Kama Bandari ya Bagamoyo lazima ijengwe, basi sio kwa masharti ya kuweka nchi rehani

kmbwembwe

JF-Expert Member
Aug 16, 2012
10,408
7,190
Tukubaliane tusikubaliane Rais Samia kashakubali mradi wa Bagamoyo kwa masharti aliyoyakataa Magufuli na ambayo Kikwete aliyakubali. Kwa hivi sasa ni kiini macho kinafanyika. Watatumwa watu kimbelembele kuendesha mazungumzo.

Nionavyo mimi viongozi wabinafsi wamejaa kwenye ranks za CCM na bungeni kuliko wananchi wanavyofikiri. Kuna wanafikiri Magufuli kuhamishia makao makuu Dodoma na kufuta mpango wa Bandari Bagamoyo na huku kuwekeza maeneo ya ziwa aliafanya upendeleo.

Kila mwananchi amejua masharti ya kuwekeza bandari ya Bagamoyo baada ya Magufuli kuyataja. Vinginevyo yalifanywa siri. Kwanini viongozi wetu wakubali mashari ya kidhalimu namna hiyo kama sio kwa sababu za maslahi binafsi?

Licha ya Rais Samia kusema yeye na Magufuli ni kitu kimoja itakua ulaghai kwa kua anayofanya ni tofauti. Mradi wa bagamoyo wananchi watataka kuona mashari yake sio yale ya kikoloni aliyowaambia Magufuli. Kama bandari lazima ijengwe sio kwa masharti ya kuweka nchi rahani. Ni bora mradi ufe au tuje tujenge wenyewe kwa fedha yetu.

Tulimsikia kikwete akisema wapwani hawangependa mji mkuu uhamie Dodoma. Tumeona samia akirejesha shughuli za rais kila wakati Dar na sasa anataka bandari ya bagamoyo kujengwa kwa vyovyote.
 
Si tunakwenda kuzungumza?, hakuna haja ya kuhofia mazungumzo.
Twende tukazungumze tukubaliane, tukiona hakuna maslahi tunaacha. Kwani shida iko wapi?
Kwa mfano, Tajiri Mkubwa aje kwenye familia yenu Kwa lengo la kukodisha uwanja ulioko mbele ya nyumba ya familia Kwa ajili ya biashara na akataka kukodisha kwa miaka 100 Kwa malipo na masharti ambayo Baba yenu anaona hayana maslahi mapana kwenye familia yenu na.vizazi vyake, na akakataa.

Mzee wako akifariki na mama yako akaanza kuwaambia tumsikilize tena huyu Tajiri hutakuwa mtovu wa nidhamu kuulizia kama masharti ni Yale Yale au yameboreshwa?..na ni lazima wanafamilia wawe makini zaidi na Nia ya Mama, just incase anarubuniwa na Tajiri ili hakubaliane na masharti aliyoyakataa Baba yako.

Therefore sioni tatizo lolote Watanzania kuwa na wasiwasi just incase Magu alikua sahihi. Jambo la msingi ni viongozi wetu kuweka hii kitu wazi kwani ni investment kubwa Sana ambayo ina maslahi makubwa Sana na too much is at stake, kuwaachia watu wasiozidi 30 kutufanyia uamuzi huu Mkubwa wakiwa wamejifungia chumbani bila kutwambia walichokubaliana ni hatari sana Kwa ustawi wa nchi yetu pendwa.
 
Kwa mfano, Tajiri Mkubwa aje kwenye familia yenu Kwa lengo la kukodisha uwanja ulioko mbele ya nyumba ya familia Kwa ajili ya biashara na akataka kukodisha kwa miaka 100 Kwa malipo na masharti ambayo Baba yenu anaona hayana maslahi mapana kwenye familia yenu na.vizazi vyake, na akakataa.

Mzee wako akifariki na mama yako akaanza kuwaambia tumsikilize tena huyu Tajiri hutakuwa mtovu wa nidhamu kuulizia kama masharti ni Yale Yale au yameboreshwa?..na ni lazima wanafamilia wawe makini zaidi na Nia ya Mama, just incase anarubuniwa na Tajiri ili hakubaliane na masharti aliyoyakataa Baba yako.

Therefore sioni tatizo lolote Watanzania kuwa na wasiwasi just incase Magu alikua sahihi. Jambo la msingi ni viongozi wetu kuweka hii kitu wazi kwani ni investment kubwa Sana ambayo ina maslahi makubwa Sana na too much is at stake, kuwaachia watu wasiozidi 30 kutufanyia uamuzi huu Mkubwa wakiwa wamejifungia chumbani bila kutwambia walichokubaliana ni hatari sana Kwa ustawi wa nchi yetu pendwa.
Ukigundua tajiri kweli anaihitaji mali na hana ujanja basi hapo unajua tu kuwa utamkamata tu atake asitake. Kwa hiyo mazungumzo bado ni muhimu, hakuna haja ya kuyahofia!
 
Kwa mfano, Tajiri Mkubwa aje kwenye familia yenu Kwa lengo la kukodisha uwanja ulioko mbele ya nyumba ya familia Kwa ajili ya biashara na akataka kukodisha kwa miaka 100 Kwa malipo na masharti ambayo Baba yenu anaona hayana maslahi mapana kwenye familia yenu na.vizazi vyake, na akakataa.

Mzee wako akifariki na mama yako akaanza kuwaambia tumsikilize tena huyu Tajiri hutakuwa mtovu wa nidhamu kuulizia kama masharti ni Yale Yale au yameboreshwa?..na ni lazima wanafamilia wawe makini zaidi na Nia ya Mama, just incase anarubuniwa na Tajiri ili hakubaliane na masharti aliyoyakataa Baba yako.

Therefore sioni tatizo lolote Watanzania kuwa na wasiwasi just incase Magu alikua sahihi. Jambo la msingi ni viongozi wetu kuweka hii kitu wazi kwani ni investment kubwa Sana ambayo ina maslahi makubwa Sana na too much is at stake, kuwaachia watu wasiozidi 30 kutufanyia uamuzi huu Mkubwa wakiwa wamejifungia chumbani bila kutwambia walichokubaliana ni hatari sana Kwa ustawi wa nchi yetu pendwa.
Huo mfano sio sahihi kabisa. Magulifu ni Rais, Kikwete ni Rais na Samia ni Rais. Ni kipimo gani unatumia kusema Magufuli ndiye baba safi na mkweli aliyeona mradi haufai? Je, ni jopo gani Magufuli alilitumia kuudadavua mradi ambalo Kikwete hakulitumia na Rais Samia hatalitumia?

Kuhamia dodoma leo kuna manufaa gani kwa taifa kiuchumi, kisiasa na hata kiutamaduni? Je, faida na hasara za kununua ndege kwa cash zikichambuliwa na kupitishwa na nani? Je, mkataba ya kujenga SGR unaujua? Je, faida na hasara ya kujenga uwanja wa ndege chato zinafahamika?

Tuache Rais Samia nae atumie akili yake na washauri wake kuliongoza taifa. Tusifuge jiinamizi linalotaka kuatamia maamuzi na utendaji wa marais wengine waliopita, waliopo na wajao.
 
Tufanye hana akili, lakini kaongea vitu vyenye akili, tusivipuuze, tuvitazame vizuri kwa ajili yetu na siyo kwa ajili ya magufuli unayemdhania ni mjinga
Hakuna Cha akili, huwezi kusikiliza upande mmoja ukahitimisha. Lazima tuangalie pande zote. Kama huo mkataba ungewekwa wazi kila mtu akaona ndipo tungechambua mbovu na nzima. Kwa sasa huwezi kutoa maoni kwa upande mmoja. Wakati utakapofika tutajua.
 
Kwa nini unamwamini Magufuli? Hao wote hawana akili ila yeye tu? Subiri mambo yakae sawa. Hakuna aliyeuona mkataba halisi.
Issue inakuja kwenye reference countries ambazo wachina wameshaweka investment kama hizi.. nchi hizo zimenasa kwenye makucha ya mkoroni mpya.

Magufuli inawezekana alituongopea na kama alidanganya basi aliwapaka matope wawekezaji na sio jambo jema wakae kimya Kwa kuzushiwa jambo ambalo si la kweli na ukaendelea na swala Hilo bila kusema ukweli halisi, nadhani watanzania ndio wakitakacho. Maadam aliyedanganya hayupo, tuambieni ukweli ni upi ili KAZI iendelee.
 
Huo mfano sio sahihi kabisa. Magulifu ni Rais, Kikwete ni Rais na Samia ni Rais. Ni kipimo gani unatumia kusema Magufuli ndiye baba safi na mkweli aliyeona mradi haufai? Je, ni jopo gani Magufuli alilitumia kuudadavua mradi ambalo Kikwete hakulitumia na Rais Samia hatalitumia?

Kuhamia dodoma leo kuna manufaa gani kwa taifa kiuchumi, kisiasa na hata kiutamaduni? Je, faida na hasara za kununua ndege kwa cash zikichambuliwa na kupitishwa na nani? Je, mkataba ya kujenga SGR unaujua? Je, faida na hasara ya kujenga uwanja wa ndege chato zinafahamika?

Tuache Rais Samia nae atumie akili yake na washauri wake kuliongoza taifa. Tusifuge jiinamizi linalotaka kuatamia maamuzi na utendaji wa marais wengine waliopita, waliopo na wajao.
Uko sahihi kabisa..lakini kumbuka hii nchi INA wazazi (Baba na Mama) wengi Sana, lakini kuna wazazi wamejenga familia madhubuti na zenye mafanikio makubwa Sana, na kuna nyingine ziko Duni,Baba mlevi,mama kahaba lakini wote tumo. Baba wote sio makini,na Baba wote sio walevi...chagua wako.
 
JPM alitaka miradi hii ifanyike kwa namna ambayo wadau watanufaika sawa na uwazi wa mkataba wenyewe. Wako watu wanao weza kuaminiwa na Watanzania wenzao wapewe kazi hiyo ya kuzungumza na wachina. Si huyu anaye kiri hadharani nimepenyezewa, haaminiki huyu.
 
Hakuna Cha akili, huwezi kusikiliza upande mmoja ukahitimisha. Lazima tuangalie pande zote. Kama huo mkataba ungewekwa wazi kila mtu akaona ndipo tungechambua mbovu na nzima. Kwa sasa huwezi kutoa maoni kwa upande mmoja. Wakati utakapofika tutajua.
Kwani upande wa pili wali/wanasemaje?
 
Uko sahihi kabisa, lakini kumbuka hii nchi INA wazazi (Baba na Mama) wengi Sana, lakini kuna wazazi wamejenga familia madhubuti na zenye mafanikio makubwa Sana, na kuna nyingine ziko Duni,Baba mlevi,mama kahaba lakini wote tumo. Baba wote sio makini,na Baba wote sio walevi, chagua wako.
Baba bora na madhubuti sio yule anaejenga nyumba ya kifahari kwa pesa ya kulipa ada za shule za watoto wake, kununulia chakula cha familia.

Kiuhalisia baba yule alitegeneza baiskeli yake mbovu kwa kuchukua spea kutoka baiskeli nyingine iliyokuwa nzima inatembea. Amefufua mbovu akaua nzima. Kila sehemu ni kilio kwa gharama za Dodoma, chato, ndege, meli, reli na madaraja.
 
Mwekezaji makini hawezi kuja kuwekeza kwenye nchi isiyo na stability kiuchumi. Hii nchi ni "one man show" Hujui baada ya SSH atakayekuja atakua na msimamo gani maana nchi kama nchi haina iliposimamia, inategemea mkuu wa wakati huo anataka nini. Kwa long term investments hali hiyo ni mashaka, hata ukiwa na mikataba ya namna gani.
 
Baba bora na madhubuti sio yule anaejenga nyumba ya kifahari kwa pesa ya kulipa ada za shule za watoto wake, kununulia chakula cha familia.

Kiuhalisia baba yule alitegeneza baiskeli yake mbovu kwa kuchukua spea kutoka baiskeli nyingine iliyokuwa nzima inatembea. Amefufua mbovu akaua nzima. Kila sehemu ni kilio kwa gharama za Dodoma, chato, ndege, meli, reli na madaraja.
Umesahau kuna wengine ata hiyo baiskeli awatengenezi wanauza scraper za baiskeli mbovu na wanauza spare za nzima ili wapate pesa ya kwenda Kula Bata. Chagua wako coz kila mtoto anasema Baba yake ndio hero wake, inategemea umekaa angle ipi.
 
Hakuna Cha akili, huwezi kusikiliza upande mmoja ukahitimisha. Lazima tuangalie pande zote. Kama huo mkataba ungewekwa wazi kila mtu akaona ndipo tungechambua mbovu na nzima. Kwa sasa huwezi kutoa maoni kwa upande mmoja. Wakati utakapofika tutajua.
Hahaaa!

Usipaniki mkuu, Nimetoa angalizo tu, hata hao unaodhani ni wajinga, wanakusaidia wewe ujione uko tofauti na wao ila sio kuwapuuza

Na unaakili na unauelewa kwa sababu pia upande mwingine kunawasio na uelewa, Jitahidi sana kupambanua mambo, Maana kuna mtu msomi ila hana maarifa, na kunaasiye msomi ila ana maarifa

Usipingane na maarifa, utakuwa mpumbavu kama prof mmoja baada ya kuingia kwenye jahazi kwenda ng'ambo ya pili, yule mpiga makasia akamuuliza, Dogo, umesoma? Dogo akasema, skusoma, prof, Akasema, Basi umepoteza 100% ya maisha yako

Jahazi likafika katikati ya bahari, Mara upepo ukavuma, jahazi likapigwa maji, Dogo akamuuliza prof, Je unajua kuogelea?

Prof huku akitetema, akasema hajui, Dogo akamwambia, Basi umepoteza 100%ya maisha yako,

Hivyo ndugu yangu usipuuze unaowaita wajinga, chukua ushauri ukiuona hauna maana tupa kule
 
Kwa nini unamwamini Magufuli? Hao wote hawana akili ila yeye tu? Subiri mambo yakae sawa. Hakuna aliyeuona mkataba halisi.
hata tukisema alikuwa karukwa na akili,hoja yake ya kupanua bandari zilizopo badala ya hiyo vipi!!!

ukiwa mtu timamu sifa ya kwanza usikubali kila jibu,lakini pia usikatae kila jibu,bali chambua kwa utulivu.

2013 wakati rais wa china amekuja bongo,walisign na jk mikataba 14,ambayo sio wewe wala mimi tunaujua hata mmoja.lakini wote tunajua bandari wanaoitaka ni wachina,je si miongoni mwa ile mikataba 14 iliyosainiwa???hakuna nayejua.

basi haya tufanye magufuli alidanganya kama mnavyosema,nini hatma ya bandari ya tanga,mtwara na dsm baada ya hiyo kubwa kabisa kufunguliwa??

bahati tuliyokuwa nayo sisi watz kwa mchina ilikuwa moja,tayari tulikuwa tumemwona mchina anafanyaje kwa nchi alizofanya nazo biashara zikateleza.sasa sijui nini kinakuja,Mungu ibariki tz.
 
Mwekezaji makini hawezi kuja kuwekeza kwenye nchi isiyo na stability kiuchumi. Hii nchi ni "one man show" Hujui baada ya SSH atakayekuja atakua na msimamo gani maana nchi kama nchi haina iliposimamia, inategemea mkuu wa wakati huo anataka nini. Kwa long term investments hali hiyo ni mashaka, hata ukiwa na mikataba ya namna gani.
Ni makosa makubwa sana kutunga katiba mpya sasa na leoleo itakayowezalinda mali za watu na mambo yetu
 
Back
Top Bottom