AMARIDONG
JF-Expert Member
- Jun 24, 2010
- 2,502
- 180
MBUNGE wa Jimbo la Kigoma Kusini kupitia chama cha NCCR- Mageuzi, anakusudia kupeleka hoja binafsi katika Bunge la Februari 2011, kutaka Serikali iwajibike kwa kuliingiza Taifa hasara kwenye sekta ya umeme.
Hoja hiyo ya Kafulila imekuja siku chache baada ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), kushindwa kesi katika Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi (ICC) na kutakiwa kuilipa Kampuni ya Dowans Sh bilioni 185 kwa kuvunja mkataba kinyume na sheria.
Katika hoja hiyo, Kafulila anataka Serikali aliyosema ndiyo inayopaswa kulipa deni hilo, kutoa maelezo ya kina ya sakata zima mpaka kufikia hapo, kwa sababu haitakuwa sahihi kulipa mabilioni ya fedha kwa kampuni aliyodai kuwa mmiliki wake hafahamiki.
Kafulila pia anakusudia katika hoja hiyo, kulitaka Bunge liazimie kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja kwa madai kuwa ameshindwa kusimamia utekelezaji wa Sera ya Nishati na Mpango Kabambe wa Usambazaji wa Umeme nchini.
Kwa mujibu wa madai ya Mbunge huyo, kushindwa kazi kwa Waziri huyo, kumesababisha kutokea kwa mgawo wa umeme nchini mara tatu ndani ya miaka miwili ya uongozaji wake.
Akizungumza jana katika makao makuu ya chama hicho Ilala jijini Dar es Salaam, Kafulila alisema kuwa mgogoro wa nishati ya umeme unaelekea kukomaa na kuwa sehemu ya maisha ya Watanzania.
Kafulila aliendelea kudai kuwa haitawezekana kufanikisha mpango wowote wa mapinduzi ya uchumi wala ya huduma nchini kwa kuwa takwimu zinaonesha asilimia 40 ya uchumi duniani inategemea nishati ya umeme.
Alidai chanzo kikubwa cha tatizo la umeme nchini ni Serikali kufumbia macho miradi ya umeme ya uhakika ambayo ingetoa majibu ya kudumu ya tatizo hilo na badala yake imebaki kusimamia sekta ya umeme kwa kudunduliza ikitumia mitambo ya kukodi ambayo alidai kwa miaka kadhaa sasa imekuwa ikinyonya vibaya uchumi wa Taifa.
Asilimia 86 ya mapato ya Tanesco yanatumika kulipia umeme unaozalishwa na mitambo ya kukodi ambayo inazalisha takribani asilimia 45 tu ya umeme wote... hivi sasa mitambo ya kukodi inayotumika ni Songas na IPTL peke yake baada ya Agreko kumaliza mkataba wake na Dowans kufutwa mkataba, alidai.
Alidai Tanesco inalipa Kampuni ya Songas takriban Sh milioni 266 kila siku kwa kununua megawati 86 za umeme na mitambo ya IPTL ikiwa imewashwa, Tanesco inailipa kampuni hiyo Sh milioni 300 kila siku.
Tangu mwaka 2006 Serikali imeshindwa japo kupunguza tatizo la mgao wa umeme huku viongozi wake hasa Waziri wa Nishati na Madini akipotosha Watanzania mara kadhaa kwamba Serikali inalishughulikia na mgao wa umeme utakuwa historia, alidai.
Alisema, Serikali inapaswa kuona athari ya matatizo ya umeme katika maendeleo kuliko hata mtikisiko wa uchumi na kuitaka ifanye maazimio magumu kwa kutenga fedha za kutosha kutekeleza mradi mkubwa wa umeme na wa uhakika kama wa makaa ya mawe Kiwira na gesi asilia ya Mnazi Bay.
Kafulila alisema miradi yote inaweza kuendeshwa na sekta binafsi iwapo kutakuwa na mazingira mazuri ya uwekezaji na kuishauri mifuko ya hifadhi ya jamii iache kujenga majengo na ijielekeze katika uwekezaji wa uzalishaji umeme ili kutatua kabisa tatizo la umeme.
Alidai kwa kuwa Serikali ndiyo iliyoielekeza Tanesco iingie mkataba na Richmond na baadaye kuuhamisha mkataba huo kwa Kampuni ya Dowans na kwa kuwa Bunge ndio lilitoa azimio la kuvunjwa kwa mkataba na Tanesco ikafanya hivyo, shirika hilo lisibebeshwe lawama.
Gazeti hili lilimtafuta Ngeleja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema ili watoe ufafanuzi kuhusu hoja hiyo lakini hawakupatikana katika simu zao.
Hata hivyo Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashililah alisema ni mara yake ya kwanza kusikia Mbunge akitaka waziri mmoja, apigiwe kura na wabunge ya kutokuwa na imani naye.
Alifafanua kuwa kisheria waziri anaweza kupigiwa kura hiyo endapo yeye binafsi atakuwa na tatizo la kimaadili. Dk. Kashililah alisema katika tatizo la umeme, Waziri Ngeleja anaiwakilisha Serikali hivyo hoja hiyo ya kupigiwa kura ya kutokuwa na imani kwake, haiwezi kuelekezwa kwake binafsi na badala yake inapaswa kuelekezwa kwa Serikali nzima.
