Kaifuta namba yangu kisa sikumpa hela!!!

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,001
112,639
Hata kuonana hatujaonana. Hajui hata naitwa Nyani nani [jina langu la ukoo], lakini huwa tunachati tu hapa na pale.

Juzi ananicheki kwa WhatsApp...bebi hivi bebi vile.

Mara ananipiga mzinga. Eti anaumwa halafu anataka kwenda kumsalimia mama'ake huko Shinyanga.

Nilipomnyima akaja juu. Eti kwa nini namnyima huku wakati anashida. Akasema anaifuta namba yangu.

Nami nilivo kichaa nikaifuta yake kabla hata hajaifuta yangu.

Hata kama ndo ujasiria-vagina lakini siyo to that extent.

Utamwombaje hela mtu ambaye hata humjui kivile?

Mi hata kumwomba tu mtu anikopeshe huwa ninafikiria karibu hata mwezi mzima na mwisho wa siku naishia kupotezea tu. Siombi wala sikopi.

Lakini kwa wengine kuomba ni kama anatoa salamu! Hata mshipa wa kujistukia hana.

Ama kweli tumeumbwa tofauti.
 
Hahaa haa the funny part unakuta kawaomba hata watu watano kwa mpigo

mwingine unakuta anakutajia shida hiyo ukimtazama wala hafanani nayo
mtu anakwambia ana shida ya nauli ya mkoa haifiki hata elfu 30
wakati simu zake mbili tu anagusa milioni....unabaki unajiuliza maswali
 
Hahaa haa the funny part unakuta kawaomba hata watu watano kwa mpigo

mwingine unakuta anakutajia shida hiyo ukimtazama wala hafanani nayo
mtu anakwambia ana shida ya nauli ya mkoa haifiki hata elfu 30
wakati simu zake mbili tu anagusa milioni....unabaki unajiuliza maswali

Ndo huwa iko hivyo.

Anakupiga mzinga wewe...anakuja kwangu...anaenda kwa yule....mwisho wa siku unakuta anazichanga hata milioni hivi hivi.

Halafu cha kuchekesha...anakwambia ana shida leo huku jana tu aliweka update kwenye WhatsApp akiwa sijui ndo Dragon garden kule Masaki....huku kavaa Gucci zake za Kariakoo.

Hahahaaaaaa hawa watu bana!
 
Hata kuonana hatujaonana. Hajui hata naitwa Nyani nani [jina langu la ukoo], lakini huwa tunachati tu hapa na pale.

Juzi ananicheki kwa WhatsApp...bebi hivi bebi vile.

Mara ananipiga mzinga. Eti anaumwa halafu anataka kwenda kumsalimia mama'ake huko Shinyanga.

Nilipomnyima akaja juu. Eti kwa nini namnyima huku wakati anashida. Akasema anaifuta namba yangu.

Nami nilivo kichaa nikaifuta yake kabla hata hajaifuta yangu.

Hata kama ndo ujasiria-vagina lakini siyo to that extent.

Utamwombaje hela mtu ambaye hata humjui kivile?

Mi hata kumwomba tu mtu anikopeshe huwa ninafikiria karibu hata mwezi mzima na mwisho wa siku naishia kupotezea tu. Siombi wala sikopi.

Lakini kwa wengine kuomba ni kama anatoa salamu! Hata mshipa wa kujistukia hana.

Ama kweli tumeumbwa tofauti.
my baby kumbe wewe ni wa extent hyo?
 
Hahaa haa the funny part unakuta kawaomba hata watu watano kwa mpigo

mwingine unakuta anakutajia shida hiyo ukimtazama wala hafanani nayo
mtu anakwambia ana shida ya nauli ya mkoa haifiki hata elfu 30
wakati simu zake mbili tu anagusa milioni....unabaki unajiuliza maswali
jiulize maswali yote ila toa elf 30
 
Ndo huwa iko hivyo.

Anakupiga mzinga wewe...anakuja kwangu...anaenda kwa yule....mwisho wa siku unakuta anazichanga hata milioni hivi hivi.

Halafu cha kuchekesha...anakwambia ana shida leo huku jana tu aliweka update kwenye WhatsApp akiwa sijui ndo Dragon garden kule Masaki....huku kavaa Gucci zake za Kariakoo.

Hahahaaaaaa hawa watu bana!

Ndo wako hivyo,,wanafikiri kuzaliwa tu na jinsia ya kike
ni sawa na kuwa na SACCOS...

unawachangisha tu
 
37 Reactions
Reply
Back
Top Bottom