Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,807
- 11,969
MAMIA WAMLILIA PADRE IRENEUS MBAHULIRA
Padre Ireneus Mbahulira(79) amezikwa leo katika makaburi ya mapadre Seminarini Rubya Jimbo Katoliki la Bukoba.
Mazishi yake yameudhuriwa na Maaskofu Desiderius Rwoma, Methodius Kilaini na Askofu Almachius Rweyongeza wa Jimbo Katoliki la Kayanga. Kuliudhuriwa pia na mapadre wapatao 70, masista 50 na mamia ya waombolezaji.
Ibada ya misa ya mazishi iliyoongozwa na Askofu Rwoma. Ilianza majira ya saa 5.15 asubuhi. Kwaya ya Seminari ya Rubya iliongoza nyimbo. Waliimba misa ya Kilatini.
Katika mahubiri yake yaliyochukua dakika 14 askofu Rwoma alimshukuru Mungu kwa maisha ya padre Irene na kusisitiza haja ya kila mtu kujiandaa.
Masomo yalitoka Kitabu cha Wamakabayo, Waraka kwa Wathesalonike na Injili ya Mathayo kuhusu Wanawali kumi. Askofu Rwoma alisema kwa Mungu hakuna kifo cha ghafla.
Padre Ireneus alizaliwa kijijini Igurugati Parokia ya Bugandika tarehe 16.10.1942 na kufariki tarehe 22.01.2021 hospitalini Mugana alikokuwa amelazwa kutokana na matatizo ya kubanwa kifua. Hadi mahuti yake Padre Irene alikuwa Paroko Msaidizi Parokia ya Minziro, parokia aliyoamia akitokea parokiani Rukindo mwezi Septemba mwaka jana. Padre Irene alirejea jimboni Bukoba akitokea Jimbo Kuu la Dar es Salaam alikofanya utume wake kwa miaka mingi. Padre Irene katika maisha yake kama padre amehudumu katika Parokia 17 katika majimbo ya Bukoba, Arusha na Dar es Salaam.
Pia katika maisha yake alisomea Uandishi wa Habari na Utangazaji huko Kenya miaka ya 70. Aliporejea Tanzania alifanya kazi katika Kitengo cha Habari Baraza la Maaskofu Tanzania.
Katika hotuba zao walioongea hapo kanisani Rubya baada ya Misa akiwemo Askofu Kilaini na Padre Faustine Kamugisha(Paroko Minziro) walimwelezea marehemu Padre Irene kama mtu aliyekuwa mcheshi na mtu mwema wa kuishi naye.
Padre Faustine Kamugisha alipopata nafasi ya kuongea alisimulia mengi kuhusiana na maisha ya marehemu wakati wa uhai wake hapo Minziro, kuugua kwake alivyopelekwa Hospitali ya Kajunguti, baadae kurudishwa Minziro na hatimaye kupelekwa hospitalini Mugana ambako alifia. Haya yote yametendeka kwa kipindi kifupi sana. Padre Faustine amekabidhi shilingi 200,000/= kwa Askofu Rwoma kama rambirambi ya Parokia ya Minziro kwa Baba Askofu. Waliotoa rambilambi wengine ni Umoja wa Mapadre ambao walikabidhi bahasha ya pesa kwa mwakilishi wa familia ya marehemu Bwana Richard Muyungi, ingawa kiwango cha pesa hakikutajwa.
Askofu Kilaini wakati wa kutoa neno lake alitoa maneno ya rambirambi Kutoka kwa mapadre kadhaa wa Dar es Salaam na maaskofu mbalimbali kutoka majimbo ya Tanzania.
Askofu Alimachius Rweyongeza naye alitoa neno lake la pole kwa wafiwa na rambirambi kwa Askofu Rwoma.
Msemaji wa familia ya marehemu Bwana Richard Muyungi katika neno laki alisema kuwa Padre Ireneus ameiinua familia yao. Maneno hayo yamedhihirishwa na uchungu ulioonyeshwa na baadhi ya wanafamilia wakati wa kushuhudia na kumuaga marehemu na kutoa mchango misa. Wanafamilia wengine walipiga mayowe na wengine kutolewa nje na kuzimia.
Katika kushughulikia mwili wa marehemu hapo kanisani Sr, na muhudumu mwingine kutoka hospitalini Mugana na pia mapadre wa Seminari waliobeba mwili wa marehemu kuuweka kwenye gari baada ya misa hapo kanisani kuupeleka makabulini walivalia barakoa.
Kutoka Minziro lilikuwa ni kundi kubwa la watu. Minziro walikuja na kikundi cha kwaya ambacho kilikuwa kimevalia nguo nyekundu. Kilipata nafasi ya kuimba wimbo mmoja wakiganda baada ya komunyo.
Kaburi alimozikwa marehemu Padre Irene lilikuwa limejengwa vyema. Kuweka udongo ilikuwa ni kupitia wawakilishi.
Mapadre waliwakilishwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Mapadre jimboni Pd Paschal Mutegaya, Pd Adeodatus RWEHUMBIZA (Chancellor), maaskofu, masista wakuu wa Mashirika na baadhi ya wanafamilia akiwemo Pd Benezeth Rwegoshora, Achilleus RWEHUMBIZA, Sr Amelberga, na Sr Praxeda.
Baada ya shughuli za mazishi hapo makaburini kulifuatia huduma ya chakula kwa maaskofu, mapadre, masista na wanafamilia.
Shughuli ya mazishi imemalizika majira ya saa nane kasoro dakika mbili mchana. Hapo kesho majira ya saa tano asubuhi itasaliwa misa ya kuanua matanga nyumbani kwao Igurugati kwa Mzee Nazari marehemu babake. Na Pd Charles RWEHUMBIZA.
Padre Ireneus Mbahulira(79) amezikwa leo katika makaburi ya mapadre Seminarini Rubya Jimbo Katoliki la Bukoba.
Mazishi yake yameudhuriwa na Maaskofu Desiderius Rwoma, Methodius Kilaini na Askofu Almachius Rweyongeza wa Jimbo Katoliki la Kayanga. Kuliudhuriwa pia na mapadre wapatao 70, masista 50 na mamia ya waombolezaji.
Ibada ya misa ya mazishi iliyoongozwa na Askofu Rwoma. Ilianza majira ya saa 5.15 asubuhi. Kwaya ya Seminari ya Rubya iliongoza nyimbo. Waliimba misa ya Kilatini.
Katika mahubiri yake yaliyochukua dakika 14 askofu Rwoma alimshukuru Mungu kwa maisha ya padre Irene na kusisitiza haja ya kila mtu kujiandaa.
Masomo yalitoka Kitabu cha Wamakabayo, Waraka kwa Wathesalonike na Injili ya Mathayo kuhusu Wanawali kumi. Askofu Rwoma alisema kwa Mungu hakuna kifo cha ghafla.
Padre Ireneus alizaliwa kijijini Igurugati Parokia ya Bugandika tarehe 16.10.1942 na kufariki tarehe 22.01.2021 hospitalini Mugana alikokuwa amelazwa kutokana na matatizo ya kubanwa kifua. Hadi mahuti yake Padre Irene alikuwa Paroko Msaidizi Parokia ya Minziro, parokia aliyoamia akitokea parokiani Rukindo mwezi Septemba mwaka jana. Padre Irene alirejea jimboni Bukoba akitokea Jimbo Kuu la Dar es Salaam alikofanya utume wake kwa miaka mingi. Padre Irene katika maisha yake kama padre amehudumu katika Parokia 17 katika majimbo ya Bukoba, Arusha na Dar es Salaam.
Pia katika maisha yake alisomea Uandishi wa Habari na Utangazaji huko Kenya miaka ya 70. Aliporejea Tanzania alifanya kazi katika Kitengo cha Habari Baraza la Maaskofu Tanzania.
Katika hotuba zao walioongea hapo kanisani Rubya baada ya Misa akiwemo Askofu Kilaini na Padre Faustine Kamugisha(Paroko Minziro) walimwelezea marehemu Padre Irene kama mtu aliyekuwa mcheshi na mtu mwema wa kuishi naye.
Padre Faustine Kamugisha alipopata nafasi ya kuongea alisimulia mengi kuhusiana na maisha ya marehemu wakati wa uhai wake hapo Minziro, kuugua kwake alivyopelekwa Hospitali ya Kajunguti, baadae kurudishwa Minziro na hatimaye kupelekwa hospitalini Mugana ambako alifia. Haya yote yametendeka kwa kipindi kifupi sana. Padre Faustine amekabidhi shilingi 200,000/= kwa Askofu Rwoma kama rambirambi ya Parokia ya Minziro kwa Baba Askofu. Waliotoa rambilambi wengine ni Umoja wa Mapadre ambao walikabidhi bahasha ya pesa kwa mwakilishi wa familia ya marehemu Bwana Richard Muyungi, ingawa kiwango cha pesa hakikutajwa.
Askofu Kilaini wakati wa kutoa neno lake alitoa maneno ya rambirambi Kutoka kwa mapadre kadhaa wa Dar es Salaam na maaskofu mbalimbali kutoka majimbo ya Tanzania.
Askofu Alimachius Rweyongeza naye alitoa neno lake la pole kwa wafiwa na rambirambi kwa Askofu Rwoma.
Msemaji wa familia ya marehemu Bwana Richard Muyungi katika neno laki alisema kuwa Padre Ireneus ameiinua familia yao. Maneno hayo yamedhihirishwa na uchungu ulioonyeshwa na baadhi ya wanafamilia wakati wa kushuhudia na kumuaga marehemu na kutoa mchango misa. Wanafamilia wengine walipiga mayowe na wengine kutolewa nje na kuzimia.
Katika kushughulikia mwili wa marehemu hapo kanisani Sr, na muhudumu mwingine kutoka hospitalini Mugana na pia mapadre wa Seminari waliobeba mwili wa marehemu kuuweka kwenye gari baada ya misa hapo kanisani kuupeleka makabulini walivalia barakoa.
Kutoka Minziro lilikuwa ni kundi kubwa la watu. Minziro walikuja na kikundi cha kwaya ambacho kilikuwa kimevalia nguo nyekundu. Kilipata nafasi ya kuimba wimbo mmoja wakiganda baada ya komunyo.
Kaburi alimozikwa marehemu Padre Irene lilikuwa limejengwa vyema. Kuweka udongo ilikuwa ni kupitia wawakilishi.
Mapadre waliwakilishwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Mapadre jimboni Pd Paschal Mutegaya, Pd Adeodatus RWEHUMBIZA (Chancellor), maaskofu, masista wakuu wa Mashirika na baadhi ya wanafamilia akiwemo Pd Benezeth Rwegoshora, Achilleus RWEHUMBIZA, Sr Amelberga, na Sr Praxeda.
Baada ya shughuli za mazishi hapo makaburini kulifuatia huduma ya chakula kwa maaskofu, mapadre, masista na wanafamilia.
Shughuli ya mazishi imemalizika majira ya saa nane kasoro dakika mbili mchana. Hapo kesho majira ya saa tano asubuhi itasaliwa misa ya kuanua matanga nyumbani kwao Igurugati kwa Mzee Nazari marehemu babake. Na Pd Charles RWEHUMBIZA.