Kagame ni mpenda Nchi yake na hana ubia na urais wake

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Salaam toka Kigali hapa mjini Rwanda.Niko hapa tangia leo asubuhi .Lakini sijaja nilikuwa kule Burundi .Nimekuwa na maongezi na Askofu wa Jimbo moja Katoliki hapa kujua ukweli wa mauaji ya wakati ule .

Baadaye nimevutiwa na Rwanda kutokana na hadithi za Kagame kuambiwa shemeji yake aliyemuoa Dada yake Kagame alitaka kujifanya na yeye ni Kagame wa eneo hilo .Wakubwa wakaogopa kumkamata kwa kuwa alikuwa anatumia jina la Kagame kufanya ujinga wake na hata tender serikalini na ushenzi zaidi .

Wakaniambia Kagame akapewa taarifa akaamuri akamatwe awekwe ndani then apelekewe funguo .Jamaa alikamatwa na funguo ikapelekwa kwa Kagame na yeye akai flash chooni akasema nione sasa wa kumtoa .Ina maana hata chakula akawa hawezi kupata tena .

Baada ya siku 4 mkewe alilia sana mbele za Kagame na Kagame akasema vunjeni atoke na aletwe hapa .ikafanyika na jamaa akapelekwa na kuambiwa next time utapotea hii ni Nchi si ukoo wala ushemeji .

Likaja soo la kugawana ardhi .Wale waliokuwa na Kagame msituni wengine wame staafu walijichukuliwa maeneo na kuishi bila wasi wasi .Kagame akasema ardhi sasa igawiwe kwa wote bila kujali mtu .Kweli likafanyika ila wale ma general na wakubwa wengine wakawa hawaguswi.Kagame akauliza anaambiwa wale ni wapiganaji wako nk .

Akaenda mwenyewe akasimamia uhawaji na hakuna kilicho endelea hadi leo Kagame anachapa mzigo .

Njoo Kigali uone usafi wa barabarani .Njoo uulizie ama ujifanye wataka kutoa hongo upate huduma ama unaomba .Kagame kama China anaua na siku chache Rwanda inategemewa kuwa mbali sana .

Nauliza sisi na hao wazee wa amani na utulivu na kulindana tutakuwa lini kama Kagame ?
 
Mkuu Lunyungu,

shukrani nyingi kwa hiyo taarifa. Unajua hapo nyuma tuliwahi kuelezea utendaji wa huyu bwana ulivyo murua.........naona ziara yako imethibitisha hilo,.........enjoy your holiday Mkuu
 
Heshima mbele!
Mi nafikiri Kagame ni "dictator" with positive visions, Rwanda ni nchi ndogo sana yenye watu wachache but with very limited/little resources ukilingalisha na Tanzania yenye kumiminika asali na maziwa ila mikondo imepindiswa na kupita kwa wajanja wachache. Mi nafikiri tunahitaji positive dictator ambaye mishipa ya aibu ilishaziba/kukatika ili akate mirija yooote ya hawa MaFis.........ahadi.
 
Mkuu afadhali umelileta hili huo ndio ukweli kuhusu Kagame, halafu vipi infrastructure Mzee nasikia kuhusu Mtandao wa Computer si haba Rwanda, alisimamia yeye mwenyewe, na wataalamu kutoka bongo.
 
..hivi maafa aliyosababisha Congo ambapo wananchi million 2 wameuawa hayawasumbui??

..wale wakimbizi waliotokana na vita vya Congo wameitia hasara Tanzania kiasi gani?

..mimi naona Kagame ni KERO na MKOSI mkubwa kwa eneo la maziwa makuu.
 
Mauji ? haya nadhani sasa hayatuhusu.Migogoro ipo na hata sisi tuna mgogoro na Zanzibar na hata kuwakamata usiku .Vipi mkuu ? Halikusumbui ?
Naomba ujue kwamba kila kitu kina magumu yake .Kagame tunamsifia kwa hili la sasa na si ya nyuma .Ya nyuma atahukumiwa nayo lakini sisi tuna angalia sasa nia na maendeleo ya Nchi bada ye yeye kuchukua madaraka .

Nasema na narudia tena kuanza barabara , majengo , mawasiliano yamesimama.Nimeongea na binti mmoja ni mwanafunzi wa University hapa na anasoma Accounting na Finance , kanipa picha nzima na wanampenda Kagame.Ubaya ni kwamba Kagame akifa Nchi itarudi nyuma kwenye machafuko .Kagame baada kuingia madarakani aliwaambia washikaje wake waheshimu madaraka ama wakae pembeni .

