Kakobe apinga nyaraka za viongozi wa dini; akemea kauli ya Pengo

Kitila Mkumbo

JF-Expert Member
Feb 25, 2006
3,354
1,943
Kakobe amempongeza Rais Kibaki kwa kuchaguliwa tena. Mwanzoni niliposoma mstari wa kwanza nilishtuka na nikaanza kusema huyu Askofu kapatwa na nini tena. Hata hivyo kadri nilivyoendelea kusoma nikajiridhisha kwamba huyu bwana anaweza akawa yupo sawa na sisi wengine wote wakiwemo wale waliandamana juzi tukawa tupo on the wrong side wakati wote wa hili sakata la Kenya.

Anachosema Kakobe ni kwamba kilichotokea Kenya ndicho hicho ambacho kimekuwa kikitokea kwetu siku zote tangu mfumo wa vyama vingi uanze na kwamba tume yetu ya uchaguzi ni mbovu kuliko ya Kenya. Anasema tuache unafiki na tutoe kwanza boriti kwenye jicho letu kabla ya kuwanyooshea wengine vidole. OK, hebu na wewe endelea kumsoma na lete maoni yako.

______________________________________________________________

Kakobe atoa mpya

na Mwandishi Wetu (Tanzania Daima)

ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Full Bible Gospel Fellowship (FBGF), Zakaria Kakobe, amesema anampongeza Rais Mwai Kibaki wa Kenya kwa ushindi alioupata katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwishoni mwa mwaka jana.

Mbali ya hilo, Askofu Kakobe amemtaka Rais Jakaya Kikwete kuchukua uamuzi wa kumpongeza rais huyo wa Kenya, akisema uamuzi huo utafuta aibu ya unafiki wa Tanzania.

"Nina ujasiri wa kumpongeza Kibaki kwa kushinda uchaguzi mkuu nchini Kenya. Kwa sababu hiyo basi, iwapo kina Raila Odinga na wenzake wana manung'uniko yoyote na matokeo ya uchaguzi, hawana budi kufuata mkondo wa sheria kwa kwenda mahakamani kupinga ushindi huo," alisema Kakobe aliyezungumza na Tanzania Daima katika mahojiano maalumu ya njia ya simu.

Askofu huyo ambaye kwa miaka kadhaa sasa amejiweka kando na masuala ya kisiasa tangu mwaka 2000, alieleza kuwashangaa Watanzania wanaotoa maneno makali ya kejeli dhidi ya ushindi wa Kibaki.

Kwa mujibu wa Askofu Kakobe, Watanzania hawana ubavu wala jeuri ya kumnyoshea mkono Kibaki au kuwakejeli Wakenya wakati ukweli ukionyesha wazi kwamba uchaguzi Tanzania uhusisha wizi mkubwa.

Akitumia neno kutoka katika Biblia, Askofu Kakobe aliwataka Watanzania wenzake kutoa boriti iliyo ndani ya jicho lao kwanza kabla ya kuanza kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwingine.

Katika hili, Kakobe alieleza kushangazwa na makundi ya watu wakiwamo wasomi na wanasiasa wanaofikia hatua ya kupanga maandamano na kuandamana ili kupinga kile wanachokiita wizi wa kura uliofanywa na Kibaki.

"Watanzania hatuna mamlaka ya kuwanyoshea kidole Wakenya, wakati tukijua kuwa hapa kwetu hali ni mbaya zaidi... ni afadhali tuwaache wengine waseme badala yetu ambao kimsingi ni wanafiki," alisema Kakobe.

Askofu huyo ambaye mwaka 2000 alimuunga mkono Augustine Mrema aliyekuwa akigombea urais kwa tiketi ya TLP, alisema Tume ya Uchaguzi ya Kenya iliyokuwa ikiongozwa na Kivuitu ni bora kuliko ilivyo ile ya Tanzania.

Akitoa mfano alisema, angalau tume hiyo ya Kivuitu miaka mitano iliyopita ilikuwa na jeuri ya kutangaza kushindwa katika uchaguzi kwa Chama cha KANU kilichokuwa madarakani nchini Kenya tangu uhuru wa nchi hiyo mwaka 1963, hatua ambayo anaamini haiwezi kufanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Tanzania.

"Hivi wewe unaamini kwamba Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi wa hapa kwetu anaweza akatangaza matokeo kwamba CCM imeshindwa? Angalau Kivuitu huyu tunayemnyoshea kidole alitangaza kushindwa kwa Moi (Rais wa zamani wa Kenya) na KANU," alisema Askofu Kakobe.

Alisema kuna matukio mengi ya ushahidi yanayoonyesha kuwa katika chaguzi mbalimbali hapa nchini kumekuwa na matukio mbalimbali yanayoonyesha kuwapo kwa vitendo vya wizi wa kura.

"
Tumepata kumsikia Cheyo (John) akilalamikia kuibiwa kura kwenye uchaguzi wa ubunge kule kwao, hivyo hivyo kule Zanzibar CUF wamekuwa wakilalamikia wizi wa kura. Mbona hatujaona maandamano ya kupinga wizi huo.

"Ni jambo la ajabu kwamba watu hawa wanataka kuandamana kuhusu Kenya na hawajapata kutaka kuandamana kuhusu Tanzania. Tunajifanya ni wasafi sana wakati ukweli ni kwamba sisi ni wanafiki," alisema Kakobe ambaye tangu kuanza kwa mahojiano hayo alikiri kuchukua uamuzi unaotofautiana na watu na makundi mbalimbali.

Mbali ya hilo, Kakobe alieleza kushangazwa na ukimya wa Watanzania wa kutozungumza lolote kuhusu ubaya wa katiba ambao umekuwa ni tatizo kubwa kabisa na kwa miaka mingi.

Alisema ni ukweli ulio wazi kwamba, katiba inayosimamia mfumo wa vyama vingi leo hii ni ya chama kimoja lakini hakuna mtu aliye tayari kulisimamia hilo na kulipigania.

Askofu Kakobe anatoa kauli hiyo siku chache tu baada ya makanisa mengine nchini likiwamo Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) kutoa tamko linaloonyesha wazi kutomuunga mkono Kibaki.

Aidha, kauli hiyo ya Kakobe inakuja siku chache tu baada ya wasomi wa vyuo vikuu kuandamana wakimpinga Kibaki na kumtaka Rais Kikwete kutoitambua serikali yake.

Kabla ya uamuzi huo wa wasomi, juhudi za wanasiasa kadhaa wa vyama vya upinzani kutaka kuandamana wakipinga ushindi wa Kibaki zilikwama kutokana na uamuzi wa Jeshi la Polisi kuzuia maandamano yao hayo.

Tangu kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi Kenya, vurugu zilizozuka katika maeneo mbalimbali nchini humo zimesababisha zaidi ya watu 700 kupoteza maisha yao huku mamia wengine wakiwa hawana makazi.
 
Last edited by a moderator:
mimi ninachotaka ni maendeleo ingawa sijui tunaendelea kwenda wapi ila maendeleo tu baas! mambo ya katiba na katibu tuwaachie kaisari ambao wanadhani kwa utashi wao sie tunapumua. Wanasiasa angalieni mijitatizo inavyozuka barani afrika kwa kuiga demokrasia ya kimagharibi. Hebu niambieni kuna kitu gani positive ktk mfumo wa maisha ambao tumeupokea kutoka magharibi ukatuletea manufaa??? Cha msingi tukae chini tutumie thinkers tulionao ili kutengeneza mfumo wetu mbadala ili hata kuwasaidia hao magharibi maana hata wao wameharibikiwa sasa

Kakobe namjua sana na anachosema ni adili ingawa naye ana boriti kibao ktk macho yake. Ila angalau amesema bila woga.
 
