Prince Kunta
JF-Expert Member
- Mar 27, 2014
- 22,783
- 28,799
Ununio imepata mteja
Kama vipi kalapina apelekwe Kibiti akapambane nao
Kama vipi kalapina apelekwe Kibiti akapambane nao
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva na mmoja wa Watu wanaoaminika kuwa ni Mbabe kama siyo Mtemi na Ngumi Jiwe wa kutukuka Kalapina jana wakati akihojiwa na Kipindi cha XXL kinachorushwa na Clouds fm aliamua kutema nyongo / kuvunja ukimya juu ya Kitendo cha Msanii mwenzake na mshikaji wake Roma Mkatoliki Kutekwa.
Kalapina ambaye anasifika mno kwa Usela / Uhuni na ukorofi ambao kiuhalisia kweli anauweza alianza kwanza kwa kumpa pole Roma Mkatoliki kwa yote yaliyomkuta ila hakusita pia kumlaumu kidogo Roma kwa kumwambia kuwa asingekubali kirahisi rahisi kubebwa na kuingizwa katika Gari na Kutekwa.
Ifuatayo ni nukuu Kuntu kabisa kutoka kwa Kalapina ambayo nadhani ni ujumbe tosha kwa Wazee wa Ununio mkabala na Mahaba Beach ( Watekaji ) “ Nakuambia Mimi nina hamu sana hao Watekaji siku wakosee tu waje waniteke Mimi kisha wajue kuwa kuna Watu tumebarikiwa kwa Ukorofi na Ukorofi tunaujua. Mimi wakija kama 10 na kutaka kuniteka basi nakuhakikishia lazima wakati wanafanikiwa kuniingiza katika Gari lao na kuniteka basi tayari name huku nyuma nitakuwa nimeshawaua Watatu au Wanne huku waliobaki nikiwaachia maumivu ya Kutukuka kabisa. Mdogo wangu Roma ulilegea sana na siku nyingine usifanye hivyo ukiona Mtu anataka kukuteka au ana nia mbaya nawe usimcheleweshe na badala yake mpe Kipondo / Kipigo pale pale “ mwisho wa kumnukuu Kalapina.
Haya Watekaji ( Wazee wa Ununio mkabala na Mahaba beach ) Kalapina huyo anawakaribisheni mkamteke na Yeye ili mkapate Kipondo / Kipigo ambacho inawezekana hata huko Chuoni Kwenu Wakufunzi wenu ama hawakuwafundisha au walisahau kuwafundisha.
Shikamoo Kalapina
Nawasilisha
Habari za rwanda mkuu
ArafatHuyo anaongea tu kuna mwenzake naye alikuwa anajiita NGUMI JIWE vijana walicho mfanya siri yake.
YapUnajua kupigana?
.......wengine tunalalia chaga tupu mbavu zetu zipo hatarini sasa na vichekesho kama hivi mtatumalizaaaaaKuna kipindi nilisomaga kitabu cha willy gamba,
Basi nikatoka hom ili nipambane na migambo waliokua wanatoza kodi mtaani maana walikua wanaboa kinyama
Namshukuru Mungu walinivunja meno mawili tu
hahahaha huyu ana tafuta kiki... hata Roma alishawai kusema leta deffender,leta wajeda lakini nasikia waliokuja walikuwa kwenye Noah.....
Huyu ana tafuta kiki
Hah hah hah weekend njema kwangu.Kuna kipindi nilisomaga kitabu cha willy gamba,
Basi nikatoka hom ili nipambane na migambo waliokua wanatoza kodi mtaani maana walikua wanaboa kinyama
Namshukuru Mungu walinivunja meno mawili tu
Iv kwel una amini kwamba kule hakuna wakorof aiseee pole yakoIla Mkuu wanaomjua Kalapina Vijana wa Mikocheni, Msasani, Mwananyamala, Temeke na Tandika wanasema Jamaa ( Kalapina ) anajua mkono / ngumi sana. Inasemekana Masela / Wahuni wote wa Mjini wanamuogopa mno Kalapina kwani ni Mpenda Fujo / Vagi halafu na hizo Fujo zenyewe nazo zinampenda na zinampa ushirikiano wa Kutukuka pale akiwa anazifanya hivyo yawezekana hao Watekaji wakawa na wakati mgumu sana Kwake kama wakimkabili siku moja.
Nzuri habari na Madafuni huko Dar es Salaam! JPM hajambo? Msalimie na mwambie GENTAMYCINE ninampenda na namkubali mno.