Kagera: Mama aliyefariki na wanaye wanne katika ajali yadaiwa alikuwa akimkimbia mume wake

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,266
5,364
WATU wanane waliokufa kwenye ajali ya gari wilayani Biharamulo mkoani Kagera wakiwemo watano wa familia moja wamezikwa katika Kijiji cha Nyamalagala, Kata ya Lusahunga wilayani Biharamulo mkoani Kagera.

Diwani wa Kata ya Lusahunga, Amos Madebwa alisema kijiji hicho kimepata simanzi kwa kupoteza watu wanane akiwemo mama na wanawe wanne.

Madebwa alisema taarifa alizozipata kwa majirani na marafiki wa karibu wa familia ni kuwa mama huyo, Jesca Leonard (45) alitoroka usiku na wanawe ili kumkimbia mumewe mwenye miaka 80 kutokana na masuala ya kifamilia.

Alisema Jesca hakuacha mtoto nyumbani kwa kuwa mwaka jana alifiwa na mtoto akabaki na watoto wanne ambao amekufa nao kwenye ajali.

"Majirani wanasema mama aliwakimbiza watoto kwenda Ngara ili kuepukana na ugomvi na mumewe ambaye kwa sasa ana miaka 80,” alisema.

Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, William Mwampaghale alisema jana kuwa ajali hiyo ilitokea Julai 11 saa moja usiku, eneo la Busiri, barabara kuu ya kutoka Lusahunga kwenda Kata ya Nyakahura wilayani Biharamulo.

Waliokufa ni Nyawenda Bihela (35), dereva na mmiliki wa gari dogo, Michael Charles (28) na Majaliwa Kanundo (32) ambao walikuwa wasindikizaji.

Watoto waliokufa na mama yao wakienda Benaco wilayani Ngara ni Margaret Sekanabo (14), Adidas Sekanabo (12), Zabron Sekanabo (6) na Vestina Sekanabo (4).


Chanzo: Habari Leo

Pia soma: Kagera: Ajali yaua watu nane wakiwemo watano wa familia moja Julai 12, 2022
 
Huyo babu sekanabo miaka 80 ni kikongwe na ana ule uchawi kutoka congo au kigoma. ILA NI MPUMBAVU MAANA ATAKUFA KWA UZEE SIKU CHACHE ZIJAZO NA UCHAWI WAKE. Huyo mama marehemu naye ni mpumbavu. Unakimbiaje na watoto wote ilhali ulikubali mwenyewe kuolewa na babu wakati bado msichana? Hapo huzuni ni hao watoto tu.
 
Huyo babu sekanabo miaka 80 ni kikongwe na ana ule uchawi kutoka congo au kigoma. ILA NI MPUMBAVU MAANA ATAKUFA KWA UZEE SIKU CHACHE ZIJAZO NA UCHAWI WAKE. Huyo mama marehemu naye ni mpumbavu. Unakimbiaje na watoto wote ilhali ulikubali mwenyewe kuolewa na babu wakati bado msichana? BORA AMEKUFA. Hapo huzuni ni hao watoto tu.
Mkuu kwako neno upumbavu ni salamu eeh?
 
Huyo babu sekanabo miaka 80 ni kikongwe na ana ule uchawi kutoka congo au kigoma. ILA NI MPUMBAVU MAANA ATAKUFA KWA UZEE SIKU CHACHE ZIJAZO NA UCHAWI WAKE. Huyo mama marehemu naye ni mpumbavu. Unakimbiaje na watoto wote ilhali ulikubali mwenyewe kuolewa na babu wakati bado msichana? BORA AMEKUFA. Hapo huzuni ni hao watoto tu.

Duuh hizi lugha hizi
 
Una uhakika kama huyo mzee ni mchawi? Usihukumu ndugu
Huyo babu sekanabo miaka 80 ni kikongwe na ana ule uchawi kutoka congo au kigoma. ILA NI MPUMBAVU MAANA ATAKUFA KWA UZEE SIKU CHACHE ZIJAZO NA UCHAWI WAKE. Huyo mama marehemu naye ni mpumbavu. Unakimbiaje na watoto wote ilhali ulikubali mwenyewe kuolewa na babu wakati bado msichana? BORA AMEKUFA. Hapo huzuni ni hao watoto tu.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom