Mwanawangurumo
Senior Member
- Nov 19, 2012
- 105
- 15
Jana majira ya asubuhi kabla kura hazijapigwa katika kata ya Kibeta manispaa ya Bukoba waliokuwa wagombea kupitia CCM katika vijiji vitatu walijiudhuru asubuhi hyo na kufanya wagombea wa CHADEMA kupita bila kupingwa na wasimamizi wakarudisha vifaa kwa msimamizi mkuu.
Kwa kweli Bukoba CCM imekuwa bidhaa adimu sana. Mitaa karibia yote manispaa wamebeba UKAWA.
Unajua kilicho fanyika Huko Nyakiziba Wilaya ya Ngara, huyo mtendaji wa kata ni wa ccm, walipo toa form za kujaza akawaelekeza wagombea wote kujaza vibaya hizo form baadaye akawaita wale wa ccm akazirekebisha, halafu wale wa Chadema akawa wekea pingamizi, ndipo wakasema kuwa wamepita bila kupingwa, wananchi waka waeleza wale wenyeviti wa ccm walio pita bila kuingwa kuwa wakatafute watu wa kuwaongoza, ila sio kwenye vitongoji hivyo maana wao hawaja wachagua, wakienda kwenye nyumba yoyote kudai chochote, atakutana na Panga au Mshale. Ndiyo maana wale jamaa wakaona huu mziki mkubwa sana wakatangaza kuachia ngazi. Chezea wahangaza wewe. NGARA ccm wameangukia pua