Ngongo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2008
- 18,921
- 31,161
NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani ambaye pia ni Mbunge wa Bukoba Mjini, Hamis Kagasheki, ametangaza kutogombea ubunge katika uchaguzi mkuu mwakani.
Akizungumza na Tanzania Daima Jumatano hivi karibuni mkoani Kigoma, kabla ya kuanza kwa ziara ya kukagua kambi mbalimbali za wakimbizi ambazo zimefungwa na zinazohitajika kufungwa kutokana na nchi walizotoka kwa sasa kuwa na hali ya utulivu, alisema hatogombea tena ubunge kwa sababu ana mambo mengi ya kufanya.
Kagasheki ambaye katika uchaguzi wa mwaka 2005 alipata ushindani mkubwa kutoka kwa aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Bara wa Chama cha Wananchi (CUF), Wilfred Lwakatare, alisema hawezi kufanya kazi kwa presha huku kukiwa na kazi nyingine za kufanya ambazo hazina presha.
Alisema anaweza kuwa mtumishi mzuri wa jamii iwapo atafanya kazi bila msukumo kuliko hivi sasa akiwa mbunge ambapo amekuwa akiishi kwa presha.
Kwa kweli ubunge sigombei tena, hiyo ni kazi ya presha, kila wakati unakuwa roho juu, lakini nimeona kuna kazi nyingine ambayo pia naweza nikafanya ya kuhudumia jamii bila ya kuwa na presha kama hii ambayo kwa sasa naifanya, alisema Kagasheki.
Alisema baada ya kumaliza kipindi chake cha ubunge mwaka 2010, atafanya shughuli nyingine ambazo ni muhimu kwa taifa, na kwamba atajitolea kuhudumia jamii kupitia kazi nyingine na si ubunge.
Akizungumzia kuhusu kuzagaa kwa silaha katika Mkoa wa Kigoma, hasa katika Wilaya ya Kibondo, alisema kuwa watajipanga kuhakikisha kuwa kunadhibitiwa.
Aidha, alikiri kuwapo na ukosefu wa vitendea kazi akitolea mfano wa magari, mafuta pamoja na vituo vya polisi, ambapo alikiri inaweza ikawa sababu kubwa ya kuongezeka kwa matukio ya ujambazi.
Source: Tanzania Daima.
Bila shaka Kagasheki amesoma alama za nyakati.
Si siri Wilfred Lwakatare wa CUF anakubalika zaidi Bukoba mjini kama si nguvu za dola kutumika vibaya Bwana Kagasheki asingekuwa mbunge.
Akizungumza na Tanzania Daima Jumatano hivi karibuni mkoani Kigoma, kabla ya kuanza kwa ziara ya kukagua kambi mbalimbali za wakimbizi ambazo zimefungwa na zinazohitajika kufungwa kutokana na nchi walizotoka kwa sasa kuwa na hali ya utulivu, alisema hatogombea tena ubunge kwa sababu ana mambo mengi ya kufanya.
Kagasheki ambaye katika uchaguzi wa mwaka 2005 alipata ushindani mkubwa kutoka kwa aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Bara wa Chama cha Wananchi (CUF), Wilfred Lwakatare, alisema hawezi kufanya kazi kwa presha huku kukiwa na kazi nyingine za kufanya ambazo hazina presha.
Alisema anaweza kuwa mtumishi mzuri wa jamii iwapo atafanya kazi bila msukumo kuliko hivi sasa akiwa mbunge ambapo amekuwa akiishi kwa presha.
Kwa kweli ubunge sigombei tena, hiyo ni kazi ya presha, kila wakati unakuwa roho juu, lakini nimeona kuna kazi nyingine ambayo pia naweza nikafanya ya kuhudumia jamii bila ya kuwa na presha kama hii ambayo kwa sasa naifanya, alisema Kagasheki.
Alisema baada ya kumaliza kipindi chake cha ubunge mwaka 2010, atafanya shughuli nyingine ambazo ni muhimu kwa taifa, na kwamba atajitolea kuhudumia jamii kupitia kazi nyingine na si ubunge.
Akizungumzia kuhusu kuzagaa kwa silaha katika Mkoa wa Kigoma, hasa katika Wilaya ya Kibondo, alisema kuwa watajipanga kuhakikisha kuwa kunadhibitiwa.
Aidha, alikiri kuwapo na ukosefu wa vitendea kazi akitolea mfano wa magari, mafuta pamoja na vituo vya polisi, ambapo alikiri inaweza ikawa sababu kubwa ya kuongezeka kwa matukio ya ujambazi.
Source: Tanzania Daima.
Bila shaka Kagasheki amesoma alama za nyakati.
Si siri Wilfred Lwakatare wa CUF anakubalika zaidi Bukoba mjini kama si nguvu za dola kutumika vibaya Bwana Kagasheki asingekuwa mbunge.
Last edited by a moderator: