hivi ndo huyo kiongozi mpya anayepeleka chama kwenye uongozi 2012?kigogo wa kwanza ni kinanda haiwezekani ana kampuni ya meli asijue amebeba nini,huyu ni mzoefu kwenye hii deal ya pembe za ndovu!!!napata uchungu sana ninapomuona mtu anayeshabikia haya magamba bila kujua muda si mrefu watoto wetu watamsoma tembo kama historia kama ilivyo kwa wale dinosor!!
Hapa Mkuu umenikumbusha niliwahi kutoa tadhari kuwa Prof. Muhongo yatamshinda sasa keshapoata doa kabla hata ya muda wa kutosha. Halafu pia umenikumbusha kuhusu Prof. Mama Tibaijuka naye aliingia na gear kali ya kutaka hata kurejesha open spaces zilizovamiwa na kuuziwa wafanyabiashara. Nakumbuka alikuja na slogan safi kuwa kama ni senti ya kula anayo na hategemei kuhongeka, au sijui niliisoma vibaya? Ila sasa yuko kimya labda anachapa kazi! Sina sababu ya kukata tamaa sana labda tungojee tuone. Loh! Tanzania, nchi yangu inashangaza ndugu zangu. Isije ikawa ni matokeo ya nchi iliyopatikana kwa muungano wa kusadikika ambao mfano wa pili duniani haupo? SITAKI iwe hivyo!
sasa kama umeshaambiwa mzigo kampuni yake ilshaukagua na ikaona kabisa hapo kuna alizeti sasa kosa liko wapi hapo?? na TRA wamekagua wakaona ni alizeti sasa kosa liko wapi hapo?? meli ya kwanza ilikamatiwa hongkong kweli ilikuwa meli ya kinana naye alikiri hilo miezi mingi iliyopita lakini hili la pili meli iliyokamatwa meno yakiwa na alizeti meli siyo yake jamani eleweni meli iliyokamatwa si ya kinana ni ya kampuni ya dubai sasa kama ni hivo mnavyosema basi uongozi wa dubai nao ni wa kulaumiwa mana ni wazembe kama TRA wetu hapa mana makontena yalishushiwa dubai yakapakiwa kwenye meli nyingine hapo dubai na ukaguzi ukafanywa hapo dubai sasa basi mamlaka za dubai nao wazembe kama zilivyo mamlaka za bongo!!.
Basi na mamlaka ya dubai inahusika pia na hili la kusafirisha meno ya tembo!! narudia tena meli iliyobeba mzigo dubai ilikuwa ni 2nd transporter ina maana nao ni wazembe kupakia mzigo wasoujua ndani kuna nini?? na TRA ya dubai nao ni wazembe kwa kuruhusu mzigo kama huo kushushwa na kupakiwa ndani ya dubai??
Eleweni hiyo meli ya dubai ilikagua mzigo na mamlaka za dubai zilikagua mzigo pia zikauruhusu uondoke,mkae mkijua mzigo wenyewe ulifichwa sana si rahisi kuujua labda mtu akuchome kwa watu au interpol ndio unaweza kujua kuwa ndani kuna nini hivi hivi bila fore-knowledge huwezi kuhisi kitu chochote kile.
musilete vitu sababu ya chuki kisa yuko ccm basi kila kitu anatupiwa yeye na uliza tena mbona GODBLESS LEMA ni haramia anayepora magari ya wa2 na kuuza madawa ya kulevya mbona ccm hawaisemi vibaya cdma kwa hilo??
kinana hana makosa yeyote yale ni chuki zeenu tu hizo kisa yuko ccm,au sababu yeye ni muislamu na GODBLESS LEMA ni MCHUNGAJI??????
acheni utoto nyie kwani uiwa na dala dala yako ikakamatwa kwa kuiba route au kuvunja sheria yeyeote barabarani unatakiwa ukamatwe au kuhukumiwa wewe?heb tuache ushabiki na tuwe fair sometimes
Hapo lazima JK, Kagasheki na vigogo wengine wana gawio lao. Haiwezekani upuuzi wa hali ya juu hivi ufanyike bila JK kujua wakati ana vyombo vykumfanya ajue. Tembo zaidi ya 200 wanauawa usalama wa taifa hawana habari!!! Wale twiga waliotoroshwa na ndege ya Qatar? Hawakujua kuna tatizo? Lazima wanajua kinachoendelea na kwa vile yalibebwa kwenye meli ya katibu mkuu wa ccm ni dhahiri hawa vigogo wa ccm wanajua dili hili au ni wahusika moja kwa moja. Kama walichota fedha EPA, kuficha mabilioni nje, kuingiza nchi gizani ili wapate tenda za Tanesco, kuleta richmond na kashfa zingine kibao. Cha ajabu ni nini?
Hii nchi inaongozwa na waendawazimu.
inaonekana kinana ni mwizi
mkubwa hapa duniani ...tunaomba intelijensia ya CDM imfatilie huyu ili
watanzania wengi waju