Dawa ya masnitch kama nyie ni kuwa piga kipapai tu..
Mtu mzima apaki gari kwa faida gani?
Kwanza jiulize gari Na. 940 halafu rufaa Dar from Rufiji, je hiyo gari todate ina hali gani, hasa ukuchukulia jinsi services za magari kwa halmashauri vilivyo za kusua sua??Mimi najiuliza, gari zima ila wameamua kulipaki, wanafaidika na nini?
Kama kweli amewekwa rumande sio kwa kudanganya huenda ni kwa uzembe wa kuacha wananchi wakihangaika huku gari ipo
Viongozi sio vichaa waseme hakuna gari huku ni zima, huenda lilikua bovu
Umeshasema lilihitaji service ndogo, sasa kitu kizima hakiwezi kuhitaji service
Naamini angesema ukweli asingekaa mahabusu
Unapoongea maafisa walioko field kuanzia ofisini mitaani hata huko gereji wanarudisha meseji kuwa gari iko hapa haiko gereji chapchap .Raisi anacheki ishara kwa msaidizi wake aliyejifichav katikati bya mikutano anmwonyesha alama ya Siri ya No muongo huyo .Hajachongewa na mtu ila usidhani unaweza kumdanganya Rais halaf mfumo usifuatilie ukweli
Angesema ukweli yasingemkutaUmesema vizuri. Gari kukosa matairi ni issue kubwa..ndiyo ubovu wenyewe huo. Kama halmashauri haina pesa za kununulia hayo matairi asemeje sasa. Jamaa mchonganishi sana.
Mtoa mada anasema Bw.Kilimba alisema hawana gariKwahio Bw.Kilimba anashtakiwa kwa kosa gani?kusema gari bovu?
Hebu tuambie kama gari lilikuwa zima kwanini walilipaki?sababu ilikuwa nini?
Kama gari imepaki na haifanyi kazi kama ulivyosema inahitaji service na kubadilisha vipuri maana yake ni mbovu hio.
Una roho mbaya sana weweNapenda kuvipongeza vyombo vya ulinzi na usalama kwa kugundua kuwa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji Bw. Brighton Kilimba alitoa taarifa za uongo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa John Magufuli kuwa gari ya wagonjwa ya Kituo cha Afya Ikwiriri haiwezi kutembea kwa sababu ni mbovu na inahitaji matengenezo makubwa.
Nikiwa mtumishi wa Wilaya hii niliumia sana kwa sababu nilikuwa najua ni uongo wa mchana kweupe na niliumia zaidi kwa kuwa aliyekuwa anadanganywa ni Rais wangu ninayempenda Dk. John Pombe Magufuli.
Hata hivyo nilifurahi muda mfupi baadaye nilipomuona kwenye mitandao ya kijamii Bw. Brighton Eliud Kilimba, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji akiwa kwenye pingu na bango linaonesha anatuhumiwa kumdanganya Rais. Nikasema kweli vyombo vya ulinzi na usalama sasa hivi vipo makini na havijalala.
Ukweli ni kwamba gari ya wagonjwa ya Kituo cha Afya Ikwiriri ipo na viongozi waliamua tu kuipaki wakati wananchi wanahangaika kupeleka wagonjwa wao Jijini Dar es Salaam pale wanapohitaji matibabu ya rufaa.
Gari hilo ni zuri, ni aina ya Toyota Landcruizer namba STL 940, ni gari imara na limekuwa msaada mkubwa sana kwa wananchi kabla viongozi hawajaamua kulipaki na kuwaacha Wananchi wanahangaika kukodi magari kwa gharama kubwa na wakati mwingine kupanda bodaboda, ni jambo la kusikitisha sana kwa viongozi kutotekeleza wajibu wao kiasi hiki.
Kumbe siku ile Mheshimiwa Rais alipopita Rufiji na kulalamikiwa na wananchi juu ya ukosefu wa gari la wagonjwa, gari lilikuwepo na lilikuwa limetelekezwa katika Kituo cha Afya Ikwiriri likiwa halina tatizo lolote zaidi ya kuhitaji kufanyiwa service ya kawaida ya kubadilishwa oil na pengine kubadili matairi yake.
Kaimu Mkurugenzi Bw. Kilimba alipokuwa anamdanganya Rais kuwa gari ni bovu sana na haliwezi kutembea, Rais kwa machale akaamua kuagiza gari hilo lipelekwe TEMESA mara moja, nikajua hapa siri lazima itafichuka.
Kwa kuwa gari halikuwa gereji kama Bw. Kilimba alivyosema hadharani, alichofanya Bw. Kilimba ni kupiga simu na kuagiza gari hilo lipelekwe gereji mara moja ili maafisa watakapofuatilia wakute lipo gereji, jamaa wa gereji waliposikia hivyo machale yakawacheza wakakataa kulipokea na ndipo maafisa wakagundua kuwa gari halikuwa gereji ambako Rais aliambiwa na halikuwa bovu kama Rais alivyoambiwa. Ni michezo tu ya viongozi.
Navipongeza sana vyombo vya ulinzi na usalama kwa kugundua mchezo huu, na kisha kumkamata na kumweka ndani Bw. Kilimba ambaye ni Afisa Kilimo wa Wilaya.
Aidha, nampongeza Rais Magufuli kwa hatua alizochukua siku ileile hata kabla hajafika Dar es Salaam kwa kumtumbua Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Bw. Juma Njwayo ambaye ndio alikuwa anaongoza kutoa taarifa za uongo kuhusu ubovu wa magari. Hawa wote ni tatizo kubwa sana hapa Rufiji na yapo mengi ya hovyo wanayafanya, endapo uchunguzi wa kina utafanyika yatabainika vizuri.
Naamini hili litakuwa funzo kwa viongozi wengine kuwajibika ipasavyo katika kuwatumikiwa wananchi kama ambavyo Mheshimiwa Rais Magufuli anasema kila siku, kuwatumikia wanyonge vizuri badala ya kuwaacha wanahangaika wakati Serikali inajitahidi kuhakikisha inapeleka huduma kwa wananchi.
Msimamo wa Mheshimiwa Rais wa kuagiza gari hilo litengenezwe ndani ya wiki 1 na wakati gari linatengenezwa gari la Mkurugenzi ndilo litumike kubeba wagonjwa ni ujumbe tosha kuwa sisi watumishi ni lazima tuweke maslahi ya wananchi mbele na tuwatumikie kama ambavyo tunapaswa kufanya.
Asante Mheshimiwa Rais kwa uongozi wako makini unaojali watu hasa wanyonge.
Pichani ni Bw. Brighton Kilimba na gari la wagonjwa la Kituo cha Afya Ikwiriri.
View attachment 1524897View attachment 1524898View attachment 1524899Ni mimi Mtumishi
Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji.
02 Agosti, 2020.
Ni kawaida kwa taasisi nyingi. Baada ya muda, gari hilo angeuziwa mtu kwa bei ya kutupwa. Kuna taasisi moja ya elimu ya juu iliuza gari la wagonjwa kwa milioni 15 wakati ni zima kabisa!!Mimi najiuliza, gari zima ila wameamua kulipaki, wanafaidika na nini?
Huyo Mkurugenzi roho yake unaijua ni nzuri? Akili ya awamu ya 4 hiyo! Kuamini wizi na uzembe ni umaarufu.Una roho mbaya sana wewe
Huna akiliSafi sana Avutwe korodani
saizi mtu akitumbuliwa anashukuru mi naishi na hawa wateuliwa hawana raha kabisa na nafasi zaoahaaaahaaa yani kuna watu watakua wanajilaumu kwanini hawakwenda kwenye gombania goli kutia nia