Wiki lilopita nilikuwa wilayani Kilolo mkoani Iringa nilijawa na furaha baada ya kuona mabadiliko makubwa katika fikra za watu wote wakisema wamechoswa na CCM, nilifika mpaka kijiji cha ukumbi ambako niliambiwa kuwa Mwenyekiti wa Kijiji ni kutoka CHADEMA, na mabadiliko hayo kwao yamewaletea neema kwani umekuwa ni uongozi sikivu na unaowajali Wananchi, nilishangaa sana kuona kijiji cha porini kama vile kukawa na mabadiliko makubwa ya namna ile na watu wakichambua udhaifu wa serikali ya CCM Iliyopo madarakani. mtazamo wangu ni kuwa vijijini sasa wamekuwa moto kuliko watu wa mijini.