Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Manji alirudisha fedha kwa niabaya "Kagoda" akidai kuwa aliyehusika ni marehemu baba yake. Serikali ikapokea fedha hizo na kuzijumlisha kwenye ile jumla ya Rais.
a. Kama wamerudisha fedha na serikali imekubali kupokea kuna haja ya kujua nani alifanya kosa kweli?
b. Kama serikali imekubali kupokea fedha hizo ina maana imekubali maelezo ya Manji na hivyo "case closed"?
c. Kama fedha zilizochukuliwa kwa kiasi kikubwa ndizo zilizotumika kumuingiza JK madarakani na sasa kazirudisha bado mnataka kumbana?
d. Rostam ndiye aliyehusika na kutumiwa kama alivyohusika kwenye Dowans na kutumiwa kwanini ni nani anaweza kumnyoshea kidole wakati wao wanajua bila yeye wasingeweza kuingia madarakani? NI kweli huwezi kumgusa Rostam bila kugusa karibu nusu ya Wabunge na Rais na huwezi kumuachilia bila kuachikilia kesi kadhaa za kifisadi! So what do you do?
e. Je kwa kujaribu kujifanya wanaichunguza Kagoda wakati tayari wanajua ni nani (ni wao wenyewe!) kwanini wasije tu na kusema mbele ya wananchi kuwa "Kagoda ndiyo sisi! hatukujijua na tumegundua kuwa tulikuwa tumezichota wakati tumelala, lakini tumezirudisha yaishe"!? vinginevyo kwanini wanajifanya kana kwamba hawajui Kagoda ni nani wakati wamepokea fedha kutoka kwake!?
f. Je wananchi wanasababu yoyote ya kujua Kagoda ni hata kama wamesharudisha fedha na fedha zishaliwa? Manake hawawezi kumkamata Manji (aliyerudisha) wala Rostam (aliyechukua kwa kutumia vyombo vyake kwa niaba yake na ya chama chake (hakufanya kama charity work!)
g. Sasa kwanini DPP asije tu na kusema kuwa hili haliwezi (kwani linamgusa Rais moja kwa moja!).
h. Kwanini Wabunge na watu mashuhuri ndani ya CCM au wana CCM hawaandamani kutaka Kagoda ifiikishwe mahakamani na wahusika wote wafikishwe mahakamani kama wanavyoshangilia kina Mramba kufikishwa mahakamani. Je mtu anaweza kuufikisha mkono wake wa kushoto mahakamani bila ye yeye mwenyewe kuwa huko huko mahakamani?
La Kagoda tulimalize vipi baada ya kujua kuwa fedha zimerudishwa, wezi wanajulikana, zilipita wapi inajulikana na zirudi nchini kwa namna gani inajulikana?
well... I was just thinking out loud. Nauliza nilivyowahi kuuliza huko nyuma kwenye hili la Kagoda tukubali yaishe? Au tuendelee kugangamala huku tukijua "haliwaki" hata tulisukume na "kushtua"?
a. Kama wamerudisha fedha na serikali imekubali kupokea kuna haja ya kujua nani alifanya kosa kweli?
b. Kama serikali imekubali kupokea fedha hizo ina maana imekubali maelezo ya Manji na hivyo "case closed"?
c. Kama fedha zilizochukuliwa kwa kiasi kikubwa ndizo zilizotumika kumuingiza JK madarakani na sasa kazirudisha bado mnataka kumbana?
d. Rostam ndiye aliyehusika na kutumiwa kama alivyohusika kwenye Dowans na kutumiwa kwanini ni nani anaweza kumnyoshea kidole wakati wao wanajua bila yeye wasingeweza kuingia madarakani? NI kweli huwezi kumgusa Rostam bila kugusa karibu nusu ya Wabunge na Rais na huwezi kumuachilia bila kuachikilia kesi kadhaa za kifisadi! So what do you do?
e. Je kwa kujaribu kujifanya wanaichunguza Kagoda wakati tayari wanajua ni nani (ni wao wenyewe!) kwanini wasije tu na kusema mbele ya wananchi kuwa "Kagoda ndiyo sisi! hatukujijua na tumegundua kuwa tulikuwa tumezichota wakati tumelala, lakini tumezirudisha yaishe"!? vinginevyo kwanini wanajifanya kana kwamba hawajui Kagoda ni nani wakati wamepokea fedha kutoka kwake!?
f. Je wananchi wanasababu yoyote ya kujua Kagoda ni hata kama wamesharudisha fedha na fedha zishaliwa? Manake hawawezi kumkamata Manji (aliyerudisha) wala Rostam (aliyechukua kwa kutumia vyombo vyake kwa niaba yake na ya chama chake (hakufanya kama charity work!)
g. Sasa kwanini DPP asije tu na kusema kuwa hili haliwezi (kwani linamgusa Rais moja kwa moja!).
h. Kwanini Wabunge na watu mashuhuri ndani ya CCM au wana CCM hawaandamani kutaka Kagoda ifiikishwe mahakamani na wahusika wote wafikishwe mahakamani kama wanavyoshangilia kina Mramba kufikishwa mahakamani. Je mtu anaweza kuufikisha mkono wake wa kushoto mahakamani bila ye yeye mwenyewe kuwa huko huko mahakamani?
La Kagoda tulimalize vipi baada ya kujua kuwa fedha zimerudishwa, wezi wanajulikana, zilipita wapi inajulikana na zirudi nchini kwa namna gani inajulikana?
well... I was just thinking out loud. Nauliza nilivyowahi kuuliza huko nyuma kwenye hili la Kagoda tukubali yaishe? Au tuendelee kugangamala huku tukijua "haliwaki" hata tulisukume na "kushtua"?