Kadiri Lowassa anavyojiimarisha CHADEMA, ndivyo chama kinavyofifia na kupotea

Chadema inakufa kifo cha mende kabisa ... tamaa ndio zinaponza chama hicho
 
Wewe unaona majukwaa ndo yanaitwa siasa!!! Si kweli ila mipango yenu baada juu ya taifa na wananchi. Ulaya hakuna mjukwaa ila watu wanaangalia sera na matangazo ya vyama mitandaoni na muda ukifika wanaamua.

Hata kwetu huku muda ukifika CCM itatoka tu hata kama haipendi. Na kweli haipendi.

Ila nani wa kuiondoa? Si upinzani wa namna hii.

Mwaka jana kura zote hazikutokana na sera ila kuchoka na CCM. Dalili za kuaminika kwa CCM ziko wazi ila upinzani unatakiwa uje na hoja za msingi za kusimamia serikali, bungeni hata mikutano ya ndani.

Hiki kitu kimekosekana. Na watu wameelewa zaidi ya mwaka jana.

Tusitegemee kusafiri kwa basi la mwaka jana kabisa!!!
Ulaya unaifananisha na hii bahari ya laana na upumbavu? Ulaya kuna fair ground ya politics sio hizi za dola kulinda wahuni kama akina Lipumba na kuiba kura!!!

Usiifananishe ulaya na wajalaana wenu!!
 
CHADEMA naitafsiri kama taasisi ya wathubutu,wakosoaji kwa kutumia hoja mujarabu na wapambanaji dhidi ya ufisadi na wizi wa mali za umma. Ni taasisi iliyojengwa na kuheshimika,kwa kuzoa maelfu ya wanachama kwa namna hiyo

CHADEMA ilipendwa na vijana makini na wasomi kwakuwa waliiona Tanzania waitakayo kupitia chama hicho kikuu cha upinzani nchini. CHADEMA ilikuwa taasisi ya kuwasemea wanyonge;kuwaumbua mafisadi;kuwakemea viongozi na kuandaa viongozi wajao. Ilikuwa CHADEMA ya kupigiwa mfano na kuaminika.

CHADEMA imebadilika baada ya kuhamia humo kwa Waziri Mkuu aliyejiuzulu,Edward Ngoyai Lowassa. Sasa,imeanza kupoteza-tena kwa kasi sifa na vivutio nilivyovieleza hapo mwanzo. Lowassa alihamia CHADEMA na watu wake. Kwa maneno mengine,alihamia na 'chama chake'. Tayari yeye na watu wake wameshachomoza na kushika nafasi mbalimbali ndani ya CHADEMA.

Kadiri Lowassa anavyojikita na kujiimarisha,ndivyo 'ile CHADEMA' inavyopotea. Kilele cha kupotea kwa CHADEMA ile kitakuwa wakati wa uchaguzi mkuu wa ndani ya CHADEMA. Hapo patakuwa ni kati ya chama cha Lowassa na chama cha CHADEMA!

Kwaheri 2016,karibu 2017!
Lowasa yeye hana muda na chama yeye anatafuta mashabiki, yaani uchaguzi utajapofika atakuwa kama mgombea binafsi ndani ya chama
 
Wewe utakua mbumbumbu sijui huo uwakili ni wa msituni? Hivi unyafuzi umeharibu akili yenu hivi? Hujui jukumu la vyama siasa ni kushinda chaguzi? Yaani ung'ang'ane na mengine then usishinde chaguzi? Ujinga ni mzigo mzito sana kwahiyo chama cha siasa kuongeza idadi ya kura ni kufifia au kuimarika? Unatia kinyaa!!

Hapo ndipo shida ilipo kwa tulioangukia kwenye "Great Dissapointment"
Wale tuliojua tunaitafuta Tanzania mpya yenye mtazamo mpya na attitude mpya, hatukujua kuwa lengo ni kupata tu kura na kushika madaraka. Hiyo ni sawa tu na zama za Afrika kudai uhuru kutoka kwa mkoloni ni kisha uongozi mpya wa kiafrika ukagawana keki ya Taifa kwa itikadi ya "Wakati wetu kula".

Wale tulioamua kukaa pembeni kwa sasa (Tuko wengi sana, hata huko juu kwenye uongozi wa Chadema tupo) hatukuwahi kutarajia Chadema ingekuwa ya kutaka madaraka tu na sio kuibadili Tanzania.
 
ngoja waje akina mwahabari huru,nibozali,erythrocity,kisu cha ngariba na vijana wengine toka ufipa wamwage povu .
 
