hawana ushahidi wa kuwapeleka mahakamani, lakini sisi chama hatuhitaji huo ushahidi wa kumchukulia Chenge hatua.
Kama nakumbuka vizuri Chenge alijiuzulu kufuatia kelele za Wananchi kwa kashfa ya kuita dola milioni moja kwenye account yake, vijisenti !Nape said:Katibu huyo alisema, wakati Chenge anawajibika kujiuzulu uwaziri, hakusubiri ushahidi wa mahakama na akaongeza kuwa huo ni mfano mzuri wa uwajibikaji wa kisiasa alioufanya mwanasiasa huyo.
Naona CCM imeamua sasa kuvaa ngozi yake halisi na kuonyesha kuwa mageuzi ya mwaka 1992 yalikuwa ni danganya toto tu, chama kumbe bado kimeshika hatamu. Hakuna cha katiba, hakuna cha serikali, hakuna cha watu milioni arobaini, hakuna cha vyama vingi na hakuna cha taifa, hapana, ni genge la watu milioni tano (?) tu. Na kwa Nape wamevuna walichopanda !Nape said:"Ndiyo maana hizi tuhuma zilichunguzwa na SFO (Serious Fraud Office) na Takukuru hadi waziri akajiuzulu," alisema Nape na kuongeza: "Kama Serikali haikupata ushahidi au imeupata wanajua wenyewe, lakini sisi kwa upande wa chama, tuhuma hizi zinatosha, ndiyo maana alijiuzulu uwaziri kukubali kuwa tuhuma hizo si ndogo."
By the way kuna jambo naomba mwongozo kutoka kwa wana JF, hivi kwenye kashfa ya rada aliyetoa tuhuma na kusababisha uchunguzi kufanywa ni aliyeibiwa (Tanzania) au aliyeiba (Uingereza) ? Ninavyofahamu aliyeibiwa hakuchukua hatua yoyote ile ama ya kulalamika au ya kutoa tuhuma hadi pale wasamaria wenye uchungu nchini Uingereza walipoanza kuuliza kulikoni. Wakafanya uchunguzi na ikabainika kuwa kuna uhalifu ulifanyika na baada ya hapo mpira tukapasiwa tuchukue hatua lakini tukashindwa hata hilo. Baada ya kuona jitihada zetu ni sufuri wakaamua kuridhia mapatano nje ya mahakama na hapo walafi kama kawaida yao na bila aibu wakapata mwanya wa kutaka kuvuna wasichopanda, loooo ! Tulioibiwa ni sisi, walioshtuka na kufanya uchunguzi ni wao ila sisi bila hata kuwafungulia wezi wetu kesi tumeshakaa mkao wa kula.