Kunguru Mjanja
JF-Expert Member
- Aug 22, 2012
- 2,036
- 3,929
Mbunge wa Kishapu (CCM), Suleiman Nchambi na viongozi watatu wa mgodi wa Stamigold ulioko Tulawaka wilayani Biharamulo mkoani Kagera, wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa.
Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Wilaya ya Biharamulo, Hassan Mosi amesema mbunge huyo na wenzake walikamatwa na kuwekwa rumande katika gereza la wilaya hiyo Jumamosi Agosti 4, 2018.
Amesema leo Jumatatu Agosti 6, 2018 watafikishwa mahakama ya wilaya ya Biharamulo kwa kosa la kufanya miamala ya kupokea rushwa.
Mosi amesema kitendo hicho ni kinyume na kifungu cha15 cha sheria namba 11 ya mwaka 2007 ya kupambana na kuzuia rushwa.
"Wakifikishwa mahakamani watasomewa mashtaka yanayowakabili. Wanaweza kukiri au kukanusha na sheria itachukua mkondo wake,” amesema.
Ndugu, jamaa na marafiki leo wamejitokeza kwa wingi katika mahakama hiyo, huku wengi wakionekana kuwa na shauku ya kujua hatima ya viongozi hao.
=====
Mbunge wa Kishapu (CCM) Suleiman Nchambi na wenzake 10 wamefikishwa katika mahakama ya wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera wakishtakiwa kwa kosa la kujihusisha na vitendo vya rushwa.
Wakizungumza mahakamani leo Jumatatu Agosti 6, 2018 waendesha mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dismas Muganyizi na Joseph Mulebya wamesema watuhumiwa hao walifanya miamala ya rushwa kinyume na kifungu cha 15 cha sheria namba 11 cha mwaka 2007 ya taasisi hiyo.
Amesema watuhumiwa hao kwa nyakati tofauti katika mgodi wa Stamigold ulioko wilayani Biharamulo kati ya Septemba 2015 hadi Oktoba 2016 walitenda kosa la kufanya miamala ya rushwa na kuvunja kifungu cha 15(1) (a&b) cha sheria namba 11 ya mwaka 2007 ya kupambana na kuzuia rushwa.
Mbele ya hakimu wa mahakama hiyo, Flora Ndale, Muganyizi amewataja washtakiwa hao kuwa ni Clara Mwaikambo, Chacha Wambura, Christopher Mwinuka, Sadick Kaswia, Fortunatus Rulemeja, Reginald Haule, Yasini Mohammed, Fabian Ngelela , Felician Edward, Braithony Luchagula na Nchambi.
Amesema Nchambi na Mohammed, Oktoba 2016 walifanya muamala wa rushwa na kumpatia Sh5 milioni mhasibu wa Stamigold co. Ltd ambaye ni Clara kama zawadi ya kupatikana malipo yao ya dola 170,945 za Marekani walizokuwa wakidai katika machimbo ya mgodi huo.
Washtakiwa hao wamekana mashtaka hayo na kuachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya dhamana ya kuwa na wadhamini wawili wenye hati ya mali isiyohamishika yenye thamani ya Sh10milioni, huku mmoja akiwa mtumishi wa umma.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 3, 2018 itakapotajwa tena.
Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Wilaya ya Biharamulo, Hassan Mosi amesema mbunge huyo na wenzake walikamatwa na kuwekwa rumande katika gereza la wilaya hiyo Jumamosi Agosti 4, 2018.
Amesema leo Jumatatu Agosti 6, 2018 watafikishwa mahakama ya wilaya ya Biharamulo kwa kosa la kufanya miamala ya kupokea rushwa.
Mosi amesema kitendo hicho ni kinyume na kifungu cha15 cha sheria namba 11 ya mwaka 2007 ya kupambana na kuzuia rushwa.
"Wakifikishwa mahakamani watasomewa mashtaka yanayowakabili. Wanaweza kukiri au kukanusha na sheria itachukua mkondo wake,” amesema.
Ndugu, jamaa na marafiki leo wamejitokeza kwa wingi katika mahakama hiyo, huku wengi wakionekana kuwa na shauku ya kujua hatima ya viongozi hao.
=====
Mbunge wa Kishapu (CCM) Suleiman Nchambi na wenzake 10 wamefikishwa katika mahakama ya wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera wakishtakiwa kwa kosa la kujihusisha na vitendo vya rushwa.
Wakizungumza mahakamani leo Jumatatu Agosti 6, 2018 waendesha mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dismas Muganyizi na Joseph Mulebya wamesema watuhumiwa hao walifanya miamala ya rushwa kinyume na kifungu cha 15 cha sheria namba 11 cha mwaka 2007 ya taasisi hiyo.
Amesema watuhumiwa hao kwa nyakati tofauti katika mgodi wa Stamigold ulioko wilayani Biharamulo kati ya Septemba 2015 hadi Oktoba 2016 walitenda kosa la kufanya miamala ya rushwa na kuvunja kifungu cha 15(1) (a&b) cha sheria namba 11 ya mwaka 2007 ya kupambana na kuzuia rushwa.
Mbele ya hakimu wa mahakama hiyo, Flora Ndale, Muganyizi amewataja washtakiwa hao kuwa ni Clara Mwaikambo, Chacha Wambura, Christopher Mwinuka, Sadick Kaswia, Fortunatus Rulemeja, Reginald Haule, Yasini Mohammed, Fabian Ngelela , Felician Edward, Braithony Luchagula na Nchambi.
Amesema Nchambi na Mohammed, Oktoba 2016 walifanya muamala wa rushwa na kumpatia Sh5 milioni mhasibu wa Stamigold co. Ltd ambaye ni Clara kama zawadi ya kupatikana malipo yao ya dola 170,945 za Marekani walizokuwa wakidai katika machimbo ya mgodi huo.
Washtakiwa hao wamekana mashtaka hayo na kuachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya dhamana ya kuwa na wadhamini wawili wenye hati ya mali isiyohamishika yenye thamani ya Sh10milioni, huku mmoja akiwa mtumishi wa umma.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 3, 2018 itakapotajwa tena.