Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,377
- 217,438
Leo kwenye shughuli za kuwaaga Wahanga 19 waliofariki kwenye ajali ya Ndege huko Kagera , kuna kitu kimenishangaza sana !
Kwenye ratiba ya kutoa rambi rambi hakukuwa na nafasi ya Mwakilishi wa Wavuvi , hawa ndio walipata uthubutu wa kuokoa Wahanga na kutumia Mashua zao duni na kamba za bei rahisi kuvuta ndege hadi ufukweni .
Mwenyekiti wa ccm wa Mkoa huo ambaye ni miongoni mwa WALIOSHIKA KIUNO pembeni ya ajali bila msaada wowote ndiye aliyepewa nafasi ya kutoa neno la rambi rambi , Huyu anapewa nafasi kama nani ? anahusikaje na masuala ya kitaifa ?
Badala ya kuwatambua Mashujaa wetu wavuvi , tunawapa nafasi watu wasio na msaada wowote ! Tumelogwa na nani ?
AMA KWELI TENDA WEMA NENDA ZAKO .
Kwenye ratiba ya kutoa rambi rambi hakukuwa na nafasi ya Mwakilishi wa Wavuvi , hawa ndio walipata uthubutu wa kuokoa Wahanga na kutumia Mashua zao duni na kamba za bei rahisi kuvuta ndege hadi ufukweni .
Mwenyekiti wa ccm wa Mkoa huo ambaye ni miongoni mwa WALIOSHIKA KIUNO pembeni ya ajali bila msaada wowote ndiye aliyepewa nafasi ya kutoa neno la rambi rambi , Huyu anapewa nafasi kama nani ? anahusikaje na masuala ya kitaifa ?
Badala ya kuwatambua Mashujaa wetu wavuvi , tunawapa nafasi watu wasio na msaada wowote ! Tumelogwa na nani ?
AMA KWELI TENDA WEMA NENDA ZAKO .