Mimi ningeku
CHADEMA naitafsiri kama taasisi ya wathubutu,wakosoaji kwa kutumia hoja mujarabu na wapambanaji dhidi ya ufisadi na wizi wa mali za umma. Ni taasisi iliyojengwa na kuheshimika,kwa kuzoa maelfu ya wanachama kwa namna hiyo

CHADEMA ilipendwa na vijana makini na wasomi kwakuwa waliiona Tanzania waitakayo kupitia chama hicho kikuu cha upinzani nchini. CHADEMA ilikuwa taasisi ya kuwasemea wanyonge;kuwaumbua mafisadi;kuwakemea viongozi na kuandaa viongozi wajao. Ilikuwa CHADEMA ya kupigiwa mfano na kuaminika.

CHADEMA imebadilika baada ya kuhamia humo kwa Waziri Mkuu aliyejiuzulu,Edward Ngoyai Lowassa. Sasa,imeanza kupoteza-tena kwa kasi sifa na vivutio nilivyovieleza hapo mwanzo. Lowassa alihamia CHADEMA na watu wake. Kwa maneno mengine,alihamia na 'chama chake'. Tayari yeye na watu wake wameshachomoza na kushika nafasi mbalimbali ndani ya CHADEMA.

Kadiri Lowassa anavyojikita na kujiimarisha,ndivyo 'ile CHADEMA' inavyopotea. Kilele cha kupotea kwa CHADEMA ile kitakuwa wakati wa uchaguzi mkuu wa ndani ya CHADEMA. Hapo patakuwa ni kati ya chama cha Lowassa na chama cha CHADEMA!

Kwaheri 2016,karibu 2017!
Mimi ningekukubalia kama fursa zote zingetolewa sawa kwa vyama vya siasa halafu ndio tuone huo ufhaifu.
Lkn huwezi kumjaji mwenzako wakati wewe anatumia jeshi, polisi, viongozi wa serikali ktk kuidhibiti chadema halafu utakuja hapa unasema inafifia.
Ni haina ya mawazo ya MTU muoga, asiependa ushindani, asijiamini na mwenyekupenda kupendelewa.
Ni sawa na bondia atakaejisifu kushinda pambano wakati upinzani wake wamefungwa MIKONO.
 
CHADEMA naitafsiri kama taasisi ya wathubutu,wakosoaji kwa kutumia hoja mujarabu na wapambanaji dhidi ya ufisadi na wizi wa mali za umma. Ni taasisi iliyojengwa na kuheshimika,kwa kuzoa maelfu ya wanachama kwa namna hiyo

CHADEMA ilipendwa na vijana makini na wasomi kwakuwa waliiona Tanzania waitakayo kupitia chama hicho kikuu cha upinzani nchini. CHADEMA ilikuwa taasisi ya kuwasemea wanyonge;kuwaumbua mafisadi;kuwakemea viongozi na kuandaa viongozi wajao. Ilikuwa CHADEMA ya kupigiwa mfano na kuaminika.

CHADEMA imebadilika baada ya kuhamia humo kwa Waziri Mkuu aliyejiuzulu,Edward Ngoyai Lowassa. Sasa,imeanza kupoteza-tena kwa kasi sifa na vivutio nilivyovieleza hapo mwanzo. Lowassa alihamia CHADEMA na watu wake. Kwa maneno mengine,alihamia na 'chama chake'. Tayari yeye na watu wake wameshachomoza na kushika nafasi mbalimbali ndani ya CHADEMA.

Kadiri Lowassa anavyojikita na kujiimarisha,ndivyo 'ile CHADEMA' inavyopotea. Kilele cha kupotea kwa CHADEMA ile kitakuwa wakati wa uchaguzi mkuu wa ndani ya CHADEMA. Hapo patakuwa ni kati ya chama cha Lowassa na chama cha CHADEMA!

Kwaheri 2016,karibu 2017!
Mkuu naona umeamua kujiunga Mtaa ule kiFIKA....ili chama...kisike ..lazima kifanye Siasa jiulize Baada ya Uchaguzi uliisiikia Chadema.kwenye Jukwaa..gani ingekuwa hivyo unavyoamini mtukufu angeshatengeu...kauli yake
 
Tatizo linavyovikabili vyama vya Upinzani Tanzania kwa sasa(CHADEMA kikiwemo), ni kunyimwa fursa ya kufanya shughuli zao za kisiasa.

Sio Lowassa wala Sumaye.

Tusitafutane Uchawi.

