Kama CHADEMA haitambui ya 2020 kwanini wanataka Wabunge 19 watoke bungeni?

mkalamo

JF-Expert Member
Sep 7, 2013
324
347
TAKRIBAN miezi sita sasa imepita tokea Chadema waseme hawatambui matokeo ya uchaguzi mkuu wa 2020.

Kutokana na msimamo huo ni wazi kwamba hawaamini,chama hicho hakitambui uwepo wa baraza la madiwani popote nchini,halitambui uwepo wa Bunge na wabunge waliopo bungeni na hawatambui pia uwepo wa Rais aliyepo madarakani,aliyetokana na uchaguzi wa 2020.

Msimamo huu uliwekwa hadharani na katibu mkuu wa CHADEMA, John Mnyika Novemba 25 mwaka jana aliposema kamati kuu ya chama ambayo inadhamana ya kupokea maombi, kupitia na kufanya uteuzi wa wabunge wa viti maalumu haikufanya mchakato huo, kutokana na chama hicho kutangaza hadharani kutoyambua matokeo ya uchaguzi uliomrejesha madarakani rais John magufuli na kupita kwa idadi kubwa ya wabunge kutoka chama cha mapinduzi CCM.

Pia Mwenyekiti wa chama hicho Freman Mbowe katika kukazia uamuzi huo alisema

"kilochofanyika si uchaguzi ni unyang'anyi wa demokrasia uliofanywa na ZEC (Tume ya Uchaguzi Zanzibar) na NEC (Tume ya Taifa ya Uchaguzi) .''

Hata yalipotangazwa nafasi ya ubunge wa viti maalum chama hicho walisema hawatapeleka wabunge.

Lakini miongoni mwao waliona msimamo huo unaminya fursa ya wao kuwa viongozi na wakayatambua matokeo yote ya 2020 na hatimaye wakaenda kuapa bungeni wakiongozwa na Halima Mdee.

Baada ya uamuzi huo,chama kiliingia katika mchakato wa kuwafukuza uanachama.

Jambo la kusikitisha sasa kila kukicha viongozi hao wanataka wale waliowatimua uanachama,pia watimuliwe katika bunge wasilolitambua

Yaani iko hivi unasema wewe si mtanzania na huutambui utanzania,lakini miongoni mwa watoto wako wakasema wao ni watanzania na mzazi ukawakana kuwa si watoto wako

Wameenda kutafuta ubini kwingine napo mzazi anataka pia huko wafukuzwe.

Wanapoulizwa je unawatambua unaosema wawafukuze jibu hakuna.

Sasa basi wajibu haya

Je, madiwani na mbunge mmoja hawa nafasi yao katika msimamo huo ni upi?

2.Kwa kuwa msimamo wa chama ni kutotambua chochote kilichotokana na uchaguzi na kwa kuwa kina Mdee wamekiuka hilo, walikuwa na haki ya kuchukua hatua waliyochukua

Katika eneo hili kwanini wasipiganie bunge lote lisiwepo kwa kuwa msimamo wa chama ni kutotambua yale yote yaliyotokana na uchaguzi wa 2020 na sasa wanajielekeza kutaka watu wasio wanachama wao kutoshitiki kile wasichokitambua(Ubunge
 
Wewe ni wa hovyo. Yaani watu wajipeke kwenda kuapa kwa kutumia chama kisichotaka ?!.

Ni nani aliyemtoa Nusrat jela usiku wa manane kuwahi kuapishwa mkoa mwingine ?!
Wameenda kuapa katika bunge lisilotambuliwa na chama,kwanini mnataka kuwatoa humo msipotambua? Na je wakitoka mtawapeleka muwatakao?
 
Wameenda kuapa katika bunge lisilotambuliwa na chama,kwanini mnataka kuwatoa humo msipotambua? Na je wakitoka mtawapeleka muwatakao?
Kwanini Cdm wapangiwe wa kuwawakilisha hasa baada ya kuhakikisha mmewapora kura zao ?!. Kama hamkuwataka bungeni, uwema huu wa Ndugai na Jiwe ulitoka wapi ?!. Mungu hachezewi
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Yaani iko hivi unasema wewe si mtanzania na huutambui utanzania,lakini miongoni mwa watoto wako wakasema wao ni watanzania na mzazi ukawakana kuwa si watoto wako

Wameenda kutafuta ubini kwingine napo mzazi anataka pia huko wafukuzwe.
Hivi mkuu umeandika baada ya kushiba makande ya jumamosi au baada ya kutoka klabuni ulikoalikwa na rafiki yako aliyelipia huduma?

Unasema watoto wameenda kutafuta ubini mwingine wakati wanajiita ni wabunge wa chadema? Umesahau dada Tulia alivyomkana yule mbunge kuwa hawajafukuzwa chadema na wanatambulika kuwa ni wa chadema?

Sometimes tumia kichwa kwa kazi zingine badala ya kukitumia kama kabati la kuhifadhia meno tu
 
Akina mzee Mdee a.k.a Covid-19 wanatumia jina la taasisi iliyotukuka kidemokrasia ....Chadema.

Hiyo ndiyo sababu.
 
Wale ni wezi Kama wezi wengine,siku nimewapa TOKA bungeni kidogo wataokota makopo nasema labda Kama mungu wangu amenisusa ila najua yu hai.
 
Kwa nini nyie ccm mmekuwa watetezi wa wabunge wa CDM ambao hawatambuliki Kuna nini nyuma yenu.
 
Wameenda kuapa katika bunge lisilotambuliwa na chama,kwanini mnataka kuwatoa humo msipotambua? Na je wakitoka mtawapeleka muwatakao?
Nadhani wanataka Bunge liseme wazi kuwa wale ni wabunge wasio na chama.Bunge likisema hivyo kuwa hawana chama halafu CDM wakaendelea kulalamika hapo ndo itabidi kuuliza kwanini wanalalamika?
 
Wameenda kuapa katika bunge lisilotambuliwa na chama,kwanini mnataka kuwatoa humo msipotambua? Na je wakitoka mtawapeleka muwatakao?
Swala la hao covid sio tu la Chadema....wamekaa huko wanalipwa kodi zetu wananchi, inatakiwa waondoke, hayo ni matumizi mabaya ya pesa.

Waondoke wakajiajiri kama ambavyo wanaambia vijana wajiajiri, wapelekwe wapi kwani ni walemavu??? Wakajiajiri
 
CHADEMA haijataka kina Mdee watoke bungeni bali katiba ndivyo inavyoagiza. Sifa mojawapo ya kuwa mbunge wa viti maalum ni kuwa mwanachama wa chama cha siasa.
 
Back
Top Bottom