Kakobe awarukia wabunge

Hollo

JF-Expert Member
Apr 21, 2008
827
165
2008-06-18 09:19:52
Na Simon Mhina

Askofu Mkuu Zakaria Kakobe wa Kanisa la Full Gosple Bible Fellowship amesema wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania, wamelidhalilisha Taifa na kuiaibisha dunia nzima, kufuatia madai ya kuhofu kuendelea na vikao kwa sababu ya uchawi.

Akizungumza na Nipashe jijini Dar es Salaam jana, alisema ni ajabu na aibu kubwa kuona wabunge wanazungumzia uchawi, wakati mabunge ya nchi zilizoendelea, yanajadili
bajeti za kuwawezesha watu wao kupaa na vyombo maalum kwenda kujenga nyumba kwenye sayari ya Mars.

Askofu Kakobe alisema dhana ya uchawi ni ujinga na upuuzi, ambayo haipaswi kupewa nafasi kwa mtu yeyote anayefahamu wajibu wake.

Alisema hofu ya uchawi iliyowaingia wabunge, hadi Spika Bw. Samweli Sitta akatoa ufafanuzi sio tu imewapandisha chati wachawi na ndumba zao, bali pia imewarudisha Watanzania enzi za ujima.

``Yaani Watanzania wanawakilishwa na wabunge wanaoogopa uchawi na wanatumia muda mwingi kujadili ndumba? Mimi nimeshangaa kusikia wamehofu kukalia viti vyao kwa kudhani eti vina ndumba, hatua hii imewapandisha chati wachawi nchini. Hivi sasa wachawi nchini wanaonekana kitu muhimu hadi wanajadiliwa bungeni? Ni aibu,`` alisema.

Alisema wabunge wamempa ushindi mkubwa shetani, kwa vile siku zote huanza kuwatia watu hofu, ili atekeleza mambo yake.

Kufuatia tukio hilo, Askofu Kakobe alisema haoni sababu ya wabunge kufungua vikao vyao kwa sala.

Alisema haelewi ni vipi wanafungua vikao kwa sala, halafu wanahofu ndumba.

`1Ina maana yule Mungu wanayemuomba asubuhi, hawamuamini, wanataka kutuambia ndumba zina nguvu kuliko Mwenyezi Mungu wanayemtaja hata wakila kiapo?`` Alihoji.

Wakati huo huo, Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Methodist Kilaini, amesema madai ya uchawi bungeni yamemshangaza.

Alisema ameshangaa kuona watu wakubwa kama wabunge wanaishi kwa hofu ya uchawi.

``Kabla Spika hajatoa ufafanuzi nilisema moyoni kwamba sasa tumefika mbali, kwamba watu wanatishiana na uchawi bungeni?`` Alisema.

* SOURCE: Nipashe
 
2008-06-18 09:19:52
Na Simon Mhina

Askofu Mkuu Zakaria Kakobe wa Kanisa la Full Gosple Bible Fellowship amesema wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania, wamelidhalilisha Taifa na kuiaibisha dunia nzima, kufuatia madai ya kuhofu kuendelea na vikao kwa sababu ya uchawi.

Akizungumza na Nipashe jijini Dar es Salaam jana, alisema ni ajabu na aibu kubwa kuona wabunge wanazungumzia uchawi, wakati mabunge ya nchi zilizoendelea, yanajadili
bajeti za kuwawezesha watu wao kupaa na vyombo maalum kwenda kujenga nyumba kwenye sayari ya Mars.

Askofu Kakobe alisema dhana ya uchawi ni ujinga na upuuzi, ambayo haipaswi kupewa nafasi kwa mtu yeyote anayefahamu wajibu wake.

Alisema hofu ya uchawi iliyowaingia wabunge, hadi Spika Bw. Samweli Sitta akatoa ufafanuzi sio tu imewapandisha chati wachawi na ndumba zao, bali pia imewarudisha Watanzania enzi za ujima.

``Yaani Watanzania wanawakilishwa na wabunge wanaoogopa uchawi na wanatumia muda mwingi kujadili ndumba? Mimi nimeshangaa kusikia wamehofu kukalia viti vyao kwa kudhani eti vina ndumba, hatua hii imewapandisha chati wachawi nchini. Hivi sasa wachawi nchini wanaonekana kitu muhimu hadi wanajadiliwa bungeni? Ni aibu,`` alisema.

Alisema wabunge wamempa ushindi mkubwa shetani, kwa vile siku zote huanza kuwatia watu hofu, ili atekeleza mambo yake.

Kufuatia tukio hilo, Askofu Kakobe alisema haoni sababu ya wabunge kufungua vikao vyao kwa sala.

Alisema haelewi ni vipi wanafungua vikao kwa sala, halafu wanahofu ndumba.

`1Ina maana yule Mungu wanayemuomba asubuhi, hawamuamini, wanataka kutuambia ndumba zina nguvu kuliko Mwenyezi Mungu wanayemtaja hata wakila kiapo?`` Alihoji.

Wakati huo huo, Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Methodist Kilaini, amesema madai ya uchawi bungeni yamemshangaza.

Alisema ameshangaa kuona watu wakubwa kama wabunge wanaishi kwa hofu ya uchawi.

``Kabla Spika hajatoa ufafanuzi nilisema moyoni kwamba sasa tumefika mbali, kwamba watu wanatishiana na uchawi bungeni?`` Alisema.

* SOURCE: Nipashe

Kweli kabisa dhana ya uchawi imepitwa na wakati kabisa!Ni aibu kujadili uchawi
 
Wandugu,
Huyu bwana nilikuwa namsikia tu. Nilipokuwa mjini Tabora nikapata bahati ya kumuona kwenye TV. Mhhh, jamaa ni mbabe kweli. Siku hiyo alikuwa akiombea akina mama wenye watoto ila hawana maziwa yaani maziwa hayatoki. Basi baada ya kuombea kwa muda akaanza kusema waje hapa. Akina mama wakaja na yeye akawa anawashika matiti na kuonyesha maziwa yakitoka. Ana bahati kuwa hakuwepo binti wa Kichaga maana ANGELIMLABUA. Ahhh, wewe washika Matiti ya akina mama wazima? Umekuwa Justin Timberlake?? Askofu mzimana joho lake na msalaba? Sijui kuna siku atakuja aombea akina mama wasio na hamu ya kutoa vitu? Ataproove vipi kuwa sasa wanatoa? Tena mbele ya watu? Au akina baba wasio-simama? Mhhh wee Kakobe? Na eti akisafiri basi watu wanasali kwa kutumia mikanda yake ya video?????
Kwangu mie huyu na wengine wengi ni MATAPELI wanautumia dini kuishi. Kwa maana nyingine ni WALA VYA BURE. Ana gari, nyumba, TOTOZ kama sikosei, fedha na nasikia pia hutumia VIJIUNGA kama vya ANDEREYA katika kufanikisha hili. Hebu mwenye MADATAZ anielezee zaidi maana wengi huyu jamaa wanamuogopa kama Andereya.
 
aende akawaombee ..... si kwamba yamepitwa na wakati mbona kanisani kwake kila kukicha ana tibu watu maradhi yanayotokana na uchawi ... anajiita nabii kwa kuondoa uchawi na mapepo mabaya yaliyowakumba watu ... na kuonyesha miujiza kedekede kwenye tiviiiii ... kwani naigeria huenda kufanya nini ... sasa anavyosema kinyume namshangaa keli keli ...

kila mmoja anahofia maisha yake ... angejitolea kwenda kuwaombea au kuomba kwenye huo ukumbi hapa ningemuelewa
 
Kakobe naye ni muumini mzuri wa imani za kishirikina, anawatia watu hofu kwa mahubiri yake kisha anawafanyia ufisadi kwa kutumia jina la Yesu, ataitwaje askofu mkuu wakati kanisa lake ni kama ofisi za mfukoni, kwani hana maaskofu wengine chini yake!
 
sasa kama nayeye anaombea wenye mambo ya kichawi kanisani kwake wanatoka kwanini asifunge safari kwenda dodoma kuombea huo uchawi tuwajua haswaa wachawi na watoke?!!!asitake kutuzingua na sera zake hapa huyu si ndo wakati flani alijiunga kupigia kampeni chama flani hadi kanisani mwake akawa anawaambia washarika wamchague huyo bosi wake???
 
kakobe kasema kila siku wabunge wanasali kwa nini waogope uchawi?sio lazima kakobe aende bungeni akaombee!wakati kila asubuhi kuna sala bungeni
 
kakobe nae amekuwa chadema siku hizi ? anapaswa aache tabia zake hizi za kuingilia mambo ya siasa yeye na watu wengine wote wa dini , kwani wameshaona wanasiasa wakiingilia imani za watu ? nao wafanye hivyo hivyo watunze na kulisha roho zilizopotea na sio kujiingiza katika masuala ya siasa
 
yeye kama haamini mambo ya kichawi kule kanisani kwake wale pepo anaowatoa wafuasi wake inakuwa ni uongo au? mbona anajichanganya kiasi hiki huyu?
 
Wandugu,
Huyu bwana nilikuwa namsikia tu. Nilipokuwa mjini Tabora nikapata bahati ya kumuona kwenye TV. Mhhh, jamaa ni mbabe kweli. Siku hiyo alikuwa akiombea akina mama wenye watoto ila hawana maziwa yaani maziwa hayatoki. Basi baada ya kuombea kwa muda akaanza kusema waje hapa. Akina mama wakaja na yeye akawa anawashika matiti na kuonyesha maziwa yakitoka. Ana bahati kuwa hakuwepo binti wa Kichaga maana ANGELIMLABUA. Ahhh, wewe washika Matiti ya akina mama wazima? Umekuwa Justin Timberlake?? Askofu mzimana joho lake na msalaba? Sijui kuna siku atakuja aombea akina mama wasio na hamu ya kutoa vitu? Ataproove vipi kuwa sasa wanatoa? Tena mbele ya watu? Au akina baba wasio-simama? Mhhh wee Kakobe? Na eti akisafiri basi watu wanasali kwa kutumia mikanda yake ya video?????
Kwangu mie huyu na wengine wengi ni MATAPELI wanautumia dini kuishi. Kwa maana nyingine ni WALA VYA BURE. Ana gari, nyumba, TOTOZ kama sikosei, fedha na nasikia pia hutumia VIJIUNGA kama vya ANDEREYA katika kufanikisha hili. Hebu mwenye MADATAZ anielezee zaidi maana wengi huyu jamaa wanamuogopa kama Andereya.

....hahahaha kubadilisha mada si kazi kubwa sana.... haha...
 
Gaijin, nasikia nyingine deal zile zinapangwa, Kwi! kwi! kwi!

mei pia nimeshawahi sikia mambo hayo wanapanga dili n stuffs ili kuvutia watu wengi waende kanisani mwake!!if its so ehh ni kweli sasa twaelekea mwisho wa dunia maana iliandikwa ikikaribia tutaona mambo mengi ikiwemo manabii wa uongo!!
 
....hahahaha kubadilisha mada si kazi kubwa sana.... haha...

Msanii,
Sikuandika ili kubadilisha mada. Hawa watu wa dini kweli wanatisha na ULAFI wao. Heri ya FISADI maana yeye anajulikana anataka nini ila watu wa DINI hujui anataka kuhubiri au anataka POWER, SEX and MONEY.
Nasikia tu kuwa wanawake wa kichaga ukamshika matiti anakulabua na kusema "hee unashika hotel ya mtoto..." Anyway this is OLD JOKE.
 
Kakobe ni kada wa CCM na mnafiki mkubwa hana huruma hata maisha ya waumini wake anawakamua nashangaa wanao mwendea sijui kufanya maombi .Jambazi in kind
 
Back
Top Bottom