Ukikamatwa kwa rushwa ama kujihusisha Kagame hana mjadala .Utawala mwingine ni wa sheria .

Narudia niliyo ambiwa nafuatilia kwa kiwangi niwezacho hadi sasa sijaona uongo.Kwanza usafi hapa Kigali huwezi kulinganisha na Dar .Lami inaonekana na watu wana ustaarabu wa kutupa vitu hovyo .

Nangoja ngoma hii kwa wireless naweza kutuma documents na kupokea kwa speed ya kawaida .Je wireless za nyumbani zinafanya haya ? Jiulize .

Kila kona watu wanaimba Kagame ni mpenda Nchi .
 
sina tatizo na ushujaa wakagame, tatizo langu ni kuwa ameiandaa rwanda kwa mabdiliko ya uongozi? isje ikawa bila yeye hakuna rwanda. manake mnaelewa kuwa urais si mtu ni taasisi. hata hivyo mugabe angebidi aletwe hapo apigwe shule kuhusu uswahiba wake na maveterani. hatutegemei kuwa ukipigana vita ukaikomboa nchi na wewe ubadilike kuwa mkoloni wa pili
 
sina tatizo na ushujaa wakagame, tatizo langu ni kuwa ameiandaa rwanda kwa mabdiliko ya uongozi? isje ikawa bila yeye hakuna rwanda. manake mnaelewa kuwa urais si mtu ni taasisi. hata hivyo mugabe angebidi aletwe hapo apigwe shule kuhusu uswahiba wake na maveterani. hatutegemei kuwa ukipigana vita ukaikomboa nchi na wewe ubadilike kuwa mkoloni wa pili

Mbona watanzania mnaogopa ku suggest JK aende akapigwe shule ? Kama ufisadi huu unatokea Tanzania ungalitokea Rwanda ndiyo mngalijua Kagame ni nani .Yeye hasemi anatenda na hahitaji magazeti wala nini kama JK .Sasa hivi naambiwa ana waanda wanyarwanda kuchukua Nchi ila anataka wale wanao amini kwamba uswahiba hautakiwi kazini .
 
huy wa kwetu jk, sidhani kama ameshafikia viwango hata vya kuletwa huko, kwa kuwa haeleweki yeye yuko mrengo gani, ytupo yupo tu. tunaambiwa kuwa huyu bwana kagame kwa jinsi anavyoiandaa nchi yake, tayari hata kijeshi ni tishio kwa maziwa makuu. sasa huyu wa kwetu tumsifie kwa lipi? jeshi imara? uchumi imara? demokrasia ya kweli? serikali yenye nidhamu? ndo maana wala simzungumzii
 
huy wa kwetu jk, sidhani kama ameshafikia viwango hata vya kuletwa huko, kwa kuwa haeleweki yeye yuko mrengo gani, ytupo yupo tu. tunaambiwa kuwa huyu bwana kagame kwa jinsi anavyoiandaa nchi yake, tayari hata kijeshi ni tishio kwa maziwa makuu. sasa huyu wa kwetu tumsifie kwa lipi? jeshi imara? uchumi imara? demokrasia ya kweli? serikali yenye nidhamu? ndo maana wala simzungumzii

Mkuu Mwikimbi JK anatakiwa akapewe somo la namna ya kuumaliza hasa uswahiba na wezi wa mchana ambao wanamzunguka angalau maana yuko gizani ama anajua anatuchezea .
 
mkuu lunyungu, wezi au watu wanaoshirikiana na wezi ni wezi na mahali peke yake wanaweza kupata somo la uhakikia ni segerea! na kama katika kuiba wamewahi pia kuua au kusababisha mauaji ni kule the hague au arusha, siyo kigali.
 
Kwa hiyo mauaji yamejiondokea siku hizi Rwanda? Hata hivyo bado alijiingiza Kongo na kuiba hili bado litampa hukumu kwa kuiba madini Kongo na kuua watu ovyo huko kwa visingizio mbalimbali. Hata yeye na mwenziye Nkunda wanatakiwa wapelekwe korti ya the Hague
 
..............WAKUU NCHI HAIENDI BILA KUWEKA DEMOKRASIA KWA WINGI KWENYE MAMBO YA MSINGI ....NA MAMBO YANAYOHUSU PUBLIC INTEREST LAZIMA UWEKE KAU DICTATOR KIDOGO......

