Kafulila: IMF wamethibisha bajeti ya 2017/2018 haitekelezeki kama ilivyokuwa ya 2016/2017

Zawadi B Lupelo

JF-Expert Member
Jul 19, 2015
2,549
3,722
Anaandika David Kafulila

REPOTI YA IMF KUHUSU UCHUMI WETU JANA INATHIBITISHA KUWA BAJETI YA 2017/18 HAITEKELEZEKI KAMA ILIVYOKUWA 2016/17

Baada ya kusoma ripoti ya IMF kuhusu mwenendo wa uchumi na Bajeti Tanzania niligundua kitu kimoja muhimu kwamba bajeti ya 2017/18 haitekelezeki kama nchi itaendelea kukosa mikopo nje kutekeleza miradi mikubwa iliyopangwa tangu bajeti ya 2016/17 na sasa 2017/18.

Kwa muda sasa kama nchi imekuwa ngumu kupata mikopo nafuu (concessional loans) kutokana na masharti yake ya demokrasia na utawala bora. Zaidi sasa mikopo ya kibiashara toka nje imebaki kuwa migumu kutokana na taasisi za kimataifa kuanza kuisoma serikali kuwa 'anti business'.na mbaya zaidi hatujafanya credit rating ili kuhakikishia wawekezaji na banks kwa maana ya kupata mikopo kama ilivyokwishafanya Kenya na Rwanda kwa upande wa Africa Mashariki.

Lakini mazingira yalivyo ningumu kupata mkopo kuendesha bajeti. Ndio maana serikali imezidi kukopa ndani na kufanya deni la ndani kwenda juu na kuvunja rekodi tangu awamu ya tatu.Awamu ya tatu iliacha deni la ndani likiwa 1.7trilion, miaka10 ya awamu ya nne deni la ndani lilifikia 7.5trn mwaka 2015, sasa miaka miwili tu, deni limefika zaidi ya 11trilion.sawa na nyongeza ya 3.5trilion kwa miaka2tu.Hii ni hatari sana kwenye nchi ambayo mzunguko wa fedha ndani upo chini mno (tight liquidity ).

Hali ikibaki ilivyo nchi itazidi kuzama kiuchumi kwa kushindwa kugharamia mahitaji ya afya , maji na elimu kwasababu ukiangalia deni lililoiva mwaka jana ilikuwa 8trilion wakati mwaka huu ni 9trilion.sasa wakati deni liloiva mwaka huu ni 9trilion bado mshahara (wagebill) ni 7.6trilion.

Hii maana yake mshahara na deni peke yake ni 16.6trilion. Katika mazingira ya sasa ambayo kodi inayokusanywa kwa mwezi TRA ni wastani wa 1.1-1.2trilion, kwamba sio zaidi ya 14trilion kwa mwaka.

Hii maanake ni kwamba makusanyo yetu ya kodi hayatoshi japo kumudu deni la mshahara.kwamba tunakopa kulipa mshahara.hatujazungumza gharama zingine za kuendesha Serikali achilia mbali miradi ya maendeleo.

Tuna njia mbili za kufanya; 1.Lazma Seriakali ishughulikie mgogoro wa Zanzibar na isitishe ukandamizaji demokrasia ili iendelee kupata mikopo nafuu kwani kwa vigezo vya mikopo nafuu Tanzania inaweza kupata mikopo nafuu (concessional loans) kufikia $2.5bn sawa Tsh6tn.kwa mwaka, hiki nikiasi ambacho kinatosha sana kwa serikali kumudu miradi yake ya kimkakati (flagship projects) kama ujenzi wa reli, umeme, Bandari nk 2.

Lazma Serikali ikae na wafanyabiashara na kuwahakikishia kwamba Tanzania ni sehemu Salama kuwekeza na hivyo waweze kuingiza mtaji zaidi kwani hatuwezi kujenga uchumi wa viwanda kama hatupati mtaji toka nje (FDI ), China tunayoitazama leo kama Taifa la pili kwa ukubwa wa uchumi duniani baada ya USA, pamoja na msimamo wake wa ujamaa imefika hapo kuwa nchi ya pili kwa ukubwa wa uchumi duniani baada ya kuwekeza zaidi kwenye elimu, ufundi na technology lakini zaidi kuvutia mitaji toka nje hususan USA.

Lazma tujenge uchumi wakisasa kwa kuangalia dunia yaleo imefika wapi.tukirekebisha mazingira hayo ya kibiashara kwa kujenga imani kwa uwekezaji na biashara tutapata mitaji zaidi na zaidi mikopo ya kibiashara (commercial loans).

