Kaini alipata wapi mke wake?

Bado mkuu
Kaini alioa dada yake sababu kipindi hicho ndio kwanza dunia ilikua inapanuka. Watu wanaweza kusema anaweza vipi kuoa dada,jibu ni kwa kipindi kile hakukua na sheria inayokataza kuoa na kuolewa na dada,baba,mama,au ndugu.

Pia Abrahamu alioa dadayeke(Sara) Isaka alienda kuoa kwa wajomba zake.

Baada ya Sodoma na Gomora wale mabint waliobak na baba yao walilala naye ili mzee wao awaachie uridhi(watoto) sababu mzee alikua kazeeka sana na hakukua na vijana wa kuwazalisha kipindi hicho.

Chanzo: Biblia
 
Kwa nini isiwezekane?,Unaposema wa kawaida unalingalisha na wanawake hawa wa siku hizi??.Mzee bibi yangu alizaa watoto 17 tena hakuna mapacha hata mmoja,na aliishai miaka 87.Sasa Eva aishi miaka zaidi ya 800 (sababu inaokenana Adam ndio alianza kufa) ashindwe kuzaa watoto 63??..
Halafu walikuwa wanahesabu watoto wakiume wakike ilikuwa kama kuangua embe nakuliweka ndani hesabu ni wanaume tu, kweli ubaguzi haujaanza Leo ulianzia huko huko tulikotokea.
 
Naomba mwenye audio ya Mwana wa Dandu "James" usemao 'mimi msafiri niko njiani nakwenda, sijui lini nitafika' au original yake ya Mzinga troup.
 
Natumai ni mzima na unaendelea vyema na majukumu, Kama unaumwa utapona kwa uwezo wa muumba wako.

HOJA YA MSINGI:

“Ikiwa Adamu na Hawa walikuwa na wana wawili, Kaini na Abeli, na baadae Seth, Je, mke wa Kaini alitoka wapi?”
Biblia ina habari za kutosha kujibu swali hilo kwa njia inayofaa, na kwenye hii mada tutajibu hili swali linalo wachanga sana watu.
MUKTASARI:
Katika Mwanzo sura ya 3 na ya 4 tunapata habari zifuatazo:

(1) Hawa alikuwa “mama ya kila mtu anayeishi.”

(2) Muda fulani ulipita kuanzia wakati Kaini alipozaliwa mpaka wakati alipotoa dhabihu ambayo ilikataliwa na Mungu.

(3) Baada ya kufukuzwa na kuwa “mwenye kutanga-tanga na mkimbizi,” Kaini alikuwa na wasiwasi kwamba huenda ‘mtu yeyote akakutana naye’ na kujaribu kumuua. [Angalia hoja hapa "Kaini anaogopa kuuwawa na watu wengine"] Hapa panaonyesha kuwa Kaini alikuwa na ndugu wengine.

(4) Mungu aliweka ishara ya kumlinda Kaini, jambo lililoonyesha kwamba ndugu au dada zake, au watu wengine wa ukoo wangejaribu kumuua. Kumbe basi Kaini alikuwa na ndugu wengine zaidi ya Abel na Seth.

(5) “Baadaye” Kaini alilala na mke wake “katika nchi ya Ukimbizi.”—Mwanzo 3:20; 4:3, 12, 14-17.

Naomba majibu tafadhari.
Adam na Eva hawakuwa wanadamu wa kwanza kuumbwa na Mungu, ila ni wanadamu wa kwanza kuumbwa katika bustani ya Edeni. Walikuwa ni aina mpya kabisa na Mungu akawatenga waishi katka bustani ya Edeni maisha yao yote. Ila nje mbali na bustani kulikuwepo binadamu wengine kabisa wakiishi. Baada ya kuasi na kufukuzwa bustanini ndo wakaja kuishi nje ya bustani ambapo pia watu wengine walkuwepo wakiishi kabla yao. Na hao watu waloumbwa mapema walokuwa wanaishi mbali na bistani walikuwa weusi kumbe ndo waafrika.
 
Nahisi Ni kwa sababu biblia inataja vizazi vya watu kwa kupitia watoto wa kiume mfano Ni :Adam kumzaa kain,Abel na Seth so hii haimaanishi kuwa hao waliotajwa ndio peke yao tu walizaliwa na ADAM NA HAWA ukute Kain hata hakuwa wakwanza kuzaliwa kwa Hawa Bali waeza kuta walizaliwa wa kike wengi alafu yeye Ndo akafatia na kwa kuwa biblia kuhesabu watu ilikuwa inahesabu wanaume tu peke yao labda ndio maana
Unataka kukubali eti walifanya mapenzi na dada zao, yaan ndugu kwa ndugu walioana? Nakama ni ndiyo ,walifanya hivyo kwa amri ya nani?
 
Adam na Eva hawakuwa wanadamu wa kwanza kuumbwa na Mungu, ila ni wanadamu wa kwanza kuumbwa katika bustani ya Edeni. Walikuwa ni aina mpya kabisa na Mungu akawatenga waishi katka bustani ya Edeni maisha yao yote. Ila nje mbali na bustani kulikuwepo binadamu wengine kabisa wakiishi. Baada ya kuasi na kufukuzwa bustanini ndo wakaja kuishi nje ya bustani ambapo pia watu wengine walkuwepo wakiishi kabla yao. Na hao watu waloumbwa mapema walokuwa wanaishi mbali na bistani walikuwa weusi kumbe ndo waafrika.
Umetoa wap hii!?😂😂😂😂
 
Natumai ni mzima na unaendelea vyema na majukumu, Kama unaumwa utapona kwa uwezo wa muumba wako.

HOJA YA MSINGI:

“Ikiwa Adamu na Hawa walikuwa na wana wawili, Kaini na Abeli, na baadae Seth, Je, mke wa Kaini alitoka wapi?”
Biblia ina habari za kutosha kujibu swali hilo kwa njia inayofaa, na kwenye hii mada tutajibu hili swali linalo wachanga sana watu.
MUKTASARI:
Katika Mwanzo sura ya 3 na ya 4 tunapata habari zifuatazo:

(1) Hawa alikuwa “mama ya kila mtu anayeishi.”

(2) Muda fulani ulipita kuanzia wakati Kaini alipozaliwa mpaka wakati alipotoa dhabihu ambayo ilikataliwa na Mungu.

(3) Baada ya kufukuzwa na kuwa “mwenye kutanga-tanga na mkimbizi,” Kaini alikuwa na wasiwasi kwamba huenda ‘mtu yeyote akakutana naye’ na kujaribu kumuua. [Angalia hoja hapa "Kaini anaogopa kuuwawa na watu wengine"] Hapa panaonyesha kuwa Kaini alikuwa na ndugu wengine.

(4) Mungu aliweka ishara ya kumlinda Kaini, jambo lililoonyesha kwamba ndugu au dada zake, au watu wengine wa ukoo wangejaribu kumuua. Kumbe basi Kaini alikuwa na ndugu wengine zaidi ya Abel na Seth.

(5) “Baadaye” Kaini alilala na mke wake “katika nchi ya Ukimbizi.”—Mwanzo 3:20; 4:3, 12, 14-17.

Naomba majibu tafadhari.
Ndugu, Ukitaka kuchuma dhambi we endela kuihoji biblia kwenye masuala ya kiutata kwa uwezo wa kibinadamu. Tafsiri ya Biblia ni kitu kizito mno - masuala mengine kwenye biblia unahitaji Roho mtakatifu kupata ufunuo !!
 
Back
Top Bottom