Kama AMRI 10 na sio Sheria za Musa tu ziliishia Msalabani; nini Maana ya DHAMBI kwa dunia?

Kaka MSEZA MKULU tukianza kufanya rejea za Biblia dhambi ni kitu chochote ambacho kinaenda kinyume na kanuni na taratibu za Uumbaji wa Mungu. (Any act of transgression against the divine law of God).
Ukikumbuka vizuri kabisa Dhambi ilikuwepo duniani hata kabla ya Torati ya Musa pale Mlimani Sinai, hivyo sidhani kutokuwepo kwa Amri Kumi za Mungu Torati kunaweza kufanya Dhambi isiwepo duniani.

MTAZAMO WA KIHISTORIA.

Tukiangalia tokea Uumbaji wa Mungu miaka mingi hata kablya MUSA dhambi ya Kwanza kutendwa ilikuwa ni KIBURI na UASI dhidi ya Mungu ambao alifanya Kerubi Lucifer pamoja na genge lake la Malaika Waovu.
Dhambi ya Pili ilikuwa ni Kiburi tena ambayo waliifanya ADAMU na HAWA katika Bustani ya Edeni baada ya Kula Tunda kwenye mti waliokatazwa na Mungu. Hapa ni lazima Ikumbukwe Mungu ametoa AMRI nyingi kwenye BIBLIA hata kabla ya Maandishi kugundulika. (Alikuwa akisema kwa kinywa Chake)


Dhambi ya tatu ni ile ya Uuji. KAINI alimuonea wivu MDOGO wake baada ya kutoa SADAKA BORA mbele za MUNGU. Hivyo hapa utakuja Kujua kwamba hata kabla ya AMRI KUMI kuwepo MUNGU aliikataa DHAMBI ya UUAJI. Alimwambia KAINI kabisa kwamba "DHAMBI INAKUNYEMELEA MLANGONI INABIDI UISHINDE". Kipindi hiki kulikuwa hakuna maandishi wala SANDUKU LA AGANO.

Unakumbuka Gharika ya NUHU na SODOMA na GOMORA ?

Majanga yote yaliwakumba wanadamu Vizazi Vingi hata kabla ya MUSA na AMRI KUMI.
Hivyo hapa tunakuja kujua kwamba hata kama Amri Kumi hazitakuwepo kufanya kitendo chochote kinachoendana na mapenzi ya Mungu ni Dhambi. Zamani kabla ya Maandishi watu walitumia Oral Tradition.

MTAZAMO WA KITHIOLOJIA

Yesu hakuja kuivunja Torati bali Kuitimiza. Hata yeye Mwenyewe alikiri na kusema "Sijaja Kuivunja Torati bali nimekuja Kuitimiza" tena akazielezea zaidi AMRI KUMI katika Mafunuo Mapya. Mfano Mzuri:

1. Usizini- Yesu akaseme "Mtu anayemwangalia mwanamke kwa kumtamani azini moyoni mwake"
2. Usiabudu Sanamu- Mtume Paulo anasema Kupenda kitu kuliko Mungu ni Ibada ya Sanamu.
3. Heshimu Wazazi- Mtume Paulo anasema Mzee Usimkaripie bali Muonye kwa hekima endapo atakosea.


HITIMISHO:

Hata kama AMRI KUMI hazitakuwepo DHAMBI bado itakuwepo kwasababu ilikuwepo kabla ya kuandikwa kwa hizo AMRI KUMI. (Rejea mifano yangu hapo juu). Japo Biblia inasema bado zipo na zinafanya kazi mpaka leo na kesho.
Mkristo yoyote anayeamini anaweza kubaliana na mimi kwamba BIBLIA ndiyo AMRI KUU inayotumiaka kumuonyesha Mwanadamu ni mambo gani ukifanya MUNGU anaweza kughafirika.
Pia ndani ya BIBLIA kuna AMRI KUU mpya ambayo haikuwepo kwenye AMRI KUMI. Inasema Mpende BWANA MUNGU WAKO KWA MOYO WAKO WOTE NA MPENDE JIRANI YAKO KAMA NAFSI YAKO. Akamalizia na kusema hakuna AMRI KUU KULIKO HIZI. ( Marko 12:30-31)


NB: Ngoja Mkuu nitarudi na kuleta vifungu vya Biblia kuhusiana na yote yaliyosemwa hapo.
amri ya upendo sio amri mpya bali sheria ya mungu imeBASE humo
 
moses.png

Katika bibilia Mungu amendika kwa Vidole vyake mwenyewe Mara nne.

1:Alipoandika Amri Kumi kwa mara ya kwanza.
2:Musa alipozivunja zile mbao, Mungu Alizirudia tena na kwa mara ya pili.
3:Alipoandika ukutani "Mene mene tekel na pelesi" mbele ya mfalme Belshaza
4:Kwa wanaoamini yesu ni Mungu: Alipoandika chini pale mafarisayo walipotaka kumponda mawe mwanamke mzinzi.

Ukitoa sehemu hizo nne, maandishi yote yaliyobaki yaliandikwa kwa wawakilishi aliowaongoza.

Tanzania hii ili tujue, Umekosea lazima iangaliwe ni sheria au amri gani uliyoivunja vinginevyo hakuna maana ya Mahakama. Tunaambiwa hata kwa Mungu siku ya Mwisho Kutakuwa na Hukumu.

ark-DSCF0019-2-3.jpg

Mfano wa sanduku, lililotumika kuhifadhi maandishi hayo/Amri za Mungu.
1:Ziliwekwa ndani ya sanduku la agano waliloagizwa na Mungu kuliunda:Kutoka 40:20
2:Ziliandikwa na MUNGU mwenyewe kwa KIDOLE: Kutoka 31:18
3:Zinaitwa sheria za kifalme:Yakobo2:8
4:Tusingeijua dhambi bila hizi:Warumi 7:7,3:20
5:Sio nzito wala mzigo kama wengi wanavyoambiana 1Yohana 5:3
6:Zitawahukumu wanadamu wote:Yakobo 2:10-12
7:Ni safi na hazina pungufu lolote: Zaburi 19:7
torah.jpg

Mfano wa sheria nyingine ambazo hazikuingizwa ndani ya Sanduku.
1:Zilitengwa kabisa na amri kumi, na kuwekwa nje ya sanduku:Torati 31:26
2:Ziliandikwa na Musa katika Vitabu:2mambo ya nyakati 35:12
KAMA HAITOSHI MBAO HIZI MBILI HAIZKUWAHI KUUNGANISHWA NA MASHERIA MENGINE MENGI WALIOPEWA WAISRAEL. SANDUKU ZILIMWOTUNZWA HIZO SHERIA NYINGINE ZA MAAGIZO ZILIWEKWA KANDO (SHERIA ZA MUSA -Torat Moshe)
Kama hizi zikikubalika kuwa hazifai, na wengine wanakwenda mbali wanasema Yesu alizifuta, Kwao nini maana ya KOSA au DHambi?



REFERENCE: AMRI KUMI ZA MUNGU KWA MUJIBU WA BIBILIA.
1. Usiwe na miungu mingine ila mimi.KUTOKA 20:3
2. Usijifanyie sanamu ya kuchonga,wala mfano wa kitu chochote kilicho juu mbinguni,wala kilicho chini duniani,wala kilich majini chini ya dunia.usivisujudie wala kuvitumikia;kwa kuwa mimi ,BWANA Mungu wako ni Mungu mwenye wivu;nawapatiliza wana maovu ya baba zao,hata kizazi cha tatu na cha nne chawanichukiao,name nawarehemu maelfu elfu wanipendao na kuzishika amri zangu.KUTOKA 20:4-6
3. Usilitaje bure jina la BWANA,Mungu wako maana BWANA hata mhesabia kuwa hana hatia mtu alitajae jina lake bure.KUTOKA 20:7
4. Ikumbuke siku ya Sabato uitakase.Kwa siku sita utafanya kazi zako zote, lakini siku ya saba ni Sabato kwa BWANA Mungu wako. Siku hiyo hutafanya kazi yo yote, wewe wala mwana wako au binti yako, wala mtumishi wako wa kiume au wa kike wala wanyama wako, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.Kwa kuwa kwa siku sita, BWANA aliumba mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo ndani yake, lakini akapumzika siku ya saba. Kwa hiyo BWANA akaibariki siku ya Sabato na kuifanya takatifu.KUTUKA 20:8-11.
5. Waheshimu baba yako na mama yako, ili upate kuishi siku nyingi katika nchi anayokupa BWANA Mungu wako.KUTOKA 20:12
6. Usiue. KUTOKA 20:13

7. Usizini. KUTOKA 20:14

8. Usiibe. KUTOKA 20:15

9. Usitoe ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yako. KUTOKA 20:16
10. Usiitamani nyumba ya jirani yako. Usimtamani mke wa jirani yako, wala mtumishi wake wa kiume au wa kike, wala ng’ombe wake au punda wake wala cho chote kile alicho nacho jirani yako.
Facts:

Yesu hakufuta sheria alitoa tafsiri sahihi tu.

Pia Yesu ndiye mbadala wa sanduku LA agano.
 
dhambi hii dhambi hii itaisha lini mungu wangu siku hizi adi wanakolomije wana foji vyeti#dhambi -ina maana kwenda kinyume na makubaliano au agano la eneo fulani au jamii fulani mf:unatakiwa uwe na vyeti halali ukifoji vyeti fake ni dhambi coz jamii yetu hairusu ishu hyo NOTE:siyo kila dhambi ni dhambi
 
Yesu ndio Sanduku la agano. Weka nyama hapa mkuu umeandika kitu mtambuka
Wakati wa agano la Kale, Sanduku la agano lilikua linakaa mahali patakatifu pa patakatifu.
Mahali hapa alifika Kuhani mtakatifu tu. Na alikua anafungwa mnyororo ili akikawia kutokana, watajua kua Mungu atakua amempiga na radi ( yaani ) amekufa, wanachofanya wanamvuta kumtoa kwa mnyororo waliomfunga nao mguuni. Manake hakuna atakayethubutu kuingia.

Mahali hapa liliwekwa sanduku la agano. Walilokua wakitembea nalo kila waendapo, kama ishara.

Wakati wa agano jipya:-
Yesu ndiye anayefananishwa na kuhani mkuu anayesimama pale mahali patakatifu pa patakatifu Kumtolea Bwana dhabihu.

Wakati Kristo alipokufa msalabani na lile pazia la hekalu lilipasuka katikati na kufanya watu wote kuona mle ndani jinsi kulivyo.

Ilikua ishara kua kila MTU anaruhusiwa kuingia.

Now, Ufalme wa Mungu Ni kwa kila individuals.

Agano la mwanzo lilifanywa na Moses kuwatoa wana waisrael kule utumwani Misri.

Now Agano la pili ni la damu ya msalaba. Alilolifanya Yesu Kristo.
Ni kupitia agano hili unaishi nalo (i.e. Sio tena kwenda nalo) kila mahali.

Nitaandaa maandiko kuweka sawa.
 
Wakati wa agano la Kale, Sanduku la agano lilikua linakaa mahali patakatifu pa patakatifu.
Mahali hapa alifika Kuhani mtakatifu tu. Na alikua anafungwa mnyororo ili akikawia kutokana, watajua kua Mungu atakua amempiga na radi ( yaani ) amekufa, wanachofanya wanamvuta kumtoa kwa mnyororo waliomfunga nao mguuni. Manake hakuna atakayethubutu kuingia.

Mahali hapa liliwekwa sanduku la agano. Walilokua wakitembea nalo kila waendapo, kama ishara.

Wakati wa agano jipya:-
Yesu ndiye anayefananishwa na kuhani mkuu anayesimama pale mahali patakatifu pa patakatifu Kumtolea Bwana dhabihu.

Wakati Kristo alipokufa msalabani na lile pazia la hekalu lilipasuka katikati na kufanya watu wote kuona mle ndani jinsi kulivyo.

Ilikua ishara kua kila MTU anaruhusiwa kuingia.

Now, Ufalme wa Mungu Ni kwa kila individuals.

Agano la mwanzo lilifanywa na Moses kuwatoa wana waisrael kule utumwani Misri.

Now Agano la pili ni la damu ya msalaba. Alilolifanya Yesu Kristo.
Ni kupitia agano hili unaishi nalo (i.e. Sio tena kwenda nalo) kila mahali.

Nitaandaa maandiko kuweka sawa.
Nimeelewa kiasi mkuu, vipi kuhusu hawa makuhani waliopo duniani ambao watu tunakwenda kuwatubia au wakituwakilisha kwa Mungu linganisha na maelezo yako hapo juu
 
Nimepewa kiasi mkuu, vipi kuhusu hawa makuhani waliopo duniani ambao watu tunakwenda kuwatubia au wakituwakilisha kwa Mungu linganisha na maelezo yako hapo juu
Iko hivi..
Yesu alikua ana karama zote za Unabii, utume, ualimu, uchungaji, uinjilisti, utume.
Akazigawa kwa wanafunzi wake kwa kadri ya Roho wake alivyowajaalia. Kupitia hawa Injili(Habari Njema ya Ufalme wa Mungu) inahubiriwa ulimwenguni kote.

1 Corinthians 12:27-28
[27]. Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake. [28]. Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha.....


Ephesians 4:5-6,8,10-12
[5], Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. [6] Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote.


[8]. Hivyo husema, Alipopaa juu aliteka mateka, Akawapa wanadamu vipawa.
[10] Naye aliyeshuka ndiye yeye aliyepaa juu sana kupita mbingu zote, ili avijaze vitu vyote. [11]Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu; [12] kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe;

Kuhusu Ukuhani wa Yesu.

Hebrews 4:15
[15] Kwa kuwa hamna KUHANI MKUU asiyeweza kuchukuana nasi katika mambo yetu ya udhaifu; bali yeye alijaribiwa sawasawa na sisi katika mambo yote, bila kufanya dhambi.


Hebrews 8:1-2,11
[1]Basi, katika hayo tunayosema, neno lililo kuu ndilo hili: Tunaye kuhani mkuu wa namna hii, aliyeketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Ukuu mbinguni, [2]. mhudumu wa patakatifu, na wa ile hema ya kweli, ambayo Bwana aliiweka wala si mwanadamu........


.....[11]Nao hawatafundishana kila mtu na jirani yake, Na kila mtu na ndugu yake, akisema, Mjue Bwana; Kwa MAANA WOTE WATANIJUA, Tangu mdogo wao hata mkubwa wao.


...Just a nutshell..
 
Warumi 10:1-4
[1]Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe.
[2]Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa.
[3]Kwa maana, wakiwa hawaijui haki ya Mungu, na wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu.
[4]Kwa maana Kristo ni mwisho wa sheria, ili kila aaminiye ahesabiwe haki.
 
Hatujajua dhumuni lako kwa kuandia hayo. Embu tuambie dini yoko ili tuwezekuku jubu vizur, tuanzie hapo
Unataka kuleta udini! Sikosei wewe muislamu? Unatakiwa kuongelea hoja iliyopo hapa siyo dini ya mtu. Na siku zote kaa katika hoja siyo nje ya hoja kama unajadili jambo au utajichanganya. Tatizo mmefundishwa kukariri na ubishi, siyo ku reason with facts and evidence. Pole sana naona Madras imekuharibu.
 
Warumi 10:1-4
[1]Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe.
[2]Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa.
[3]Kwa maana, wakiwa hawaijui haki ya Mungu, na wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu.
[4]Kwa maana Kristo ni mwisho wa sheria, ili kila aaminiye ahesabiwe haki.
Kwa maana Kristo ni mwisho wa sheria, ili kila aaminiye ahesabiwe haki.
mkuu shusha nondo hapo, maana inaonekana kuna kitu cha kujifunza.
ninavyoelewa ukiwa wa kristo huvunji sheria,
Yaani ukiwa mtoto wa jaji au mwanasheria hatutegemei uwe champion wa kuvunja sheria bali tunategemea utakuwa huru maisha yako yote maana unajua zaidi ya wengine maana unaishi na mwenye sheria.
Ukimwamini Utamtii.

Hebu weka sawa hapa mkuu...
 
imani ipi hiyo mkuu au ni yako binafsi uliyojiwekea kama independent and free being
atakuwa ni msabato ndo wanaokomaa na amri hizi kumi na zaidi wanaikazia sabato na huku wanazini.
hakuna aliye salama maana dunia yote imkosa na mtu asije akajisifu kuwa ni kwa kufuata hizo sheria ila huruma ya mnyaazi Mungu Jehovah
 
Kuna kitu unataka watu wafikie wakione lakin umekiacha katika Fikra zako

Nashindwa kuchangia sababu sijajua yan nachangia nini au sijaelewa umemaanisha nini kwa huu uelewa wangu mdogo
 
kilichotokea pale msalabani ni sadaka au malipizi ya dhambi zote. ukifanya dhambi badala ya wewe kutoa sadaka ya dhambi unatumia damu ya yesu kuiondoa dhambi yako, ndivyo ninavyoelewa mimi, japo nami ninamengi ya kuuliza.

Sadaka ya damu ya mtu si ya kichawi na kishetani hiyo?
 
Kaka MSEZA MKULU tukianza kufanya rejea za Biblia dhambi ni kitu chochote ambacho kinaenda kinyume na kanuni na taratibu za Uumbaji wa Mungu. (Any act of transgression against the divine law of God).
Ukikumbuka vizuri kabisa Dhambi ilikuwepo duniani hata kabla ya Torati ya Musa pale Mlimani Sinai, hivyo sidhani kutokuwepo kwa Amri Kumi za Mungu Torati kunaweza kufanya Dhambi isiwepo duniani.

MTAZAMO WA KIHISTORIA.

Tukiangalia tokea Uumbaji wa Mungu miaka mingi hata kablya MUSA dhambi ya Kwanza kutendwa ilikuwa ni KIBURI na UASI dhidi ya Mungu ambao alifanya Kerubi Lucifer pamoja na genge lake la Malaika Waovu.
Dhambi ya Pili ilikuwa ni Kiburi tena ambayo waliifanya ADAMU na HAWA katika Bustani ya Edeni baada ya Kula Tunda kwenye mti waliokatazwa na Mungu. Hapa ni lazima Ikumbukwe Mungu ametoa AMRI nyingi kwenye BIBLIA hata kabla ya Maandishi kugundulika. (Alikuwa akisema kwa kinywa Chake)


Dhambi ya tatu ni ile ya Uuji. KAINI alimuonea wivu MDOGO wake baada ya kutoa SADAKA BORA mbele za MUNGU. Hivyo hapa utakuja Kujua kwamba hata kabla ya AMRI KUMI kuwepo MUNGU aliikataa DHAMBI ya UUAJI. Alimwambia KAINI kabisa kwamba "DHAMBI INAKUNYEMELEA MLANGONI INABIDI UISHINDE". Kipindi hiki kulikuwa hakuna maandishi wala SANDUKU LA AGANO.

Unakumbuka Gharika ya NUHU na SODOMA na GOMORA ?

Majanga yote yaliwakumba wanadamu Vizazi Vingi hata kabla ya MUSA na AMRI KUMI.
Hivyo hapa tunakuja kujua kwamba hata kama Amri Kumi hazitakuwepo kufanya kitendo chochote kinachoendana na mapenzi ya Mungu ni Dhambi. Zamani kabla ya Maandishi watu walitumia Oral Tradition.

MTAZAMO WA KITHIOLOJIA

Yesu hakuja kuivunja Torati bali Kuitimiza. Hata yeye Mwenyewe alikiri na kusema "Sijaja Kuivunja Torati bali nimekuja Kuitimiza" tena akazielezea zaidi AMRI KUMI katika Mafunuo Mapya. Mfano Mzuri:

1. Usizini- Yesu akaseme "Mtu anayemwangalia mwanamke kwa kumtamani azini moyoni mwake"
2. Usiabudu Sanamu- Mtume Paulo anasema Kupenda kitu kuliko Mungu ni Ibada ya Sanamu.
3. Heshimu Wazazi- Mtume Paulo anasema Mzee Usimkaripie bali Muonye kwa hekima endapo atakosea.


HITIMISHO:

Hata kama AMRI KUMI hazitakuwepo DHAMBI bado itakuwepo kwasababu ilikuwepo kabla ya kuandikwa kwa hizo AMRI KUMI. (Rejea mifano yangu hapo juu). Japo Biblia inasema bado zipo na zinafanya kazi mpaka leo na kesho.
Mkristo yoyote anayeamini anaweza kubaliana na mimi kwamba BIBLIA ndiyo AMRI KUU inayotumiaka kumuonyesha Mwanadamu ni mambo gani ukifanya MUNGU anaweza kughafirika.
Pia ndani ya BIBLIA kuna AMRI KUU mpya ambayo haikuwepo kwenye AMRI KUMI. Inasema Mpende BWANA MUNGU WAKO KWA MOYO WAKO WOTE NA MPENDE JIRANI YAKO KAMA NAFSI YAKO. Akamalizia na kusema hakuna AMRI KUU KULIKO HIZI. ( Marko 12:30-31)


NB: Ngoja Mkuu nitarudi na kuleta vifungu vya Biblia kuhusiana na yote yaliyosemwa hapo.
Safiiii kabisa safi saana.barikiwa mkuu.

ROHO MTAKATIFU tunakushukuru maana ww ni mwema sana.Endelea kutufundisha maana tunahitaji tujue zaid.Si kwa akili,damu wala nyama tumeyatambua haya ila ni neema yako inayo tufanya tujue haya na uweza utokao juu.

~Tunajifunza kwako BWANA YESU.

~KWELI ANAKUJA YESU.
 
Back
Top Bottom