mimi ninachotaka ni maendeleo ingawa sijui tunaendelea kwenda wapi ila maendeleo tu baas! mambo ya katiba na katibu tuwaachie kaisari ambao wanadhani kwa utashi wao sie tunapumua. Wanasiasa angalieni mijitatizo inavyozuka barani afrika kwa kuiga demokrasia ya kimagharibi. Hebu niambieni kuna kitu gani positive ktk mfumo wa maisha ambao tumeupokea kutoka magharibi ukatuletea manufaa??? Cha msingi tukae chini tutumie thinkers tulionao ili kutengeneza mfumo wetu mbadala ili hata kuwasaidia hao magharibi maana hata wao wameharibikiwa sasa

Kakobe namjua sana na anachosema ni adili ingawa naye ana boriti kibao ktk macho yake. Ila angalau amesema bila woga.

Msanii unataka kukubaliana na yule dikteta wa Central Republic Jean Bokasa aliyewahi kupiga marufuku matumizi ya maneno "demokrasia na uchaguzi" katika nchi yake? Yeye alisema haya ni maneno ya magharibi sio Africa, kwe hiyo ilkuwa ni criminal offence wakati ulikuwa ukikutwa unatamka hayo maneno! Unataka twende huko?
 
Msanii unataka kukubaliana na yule dikteta wa Central Republic Jean Bokasa aliyewahi kupiga marufuku matumizi ya maneno "demokrasia na uchaguzi" katika nchi yake? Yeye alisema haya ni maneno ya magharibi sio Africa, kwe hiyo ilkuwa ni criminal offence wakati ulikuwa ukikutwa unatamka hayo maneno! Unataka twende huko?

hata siku moja mkuu kitila
ninachosema ni kuwa hii demokrasia tuliyoipokea bila ya kuichunguza kwanza kama itatufaa ndo imetuletea haya matatizo ya chama tawala na wapinzani. hivi sasa wapinzani wanaonekana as wametoka mars yaani alliens fulani hivi. demokrasia ndiyo iliyoleta magaidi na mafisadi maana dhamana ya nchi sasa inabebwa na wasaiasa ambao hata namna jembe linavyoshikwa hawajui. kazi nyingi za kitaalam afrika zinatupwa mkono kwani wataalam wetu wanakimbilia siasa as suluhisho la madhila ya maisha yao. ukiangalia maendeleo ya nchi yanategemea utashi wa kiasa, je utanishawishi hapo nikubali kuwa demokrasia hii ni halali??

nilikuwa natoa changamoto kwa wanafikra wa kiafrika hususani tanzania kuchachamiza bongo zao ili kuangalia mfumo upi utatufaa na kama hii demokrasia tuliyoimeza wimawima kutoka magharibi kamainatufaa. nilitegemea wazee wetu wangeitafiti kwanza na kuiweka iwiane na ustaarab wa maisha yetu kiafrika. Je demokrasia bila mapinduzi ya kiteknolojia itasimama kweli?? demokrasia bila uhuru wa habari itasimama kweli? je demokrasia bila tumehuru za uchaguzi itasimama kweli? hivyo badala ya kuikubali demokrasia kichwakichwa (kama wazungu watakavyo) wangeanza kuandaa mazingira ya demokrasia. bila mbegu ya kuime mtoto hazaliwi.... lazima kuna suluhisho mbadala na tuwape nafasi thinkers (akumbukwe chachage RIP) watoe maoni yao na tuone mwelekeo chanya.

kwa mfano mimi nina uwezo wa kuongoza ila sipendi chama chochote je hapo inawezekana??

simuungi mkono bokasa, amini, abacha na wengineo walioibaka demokrasia ila pia siungi mkono aina ya demokrasia tuliyonao sasa.
 
kuna mtu alimuuliza msimamo wake kuhusu Kikwete kabla ya uchaguzi wa 2005 na baadaye... watu wanakumbuka.. Kama ni unafiki ni ule nilioandika kwenye "Barua kwa wachungaji".. baada ya kondoo kutawanyika kama wasio na mchungaji leo wanasimama na kujifanya wananyosha fimbo ya uongozi!!? Ashindwe na kulegea....
 
