Kama AMRI 10 na sio Sheria za Musa tu ziliishia Msalabani; nini Maana ya DHAMBI kwa dunia?

MSEZA MKULU

JF-Expert Member
Jul 22, 2011
3,752
5,497
moses.png

Katika bibilia Mungu amendika kwa Vidole vyake mwenyewe Mara nne.

1: Alipoandika Amri Kumi kwa mara ya kwanza.
2: Musa alipozivunja zile mbao, Mungu Alizirudia tena na kwa mara ya pili.
3: Alipoandika ukutani "Mene mene tekel na pelesi" mbele ya mfalme Belshaza
4: Kwa wanaoamini yesu ni Mungu: Alipoandika chini pale mafarisayo walipotaka kumponda mawe mwanamke mzinzi.

Ukitoa sehemu hizo nne, maandishi yote yaliyobaki yaliandikwa kwa wawakilishi aliowaongoza.

Tanzania hii ili tujue, Umekosea lazima iangaliwe ni sheria au amri gani uliyoivunja vinginevyo hakuna maana ya Mahakama. Tunaambiwa hata kwa Mungu siku ya Mwisho Kutakuwa na Hukumu.

ark-DSCF0019-2-3.jpg
Mfano wa sanduku, lililotumika kuhifadhi maandishi hayo/Amri za Mungu.
1: Ziliwekwa ndani ya sanduku la agano waliloagizwa na Mungu kuliunda:Kutoka 40:20
2: Ziliandikwa na MUNGU mwenyewe kwa KIDOLE: Kutoka 31:18
3: Zinaitwa sheria za kifalme:Yakobo2:8
4: Tusingeijua dhambi bila hizi:Warumi 7:7,3:20
5: Sio nzito wala mzigo kama wengi wanavyoambiana 1Yohana 5:3
6: Zitawahukumu wanadamu wote:Yakobo 2:10-12
7: Ni safi na hazina pungufu lolote: Zaburi 19:7

torah.jpg

Mfano wa sheria nyingine ambazo hazikuingizwa ndani ya Sanduku.
1:Zilitengwa kabisa na amri kumi, na kuwekwa nje ya sanduku:Torati 31:26
2:Ziliandikwa na Musa katika Vitabu:2mambo ya nyakati 35:12

KAMA HAITOSHI MBAO HIZI MBILI HAIZKUWAHI KUUNGANISHWA NA MASHERIA MENGINE MENGI WALIOPEWA WAISRAEL. SANDUKU ZILIMWOTUNZWA HIZO SHERIA NYINGINE ZA MAAGIZO ZILIWEKWA KANDO (SHERIA ZA MUSA -Torat Moshe)

Kama hizi zikikubalika kuwa hazifai, na wengine wanakwenda mbali wanasema Yesu alizifuta, Kwao nini maana ya KOSA au DHambi?


REFERENCE: AMRI KUMI ZA MUNGU KWA MUJIBU WA BIBILIA

1. Usiwe na miungu mingine ila mimi.KUTOKA 20:3
2. Usijifanyie sanamu ya kuchonga,wala mfano wa kitu chochote kilicho juu mbinguni,wala kilicho chini duniani,wala kilich majini chini ya dunia.usivisujudie wala kuvitumikia;kwa kuwa mimi ,BWANA Mungu wako ni Mungu mwenye wivu;nawapatiliza wana maovu ya baba zao,hata kizazi cha tatu na cha nne chawanichukiao,name nawarehemu maelfu elfu wanipendao na kuzishika amri zangu.KUTOKA 20:4-6
3. Usilitaje bure jina la BWANA,Mungu wako maana BWANA hata mhesabia kuwa hana hatia mtu alitajae jina lake bure.KUTOKA 20:7
4. Ikumbuke siku ya Sabato uitakase.Kwa siku sita utafanya kazi zako zote, lakini siku ya saba ni Sabato kwa BWANA Mungu wako. Siku hiyo hutafanya kazi yo yote, wewe wala mwana wako au binti yako, wala mtumishi wako wa kiume au wa kike wala wanyama wako, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.Kwa kuwa kwa siku sita, BWANA aliumba mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo ndani yake, lakini akapumzika siku ya saba. Kwa hiyo BWANA akaibariki siku ya Sabato na kuifanya takatifu.KUTUKA 20:8-11.
5. Waheshimu baba yako na mama yako, ili upate kuishi siku nyingi katika nchi anayokupa BWANA Mungu wako.KUTOKA 20:12
6. Usiue. KUTOKA 20:13
7. Usizini. KUTOKA 20:14
8. Usiibe. KUTOKA 20:15
9. Usitoe ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yako. KUTOKA 20:16
10. Usiitamani nyumba ya jirani yako. Usimtamani mke wa jirani yako, wala mtumishi wake wa kiume au wa kike, wala ng’ombe wake au punda wake wala cho chote kile alicho nacho jirani yako.
 
Ukweli kabisa sijaelewa ulikua unalenga nini, au tatizo ni mm mwenyewe
usijali mkuu, hapa tunajadili nini maana ya DHAMBI kwa wanaoamini uwepo wa Mungu Lakini wanakataa AMRI zake/Sheria zake 10 alizozitoa kama nchi ilivyo na sheria ambazo zikivunjwa kisutu wanafanya yao.
Yaani watu wao, Definition ya dhambi kwao ni ipi na wanaitoa kwenye reference ipi?
 
usijali mkuu, hapa tunajadili nini maana ya DHAMBI kwa wanaoamini uwepo wa Mungu Lakini wanakataa AMRI zake/Sheria zake 10 alizozitoa kama nchi ilivyo na sheria ambazo zikivunjwa kisutu wanafanya yao.
Yaani watu wao, Definition ya dhambi kwao ni ipi na wanaitoa kwenye reference ipi?
Hapo nimekuelewa mkuu, shukrani ngoja wajuvi wa mambo waje tupate
Maarifa. Be blessed
 
Ndugu hizo sheria zipo. Yesu hakuzifuta, yesu msalabani alikomesha sadaka za kafara walizokuwa wakitoa waisrael badala yake damu yake ndiyo ikawa inatakasa. Ila sheria hakuna zilizositishwa hata zile walizopewa wanaisrael tofauti na zile kumi baadhi zipo na zinatuhusu.
 
Kaka MSEZA MKULU tukianza kufanya rejea za Biblia dhambi ni kitu chochote ambacho kinaenda kinyume na kanuni na taratibu za Uumbaji wa Mungu. (Any act of transgression against the divine law of God).
Ukikumbuka vizuri kabisa Dhambi ilikuwepo duniani hata kabla ya Torati ya Musa pale Mlimani Sinai, hivyo sidhani kutokuwepo kwa Amri Kumi za Mungu Torati kunaweza kufanya Dhambi isiwepo duniani.

MTAZAMO WA KIHISTORIA.

Tukiangalia tokea Uumbaji wa Mungu miaka mingi hata kablya MUSA dhambi ya Kwanza kutendwa ilikuwa ni KIBURI na UASI dhidi ya Mungu ambao alifanya Kerubi Lucifer pamoja na genge lake la Malaika Waovu.
Dhambi ya Pili ilikuwa ni Kiburi tena ambayo waliifanya ADAMU na HAWA katika Bustani ya Edeni baada ya Kula Tunda kwenye mti waliokatazwa na Mungu. Hapa ni lazima Ikumbukwe Mungu ametoa AMRI nyingi kwenye BIBLIA hata kabla ya Maandishi kugundulika. (Alikuwa akisema kwa kinywa Chake)

Dhambi ya tatu ni ile ya Uuji. KAINI alimuonea wivu MDOGO wake baada ya kutoa SADAKA BORA mbele za MUNGU. Hivyo hapa utakuja Kujua kwamba hata kabla ya AMRI KUMI kuwepo MUNGU aliikataa DHAMBI ya UUAJI. Alimwambia KAINI kabisa kwamba "DHAMBI INAKUNYEMELEA MLANGONI INABIDI UISHINDE". Kipindi hiki kulikuwa hakuna maandishi wala SANDUKU LA AGANO.

Unakumbuka Gharika ya NUHU na SODOMA na GOMORA ?
Majanga yote yaliwakumba wanadamu Vizazi Vingi hata kabla ya MUSA na AMRI KUMI.
Hivyo hapa tunakuja kujua kwamba hata kama Amri Kumi hazitakuwepo kufanya kitendo chochote kinachoendana na mapenzi ya Mungu ni Dhambi. Zamani kabla ya Maandishi watu walitumia Oral Tradition.

MTAZAMO WA KITHIOLOJIA

Yesu hakuja kuivunja Torati bali Kuitimiza. Hata yeye Mwenyewe alikiri na kusema "Sijaja Kuivunja Torati bali nimekuja Kuitimiza" tena akazielezea zaidi AMRI KUMI katika Mafunuo Mapya. Mfano Mzuri:

1. Usizini- Yesu akaseme "Mtu anayemwangalia mwanamke kwa kumtamani azini moyoni mwake"
2. Usiabudu Sanamu- Mtume Paulo anasema Kupenda kitu kuliko Mungu ni Ibada ya Sanamu.
3. Heshimu Wazazi- Mtume Paulo anasema Mzee Usimkaripie bali Muonye kwa hekima endapo atakosea.

HITIMISHO:

Hata kama AMRI KUMI hazitakuwepo DHAMBI bado itakuwepo kwasababu ilikuwepo kabla ya kuandikwa kwa hizo AMRI KUMI. (Rejea mifano yangu hapo juu). Japo Biblia inasema bado zipo na zinafanya kazi mpaka leo na kesho.
Mkristo yoyote anayeamini anaweza kubaliana na mimi kwamba BIBLIA ndiyo AMRI KUU inayotumiaka kumuonyesha Mwanadamu ni mambo gani ukifanya MUNGU anaweza kughafirika.
Pia ndani ya BIBLIA kuna AMRI KUU mpya ambayo haikuwepo kwenye AMRI KUMI. Inasema Mpende BWANA MUNGU WAKO KWA MOYO WAKO WOTE NA MPENDE JIRANI YAKO KAMA NAFSI YAKO. Akamalizia na kusema hakuna AMRI KUU KULIKO HIZI. ( Marko 12:30-31)

NB: Ngoja Mkuu nitarudi na kuleta vifungu vya Biblia kuhusiana na yote yaliyosemwa hapo.
 
Kaka MSEZA MKULU tukianza kufanya rejea za Biblia dhambi ni kitu chochote ambacho kinaenda kinyume na kanuni na taratibu za Uumbaji wa Mungu. (Any act of transgression against the divine law of God).
Ukikumbuka vizuri kabisa Dhambi ilikuwepo duniani hata kabla ya Torati ya Musa pale Mlimani Sinai, hivyo sidhani kutokuwepo kwa Amri Kumi za Mungu Torati kunaweza kufanya Dhambi isiwepo duniani.

MTAZAMO WA KIHISTORIA.

Tukiangalia tokea Uumbaji wa Mungu miaka mingi hata kablya MUSA dhambi ya Kwanza kutendwa ilikuwa ni KIBURI na UASI dhidi ya Mungu ambao alifanya Kerubi Lucifer pamoja na genge lake la Malaika Waovu.
Dhambi ya Pili ilikuwa ni Kiburi tena ambayo waliifanya ADAMU na HAWA katika Bustani ya Edeni baada ya Kula Tunda kwenye mti waliokatazwa na Mungu. Hapa ni lazima Ikumbukwe Mungu ametoa AMRI nyingi kwenye BIBLIA hata kabla ya Maandishi kugundulika. (Alikuwa akisema kwa kinywa Chake)

Dhambi ya tatu ni ile ya Uuji. KAINI alimuonea wivu MDOGO wake baada ya kutoa SADAKA BORA mbele za MUNGU. Hivyo hapa utakuja Kujua kwamba hata kabla ya AMRI KUMI kuwepo MUNGU aliikataa DHAMBI ya UUAJI. Alimwambia KAINI kabisa kwamba "DHAMBI INAKUNYEMELEA MLANGONI INABIDI UISHINDE". Kipindi hiki kulikuwa hakuna maandishi wala SANDUKU LA AGANO.

Unakumbuka Gharika ya NUHU na SODOMA na GOMORA ?
Majanga yote yaliwakumba wanadamu Vizazi Vingi hata kabla ya MUSA na AMRI KUMI.
Hivyo hapa tunakuja kujua kwamba hata kama Amri Kumi hazitakuwepo kufanya kitendo chochote kinachoendana na mapenzi ya Mungu ni Dhambi. Zamani kabla ya Maandishi watu walitumia Oral Tradition.

