VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
================
TAARIFA:
Mhe. Kafulila kakanusha kutoa kauli iliyowekwa chini na kasema "Kilichoandikwa kimewekwa na wabaya wa Mhe. Zitto kwa nia wanazojua wao." Tumeufunga mjadala huu kwakuwa ni sawa na kujadili kitu kisichokuwepo!
Kafulila:
"Ni kweli pendekezo la Zitto nilisimama kutaka kurekebisha kwasababu lilikuwa la jumla kwa wahusika wote. Wakati nasimama Werema akachomeka kwamba hilo pendekezo lilikuwa sawa kisheria, ndipo Mnyika naye akamchomekea Werema kuwa "Hata wewe?" Kwamba hata Werema alokwisha kukiri kukosea naye tusimuhukumu tumwachie rais. Ndio ulikuwa msingi na si kama mdau alivyoandika"
================
TAARIFA:
Mhe. Kafulila kakanusha kutoa kauli iliyowekwa chini na kasema "Kilichoandikwa kimewekwa na wabaya wa Mhe. Zitto kwa nia wanazojua wao." Tumeufunga mjadala huu kwakuwa ni sawa na kujadili kitu kisichokuwepo!
Kafulila:
"Ni kweli pendekezo la Zitto nilisimama kutaka kurekebisha kwasababu lilikuwa la jumla kwa wahusika wote. Wakati nasimama Werema akachomeka kwamba hilo pendekezo lilikuwa sawa kisheria, ndipo Mnyika naye akamchomekea Werema kuwa "Hata wewe?" Kwamba hata Werema alokwisha kukiri kukosea naye tusimuhukumu tumwachie rais. Ndio ulikuwa msingi na si kama mdau alivyoandika"
================
Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi) David Kafulila amesema kuwa ameshamsamehe Mbunge Zitto Kabwe lakini hatamsahau kamwe. Kafulila alikuwa akiongelea suala la Zitto kuungana kihoja na kiuandishi wa maazimio na Mbunge Andrew Chenge.
Kafulila,anayesemwa kushibana na Zitto,amesema kuwa katika nyakati ngumu maishani ule wa Zitto kuungana na Chenge ni mmoja wao. "Nikajikuta nauliza kwa sauti:hata wewe!?. Lakini nimemsamehe na mambo yanaendelea. Lakini,sitamsahau" alisema Kafulila.
Ni dhahiri Zitto alijikwaa na kupepesuka Ijumaa. Awe makini wakati mwingine.
Mzee Tupatupa wa Escrow,Dar es Salaam