Mdau
JF-Expert Member
- Mar 29, 2008
- 1,789
- 470
Nimekua nikifuatila kwa karibu sana mienendo na kauli za 'Askofu' zakaria Kakobe wa Full Gospel Fellowship, Mwenge, Dar Es Salaam...naanza kuamini sasa kwamba mtu huyu ni Mwanasiasa zaidi kuliko mchungaji wa kondoo wa Bwana kama navyotaka wengi tuamini...kuanzia sakata lake la kumuunga mkono Mrema, majibizano yake na viongozi wenzake wa kiroho,na sasa hili sakata la TANESCO, vimenifanya nielekee kwenye kumtazama kisiasa na kifedha zaidi kuliko kichungaji..sijaona mantiki ya yeye kuruhusu ama ku-support Tshirts zenye maandishi ya uchochezi na kutoa maneno yenye mwelekeo wa chuki na migongano kwa jamii..TANESCO kupitisha nguzo mbele ya kanisa lake kunahusiana vipi na RICHMOND??? kama alikuwa na la kusema kuhusu RICHMOND, aliwahi kuongea nini kuhusu RICHMOND? Kakobe anaongoza maelfu ya waumini,ambao ana uwezo mkubwa sana wa KU-CONTROL & MANIPULATE their mindsets, sasa anataka kutuambia nini hapa?? jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es Salaam,na vyombvo vingine vya usalama mnasubiri nini kumkamata mtu anayeweka amani rehani naman hii? mbona mara kadhaa tumeshuhudia mkipita palepale kwa kakobe kwenda kukabiliana na vijana wasomi wa ARDHI UNIVERSITY or UDSM ambao huwa wanadai madai halali na ya msingi?? sidhani kama ni haki kuacha kumpatia haki yake mtu anayevunja haki!!! mkamateni kakobe,liwe funzo kwa wengine..... kwa sasa simtofautishi sana na PROPHET AKABA, yule mchungaji wa kwenye Novel ya Danny Safo His Excellency the Head of State,kwa waliobahatika kuisoma novel hii..........