MTAZAMO WA KITHIOLOJIA

Yesu hakuja kuivunja Torati bali Kuitimiza. Hata yeye Mwenyewe alikiri na kusema "Sijaja Kuivunja Torati bali nimekuja Kuitimiza" tena akazielezea zaidi AMRI KUMI katika Mafunuo Mapya. Mfano Mzuri:

1. Usizini- Yesu akaseme "Mtu anayemwangalia mwanamke kwa kumtamani azini moyoni mwake"
2. Usiabudu Sanamu- Mtume Paulo anasema Kupenda kitu kuliko Mungu ni Ibada ya Sanamu.
3. Heshimu Wazazi- Mtume Paulo anasema Mzee Usimkaripie bali Muonye kwa hekima endapo atakosea.

HITIMISHO:

Hata kama AMRI KUMI hazitakuwepo DHAMBI bado itakuwepo kwasababu ilikuwepo kabla ya kuandikwa kwa hizo AMRI KUMI. (Rejea mifano yangu hapo juu). Japo Biblia inasema bado zipo na zinafanya kazi mpaka leo na kesho.
Mkristo yoyote anayeamini anaweza kubaliana na mimi kwamba BIBLIA ndiyo AMRI KUU inayotumiaka kumuonyesha Mwanadamu ni mambo gani ukifanya MUNGU anaweza kughafirika.
Pia ndani ya BIBLIA kuna AMRI KUU mpya ambayo haikuwepo kwenye AMRI KUMI. Inasema Mpende BWANA MUNGU WAKO KWA MOYO WAKO WOTE NA MPENDE JIRANI YAKO KAMA NAFSI YAKO. Akamalizia na kusema hakuna AMRI KUU KULIKO HIZI. ( Marko 12:30-31)

NB: Ngoja Mkuu nitarudi na kuleta vifungu vya Biblia kuhusiana na yote yaliyosemwa hapo.

Kwa ufahamu wangu dhambi ilitokea kipindi cha uasi katika bustani ya edeni. Adamu na Hawa walipo muasi Mungu ndipo dhambi ikawa ndani yetu.

Dhambi ni kwenda kinyume na sheria na maagizo ya Mungu wako. Pia Sheria na maagizo ya Mungu hayakuja kwa mara ya kwanza kwa Musa ili awape wana israel waliokuwa utumwani Misri, bali ni UKUMBUSHO wa sheria hizo maana walipotelea dhambini na mioyo yao ilikuwa mbali wa upeo wa Mungu wa kweli.

Ninaposema ni UKUMBUSHO, ina maana sheria ilikuwaga tangia mwanzo baada ya uasi kufanyika. Nikurudishe nyuma kipindi cha KAINI na ABELI; Baada ya Kaini kumuua Nduguye, Mungu alimuuliza "yu wapi nduguyo?" alichojibu alisema hajui... ikimaanisha kuwa alitambua kosa alilolifanya, hivyo akadanganya.

Ukiangalia kipindi hicho alijuaje kuua ni kosa (Dhambi)?.

Hvyo kuanzia mwanzo mpaka Yesu kuja na kufa kwa ajili kwa dhambi zetu, bado maana ya dhambi ni ileile...
Yesu alikuja kutimiza torati ya Musa, yani kupata msamaha wa dhambi kipindi cha Musa lazima mnyama achinjwe na kuhani apokee makosa yako na kuyaombea yasamehewe... sasa wakati wa Yesu yeye ndo kama mnyama achinjwae kipindi cha Musa, na kipindi anakufa pazia la kuhani mkuu lilipasuka vipande ikiashiria kwa jina lake na damu yake umesamehewa.

Hivyo dhambi ni kukiuka maagizo ya Muumba wako... period....
 
Kwa ufahamu wangu dhambi ilitokea kipindi cha uasi katika bustani ya edeni. Adamu na Hawa walipo muasi Mungu ndipo dhambi ikawa ndani yetu.

Dhambi ni kwenda kinyume na sheria na maagizo ya Mungu wako. Pia Sheria na maagizo ya Mungu hayakuja kwa mara ya kwanza kwa Musa ili awape wana israel waliokuwa utumwani Misri, bali ni UKUMBUSHO wa sheria hizo maana walipotelea dhambini na mioyo yao ilikuwa mbali wa upeo wa Mungu wa kweli.

Ninaposema ni UKUMBUSHO, ina maana sheria ilikuwaga tangia mwanzo baada ya uasi kufanyika. Nikurudishe nyuma kipindi cha KAINI na ABELI; Baada ya Kaini kumuua Nduguye, Mungu alimuuliza "yu wapi nduguyo?" alichojibu alisema hajui... ikimaanisha kuwa alitambua kosa alilolifanya, hivyo akadanganya.

Ukiangalia kipindi hicho alijuaje kuua ni kosa (Dhambi)?.

Hvyo kuanzia mwanzo mpaka Yesu kuja na kufa kwa ajili kwa dhambi zetu, bado maana ya dhambi ni ileile...
Yesu alikuja kutimiza torati ya Musa, yani kupata msamaha wa dhambi kipindi cha Musa lazima mnyama achinjwe na kuhani apokee makosa yako na kuyaombea yasamehewe... sasa wakati wa Yesu yeye ndo kama mnyama achinjwae kipindi cha Musa, na kipindi anakufa pazia la kuhani mkuu lilipasuka vipande ikiashiria kwa jina lake na damu yake umesamehewa.

Hivyo dhambi ni kukiuka maagizo ya Muumba wako... period....

Mkuu kwani mimi nimesemaje au nimepinga sehemu?
Bandiko langu umelisoma Vizuri lakini?
 
Kaka MSEZA MKULU tukianza kufanya rejea za Biblia dhambi ni kitu chochote ambacho kinaenda kinyume na kanuni na taratibu za Uumbaji wa Mungu. (Any act of transgression against the divine law of God).
Ukikumbuka vizuri kabisa Dhambi ilikuwepo duniani hata kabla ya Torati ya Musa pale Mlimani Sinai, hivyo sidhani kutokuwepo kwa Amri Kumi za Mungu Torati kunaweza kufanya Dhambi isiwepo duniani.

MTAZAMO WA KIHISTORIA.

Tukiangalia tokea Uumbaji wa Mungu miaka mingi hata kablya MUSA dhambi ya Kwanza kutendwa ilikuwa ni KIBURI na UASI dhidi ya Mungu ambao alifanya Kerubi Lucifer pamoja na genge lake la Malaika Waovu.
Dhambi ya Pili ilikuwa ni Kiburi tena ambayo waliifanya ADAMU na HAWA katika Bustani ya Edeni baada ya Kula Tunda kwenye mti waliokatazwa na Mungu. Hapa ni lazima Ikumbukwe Mungu ametoa AMRI nyingi kwenye BIBLIA hata kabla ya Maandishi kugundulika. (Alikuwa akisema kwa kinywa Chake)

Dhambi ya tatu ni ile ya Uuji. KAINI alimuonea wivu MDOGO wake baada ya kutoa SADAKA BORA mbele za MUNGU. Hivyo hapa utakuja Kujua kwamba hata kabla ya AMRI KUMI kuwepo MUNGU aliikataa DHAMBI ya UUAJI. Alimwambia KAINI kabisa kwamba "DHAMBI INAKUNYEMELEA MLANGONI INABIDI UISHINDE". Kipindi hiki kulikuwa hakuna maandishi wala SANDUKU LA AGANO.

Unakumbuka Gharika ya NUHU na SODOMA na GOMORA ?
Majanga yote yaliwakumba wanadamu Vizazi Vingi hata kabla ya MUSA na AMRI KUMI.
Hivyo hapa tunakuja kujua kwamba hata kama Amri Kumi hazitakuwepo kufanya kitendo chochote kinachoendana na mapenzi ya Mungu ni Dhambi. Zamani kabla ya Maandishi watu walitumia Oral Tradition.

MTAZAMO WA KITHIOLOJIA

Yesu hakuja kuivunja Torati bali Kuitimiza. Hata yeye Mwenyewe alikiri na kusema "Sijaja Kuivunja Torati bali nimekuja Kuitimiza" tena akazielezea zaidi AMRI KUMI katika Mafunuo Mapya. Mfano Mzuri:

1. Usizini- Yesu akaseme "Mtu anayemwangalia mwanamke kwa kumtamani azini moyoni mwake"
2. Usiabudu Sanamu- Mtume Paulo anasema Kupenda kitu kuliko Mungu ni Ibada ya Sanamu.
3. Heshimu Wazazi- Mtume Paulo anasema Mzee Usimkaripie bali Muonye kwa hekima endapo atakosea.

HITIMISHO:

Hata kama AMRI KUMI hazitakuwepo DHAMBI bado itakuwepo kwasababu ilikuwepo kabla ya kuandikwa kwa hizo AMRI KUMI. (Rejea mifano yangu hapo juu). Japo Biblia inasema bado zipo na zinafanya kazi mpaka leo na kesho.
Mkristo yoyote anayeamini anaweza kubaliana na mimi kwamba BIBLIA ndiyo AMRI KUU inayotumiaka kumuonyesha Mwanadamu ni mambo gani ukifanya MUNGU anaweza kughafirika.
Pia ndani ya BIBLIA kuna AMRI KUU mpya ambayo haikuwepo kwenye AMRI KUMI. Inasema Mpende BWANA MUNGU WAKO KWA MOYO WAKO WOTE NA MPENDE JIRANI YAKO KAMA NAFSI YAKO. Akamalizia na kusema hakuna AMRI KUU KULIKO HIZI. ( Marko 12:30-31)

NB: Ngoja Mkuu nitarudi na kuleta vifungu vya Biblia kuhusiana na yote yaliyosemwa hapo.
nakupata mkulu,
asante kwa kutanua wigo, ingawa inabidi tujadili yawezekana alichokifanya kwenye zile amri 10 ni aggregation ya makosa na dhambi ambazo hapo nyuma zilikuwa zimesambaa. na yesu na mitume hasa paulo akaja akazizoom zaidi katika vina vyake...
Ila kwa sasa.
Dhambi inakuwa defined kwenye biblia
1Yohana 3:4 "Dhambi ni uasi wa Sheria"
Makosa yote AU dhambi Duniani kwa mtazamo waku ziko katika makundi makuu mawili.

1:Kumkosea Mwandamu mwezako
2:Kumkosea Mungu.
Katika makundi haya mawili ndimo Amri kumi zinamezwa pamoja na maagizo yote ya mungu toka Mwanzo hadi Ufunuo.

Pia amri ambazo yesu alizzta mpya kwa adhira aliyokuwa anaongea nayo ni kweli ni mpya lakini katk uhalisia wa sisi leo ambao tunasoma mwanzo hadi ufunuo sio mpya bali ni summary ya Amri kumi za Mungu na makatazo yake.

yaani;
1:Mpende Bwana Mungu wako wote na kwa Moyo wako wote (HII NI AMRI YA KWANZA HADI YA NNE)
i/Usiwe na Miungu Mingine ila mimi
ii/Usijichongee sanamu wala chochote na usikiabudu
iii/Usilitaje sina lake bure
iv/Ikumbuke siku ya sabato, ukikumbuka unaonyesha ishara ya utii kwake na kutambua mwanadamu hakuibuka(evolve) bali tuliumbwa and you will appreciate his wonderful creative power

2:MPENDE jirani yako (HII YOTE IMEKWISHA KUWA DEFINED KATIKA AMRI YA TANO HADI YA KUMI) KWA MUJIBU WA KUTOKA 20.
i: waheshimu baba na mama
ii:usiue
iii/usizini
iv/usiibe
v/Usihuhudie uongo
vi:Usitamani.. REF:Kutoka 20
kUSISITIZA SIO MPYA KWETU ILA YESU ALIZIITA MPYA KWA MAANA YA WASIKILIZAJI WAKE, NA SISI AMBAO TUNAZIANGALIA KWA MTAZAMO HAFIFU NA YEYE ALIKUJA KUZINGARISHA NA KUZIONGEZEA SCOPE ZAIDI. TAYARI yesu (Alikuwepo siku zote) alikuwa anajua hayo maneno yameshaandikwa kwenye agano la kale,

1deuteronomy 6:5"You shall love the LORD your God with all your heart and with all your soul and with all your might."
2:LEVITICUS 19:18You shall not take vengeance or bear a grudge against the sons of your own people, but you shall love your neighbor as yourself: I am the Lord.
 
Hatujajua dhumuni lako kwa kuandia hayo. Embu tuambie dini yoko ili tuwezekuku jubu vizur, tuanzie hapo

Mkulu hapo ni bibilia na uelewa wetu, dini au dhehebu ukitaka nitakuambia ila ningekuambia kule kwenye jukwaa la dini hapa ni intelligence and facts sio ligi. Maana thread hii sio mahubiri au kubadilishana dini. Hapa ni biblical facts vs our current understanding.

Jibu thread tushirikishe mtazamo wako juu ya mada toa changamoto.
 
Back
Top Bottom