Hoja hiyo ya Kafulila imekuja siku chache baada ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), kushindwa kesi katika Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi (ICC) na kutakiwa kuilipa Kampuni ya Dowans Sh bilioni 185 kwa kuvunja mkataba kinyume na sheria.
Katika hoja hiyo, Kafulila anataka Serikali aliyosema ndiyo inayopaswa kulipa deni hilo, kutoa maelezo ya kina ya sakata zima mpaka kufikia hapo, kwa sababu haitakuwa sahihi kulipa mabilioni ya fedha kwa kampuni aliyodai kuwa mmiliki wake hafahamiki.
Kafulila pia anakusudia katika hoja hiyo, kulitaka Bunge liazimie kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja kwa madai kuwa ameshindwa kusimamia utekelezaji wa Sera ya Nishati na Mpango Kabambe wa Usambazaji wa Umeme nchini.
Kwa mujibu wa madai ya Mbunge huyo, kushindwa kazi kwa Waziri huyo, kumesababisha kutokea kwa mgawo wa umeme nchini mara tatu ndani ya miaka miwili ya uongozaji wake.
Akizungumza jana katika makao makuu ya chama hicho Ilala jijini Dar es Salaam, Kafulila alisema kuwa mgogoro wa nishati ya umeme unaelekea kukomaa na kuwa sehemu ya maisha ya Watanzania.
Kafulila aliendelea kudai kuwa haitawezekana kufanikisha mpango wowote wa mapinduzi ya uchumi wala ya huduma nchini kwa kuwa takwimu zinaonesha asilimia 40 ya uchumi duniani inategemea nishati ya umeme.
Alidai chanzo kikubwa cha tatizo la umeme nchini ni Serikali kufumbia macho miradi ya umeme ya uhakika ambayo ingetoa majibu ya kudumu ya tatizo hilo na badala yake imebaki kusimamia sekta ya umeme kwa kudunduliza ikitumia mitambo ya kukodi ambayo alidai kwa miaka kadhaa sasa imekuwa ikinyonya vibaya uchumi wa Taifa.
Asilimia 86 ya mapato ya Tanesco yanatumika kulipia umeme unaozalishwa na mitambo ya kukodi ambayo inazalisha takribani asilimia 45 tu ya umeme wote... hivi sasa mitambo ya kukodi inayotumika ni Songas na IPTL peke yake baada ya Agreko kumaliza mkataba wake na Dowans kufutwa mkataba, alidai.
Alidai Tanesco inalipa Kampuni ya Songas takriban Sh milioni 266 kila siku kwa kununua megawati 86 za umeme na mitambo ya IPTL ikiwa imewashwa, Tanesco inailipa kampuni hiyo Sh milioni 300 kila siku.
Tangu mwaka 2006 Serikali imeshindwa japo kupunguza tatizo la mgao wa umeme huku viongozi wake hasa Waziri wa Nishati na Madini akipotosha Watanzania mara kadhaa kwamba Serikali inalishughulikia na mgao wa umeme utakuwa historia, alidai.
Alisema, Serikali inapaswa kuona athari ya matatizo ya umeme katika maendeleo kuliko hata mtikisiko wa uchumi na kuitaka ifanye maazimio magumu kwa kutenga fedha za kutosha kutekeleza mradi mkubwa wa umeme na wa uhakika kama wa makaa ya mawe Kiwira na gesi asilia ya Mnazi Bay.
Kafulila alisema miradi yote inaweza kuendeshwa na sekta binafsi iwapo kutakuwa na mazingira mazuri ya uwekezaji na kuishauri mifuko ya hifadhi ya jamii iache kujenga majengo na ijielekeze katika uwekezaji wa uzalishaji umeme ili kutatua kabisa tatizo la umeme.
Alidai kwa kuwa Serikali ndiyo iliyoielekeza Tanesco iingie mkataba na Richmond na baadaye kuuhamisha mkataba huo kwa Kampuni ya Dowans na kwa kuwa Bunge ndio lilitoa azimio la kuvunjwa kwa mkataba na Tanesco ikafanya hivyo, shirika hilo lisibebeshwe lawama.
Gazeti hili lilimtafuta Ngeleja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema ili watoe ufafanuzi kuhusu hoja hiyo lakini hawakupatikana katika simu zao.
Hata hivyo Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashililah alisema ni mara yake ya kwanza kusikia Mbunge akitaka waziri mmoja, apigiwe kura na wabunge ya kutokuwa na imani naye.
Alifafanua kuwa kisheria waziri anaweza kupigiwa kura hiyo endapo yeye binafsi atakuwa na tatizo la kimaadili. Dk. Kashililah alisema katika tatizo la umeme, Waziri Ngeleja anaiwakilisha Serikali hivyo hoja hiyo ya kupigiwa kura ya kutokuwa na imani kwake, haiwezi kuelekezwa kwake binafsi na badala yake inapaswa kuelekezwa kwa Serikali nzima.