Lazma tufanye hivyo ili tuelekee ndoto ya Dira ya Taifa ya 2025, ambayo Kwa mujibu wa Poverty&Human Development Report 2014 inasema ili tufikie dira hiyo lazma pamoja na mambo mengine tuajiri walimu900,000 sawa na wastani wa walimu 90,000 kila mwaka. Leo ajira za walimu tumeajiri sana mwaka2015 hawakuzidi 30,000.Kilimo kinachoajiri 70% sasa kinakua kwa1.7% , kiasi ambacho nichini kupata kutokea tangu Uhuru.

David KAFULILA
Juni27,2017
 
IMF ya Kibondo au Ujiji?
hahahahah, ndiyo ushangae mtu anaposhabikia wazungu wakati wao wanatuona kama manyani hatuna uwezo wa kujitegemea. Uchumi unasema anakupatia msaada ndiye anayefaidika, wazungu wamekuwa wakitupatia hizo hela na wao wanaleta miradi yao na watu wao, unajikuta mwisho wa siku hela inarudi kwao, na kibaya kama wa USA wanapomaliza project zao wanauza na asset zote walizokuwa wanatumia, yaani wanapata soko jingine, kafulila atulie maana hajui
 
Anaandika David Kafulila

REPOTI YA IMF KUHUSU UCHUMI WETU JANA INATHIBITISHA KUWA BAJETI YA 2017/18 HAITEKELEZEKI KAMA ILIVYOKUWA 2016/17

Baada ya kusoma ripoti ya IMF kuhusu mwenendo wa uchumi na Bajeti Tanzania niligundua kitu kimoja muhimu kwamba bajeti ya 2017/18 haitekelezeki kama nchi itaendelea kukosa mikopo nje kutekeleza miradi mikubwa iliyopangwa tangu bajeti ya 2016/17 na sasa 2017/18.

Kwa muda sasa kama nchi imekuwa ngumu kupata mikopo nafuu (concessional loans) kutokana na masharti yake ya demokrasia na utawala bora. Zaidi sasa mikopo ya kibiashara toka nje imebaki kuwa migumu kutokana na taasisi za kimataifa kuanza kuisoma serikali kuwa 'anti business'.na mbaya zaidi hatujafanya credit rating ili kuhakikishia wawekezaji na banks kwa maana ya kupata mikopo kama ilivyokwishafanya Kenya na Rwanda kwa upande wa Africa Mashariki.

Lakini mazingira yalivyo ningumu kupata mkopo kuendesha bajeti. Ndio maana serikali imezidi kukopa ndani na kufanya deni la ndani kwenda juu na kuvunja rekodi tangu awamu ya tatu.Awamu ya tatu iliacha deni la ndani likiwa 1.7trilion, miaka10 ya awamu ya nne deni la ndani lilifikia 7.5trn mwaka 2015, sasa miaka miwili tu, deni limefika zaidi ya 11trilion.sawa na nyongeza ya 3.5trilion kwa miaka2tu.Hii ni hatari sana kwenye nchi ambayo mzunguko wa fedha ndani upo chini mno (tight liquidity ).

Hali ikibaki ilivyo nchi itazidi kuzama kiuchumi kwa kushindwa kugharamia mahitaji ya afya , maji na elimu kwasababu ukiangalia deni lililoiva mwaka jana ilikuwa 8trilion wakati mwaka huu ni 9trilion.sasa wakati deni liloiva mwaka huu ni 9trilion bado mshahara (wagebill) ni 7.6trilion.

Hii maana yake mshahara na deni peke yake ni 16.6trilion. Katika mazingira ya sasa ambayo kodi inayokusanywa kwa mwezi TRA ni wastani wa 1.1-1.2trilion, kwamba sio zaidi ya 14trilion kwa mwaka.

Hii maanake ni kwamba makusanyo yetu ya kodi hayatoshi japo kumudu deni la mshahara.kwamba tunakopa kulipa mshahara.hatujazungumza gharama zingine za kuendesha Serikali achilia mbali miradi ya maendeleo.

Tuna njia mbili za kufanya; 1.Lazma Seriakali ishughulikie mgogoro wa Zanzibar na isitishe ukandamizaji demokrasia ili iendelee kupata mikopo nafuu kwani kwa vigezo vya mikopo nafuu Tanzania inaweza kupata mikopo nafuu (concessional loans) kufikia $2.5bn sawa Tsh6tn.kwa mwaka, hiki nikiasi ambacho kinatosha sana kwa serikali kumudu miradi yake ya kimkakati (flagship projects) kama ujenzi wa reli, umeme, Bandari nk 2.

Lazma Serikali ikae na wafanyabiashara na kuwahakikishia kwamba Tanzania ni sehemu Salama kuwekeza na hivyo waweze kuingiza mtaji zaidi kwani hatuwezi kujenga uchumi wa viwanda kama hatupati mtaji toka nje (FDI ), China tunayoitazama leo kama Taifa la pili kwa ukubwa wa uchumi duniani baada ya USA, pamoja na msimamo wake wa ujamaa imefika hapo kuwa nchi ya pili kwa ukubwa wa uchumi duniani baada ya kuwekeza zaidi kwenye elimu, ufundi na technology lakini zaidi kuvutia mitaji toka nje hususan USA.

Lazma tujenge uchumi wakisasa kwa kuangalia dunia yaleo imefika wapi.tukirekebisha mazingira hayo ya kibiashara kwa kujenga imani kwa uwekezaji na biashara tutapata mitaji zaidi na zaidi mikopo ya kibiashara (commercial loans).

Lazma tufanye hivyo ili tuelekee ndoto ya Dira ya Taifa ya 2025, ambayo Kwa mujibu wa Poverty&Human Development Report 2014 inasema ili tufikie dira hiyo lazma pamoja na mambo mengine tuajiri walimu900,000 sawa na wastani wa walimu 90,000 kila mwaka. Leo ajira za walimu tumeajiri sana mwaka2015 hawakuzidi 30,000.Kilimo kinachoajiri 70% sasa kinakua kwa1.7% , kiasi ambacho nichini kupata kutokea tangu Uhuru.

David KAFULILA
Juni27,2017
WACHA AJIANDIKIE ,,,KWANI UPINZANI WA TANZANIA UMEKUWA MCHAKAVU NA WAMEKUWA WANAJENGA HOJA ZA KITOTO..... NI DHAHIRI KIZAZI CHA UPINZANI MPYA KINAHITAJIKA....
 
Kafulila ni bora ukakaa kimya, katika pande hii ya dunia ukweli huitwa uchochezi na inaweza pelekea kuhojiwa!
Ila mimi nilikuwa nadhani kuwa kama utekelezaji wa bajeti iliyopita haukufikia 50% basi wangepanga bajeti ya trillion 18 ili kuwa realistic. Haya mambo ya 'aiming higher' yanatupotosha maana ni sawa na mtu wa miaka 45 anayefanya mazoezi kwa bidii ili aweze kucheze world cup.
 
Kafulila anajichanganya kwenye mada yake.

Anatoa mfano wa china kupata mitaji kutoka USA anasahau kuwa huko China hakuna demokrasia inayopigiwa chapuo na nchi za Magharibi. Kafulila akamuulize Dalai Lama kuhusu demokrasia ya China.

Kafulila anashindwa kuelewa kuwa hakuna bajeti iliyotekelezwa 100% kwenye nchi ambazo zinategemea sehemu ya bajeti yake kujazwa na nchi nyingine wahisani. Tanzania tokea uhuru hatujaweza kutekeleza bajeti 100%.

Kukosa mitaji kutoka nje sio kwa sababu eti nchi haina demokrasia bali kwa sababu nchi haitaki kutoa raslimali zake kwa faida ya kunufaisha watoa mitaji pekee.

European Union na makampuni yao kwa sasa hawawezi kutupa mikopo nafuu kwa sababu tumekataa kuingia kwenye EPA. Tanzania ikisema kesho kuwa inaingia kwenye EPA utaona mikopo nafuu inaanza kutolewa.
 
Kafulila anajichanganya kwenye mada yake.

Anatoa mfano wa china kupata mitaji kutoka USA anasahau kuwa huko China hakuna demokrasia inayopigiwa chapuo na nchi za Magharibi. Kafulila akamuulize Dalai Lama kuhusu demokrasia ya China.

Kukosa mitaji kutoka nje sio kwa sababu eti nchi haina demokrasia bali kwa sababu nchi haitaki kutoa raslimali zake kwa faida ya kunufaisha watoa mitaji pekee.
toa mfano wa rasilimali ambayo hatutaki kutoa
 
Akili ya kukopa kopa tu kwa nini hazungumzii kuongeza nguvu ya kudai trn 108 za Acacia?
Mdai ile yenu?Wenyewe wamesema hawadaiwi na hawajahidi kulipa nyie mseme mnadai,kama mnadai mbona wanaendelea kuzalisha matofali?
 
Huu ni ukweli ambao wananchi wote tunaujua isipokuwa siasa za uvyama ndio zinapofua baadhi, hakuna mwaka ambao TZ ilikuwa na bajeti iliyotekelezeka, kila mwaka hakuna wizara ilipata hela zote za bajeti, ni blabla tu na uhuni wa kijinga pale bungeni.
 
Anaandika David Kafulila

REPOTI YA IMF KUHUSU UCHUMI WETU JANA INATHIBITISHA KUWA BAJETI YA 2017/18 HAITEKELEZEKI KAMA ILIVYOKUWA 2016/17

Baada ya kusoma ripoti ya IMF kuhusu mwenendo wa uchumi na Bajeti Tanzania niligundua kitu kimoja muhimu kwamba bajeti ya 2017/18 haitekelezeki kama nchi itaendelea kukosa mikopo nje kutekeleza miradi mikubwa iliyopangwa tangu bajeti ya 2016/17 na sasa 2017/18.

