Kafulila afichua siri za watumishi - kuna wanaolipwa 20,000,000/= kwa mwezi

Kafulila akiombewa na pepo anayemsumbua akitoka,ni mwanasiasa mzuri na angekuja kuwa chachu ya ukombozi wa taifa hili...
 
jadili hoja hakuna sababu ya kumshambulia kafulila. We rajeo unaonaje juu ya tofauti za mishahara ya watumishi wa umma bila kufuata uwiano wa utendaji na uwajibikaji wao katika utumishi?

usikonde na mchumia tumboni huyo atakuwa anafanya kwenye hayo mashirika yanayokwapua, mmsahau nhc mkurugenzi anakwapua ml 23, hi tofauti kubwa za mishahara ndiyo zinaleta viongozi jeuri na miungu watumishi, turudi enzi za mwl kulikuwa hakuna suala la wala nchi na wananchi, inabidi mfumo mzima wa mishahara ubadilishwe, na maposhoposho yote yafutwe, ndiyo yanaangamiza uchumi, safari nje ya kituo zitafutiwe utaratibu
 
Iyo mishahara inalipwa kwa nchi ambayo watu wake wanaishi chini ya dola moja kwa siku.
Mdr kilo tisa tuu na ambao wanasimamia uhai wa watu wenu wanyonge,ukienda kwa walimu ndo unaweza tapika zimia ela wanazopewa.
No wonder mtoto anamaliza std 7 hajui kusoma wala kuandika
 
Hili la posho za kusafiri nje pamoja na sitting allowance madhara yake ni makubwa sana kwa mustakabali wa Taifa. Ukiangalia kwa undani, moja ya sababu kubwa kwa nchi yetu kuwa na mikataba mibovu katika uendeshaji na utekelezaji wa miradi mbalimbali ni hili suala la sitting allowance pamoja na posho za kusafiri nje.

Mara nyingi pale linapotokea suala la kwenda kujadili ama kuandaa rasimu za mikataba mbalimbali wanaoteuliwa kwenda kufanya shughuli hizo sio wale wataalamu husika bali huteuliwa watu fulani ama hujiteua (kwa manufaa yao binafsi) kwenda kufanya shughuli hizo pasipo kuwa na uelewa wowote ili tu waweze kukomba hizo posho za safari na mwisho wa siku wanaishia kwenda kutalii tu bila kutekeleza kilichowapeleka huko.

Tatizo hili pia linaadhiri mfumo wa ajira katika maeneo fulani ya Serikali kwani waajiri wenyewe wanaangalia wapi kuna safari nyingi ama mishahara yake iko juu ili waweze kujichomeka wenyewe ama kuwaingiza wale wanaowafahamamu pasipo kuangalia uwezo wa kiutendaji na uadilifu kwa wale wanaowaweka kwenye nafasi hizo.

Hivi ni kwa nini watu hupenda kutoa takwimu za kubuni bila kuzifanyia uchunguzi...? Kwa mfano mimi nina ushahidi kuwa gavana wa BOT hulipwa USD 25,000 sio Tzs 20m . kwa hiyo natilia mashaka takwimu nyingine kwa kuwa kwa hii niiijuayo ya BOT governor imepunguzwa sana Tzs 20m sidhani kama Tanzania ingeweza kumpata ndulu kutoka WB!!!
 
Tanzania baada ya Mwl na azimio la Arusha tumebaki na Ubinafsi na wizi. Kama watawala wakisubutu kurudi kwenye chanzo tutasogea lasivyo tutaangamia kwa mikono yetu wenyewe.
 
kwa hio kwa kusema hivi anataka kuhalalisha hizo posho zao,ilituzione ni ndogo sana
alitakiwa kusema mwalimu naye anapata posho shilingi ngapi na kwa mwaka anapata emina ngapi-
 
Hivi ni kwa nini watu hupenda kutoa takwimu za kubuni bila kuzifanyia uchunguzi...? Kwa mfano mimi nina ushahidi kuwa gavana wa BOT hulipwa USD 25,000 sio Tzs 20m . kwa hiyo natilia mashaka takwimu nyingine kwa kuwa kwa hii niiijuayo ya BOT governor imepunguzwa sana Tzs 20m sidhani kama Tanzania ingeweza kumpata ndulu kutoka WB!!!