Umenena kweli, bunduki na mabomu yanapotumika kufinya demokrasia ndiyo tatizo
 
Kazi ya wataalam ni kuchambua hali halisi na kazi ya watendaji ni kuandaa sera na kutekeleza. Huu uchambuzi uko vizuri sana.

Ila wasiwasi wangu ni wale wanaoona kila uchambuzi ni kinyume na chama au kiongozi fulani hasa wa upinzani.

Nafikiri CHADEMA inaweza okolewa na sisi tusiotaka vyeo na tunataka chama kisimame kabla ya kusimamia.

Tunahitaji fikra mbadala za chama na kuwaambia kwa uwazi Mbowe na EL wasitafute vyeo tena humo ndani, maana walipofikisha chama 2015 inaonyesha ni hatua za mwisho kabisa za ukuaji wa upinzani Tanzania.

Tunahitaji viongozi watakaofikiri tofauti na kwenda na changamoto mpya na mawazo mapya.

Heri ya mwaka mpya wote.
Natamani mbowe angesoma ulichokiandika hapa
Safi sana muraaaaaa
 
Chama kikiimarika,kura huongezeka tu Mkuu. Punguza lugha kali tujadiliane kwa kujenga
Siku hizi mnajitoa akili sanaa,unafikir watu dizain ya kina lipumba wameishaaa.Mpo wengi sana,mmeanza kujilipua taratibu kwa kujidai kuipenda CDM hata kina Machali wamejitoa ufahamu kidogo.Inshort wamekosa dira,kwa sasa hakuna kelele yoyote itayoturudisha nyuma zaid ya 2020 kumuondoa mtu madarakani
 
Hilo lipo dhahiri.

Watu wa Lowassa hawataki kukubali ukweli
Mbowe anaogopa kugeuka jiwe.

CDM mpya lazima iwatose Lowassa na Mbowe. Je inawezekana?
 
Tatizo linavyovikabili vyama vya Upinzani Tanzania kwa sasa(CHADEMA kikiwemo), ni kunyimwa fursa ya kufanya shughuli zao za kisiasa.

Sio Lowassa wala Sumaye.

Tusitafutane Uchawi.
Chama ni vikao,wapi mmenyimwa ruhusa ya kufanya vikao?
 
Hapo ndipo shida ilipo kwa tulioangukia kwenye "Great Dissapointment"
Wale tuliojua tunaitafuta Tanzania mpya yenye mtazamo mpya na attitude mpya, hatukujua kuwa lengo ni kupata tu kura na kushika madaraka. Hiyo ni sawa tu na zama za Afrika kudai uhuru kutoka kwa mkoloni ni kisha uongozi mpya wa kiafrika ukagawana keki ya Taifa kwa itikadi ya "Wakati wetu kula".

Wale tulioamua kukaa pembeni kwa sasa (Tuko wengi sana, hata huko juu kwenye uongozi wa Chadema tupo) hatukuwahi kutarajia Chadema ingekuwa ya kutaka madaraka tu na sio kuibadili Tanzania.
Umenena vyema, lengo si tu kubadili jina la chama tawala na sura za wanaotawala, tunahitaji mabadiliko ya kweli yanayolenga kumkomboa mtanzania
 
kwa uongozi wa jpm hata dr slaa angekuwepo angeishia kisongo.kwa sasa nchi yetu inaongozwa kwa mkono wa chuma...siasa mpaka 2020.
 
Hivi Tanzania bado shughuli za kisiasa zinaruhusiwa? Au mimi nipo nchi nyingine? Maana nijuavyo kwa sasa shughuli za kisiasa Tanzania zimesimamishwa na zinaelekea kuuawa. Na mimi napendekeza wapinzani wanyamaze tu wala wasihangaike na siasa maana kila wakati wakitaka kufanya siasa wanaumizwa tu na vyombo vya dola wakati akina Mselewa wakidunda ofisini. Huwa nawashangaa sana watanzania wanapoona kama vile uwepo wa wapinzani ni faida ya wapinzani wenyewe badala ya kujua kuwa ni faida kwa Taifa na serikali iliyopo madarakani. Hivi kweli unafikiri bila upinzani kuna kila cha maendeleo kitafanyika? Kwa kawaida mwanasiasa na serikali huwajibika kwa kuogopa kunyimwa kura tu na si vinginevyo. Sasa kama mwanasiasa aliyepo madarakani hana mpinzani ataogopa nini? Utamnyima kura halafu umpe nani? Watanzania hata 'waliosoma' ni shida tu. Hivi ni kwa nini? Natamani zije zile zama za kupigia kura mtu na kivuli ili wanasiasa watuadabishe watanzania labda akili zitakuja.
 
Back
Top Bottom