Viol
JF-Expert Member
- Dec 15, 2009
- 25,426
- 18,223
Jana akihojiwa East Africa Radio amesema uchaguzi ujao atagombea ubunge Kinondoni ili aungane na makamanda wenzake mjengoni.
Pia wiki iliyopita hii radio ilimhoji afande sele akasema atagombea Morogoro Mjini.
Profesa Jay naye amekiri atagombea kwa tiket ya CHADEMA jimbo la Mikumi Morogoro.
Nadhani jinsi siku zinavyoenda wasanii wengi watatangaza nia kupitia CHADEMA.
Uwezekano pia upo wakaingia bungeni.
Kugombea ni haki ya kila mtu ila uongozi wa juu wa CHADEMA waliangalie vizuri hilo swala wanapopitisha majina ya wagombea,maana chama kitajaa wasanii.
Wakuu nye mna maoni gani!!
Pia wiki iliyopita hii radio ilimhoji afande sele akasema atagombea Morogoro Mjini.
Profesa Jay naye amekiri atagombea kwa tiket ya CHADEMA jimbo la Mikumi Morogoro.
Nadhani jinsi siku zinavyoenda wasanii wengi watatangaza nia kupitia CHADEMA.
Uwezekano pia upo wakaingia bungeni.
Kugombea ni haki ya kila mtu ila uongozi wa juu wa CHADEMA waliangalie vizuri hilo swala wanapopitisha majina ya wagombea,maana chama kitajaa wasanii.
Wakuu nye mna maoni gani!!
Msanii maarufu wa muziki wa kufoka foka (hiphop) anasema baada ya kumzingua na kumletea uzinguzi katika nafasi ya udiwani aliyoigombea uchaguzi uliopita, sasa amejipanga vema katika idara zote ili kulinyakua jimbo la Kinondoni na kuwapigania wanyonge wa Kinondoni wanaoliwa vya kwao na wachache.
Hayo ameyasema leo wakati akihojiwa katika kipindi cha Leo Tena (clouds fm). Ameongeza kuwa angekuwepo bungeni wakati wa sakata la escrow angewapigania wanakinondoni by any means hata kama ni kwa kuwapa vitasa wahusika.