Usitilie mashaka takwimu pekee bali pia hicho kiwango kufuru kwa watumishi wa umma..hivi ni kweli alikosekana mtanzania mwingine ambae angeongoza BoT bila ya kuingia hii migharama ya mishahara?
 
afanye haraka kuyasema na mengine kabla ruling haijatoka maana atakosa pa kuyasemea
 
Good boy Kafulila angalau kwa kuthubutu kutujulisha mishahara na posho za hawa wakubwa;

1.Gavana wa benki kuu tsh.20m/-
2.Mkurugenzi mkuu NSSF tsh.18m/-
3.Junior Officer TRA & BOT tsh.7m/-
4.Mbunge tsh.1.8m/-

Pinda alitueleza mishahara ya hawa wafuatao;
5. Daktari tsh.900,000.00
6.Mhandisi tsh.600,000.00
7.Mhasibu tsh.368,000.00


Nami naongezea;
8.Mkurugenzi mkuu NHC tsh.20m/-

Hii nchi inaliwa na watu wachache sana, as if wao tu ndio watanzania!

Dah! Sijui Mizengo atakuwa analamba ngapi hapo!!
 
QUOTE=MANI;3252860]Ni kweli mkuu lakini kwa serekali gani? Bila kuiondoa CCM ili tuanze upya hii itakuwa ndoto. Angalia Zambia wenzetu wameanza kuangalia mikataba ambayo haina maslahi kwa nchi na ufisadi serekalini, lakini ni baada ya chama mbadala kuingia shime shime wa tz![/QUOTE]Sasa MANI ni nani atakayeiondoa CCM? Hawa jamaa wanaiba kura ni balaa! Hiki chama hakipo madarakani kwa ridhaa ya wananchi hata kidogo usidanganyike. uchaguzi uliopita jimboni segerea mahanga hakushinda waliingiza masanduku yenye kura izilizopigiwa kwenye ofisi za msimamizi wa uchaguzi mpaka ikaonekana mpendazoe kashindwa. amini ausiamini mahanga aliandaa sherehe ya shukrani wananchi wa kimanga na kisukuru na migobani wakakataa kwenda na wakamwambia akawashukuru waliomsaidia kuiba kura kwani wao hawajampa kura zao. Ifakara hivyo hivyo masanduku ya kummaliza Regia mtema yalitengenezwa mpaka mengine ikabidi zile kura wazimwage maporini maana walikuwa hawana pa kuzipeleka. madereva waliokuwa wanaendesha magari ya uchaguzi kama wapo humu jamvini watakuwa mashaidi wangu .
 
Hoja ya Mheshimiwa Kafulila ni nzuri lakini haina uliganifu. Inawezekana ni kweli kuwa hao waliotajwa wanalipwa fedha hiyo kama mshahara wao. Tatizo lipo katika watu waliotajwa hawalingani kwa nafasi zao, muda waliopo kazini elimu, umahiri wa kazi na kadhalika. Unaweza vipi kuliganisha Gavana wa benki na daktari anayeanza kazi leo au amefanya kazi miaka minne hivi. Nadhani ilikuwa sahihi kuliganisha Mkurungezi wa Muhimbili na Gavana wa benki.
Inasemwa maoofisa wa kawaida wa TRA wanalipwa milioni sita mpaka saba. Huyo ofisa wa kawaida wa TRA ni wa ngazi ipi? ana sifa zipi amefanya kazi miaka mingapi ana elimu ipi? Je madakitari mabingwa wanalipwa kiasi gani ? Maprofesa wanalipwa kiasi gani? Hoja yangu hapa ni kuwa tusijaribu kuwakinga wabunge tokana na nia mbaya ya kujilundikia mshahara kwa jina la posho bila kuhojiwa.
Mheshimiwa Kafulila na wengine wenye upeo kama wake waje na hoja za uliganifu wa mapato katika sekta zote na kutoa motisha kwa sekta ambazo tunahitaji kuziinua kwa haraka kuliko sekta nyingine, hiyo ni kawaida popote duniani.
Madaktari sio kwamba wanastahili malipo zaidi kwa kuwa watu wengine wanalipwa zaidi, la hasha wanastahili malipo kulingana na vyanzo vyetu vya mapato, na kujaribu kuwaweshesha kumudu maisha na kuwamotisha wafanye kazi yao ya kitaalamu. hakuna mtu ambaye anastahili kulipwa fedha ya walipaodi eti ili akitoka nje ya mlango wa bunge aweze kuwagawia watu fedha, yaani ni halali sasa kwa wapiga kura kuwa omba omba kwa wabunge wao na ni fahari kwa wabunge kugawa fedha kwa wapiga kura wao. Hii ni tabia chafu sana haipasi kuendekezwa hata kidogo. Ni fedha ngapi itawatosha wabunge hadi waweze kugawa fedha kwa wapiga kura wao wenye shida zisizo na ukomo.
Daktari naye sasa alipwe posho ambazo zitawawezesha wao kuwapa fedha wagonjwa za kununlia madawa maana hata wagonjwa huwa wanoomba fedha kwa madakitari. tuache uupuzi tujadili hoja ya msingi ya ulinganifu wa malipo kwa sekta zote na sio ulafi wa wabunge.
 
Badala ya kuwa tunalalamika tu hapa jukwaani, ingekuwa ni busara zaidi kama tungejikita kulijadili hili suala liandikwe vipi kwenye katiba mpya.
 
Japo aliosema ni ukweli usiopingika lakin ndio kaulizake nzuri za mwisho mwisho kwani Dr Mvungi alimshamfukuza huyo.

labda abaki kama Mbunge wa jimbo la mahakama
 
Hivi ni kwa nini watu hupenda kutoa takwimu za kubuni bila kuzifanyia uchunguzi...? Kwa mfano mimi nina ushahidi kuwa gavana wa BOT hulipwa USD 25,000 sio Tzs 20m . kwa hiyo natilia mashaka takwimu nyingine kwa kuwa kwa hii niiijuayo ya BOT governor imepunguzwa sana Tzs 20m sidhani kama Tanzania ingeweza kumpata ndulu kutoka WB!!!
Pamoja na mshahara mkubwa anaolipwa ndulu hakuna deliverables zozote uchumi hovyo kabisa, shilingi yetu inadorora kila siku bora aondoke kuliko kuzidi kuharibu uchumi wa nchi
 
Tukumbuke kuwa mishara inayojadiliwa hapa ni mishara ya taasi za serikali/agencies. Ukitaka kuziangalia, hizi taasisi/mashirika yameanzishwa kisheria kwa ajili ya kuregulate masuala fulani either fedha, hifadhi za jamii, miindombinu, mawasiliano, biashara, afya nk. Hawa wanafanya kazi independently na central/local government. Hawa ni kama semi-government, wanajiamulia mambo yao wenyewe, including mishahara.
Sioni kama haya mashirika yanatakiwa yalaumiwe kwa kuwa na kiwango kikubwa cha mishahara cuz ni kutokana na majukumu na dhamana waliyoibeba. Ndani ya hayo mashirika kuna madaktari, waalimu, wahandisi, wahasibu na watu wa kila professional!
Chamuhumu hapa ni kuangalia serikali itainua vipi mishahara ya watumishi wake wa Central n Local government ireflect current state ya economy na mfumuko wa bei uliopo!

Hongera angalau kwa kuanza kujadili mada hata kama ina mapungufu!
 
Back
Top Bottom