Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Kaimu Mkurugenzi wa mji wa Arusha, Estomi Changah jana alianza kazi rasmi kwa kasi ya aina yake, baada ya kukubali malalamiko ya Chama cha Mapinduzi (CCM) juu ya mgombea wa Chadema Jimbo la Arusha, Godbless Lema kuendesha kampeni za uchochezi na hivyo kumpa onyo kali na kumpiga faini ya Sh 100,000/-
Maamuzi malalmiko hayo ya CCM ambayo ni sehemu ya malalmiko ambayo Mkurugenzi wa zamani Raphael Mbunda aliyehamishiwa ghafla mkoani Kigoma alishindwa kutolea maamuzi.
Kaimu M kurugenzi mpya alitoa adhabu hiyo kufuatia kikao cha kamati ya maadili ya uchaguzi kilichofanyika jana ofisi za tume ya uchaguzi, Arusha.
Kwa mujibu wa maamuzi hayo, kama mgombea huyo wa Chadema ataendelea tena kutoa lugha chafu atapigwa marufuku kupiga kampeni hadi uchaguzi mkuu utakapofanyika Octoba 31 mwaka huu.
Katika kikao hicho cha maadili, ambacho kilihudhuriwa na viongozi wa vyama vyote, CCM walikuwa wakimlalamikia mgombea huyo wa Chadema kutokana na kuendesha kampeni chafu dhidi ya mgombea wa CCM, Dk Batila Burian ambaye pia ni Waziri wa Nchi ofisi ya makamu wa Rais Mazingira.
Kwa mujibu wa habari kutoka ndani ya kikao hicho, maneno yaliyomtia hatiani Lema ni kutumia lugha za matusi.
Chanzo: Mwananchi ya leo.