Kalenda ya Masoko kwa Baadhi ya Mazao Tanzania

Mar 3, 2018
64
53
Ni ukweli usiopingika kwamba kupata faida katika kilimo kwa kufanya kilimo biashara kuna hitaji mambo mengi sana lakini katika vitu muhimu zaidi ni timing ya soko kwa zao husika.Wakulima wengi katika nchi yetu wamekuwa wakikata tamaa kuendelea na kilimo kutokana na hasara wanayoipata katika kilimo na kitu kikubwa kinacho changia hili ni ukosefu wa taarifa sahihi,sio tu taarifa sahihi za mbegu zipi ni bora kwa kilimo au ni udongo upi ni bora kwa kilimo cha zao fulani bali ni muda gani muafaka huwa na bei nzuri kwa zao fulani.Kilimo biashara kimejikita zaidi katika utaalamu unaotumika katika shughuli nzima za kilimo lakini masoko mazuri ni jambo la kuzingatia kabla hata hujaanza kilimo.
Kutokana na changamoto inayowakumba wakulima kutofahamu ni muda gani nizalishe nini ili nipate soko zuri la zao husika basi tumekuja na KALENDA YA MASOKO KWA BAADHI YA MAZAO TANZANIA yenye mazao tofauti tofauti.
Kalenda hii inaonesha ni mwezi gani zao fulani hua na bei nzuri hivyo basi mkulima anachotakiwa kukifanya ni kuhakikisha kipindi hicho ndicho anachopaswa kuvuna zao husika ili aweze kupata faida nzuri kwenye kilimo.kipindi ambacho zao husika huwa na soko zuri kimeoneshwa kwa rangi tofauti tofauti lakini kikubwa ni kwamba kipndi ambacho hakijaoneshwa kwenye kalenda hii basi ni kipindi ambacho zao hilo huwa na bei ndogo inayopelekea mkulima kupata hasara.Kiuhalisa ni kwamba katika vipindi hivi ambavyo masoko huwa mazuri kwa zao husika huwa kunakuwa na changamoto kubwa kuzalisha zao hilo moja wapo ikiwa ukame lakini ni vyema ukatafuta njia mbadala za kupambana na changamoto hizo upate faida nzuri kuliko kusubiria msimu wake na kuishia kuuza mazao kwa hasara.Kwa maswali na maelezo juu ya kalenda hii unaweza ukacomment swali lako na ukajibiwa hapa.Tuache kulima kwa kufata mkumbo kilimo kinalipa.-Agrila Farming
 

Attachments

  • cropscalendar.jpg
    cropscalendar.jpg
    220.2 KB · Views: 257
Nimependa uzi wako ila naomba ufafanuzi wa rangi nyekundu hapo je inaonyesha sio kipindi kizuri au kipindi kizuri, pia ingekua vyema kama ungefafanua rangi zote kwa ajili ya faida ya wengine ndugu
 
Ni ukweli usiopingika kwamba kupata faida katika kilimo kwa kufanya kilimo biashara kuna hitaji mambo mengi sana lakini katika vitu muhimu zaidi ni timing ya soko kwa zao husika.Wakulima wengi katika nchi yetu wamekuwa wakikata tamaa kuendelea na kilimo kutokana na hasara wanayoipata katika kilimo na kitu kikubwa kinacho changia hili ni ukosefu wa taarifa sahihi,sio tu taarifa sahihi za mbegu zipi ni bora kwa kilimo au ni udongo upi ni bora kwa kilimo cha zao fulani bali ni muda gani muafaka huwa na bei nzuri kwa zao fulani.Kilimo biashara kimejikita zaidi katika utaalamu unaotumika katika shughuli nzima za kilimo lakini masoko mazuri ni jambo la kuzingatia kabla hata hujaanza kilimo.
Kutokana na changamoto inayowakumba wakulima kutofahamu ni muda gani nizalishe nini ili nipate soko zuri la zao husika basi tumekuja na KALENDA YA MASOKO KWA BAADHI YA MAZAO TANZANIA yenye mazo tofauti tofauti.
Kalenda hii inaonesha ni mwezi gani zao fulani hua na bei nzuri hivyo basi mkulima anachotakiwa kukifanya ni kuhakikisha kipindi hicho ndicho anachopaswa kuvuna zao husika ili aweze kupata faida nzuri kwenye kilimo.kipindi ambacho zao husika huwa na soko zuri kimeoneshwa kwa rangi tofauti tofauti lakini kikubwa ni kwamba kipndi ambacho hakijaoneshwa kwenye kalenda hii basi ni kipindi ambacho zao hilo huwa na bei ndogo inayopelekea mkulima kupata hasara.Kiuhalisa ni kwamba katika vipindi hivi ambavyo masoko huwa mazuri kwa zao husika huwa kunakuwa na changamoto kubwa kuzalisha zao hilo moja wapo ikiwa ukame lakini ni vyema ukatafuta njia bora za kupambana na changamoto hizo upate faida nzuri kuliko kusubiria msimu wake na kuishia kuuza mazo kwa hasara.Kwa maswali na maelezo juu ya kalenda hii unaweza ukacomment swali lako na ukajibiwa hapa.Tuache kulima kwa kufata mkumbo kilimo kinalipa.-Agrila Farming
Mkuu nashukuru kweli kwa huu uzi lakin nngeomb uongezee na mazo mengine
 
Kuna baadhi ya mazao nimeikubali hiyo kalenda ila mengine daaaa!
Mfano chainizi msimu uliyoweka kwa huku hapana aiseee
 
Nimependa uzi wako ila naomba ufafanuzi wa rangi nyekundu hapo je inaonyesha sio kipindi kizuri au kipindi kizuri, pia ingekua vyema kama ungefafanua rangi zote kwa ajili ya faida ya wengine ndugu
yaani ipo hivi boss kwenye zao husika sehemu yenye rangi ndio kipindi ambacho soko hua zuri haijalishi ni njano,nyekundu au nyeusi
 
hapa ni lazima kulima kwa umwagiliaji boss,maana katika kipindi hiki demand huwa ni kubwa kuliko supply ya zao husika na hii inaonesha moja kwa moja kuwa ni kipindi ambacho si kila mtu anaweza kulima hasa kwa wale wanaolima kwa kutegemea mvua
Shukran sana nimekuelewa vizuri
 
Back
Top Bottom