Kwa muda sasa kama nchi imekuwa ngumu kupata mikopo nafuu (concessional loans) kutokana na masharti yake ya demokrasia na utawala bora. Zaidi sasa mikopo ya kibiashara toka nje imebaki kuwa migumu kutokana na taasisi za kimataifa kuanza kuisoma serikali kuwa 'anti business'.na mbaya zaidi hatujafanya credit rating ili kuhakikishia wawekezaji na banks kwa maana ya kupata mikopo kama ilivyokwishafanya Kenya na Rwanda kwa upande wa Africa Mashariki.

Lakini mazingira yalivyo ningumu kupata mkopo kuendesha bajeti. Ndio maana serikali imezidi kukopa ndani na kufanya deni la ndani kwenda juu na kuvunja rekodi tangu awamu ya tatu.Awamu ya tatu iliacha deni la ndani likiwa 1.7trilion, miaka10 ya awamu ya nne deni la ndani lilifikia 7.5trn mwaka 2015, sasa miaka miwili tu, deni limefika zaidi ya 11trilion.sawa na nyongeza ya 3.5trilion kwa miaka2tu.Hii ni hatari sana kwenye nchi ambayo mzunguko wa fedha ndani upo chini mno (tight liquidity ).

Hali ikibaki ilivyo nchi itazidi kuzama kiuchumi kwa kushindwa kugharamia mahitaji ya afya , maji na elimu kwasababu ukiangalia deni lililoiva mwaka jana ilikuwa 8trilion wakati mwaka huu ni 9trilion.sasa wakati deni liloiva mwaka huu ni 9trilion bado mshahara (wagebill) ni 7.6trilion.

Hii maana yake mshahara na deni peke yake ni 16.6trilion. Katika mazingira ya sasa ambayo kodi inayokusanywa kwa mwezi TRA ni wastani wa 1.1-1.2trilion, kwamba sio zaidi ya 14trilion kwa mwaka.

Hii maanake ni kwamba makusanyo yetu ya kodi hayatoshi japo kumudu deni la mshahara.kwamba tunakopa kulipa mshahara.hatujazungumza gharama zingine za kuendesha Serikali achilia mbali miradi ya maendeleo.

Tuna njia mbili za kufanya; 1.Lazma Seriakali ishughulikie mgogoro wa Zanzibar na isitishe ukandamizaji demokrasia ili iendelee kupata mikopo nafuu kwani kwa vigezo vya mikopo nafuu Tanzania inaweza kupata mikopo nafuu (concessional loans) kufikia $2.5bn sawa Tsh6tn.kwa mwaka, hiki nikiasi ambacho kinatosha sana kwa serikali kumudu miradi yake ya kimkakati (flagship projects) kama ujenzi wa reli, umeme, Bandari nk 2.

Lazma Serikali ikae na wafanyabiashara na kuwahakikishia kwamba Tanzania ni sehemu Salama kuwekeza na hivyo waweze kuingiza mtaji zaidi kwani hatuwezi kujenga uchumi wa viwanda kama hatupati mtaji toka nje (FDI ), China tunayoitazama leo kama Taifa la pili kwa ukubwa wa uchumi duniani baada ya USA, pamoja na msimamo wake wa ujamaa imefika hapo kuwa nchi ya pili kwa ukubwa wa uchumi duniani baada ya kuwekeza zaidi kwenye elimu, ufundi na technology lakini zaidi kuvutia mitaji toka nje hususan USA.

Lazma tujenge uchumi wakisasa kwa kuangalia dunia yaleo imefika wapi.tukirekebisha mazingira hayo ya kibiashara kwa kujenga imani kwa uwekezaji na biashara tutapata mitaji zaidi na zaidi mikopo ya kibiashara (commercial loans).

Lazma tufanye hivyo ili tuelekee ndoto ya Dira ya Taifa ya 2025, ambayo Kwa mujibu wa Poverty&Human Development Report 2014 inasema ili tufikie dira hiyo lazma pamoja na mambo mengine tuajiri walimu900,000 sawa na wastani wa walimu 90,000 kila mwaka. Leo ajira za walimu tumeajiri sana mwaka2015 hawakuzidi 30,000.Kilimo kinachoajiri 70% sasa kinakua kwa1.7% , kiasi ambacho nichini kupata kutokea tangu Uhuru.

David KAFULILA
Juni27,2017

IMF sio Internatonal Ministry of Finance
Ni International Monetary Fund
Kwa mambo ya bajeti yetu na itatekelezajwe hayawahusu
Hizo ndio taasisi zilizoundwa mahususi na mabepari, kukandaniza nchi maskini
Don't trust them,hawapo pale kwa kusaidia nchi maskini
Wapo pale kwa kukandaniza
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom