MOTOCHINI
JF-Expert Member
- Jan 20, 2014
- 27,502
- 29,547
KIGALI, Rwanda
RAIS Paul Kagame amewaambia wafuasi wake wa Chama cha Rwandan Patriotic Front (RPF) kuwa atagombea urais kwa mara ya mwisho.
Kagame alisema hayo mwishoni mwa wiki iliyopita alipokuwa akitoa hotuba yake ya shukrani baada ya kuchaguliwa kuwa mgombea urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Agosti 3, 2017.
Katika mkutano mkuu alichaguliwa kwa kura 1,929 kati ya kura 1,930 zilizopigwa. Kura moja iliharibika.
Katika hotuba yake Kagame alisema,”Natoa wito kwamba ama tofauti au vizuri zaidi au tufanye kazi kwa bidii sana ili katika kipindi cha miaka saba kiwe kama cha mpito.
Aliwahimiza vijana kujiunga na siasa lakini aliwataka wachukue tahadhari.
“Jihadharini huku.
Si suala la kuwa rais tu. Si suala la kuwa na haki ya kuwa rais. Rwanda inataka na kwa dhati inahitaji rais sahihi,” aliongeza.
Mkutano huo ulihudhuriwa na wageni kutoka nchi za China, Ethiopia, Afrika Kusini na Uganda.
RAIS Paul Kagame amewaambia wafuasi wake wa Chama cha Rwandan Patriotic Front (RPF) kuwa atagombea urais kwa mara ya mwisho.
Kagame alisema hayo mwishoni mwa wiki iliyopita alipokuwa akitoa hotuba yake ya shukrani baada ya kuchaguliwa kuwa mgombea urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Agosti 3, 2017.
Katika mkutano mkuu alichaguliwa kwa kura 1,929 kati ya kura 1,930 zilizopigwa. Kura moja iliharibika.
Katika hotuba yake Kagame alisema,”Natoa wito kwamba ama tofauti au vizuri zaidi au tufanye kazi kwa bidii sana ili katika kipindi cha miaka saba kiwe kama cha mpito.
Aliwahimiza vijana kujiunga na siasa lakini aliwataka wachukue tahadhari.
“Jihadharini huku.
Si suala la kuwa rais tu. Si suala la kuwa na haki ya kuwa rais. Rwanda inataka na kwa dhati inahitaji rais sahihi,” aliongeza.
Mkutano huo ulihudhuriwa na wageni kutoka nchi za China, Ethiopia, Afrika Kusini na Uganda.