.......THE PRESIDENT CAN SELDOM FULLY EXERCISE HIS TOTAL POWERS WITHOUT AT SOME INCIDENCES BEING SMALL DICTATOR ...HATA KWA MUDA MFUPI AU KWA SIRI!!!!.....AND AT THOSE TIMES WHERE HE PRACTICE SMALL DOCTORSHIP[Assisted by the SECRET SERVICE] LAZIMA ALINDWE NA USIRI...AS NOT TO DISTORT HIS PUBLIC IMAGE OR POPULARITY

....kwa mfano mimi ningelikuwa president ...baada ya kuwajua mafisadi singekuwa na kazi ngumu..tena kabla ya kuwatangazia wananchi kuwa kuna ufisadi ..ningeshika mmoja mmoja bila hata wake zao kujua wako wapi.....ningewabana watoe pesa kimya kimya ..na wasaini ku release assets zao kimya kimya ...after that ningeweka nao deal kuwa wakae kimya....ningewaachia na kuendelea kuwafanyia monitoring ...PESA ZINGERUDI ZOTE!!!.....sasa sometimes ukitaka kudai hizi pesa hadharani ..kuna issue za haki za binadamu na mikataba mingine inayozuia kutaifisha mali za watu bila kuwa na vivid evidences.....SIDHANI KAMA PESA ZA EPA ZIMERUDI ...I BET ITS JUST POLITICS!!!
 
ebwana eeeh

hii itakuwa off topic na naomba mniwie radhi

Ebwana hebu kwanza niambie kuhusu mademu wa Kinyarwanda

hayo mambo ya siasa mie yeshanshinda
 
kagame yuko siliasi sana naweza kusema baada ya kuchukua madaraka na kuonyesha hilo kuna watu wengi wataalamu wameondoka kwenye nchi yetu ya kinafiki na kuelekea Rwanda nawajua wengi wanaofanya vizuri sana huko.
 
Salaam toka Kigali hapa mjini Rwanda.Niko hapa tangia leo asubuhi .Lakini sijaja nilikuwa kule Burundi .Nimekuwa na maongezi na Askofu wa Jimbo moja Katoliki hapa kujua ukweli wa mauaji ya wakati ule .

Baadaye nimevutiwa na Rwanda kutokana na hadithi za Kagame kuambiwa shemeji yake aliyemuoa Dada yake Kagame alitaka kujifanya na yeye ni Kagame wa eneo hilo .Wakubwa wakaogopa kumkamata kwa kuwa alikuwa anatumia jina la Kagame kufanya ujinga wake na hata tender serikalini na ushenzi zaidi .

Wakaniambia Kagame akapewa taarifa akaamuri akamatwe awekwe ndani then apelekewe funguo .Jamaa alikamatwa na funguo ikapelekwa kwa Kagame na yeye akai flash chooni akasema nione sasa wa kumtoa .Ina maana hata chakula akawa hawezi kupata tena .

Baada ya siku 4 mkewe alilia sana mbele za Kagame na Kagame akasema vunjeni atoke na aletwe hapa .ikafanyika na jamaa akapelekwa na kuambiwa next time utapotea hii ni Nchi si ukoo wala ushemeji .

Likaja soo la kugawana ardhi .Wale waliokuwa na Kagame msituni wengine wame staafu walijichukuliwa maeneo na kuishi bila wasi wasi .Kagame akasema ardhi sasa igawiwe kwa wote bila kujali mtu .Kweli likafanyika ila wale ma general na wakubwa wengine wakawa hawaguswi.Kagame akauliza anaambiwa wale ni wapiganaji wako nk .

Akaenda mwenyewe akasimamia uhawaji na hakuna kilicho endelea hadi leo Kagame anachapa mzigo .

Njoo Kigali uone usafi wa barabarani .Njoo uulizie ama ujifanye wataka kutoa hongo upate huduma ama unaomba .Kagame kama China anaua na siku chache Rwanda inategemewa kuwa mbali sana .

Nauliza sisi na hao wazee wa amani na utulivu na kulindana tutakuwa lini kama Kagame ?

Ulichoandika ni kweli tupu. Mimi nina marafiki zangu wanyarwanda na warundi kwa kweli wote wanamsifia sana huyu jamaa kwa kuleta mabadiliko ya kweli Rwanda. Wananchi wanafurahia hali hiyo na kuridhika na uongozi wake.

Je, kwa nini anayofanya Kagame Rwanda yasiwezekane Tanzania? Kwanini JK anaendelea kuwalinda na kuwaogopa mafisadi? Kwanini pamoja na kuwa Tanzania ni nchi ya 'amani' na tuna utajiri mkubwa kuliko Rwanda lakini Watanzania hatuoni positive changes zozote kuhusiana na maisha ya Watanzania walio wengi? Kwanini kila kukicha asilimia kubwa ya Watanzania wanaona maisha yanazidi kuwa magumu na wengine kushindwa hata kugharamia mlo mmoja na maendeleo ya familia zao? Kwa nini chama cha mafisadi wanang'ang'ania madarakani wakati uongozi wa kuwaongoza Watanzania umewashinda?
:(:(
 
Hakosoleki Kagame wetu. Havumilii maoni ya upande wa pili. Anayoyasimamia hayatakuwa endelevu kwa kuwa Uraisi kwake sio TAASISI; ni yeye mwenyewe.
 
Ulichoandika ni kweli tupu. Mimi nina marafiki zangu wanyarwanda na warundi kwa kweli wote wanamsifia sana huyu jamaa kwa kuleta mabadiliko ya kweli Rwanda. Wananchi wanafurahia hali hiyo na kuridhika na uongozi wake.

Je, kwa nini anayofanya Kagame Rwanda yasiwezekane Tanzania? Kwanini JK anaendelea kuwalinda na kuwaogopa mafisadi? Kwanini pamoja na kuwa Tanzania ni nchi ya 'amani' na tuna utajiri mkubwa kuliko Rwanda lakini Watanzania hatuoni positive changes zozote kuhusiana na maisha ya Watanzania walio wengi? Kwanini kila kukicha asilimia kubwa ya Watanzania wanaona maisha yanazidi kuwa magumu na wengine kushindwa haya kugharamia mlo mmoja na maendeleo ya familia zao? Kwa nini chama cha mafisadi wanang'ang'ania madarakani wakati uongozi wa kuwaongoza Watanzania umewashinda?
:(:(


Mkuu sikuandika haya kwa kuwa nimetaka kuandika nimeandika baada ya kuwa nimehudhuria mkutano mmoja wa usuluhishi na kuwekeza Nchi Burundi ulio fanyika mwezi uliopita Ulaya .Huko nikautana na Askofu Mkatoliki toka Burundi tukasema sana na kusikia haya .Akanialika na mimi nime itikia witu ndipo nimeamua kuja kujionea .

Kwa sasa nadhani si swala la taasisi wala udikteta .Kwa sasa ni kazi moja kuleta maendeleo kwanza .Nchi ilikuwa pabaya na sasa ina heshimika .Mambo ya Muungwana na taasisi ndiyo haya yanatufikisha hapa na yeye jambo moja nasema ni kwamba Kagame hana Ubia na mtu kwenye Urais.Kagame naamini ana ijenga taasisi maana si yeye pekee anaendesha ile Nchi ina viongozi wengine .Kama hapendi kusikia ya upande wa pili ambayo yana nia ya kuangamiza Rwanda fine.

Kuhusu wanawame wa Kinyarwanda duh !!!Wako wanapendeza sana sana .Na hasa mjini Kigali ukiwa mtu wa mambo basi hapa utapata shida hapa lugha .Wanaongea kinywaranda na French sasa kazi kwako GT karibu .Ama nikutafutie mmoja nikupe contact ? Later naenda kwenye taasisi moja naweza kukupa link .
 
Lunyungu leo "Utakandamiza kibara" mademu wa kinyarwanda??

Mkuu kwa Umri huu hapana ila ninawaona tu mtaani na hata maeneo mengi ninayo tembelea wanajua huyu ni Mtanganyika maana niko makini na vi begi vyangu .Unawajua hawa wana maumbo yao so wanajua tu huyu wa kuja .Mimi nakandamiza habari na tafiti zangu juu ya nini Kagame kafanya hata akaiweka Nchi sawa na sasa inaanza kasi ili ipae sie tunaimba mara mafisadi mara amani na utulivu mara Utawala bora huku Richmond bado wanachota mamilioni kwa mwezi na hata Bunge kimyaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom