Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,495
- 51,090
Askofu Benson Lwakalinda Bagonza (PhD) Ameandika
KABLA YA KATIBA MPYA...
1. Kabla ya Katiba Mpya ya Afrika ya Kusini, Nelson Mandela aliitwa gaidi.
2. Kabla ya "Katiba Mpya" iliyoandikiwa Lancaster, Julius Nyerere alikuwa ni Mchochezi aliyekuwa nje ya gereza kwa kulipa faini.
3. Kabla ya Agano Jipya (Katiba Mpya), Musa alikuwa ni gaidi machoni pa Farao (Firauni).
4. Kabla ya ufufuko (Katiba Mpya) Bwana Yesu Kristo alikuwa na tuhuma za ugaidi na uhaini mbele ya utawala wa Kiyahudi.
5. Kabla ya Muswada ulioleta "Tamko la Haki kwa wote" (Katiba Mpya) huko Marekani, Mwanamke na mtu mweusi kudai kupiga kura ilikuwa ni kitendo cha ugaidi.
6. Kabla ya SUK huko Zanzibar, hayati Maalim Seif alikuwa gaidi, kibaraka wa Usultani na mtuhumiwa wa uhaini.
7. Kabla ya CCM Mpya ("Katiba Mpya"), Waitara, Prof Mkumbo, Mollel, Gekul, Katambi, Silinde, Kafulila, hayati Mgwira nk walikuwa vibaraka wa ubeberu na sasa ni wazalendo.
8.Kabla ya msiba wa kitaifa (Katiba Mpya), Mama SSH alikuwa ni Mshauri wa Rais (Asiyelazimisha ushauri wake), Sasa ni Mshauriwa (Asiyelazimishwa na washauri).
Tunajifunza Nini?
A. Ugaidi ni dhana na silaha ya mtawala dhidi ya mtawaliwa.
B. Muda ndio mwamuzi wa kweli na WA haki.
C. Watawaliwa huteseka; watawala hujuta.
D. Bora mateso kuliko majuto.
E. Katika harakati za kupata madaraka, kila aliyewahi kutawala aliwahi kuonekana ni gaidi mbele ya anaoshindana nao. Hata ndani ya CCM "Magaidi" ni wengi dhidi ya SSH.
Wanaomtuhumu Mbowe kuwa gaidi leo, watakuwa Magaidi wa mfumo wakati ujao.
KABLA YA KATIBA MPYA...
1. Kabla ya Katiba Mpya ya Afrika ya Kusini, Nelson Mandela aliitwa gaidi.
2. Kabla ya "Katiba Mpya" iliyoandikiwa Lancaster, Julius Nyerere alikuwa ni Mchochezi aliyekuwa nje ya gereza kwa kulipa faini.
3. Kabla ya Agano Jipya (Katiba Mpya), Musa alikuwa ni gaidi machoni pa Farao (Firauni).
4. Kabla ya ufufuko (Katiba Mpya) Bwana Yesu Kristo alikuwa na tuhuma za ugaidi na uhaini mbele ya utawala wa Kiyahudi.
5. Kabla ya Muswada ulioleta "Tamko la Haki kwa wote" (Katiba Mpya) huko Marekani, Mwanamke na mtu mweusi kudai kupiga kura ilikuwa ni kitendo cha ugaidi.
6. Kabla ya SUK huko Zanzibar, hayati Maalim Seif alikuwa gaidi, kibaraka wa Usultani na mtuhumiwa wa uhaini.
7. Kabla ya CCM Mpya ("Katiba Mpya"), Waitara, Prof Mkumbo, Mollel, Gekul, Katambi, Silinde, Kafulila, hayati Mgwira nk walikuwa vibaraka wa ubeberu na sasa ni wazalendo.
8.Kabla ya msiba wa kitaifa (Katiba Mpya), Mama SSH alikuwa ni Mshauri wa Rais (Asiyelazimisha ushauri wake), Sasa ni Mshauriwa (Asiyelazimishwa na washauri).
Tunajifunza Nini?
A. Ugaidi ni dhana na silaha ya mtawala dhidi ya mtawaliwa.
B. Muda ndio mwamuzi wa kweli na WA haki.
C. Watawaliwa huteseka; watawala hujuta.
D. Bora mateso kuliko majuto.
E. Katika harakati za kupata madaraka, kila aliyewahi kutawala aliwahi kuonekana ni gaidi mbele ya anaoshindana nao. Hata ndani ya CCM "Magaidi" ni wengi dhidi ya SSH.
Wanaomtuhumu Mbowe kuwa gaidi leo, watakuwa Magaidi wa mfumo wakati ujao.