Zawadi B Lupelo
JF-Expert Member
- Jul 19, 2015
- 2,549
- 3,722
Anaandika David Kafulila
REPOTI YA IMF KUHUSU UCHUMI WETU JANA INATHIBITISHA KUWA BAJETI YA 2017/18 HAITEKELEZEKI KAMA ILIVYOKUWA 2016/17
Baada ya kusoma ripoti ya IMF kuhusu mwenendo wa uchumi na Bajeti Tanzania niligundua kitu kimoja muhimu kwamba bajeti ya 2017/18 haitekelezeki kama nchi itaendelea kukosa mikopo nje kutekeleza miradi mikubwa iliyopangwa tangu bajeti ya 2016/17 na sasa 2017/18.
Kwa muda sasa kama nchi imekuwa ngumu kupata mikopo nafuu (concessional loans) kutokana na masharti yake ya demokrasia na utawala bora. Zaidi sasa mikopo ya kibiashara toka nje imebaki kuwa migumu kutokana na taasisi za kimataifa kuanza kuisoma serikali kuwa 'anti business'.na mbaya zaidi hatujafanya credit rating ili kuhakikishia wawekezaji na banks kwa maana ya kupata mikopo kama ilivyokwishafanya Kenya na Rwanda kwa upande wa Africa Mashariki.
Lakini mazingira yalivyo ningumu kupata mkopo kuendesha bajeti. Ndio maana serikali imezidi kukopa ndani na kufanya deni la ndani kwenda juu na kuvunja rekodi tangu awamu ya tatu.Awamu ya tatu iliacha deni la ndani likiwa 1.7trilion, miaka10 ya awamu ya nne deni la ndani lilifikia 7.5trn mwaka 2015, sasa miaka miwili tu, deni limefika zaidi ya 11trilion.sawa na nyongeza ya 3.5trilion kwa miaka2tu.Hii ni hatari sana kwenye nchi ambayo mzunguko wa fedha ndani upo chini mno (tight liquidity ).
Hali ikibaki ilivyo nchi itazidi kuzama kiuchumi kwa kushindwa kugharamia mahitaji ya afya , maji na elimu kwasababu ukiangalia deni lililoiva mwaka jana ilikuwa 8trilion wakati mwaka huu ni 9trilion.sasa wakati deni liloiva mwaka huu ni 9trilion bado mshahara (wagebill) ni 7.6trilion.
Hii maana yake mshahara na deni peke yake ni 16.6trilion. Katika mazingira ya sasa ambayo kodi inayokusanywa kwa mwezi TRA ni wastani wa 1.1-1.2trilion, kwamba sio zaidi ya 14trilion kwa mwaka.
Hii maanake ni kwamba makusanyo yetu ya kodi hayatoshi japo kumudu deni la mshahara.kwamba tunakopa kulipa mshahara.hatujazungumza gharama zingine za kuendesha Serikali achilia mbali miradi ya maendeleo.
Tuna njia mbili za kufanya; 1.Lazma Seriakali ishughulikie mgogoro wa Zanzibar na isitishe ukandamizaji demokrasia ili iendelee kupata mikopo nafuu kwani kwa vigezo vya mikopo nafuu Tanzania inaweza kupata mikopo nafuu (concessional loans) kufikia $2.5bn sawa Tsh6tn.kwa mwaka, hiki nikiasi ambacho kinatosha sana kwa serikali kumudu miradi yake ya kimkakati (flagship projects) kama ujenzi wa reli, umeme, Bandari nk 2.
Lazma Serikali ikae na wafanyabiashara na kuwahakikishia kwamba Tanzania ni sehemu Salama kuwekeza na hivyo waweze kuingiza mtaji zaidi kwani hatuwezi kujenga uchumi wa viwanda kama hatupati mtaji toka nje (FDI ), China tunayoitazama leo kama Taifa la pili kwa ukubwa wa uchumi duniani baada ya USA, pamoja na msimamo wake wa ujamaa imefika hapo kuwa nchi ya pili kwa ukubwa wa uchumi duniani baada ya kuwekeza zaidi kwenye elimu, ufundi na technology lakini zaidi kuvutia mitaji toka nje hususan USA.
Lazma tujenge uchumi wakisasa kwa kuangalia dunia yaleo imefika wapi.tukirekebisha mazingira hayo ya kibiashara kwa kujenga imani kwa uwekezaji na biashara tutapata mitaji zaidi na zaidi mikopo ya kibiashara (commercial loans).
Lazma tufanye hivyo ili tuelekee ndoto ya Dira ya Taifa ya 2025, ambayo Kwa mujibu wa Poverty&Human Development Report 2014 inasema ili tufikie dira hiyo lazma pamoja na mambo mengine tuajiri walimu900,000 sawa na wastani wa walimu 90,000 kila mwaka. Leo ajira za walimu tumeajiri sana mwaka2015 hawakuzidi 30,000.Kilimo kinachoajiri 70% sasa kinakua kwa1.7% , kiasi ambacho nichini kupata kutokea tangu Uhuru.
David KAFULILA
Juni27,2017
REPOTI YA IMF KUHUSU UCHUMI WETU JANA INATHIBITISHA KUWA BAJETI YA 2017/18 HAITEKELEZEKI KAMA ILIVYOKUWA 2016/17
Baada ya kusoma ripoti ya IMF kuhusu mwenendo wa uchumi na Bajeti Tanzania niligundua kitu kimoja muhimu kwamba bajeti ya 2017/18 haitekelezeki kama nchi itaendelea kukosa mikopo nje kutekeleza miradi mikubwa iliyopangwa tangu bajeti ya 2016/17 na sasa 2017/18.
Kwa muda sasa kama nchi imekuwa ngumu kupata mikopo nafuu (concessional loans) kutokana na masharti yake ya demokrasia na utawala bora. Zaidi sasa mikopo ya kibiashara toka nje imebaki kuwa migumu kutokana na taasisi za kimataifa kuanza kuisoma serikali kuwa 'anti business'.na mbaya zaidi hatujafanya credit rating ili kuhakikishia wawekezaji na banks kwa maana ya kupata mikopo kama ilivyokwishafanya Kenya na Rwanda kwa upande wa Africa Mashariki.
Lakini mazingira yalivyo ningumu kupata mkopo kuendesha bajeti. Ndio maana serikali imezidi kukopa ndani na kufanya deni la ndani kwenda juu na kuvunja rekodi tangu awamu ya tatu.Awamu ya tatu iliacha deni la ndani likiwa 1.7trilion, miaka10 ya awamu ya nne deni la ndani lilifikia 7.5trn mwaka 2015, sasa miaka miwili tu, deni limefika zaidi ya 11trilion.sawa na nyongeza ya 3.5trilion kwa miaka2tu.Hii ni hatari sana kwenye nchi ambayo mzunguko wa fedha ndani upo chini mno (tight liquidity ).
Hali ikibaki ilivyo nchi itazidi kuzama kiuchumi kwa kushindwa kugharamia mahitaji ya afya , maji na elimu kwasababu ukiangalia deni lililoiva mwaka jana ilikuwa 8trilion wakati mwaka huu ni 9trilion.sasa wakati deni liloiva mwaka huu ni 9trilion bado mshahara (wagebill) ni 7.6trilion.
Hii maana yake mshahara na deni peke yake ni 16.6trilion. Katika mazingira ya sasa ambayo kodi inayokusanywa kwa mwezi TRA ni wastani wa 1.1-1.2trilion, kwamba sio zaidi ya 14trilion kwa mwaka.
Hii maanake ni kwamba makusanyo yetu ya kodi hayatoshi japo kumudu deni la mshahara.kwamba tunakopa kulipa mshahara.hatujazungumza gharama zingine za kuendesha Serikali achilia mbali miradi ya maendeleo.
Tuna njia mbili za kufanya; 1.Lazma Seriakali ishughulikie mgogoro wa Zanzibar na isitishe ukandamizaji demokrasia ili iendelee kupata mikopo nafuu kwani kwa vigezo vya mikopo nafuu Tanzania inaweza kupata mikopo nafuu (concessional loans) kufikia $2.5bn sawa Tsh6tn.kwa mwaka, hiki nikiasi ambacho kinatosha sana kwa serikali kumudu miradi yake ya kimkakati (flagship projects) kama ujenzi wa reli, umeme, Bandari nk 2.
Lazma Serikali ikae na wafanyabiashara na kuwahakikishia kwamba Tanzania ni sehemu Salama kuwekeza na hivyo waweze kuingiza mtaji zaidi kwani hatuwezi kujenga uchumi wa viwanda kama hatupati mtaji toka nje (FDI ), China tunayoitazama leo kama Taifa la pili kwa ukubwa wa uchumi duniani baada ya USA, pamoja na msimamo wake wa ujamaa imefika hapo kuwa nchi ya pili kwa ukubwa wa uchumi duniani baada ya kuwekeza zaidi kwenye elimu, ufundi na technology lakini zaidi kuvutia mitaji toka nje hususan USA.
Lazma tujenge uchumi wakisasa kwa kuangalia dunia yaleo imefika wapi.tukirekebisha mazingira hayo ya kibiashara kwa kujenga imani kwa uwekezaji na biashara tutapata mitaji zaidi na zaidi mikopo ya kibiashara (commercial loans).
Lazma tufanye hivyo ili tuelekee ndoto ya Dira ya Taifa ya 2025, ambayo Kwa mujibu wa Poverty&Human Development Report 2014 inasema ili tufikie dira hiyo lazma pamoja na mambo mengine tuajiri walimu900,000 sawa na wastani wa walimu 90,000 kila mwaka. Leo ajira za walimu tumeajiri sana mwaka2015 hawakuzidi 30,000.Kilimo kinachoajiri 70% sasa kinakua kwa1.7% , kiasi ambacho nichini kupata kutokea tangu Uhuru.
David KAFULILA
Juni27,2017