hata siku moja mkuu kitila
ninachosema ni kuwa hii demokrasia tuliyoipokea bila ya kuichunguza kwanza kama itatufaa ndo imetuletea haya matatizo ya chama tawala na wapinzani. hivi sasa wapinzani wanaonekana as wametoka mars yaani alliens fulani hivi. demokrasia ndiyo iliyoleta magaidi na mafisadi maana dhamana ya nchi sasa inabebwa na wasaiasa ambao hata namna jembe linavyoshikwa hawajui. kazi nyingi za kitaalam afrika zinatupwa mkono kwani wataalam wetu wanakimbilia siasa as suluhisho la madhila ya maisha yao. ukiangalia maendeleo ya nchi yanategemea utashi wa kiasa, je utanishawishi hapo nikubali kuwa demokrasia hii ni halali??

nilikuwa natoa changamoto kwa wanafikra wa kiafrika hususani tanzania kuchachamiza bongo zao ili kuangalia mfumo upi utatufaa na kama hii demokrasia tuliyoimeza wimawima kutoka magharibi kamainatufaa. nilitegemea wazee wetu wangeitafiti kwanza na kuiweka iwiane na ustaarab wa maisha yetu kiafrika. Je demokrasia bila mapinduzi ya kiteknolojia itasimama kweli?? demokrasia bila uhuru wa habari itasimama kweli? je demokrasia bila tumehuru za uchaguzi itasimama kweli? hivyo badala ya kuikubali demokrasia kichwakichwa (kama wazungu watakavyo) wangeanza kuandaa mazingira ya demokrasia. bila mbegu ya kuime mtoto hazaliwi.... lazima kuna suluhisho mbadala na tuwape nafasi thinkers (akumbukwe chachage RIP) watoe maoni yao na tuone mwelekeo chanya.

kwa mfano mimi nina uwezo wa kuongoza ila sipendi chama chochote je hapo inawezekana??

simuungi mkono bokasa, amini, abacha na wengineo walioibaka demokrasia ila pia siungi mkono aina ya demokrasia tuliyonao sasa.


You are right, tunahitaji taasisi za demokrasia ziwepo. Kosa letu tunaendelea kutegemea busara ya viongozi wetu na bahati mbaya viongozi wenyewe wa leo hawana busara. lazima tufike mahala tuwekeze katika taasisi maana tukishakuwa na taasisi imara hata mkawa na bahati mbaya mkapata Rais kichakaa bado hamntayumba. Wenzetu wamewekeza sana kwenye hizi taasisi za demokrasia ndio maana hata wanapopata marais hamnazo kama akina Bush bado hawayumbi. Lakini pia bado tuna tatizo na watu wetu pia. Watu wetu wengi tuliowakabidi mamlaka hawajiamini kabisa hata kama taasisi zinawapa nafasi ya kufanya kazi. Kwa hiyo kasafari ketu ni karefu kidogo lakini inabidi tufike hatuna short cut.
 
kuna mtu alimuuliza msimamo wake kuhusu Kikwete kabla ya uchaguzi wa 2005 na baadaye... watu wanakumbuka.. Kama ni unafiki ni ule nilioandika kwenye "Barua kwa wachungaji".. baada ya kondoo kutawanyika kama wasio na mchungaji leo wanasimama na kujifanya wananyosha fimbo ya uongozi!!? Ashindwe na kulegea....


Mkuu,

Napenda kutokubariana na wewe hapa.

Nadhani Mchungaji yupo right kwa hili,ingawa sikatai nini anaweza kua alifanya na kunena huko nyuma.Kutokana na siasa za kitanzania mabadiliko kama haya ni ya kuyategemea kwa yoyote (mfano Tambwe Hiza wa Cuf aliyeenda CCM)

Ambapo kwa lugha nyingine unaweza kusema MAFISADi wanapoona una faida nao watakupa kila unachoihitaji alafu when they are done with you they dump you na unabidi uanze square one wewe mwenyewe.
Ninacho jaribu kusema hapa mkuu,Mchungaji ndio anafanya "NITOKE VIPI TENA HAPA".
Yeye mwenyewe na wao wanajua kwamba hiyo ni sehemu ya huo mchezo mchafu,anawakosoa na Tume yao ya uchaguzi ili tena wam-notice kwamba yupo na anaweza kuwaokoa na nini kinaendelea kwa sasa nchini.
Ila Bwana kakobe yuko sawa sisi wa TZ ni wanafiki iweje leo tuandamane kewa ajiri ya wakenya wakati mambo hayo ni kawaida kwetu?Kila pawapo ushindi wa KISHINDO basi wapinzani wanalia na hamna hata mmoja katika hao wasomi wanao bother hajata kuandaa kongamano kupinga ila leo mmhh.!inashangaza! Badala yake hao hao wenye uchungu na wakenya wana line from Bongo to Uingeleza kupata kadi za chama cha MFISADI na kupiga picha na Muungwana.
 
Two wrongs do not make a right.Kikobe msanii, Kiwete msanii Kibaki msanii.
 
Mimi nakubaliana na Kakobe kwa kiasi fulani. Ni kweli tumeshindwa kufanya lolote wakati CCM wanaiba waziwazi. Lakini kuandamana kuhusu Kenya siyo jambo baya maana inawezekana ndiyo ukawa mwanzo wa waTZ kuamka hivyo 2010 wakiibiwa CCM wajue wanategemea nini. Vilevile CCM kutokumtambua Kibaki wanajipalia makaa, kwani 2010 Kibaki atajibu mapigo, unafikiri M7 mjinga mpaka kajitanguliza kumpongeza? Anajua wizi ndiyo deal la viongozi wote Africa wakiongozwa na CCM nambari wani (No. 1)
 
kuna mtu alimuuliza msimamo wake kuhusu Kikwete kabla ya uchaguzi wa 2005 na baadaye... watu wanakumbuka.. Kama ni unafiki ni ule nilioandika kwenye "Barua kwa wachungaji".. baada ya kondoo kutawanyika kama wasio na mchungaji leo wanasimama na kujifanya wananyosha fimbo ya uongozi!!? Ashindwe na kulegea....

Halafu akishalegea iweje....
 
Mimi nakubaliana na Kakobe kwa kiasi fulani. Ni kweli tumeshindwa kufanya lolote wakati CCM wanaiba waziwazi. Lakini kuandamana kuhusu Kenya siyo jambo baya maana inawezekana ndiyo ukawa mwanzo wa waTZ kuamka hivyo 2010 wakiibiwa CCM wajue wanategemea nini. Vilevile CCM kutokumtambua Kibaki wanajipalia makaa, kwani 2010 Kibaki atajibu mapigo, unafikiri M7 mjinga mpaka kajitanguliza kumpongeza? Anajua wizi ndiyo deal la viongozi wote Africa wakiongozwa na CCM nambari wani (No. 1)

HUYO MU-7 HANA BAO LABDA AFANIKIWE KWANZA KUBADILI HIYO KATIBA YAO ILI AONGEZEWE KIPINDI KINGINE.
ILA JAMAA KAMA KIBAKA ....or sorry KIBAKI DIKTETA TU WOTE
 
Namsikiliza, nadhani jamaa ana pointi, kweli sisi tumezidi woga, na pengine tunashida zaidi ya huko Kenya! kanifurahisha alivo ipondea miafaka isiyo isha!
 
Namsikiliza, nadhani jamaa ana pointi, kweli sisi tumezidi woga, na pengine tunashida zaidi ya huko Kenya! kanifurahisha alivo ipondea miafaka isiyo isha!

I tell you this guy is smarter than we think of him!
 
Back
Top Bottom