Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa, Shaka apokea wanachama 283 Zanzibar

KADA08

Member
Dec 2, 2017
44
152
Mbali na kupokea na kukabidhi kadi kwa wanachama wapya 283 katika Mkoa wa Mjini Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Tanzania Ndugu Shaka Hamdu Shaka amezindua pia madaftari maalum ya wanachama kwa ajili ya kusajili upya wanachama wa UVCCM na kuhuisha takwimu zilizopo za wanachama. Vile vile aliyafungua rasmi mafunzo ya siku mbili kwa viongozi wakuu wa UVCCM kuanzia matawi, wadi, Jimbo, wilaya na mkoa.

Ndugu Shaka aliwasisitiza viongozi hao kuchapakazi kwa bidii, uadilifu, nidhamu na utii kwa kufuata kanuni, katiba na miongozo mbalimbali itokanayo na vikao vya CCM. Aliwahimiza kuhakikisha wanayatembelea makundi ya vijana waliopo nje ya UVCCM ili kuwaelimisha na kuwahamasisha juu ya madhumuni ya UVCCM, siasa na itikadi ya CCM, umuhimu wa kulinda na kudumisha mapinduzi ya Zanzibar na Muungano wetu.

Aliwataka viongozi hao kuhakikisha wanasikiliza kero na changamoto zinazowakabili vijana wote na kuzipatia ufumbuzi. Kwa kufanya hivyo aliwaeleza kutaiongezea CCM marafiki, wakereketwa na wanachama wapya kutoka kundi hili la vijana ambalo kitakwimu ni wengi zaidi hivyo kukipa Chama Cha Mapinduzi matumaini makubwa ya ushindi katika kila chaguzi.

Ndugu Shaka aliwataka viongozi hao wawe mstari wa mbele kufuatilia utekelezaji wa ilani katika maeneo yao pamoja na kusemea utekelezaji wake kwa wananchi Alieleza kuwa Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli na Dkt Ali Mohamed Shein wanafanya kazi nzuri sana ya kutuletea maendeleo ni jukumu letu kuwatetea, kuwasemea na kuwalinda dhidi ya wapingaji wa kila jambo.
IMG-20180421-WA0148.jpg
IMG-20180421-WA0132.jpg
 
Mbali na kupokea na kukabidhi kadi kwa wanachama wapya 283 katika Mkoa wa Mjini Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Tanzania Ndugu Shaka Hamdu Shaka amezindua pia madaftari maalum ya wanachama kwa ajili ya kusajili upya wanachama wa UVCCM na kuhuisha takwimu zilizopo za wanachama. Vile vile aliyafungua rasmi mafunzo ya siku mbili kwa viongozi wakuu wa UVCCM kuanzia matawi, wadi, Jimbo, wilaya na mkoa.

Ndugu Shaka aliwasisitiza viongozi hao kuchapakazi kwa bidii, uadilifu, nidhamu na utii kwa kufuata kanuni, katiba na miongozo mbalimbali itokanayo na vikao vya CCM. Aliwahimiza kuhakikisha wanayatembelea makundi ya vijana waliopo nje ya UVCCM ili kuwaelimisha na kuwahamasisha juu ya madhumuni ya UVCCM, siasa na itikadi ya CCM, umuhimu wa kulinda na kudumisha mapinduzi ya Zanzibar na Muungano wetu.

Aliwataka viongozi hao kuhakikisha wanasikiliza kero na changamoto zinazowakabili vijana wote na kuzipatia ufumbuzi. Kwa kufanya hivyo aliwaeleza kutaiongezea CCM marafiki, wakereketwa na wanachama wapya kutoka kundi hili la vijana ambalo kitakwimu ni wengi zaidi hivyo kukipa Chama Cha Mapinduzi matumaini makubwa ya ushindi katika kila chaguzi.

Ndugu Shaka aliwataka viongozi hao wawe mstari wa mbele kufuatilia utekelezaji wa ilani katika maeneo yao pamoja na kusemea utekelezaji wake kwa wananchi Alieleza kuwa Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli na Dkt Ali Mohamed Shein wanafanya kazi nzuri sana ya kutuletea maendeleo ni jukumu letu kuwatetea, kuwasemea na kuwalinda dhidi ya wapingaji wa kila jambo.
View attachment 752228View attachment 752280
Kwani hakwenda mombasa kwenye harusi?
 
Z'b yenyewe inawakazi laki 3, wazee, vijana na watoto. Hao 250 pamoja na mimba!! acha kuhamisha mada watanzania wanataka kujua kwanini madini, hayajakaguliwa!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom