Kadampinzani asema: MBOWE AHOJIWE!

Status
Not open for further replies.

KadaMpinzani

JF-Expert Member
Jan 31, 2007
3,715
86
Naam ni yule mwenyekiti chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) Freeman Aikaeli Mbowe. Wiki iliyopita aliweza kutoa maneno makali ambayo kwa kweli ukiangalia kiundani kama unaipenda nchi yako basikamwe hutoweza kuacha hizo kauli ziende tu hivi hivi !

Mbowe ambae anakabiriwa na kesi ya kutolipa mamilioni ya shilingi aliyokopa NSSF aliyokopa kuendesha biashara yake, alisema kwamba vifo vya Marehemu Amina Chifupa na Ballali ambae alikuwa gavana wa benki kuu ya Tanzania wameuliwa na CCM.

Sidhani kama kweli mtu ambae hakumaanisha anaweza kuongea mambo mazito kama haya. Hata kama tofauti za kisiasa mtu mwenye akili timamu hawezi kuongea maneno mazito kama haya halafu ategemee asihojiwe na vyombo vya dola. Kwa kweli nchi yangu ya Tanzania naipenda, na ndio maana nasema Mbowe ahojiwe ili aweze kutoa ushahidi wa kutosha na hao walioshiriki waweze kukamatwa na sheria ishike mkondo wake.

Bwana Mbowe alinukuliwa akisema, "Kuteketea kwa Ballali, tutaamini kuna mkono mchafu wa baadhi ya viongozi wa serikali, kwa sababu ni shahidi muhimu katika vita ya ufisadi. Wasifikiri kufa kwa Ballali, ndiyo mwisho wa mapambano, lakini nawaambia ndiyo kwanza vita ya ufisadi itapamba moto." hapo hapo pia aliendelea na kusema, "“Ufisadi na mchezo mchafu wa CCM, umewatesa watoto wetu, wazazi wetu na sasa basi, tutapambana hadi watakapouana wote waishe. Wamemuua Ballali, Amina Chifupa wataendelea kuuana,” . Hata hivyo Mbowe aliendea kuongea maneno hayo bilaya kutoa ushahidi wa kina ambao unaweza kuwafunga CCM na hao marehemu waliofariki.

- - - - - - - - - - - - - -MWISHO - - - - - - - - - - - - - - - -

Nini kinachotakiwa kifanyike:

(a) Kwa kuwa mbowe ana uhakika kwamba ccm imewaua hao watu, basi afikishwe kwenye vyombo vya dola na kuhojiwa ili kutoa ushahidi mzima.

(b) Kutokana na ushahidi atakaotoa, hao wafuatiliaji waweze kulinganisha na hali halisi ya matukio yaliyotokea ili kupata ukweli !

Naamini Mbowe atakuwa anajua zaidi ya hayo aliyosema, hivyo ahojiwe ili kupatikana ukweli !
 
KadaMpinzani,

Hata kama unamchukia Mbowe hivyo, kweli unataka ahojiwe kwa hili?

Huo muda si afadhali tuwahoji hao majambazi wa EPA, Richmond, Meremeta nk. badala ya kuhangaika na akina Mbowe?

Nafikiri pia ni muumini wa freedom of speech kama ambavyo wewe mwenyewe unafaidika na uhuru huo haja JF, kweli kuna haja ya kuandika uliyoyaandika hapo juu?

Mwacheni Mbowe afanye kazi za chama chake.
 
KadaMpinzani,

Hata kama unamchukia Mbowe hivyo, kweli unataka ahojiwe kwa hili?

Huo muda si afadhali tuwahoji hao majambazi wa EPA, Richmond, Meremeta nk. badala ya kuhangaika na akina Mbowe?

Nafikiri pia ni muumini wa freedom of speech kama ambavyo wewe mwenyewe unafaidika na uhuru huo haja JF, kweli kuna haja ya kuandika uliyoyaandika hapo juu?

Mwacheni Mbowe afanye kazi za chama chake.

hachukiwi mbowe, bali naomba nikuulize swali ! wewe kama kweli unaipenda nchi yako, ungependa kuona viongozi zaidi na zaidi wakiuliwa WAKATI MBOWE ANAO USHAHIDI KUONYESHA KWAMBA CCM NDIO WANAUWA VIONGOZI WENZAO ?? na yeye mwenyewe keshasema hadi wamalizane hao (huoni uchochezi huo?)!!

Mbowe anayo evidence maana siamini kama aliropoka alivyokuwa akitoa kauli zile !

wewe unaiita freedom of speech wakati ndio kitu kitakachomjenga kisiasa ! anajua akipakazia vitu vya uongo ndo atajijenga zaidi kisiasa, lakini sidhani kama nina chuki dhidi ya mbowe ! sipendi na sipendi kuona viongozi zaidi wakiuliwa wakati mbowe anajua njia inayotumika kuwaua hao viongozi ! ahojiwe ili matukio zaidi yasitokee !
 
wewe unaiita freedom of speech wakati ndio kitu kitakachomjenga kisiasa ! anajua akipakazia vitu vya uongo ndo atajijenga zaidi kisiasa, lakini sidhani kama nina chuki dhidi ya mbowe ! sipendi na sipendi kuona viongozi zaidi wakiuliwa wakati mbowe anajua njia inayotumika kuwaua hao viongozi ! ahojiwe ili matukio zaidi yasitokee !

Kada Mpinzani
Sijui hili jina unalitumia kwa nini!! Narudia kukuuliza tena wewe unapojiita kada Mpinzani Unapinga nini?? Sisi tunajiita Wapinzani maana tunapinga UFISADI wa CCM!!!

Unamshambulia Mbowe mpaka kila mmoja wetu amesharidhika kuwa assignment uliyopewa ni kum-embarass Mbowe. Najua wazi unafanya kazi ambayo huijui. Pili najua kuwa unamshambulia mtu ambaye humjui!!
Kama ungeijua task uliyopewa na ungejua unapambana na nani ungekuwa umeshaacha zamani. Maana kelele zako, unafiki wako, majungu yako, ushambenga wako na kila maudhi unayoingiza katika jukwaa dhidi ya Mbowe hayamshtui hata dakika moja.
Sana sana anakuhurumia tu mlala hoi wewe unatumiwa hovyo bila kujua thamani yako halisi.

Kwaheri.
 
Nakupongeza kada mpinzani kwa hoja yako namimi. Nakuunga mkonokwamba Mbowe ahojiwe na wala sio swala la kumchukia huyo ni kiongozi wa chama kikubwa cha siasa.

Hivyo kauli yake una ushawishi mkubwa mbele ya wanachama wake na wananchi kwa ujumla. Ili kukomesha kauli hizo kwa maana yeye anawatambua wauwaji wa viongozi hao aisaidie polisi kwa kuwataja wauwaji hao ili waweze kukamatwa na kufikishwa kwenye mbele ya sheria nakupongeza sana.
 
KadaMpinzani,

Hata kama unamchukia Mbowe hivyo, kweli unataka ahojiwe kwa hili?

Huo muda si afadhali tuwahoji hao majambazi wa EPA, Richmond, Meremeta nk. badala ya kuhangaika na akina Mbowe?

Nafikiri pia ni muumini wa freedom of speech kama ambavyo wewe mwenyewe unafaidika na uhuru huo haja JF, kweli kuna haja ya kuandika uliyoyaandika hapo juu?

Mwacheni Mbowe afanye kazi za chama chake.

Mkuu naona umemrudisha huko huko maana yeye anachagua moja
 
Nakupongeza kada mpinzani kwa hoja yako namimi. Nakuunga mkonokwamba Mbowe ahojiwe na wala sio swala la kumchukia huyo ni kiongozi wa chama kikubwa cha siasa.

Hivyo kauli yake una ushawishi mkubwa mbele ya wanachama wake na wananchi kwa ujumla. Ili kukomesha kauli hizo kwa maana yeye anawatambua wauwaji wa viongozi hao aisaidie polisi kwa kuwataja wauwaji hao ili waweze kukamatwa na kufikishwa kwenye mbele ya sheria nakupongeza sana
.

ni kweli kabisa mzee, maana hata mimi binafsi nisingependa siku naamka nasikia mbowe hatunae tena, kama atahojiwa it will work for him, for her, for them and most of all for us ! ila yeye kama anaamini alichosema ni kweli, basi ahojiwe !

atoe evidence inayoonyesha amina chifupa na ballali wameuliwa na ccm ! maana kuna wengi saaaaaaaaana ambao wanajua siri za ufisadi uliobakia na sidhani kama tungependa kuona hao mashahidi nao wakiondoka hivi hivi !

au kama pia alikuwa anapakazia tu kisiasa, basi aseme watu wamove-on ! lakini for the time being, HALALI MTU HADI KIELEWEKE !!
 
Ipole!!!!!!!!!!!!
Pole sana

hatuhitaji kupotoshwa hata kidogo. Sasa hivi our main concern ni UFISADI and herewith KIFO CHA KUTATANISHA CHA BALALI.
Tunamtafuta Mbowe ahojiwe kwa kutaka ukweli gani usiofahamika. Kifo cha Balali ni Kutoa magamba kwa Game la UFISADI. Tutumie nguvu zetu zote kwa pamoja kushambulia ufisadi.
 
Ipole!!!!!!!!!!!!
Pole sana

hatuhitaji kupotoshwa hata kidogo. Sasa hivi our main concern ni UFISADI and herewith KIFO CHA KUTATANISHA CHA BALALI.
Tunamtafuta Mbowe ahojiwe kwa kutaka ukweli gani usiofahamika. Kifo cha Balali ni Kutoa magamba kwa Game la UFISADI. Tutumie nguvu zetu zote kwa pamoja kushambulia ufisadi.
 
Mkuu KM,

Naona umehitimu sasa maana hata mkapa wakati anaambiwa kuwa watu wanapora pesa za wananchi na yeye alijibu kama wewe kuwa mwenye ushaidi apeleke, lakini sasa ushaidi upo njenje, subiri siku moja mizimu ya watu mnaowaua itakapoamka na kudai haki yao ndo utajua kuwa na wewe umeponea chupuchupu kwa kuwa hauropoki hovyo au huna data za kutosha kusababisha wenzako wakuone kama tishio na kukukolimba.
 
Kada Mpinzani
Sijui hili jina unalitumia kwa nini!! Narudia kukuuliza tena wewe unapojiita kada Mpinzani Unapinga nini?? Sisi tunajiita Wapinzani maana tunapinga UFISADI wa CCM!!!

mzee nashukuru sana kwa hili swali lako ! lakini nakushauri bonyeza profile yangu then angalia posts zangu za mwanzoni kabisa, nafikiri ndio utajua kwa nini nina jina la KadaMpinzani !! Hili swali nafikiri sio wewe tu unayeuliza, bali ni wengi sana humu ndani. Kama utaweza pia, jaribu kuuliza members wachache ambao walikuwa hapa from the beginning kabisa ndio utaelewa zaidi !

Nilipoingia humu kazi yangu ilikuwa ni moja na moja TU ! Kuipinga, kuishauri, kupendekeza machache kwa serikali lakini sikuwa based on any chama ! Lakini baadae nikagundua uchochezi unaongezeka humu ndani, kipindi hicho hata mbowe alikuwa member humu ndani, na nakumbuka nikamwandikia email mbowe kuhusu kumshauri masuala ya kuishinda ccm kwenye chaguzi, na haki ya Mungu alinijibu papo hapo ! But thats not what i was turned off by, lakini kulikuwa na increasingly pressure na uchochezi uliojaa na uonevu dhidi ya chama kimoja. Nilijaribu kugeuza mtazamo wa forum, kuhusu kuwajadili na wapinzani pia, lakini wapi, watu wakasema kwa nini wewe kada usiendelee kuwajadili hao wapinzani ? well, sikukata tamaa, lakini trust me mambo mengi i was turned off by. for more info, nenda kwenye posts zangu za mwanzoni kabisa !!
 
Kada Mpinzani
Sijui hili jina unalitumia kwa nini!! Narudia kukuuliza tena wewe unapojiita kada Mpinzani Unapinga nini?? Sisi tunajiita Wapinzani maana tunapinga UFISADI wa CCM!!!

Unamshambulia Mbowe mpaka kila mmoja wetu amesharidhika kuwa assignment uliyopewa ni kum-embarass Mbowe. Najua wazi unafanya kazi ambayo huijui. Pili najua kuwa unamshambulia mtu ambaye humjui!!
Kama ungeijua task uliyopewa na ungejua unapambana na nani ungekuwa umeshaacha zamani. Maana kelele zako, unafiki wako, majungu yako, ushambenga wako na kila maudhi unayoingiza katika jukwaa dhidi ya Mbowe hayamshtui hata dakika moja.
Sana sana anakuhurumia tu mlala hoi wewe unatumiwa hovyo bila kujua thamani yako halisi.


Kwaheri.


thats my own personal welfare, and i dont think kadampinzani here is the talk of the thread ! ishu hapa ni mbowe kuhojiwa kwa kauli alizotoa na sio kadampinzani ! shukrani !
 
Mkuu KM,

Naona umehitimu sasa maana hata mkapa wakati anaambiwa kuwa watu wanapora pesa za wananchi na yeye alijibu kama wewe kuwa mwenye ushaidi apeleke, lakini sasa ushaidi upo njenje, subiri siku moja mizimu ya watu mnaowaua itakapoamka na kudai haki yao ndo utajua kuwa na wewe umeponea chupuchupu kwa kuwa hauropoki hovyo au huna data za kutosha kusababisha wenzako wakuone kama tishio na kukukolimba
.

hehe ! tusubiri mzee ! na kabla hilo halijatokea naamini kama mbowe atasema hiyo njia inayotumika kuua viongozi, basi naamini watu wenye ushahidi hawatokuwa na wasi wasi wa kutoa ushahidi pale wanapokuwa nao na hatimae kusaidia kukamatwa kwa hao mafisadi !

pengine ni kweli kwamba watu wengi wanao ushahidi lakini tatizo ni kupresent huo ushahidi kwa kuhofia kuuliwa (kitu ambacho mbowe anakijua nje ndani) ! Mbowe atasaidia sana kwa hili !
 
mzee nashukuru sana kwa hili swali lako ! lakini nakushauri bonyeza profile yangu then angalia posts zangu za mwanzoni kabisa, nafikiri ndio utajua kwa nini nina jina la KadaMpinzani !! Hili swali nafikiri sio wewe tu unayeuliza, bali ni wengi sana humu ndani. Kama utaweza pia, jaribu kuuliza members wachache ambao walikuwa hapa from the beginning kabisa ndio utaelewa zaidi !

Nilipoingia humu kazi yangu ilikuwa ni moja na moja TU ! Kuipinga, kuishauri, kupendekeza machache kwa serikali lakini sikuwa based on any chama ! Lakini baadae nikagundua uchochezi unaongezeka humu ndani, kipindi hicho hata mbowe alikuwa member humu ndani, na nakumbuka nikamwandikia email mbowe kuhusu kumshauri masuala ya kuishinda ccm kwenye chaguzi, na haki ya Mungu alinijibu papo hapo ! But thats not what i was turned off by, lakini kulikuwa na increasingly pressure na uchochezi uliojaa na uonevu dhidi ya chama kimoja. Nilijaribu kugeuza mtazamo wa forum, kuhusu kuwajadili na wapinzani pia, lakini wapi, watu wakasema kwa nini wewe kada usiendelee kuwajadili hao wapinzani ? well, sikukata tamaa, lakini trust me mambo mengi i was turned off by. for more info, nenda kwenye posts zangu za mwanzoni kabisa !!

Kwa hiyo wewe ni kati ya wale wanaofanya kazi sio kwa imani yao bali kwa kile ambacho wengine wamefanya? Yaani kwa sababu wengi hapa walikuwa wanakipinga ccm basi wewe ukaamua kuwa mtetezi wa ufisadi?

Watu kama wewe ndio walikuwa wanauza wenzao kuwa watumwa kwa waarabu.

Swali,

Je ulifanikiwa kubadili mwelekeo wa Forum? Wewe unatumiwa na mafisadi na hata mungu hawezi kuwa upande wako. Ndio maana juhudi zako zimeshindwa maana forum imebakia na imeongezeka kupinga ufisadi wa ccm kuliko hata uhamie huko.

Kwa maneno mengine, Kejeli zako dhidi ya wapinzani wa ccm zimejenga watu wengi kuipinga ccm.
 
thats my own personal welfare, and i dont think kadampinzani here is the talk of the thread ! ishu hapa ni mbowe kuhojiwa kwa kauli alizotoa na sio kadampinzani ! shukrani !

Fisadi ni fisadi tu, watu wanapigana na wizi wa mali ya watanzania na yeye anapigana na wapiganaji wenzake?
 
CCM naichukia kupita kiasi, lakini kama ni wajanja, hii ni golden opportunity, yani golden opportunity ya kunawisha mikono yao inayoshutumiwa ina damu ya Ballali.

Wamfungulie Mbowe kesi ya madai ya defamation and libel. Akishindwa kuthibitisha kwamba Ballali kauawa, kina Mbowe na wenzake watajifunza kwamba conspiracy theories sio za kuzisema hadharani kana kwamba una uhakika, na wataacha kuendekeza kupotosha Umma na vitu visivyo thibitika.

Lakini sidhani kama ni nguvu ya dola itumike. Kesi isiwe Criminal inayoendeshwa na Serikali, bali Civil case ya CCM dhidhi ya Mbowe. Ubaya wa kamata-hoji inayotumia nguvu za dola ni kwamba nchi inaweza kugeuka Police State, ambamo kila tamshi la maoni ya mtu linakuwa Criminal. Katika Civil Law framework, aliye udhiwa akashitaki bila kuingiza nguvu za dola.

CCM kama wajanja hapa lazima wamshtaki Mbowe.
 
CCM naichukia kupita kiasi, lakini kama ni wajanja, hii ni golden opportunity, yani golden opportunity ya kunawisha mikono yao inayoshutumiwa ina damu ya Ballali.

Wamfungulie Mbowe kesi ya madai ya defamation and libel. Akishindwa kuthibitisha kwamba Ballali kauawa, kina Mbowe na wenzake watajifunza kwamba conspiracy theories sio za kuzisema hadharani kana kwamba una uhakika, na wataacha kuendekeza kupotosha Umma na vitu visivyo thibitika.

Lakini sidhani kama ni nguvu ya dola itumike. Kesi isiwe Criminal inayoendeshwa na Serikali, bali Civil case ya CCM dhidhi ya Mbowe. Ubaya wa kamata-hoji inayotumia nguvu za dola ni kwamba nchi inaweza kugeuka Police State, ambamo kila tamshi la maoni ya mtu linakuwa Criminal. Katika Civil Law framework, aliye udhiwa akashitaki bila kuingiza nguvu za dola.

CCM kama wajanja hapa lazima wamshtaki Mbowe.

Wataweza,

wajaribu kufungua kesi waone nguvu ya watanzania kwenye hii case. Kila mtanzania mwenye uwelewa kidogo tu wa sheria atakuja kumtetea Mbowe.

Na katika hii case ndipo wizi wote na pesa zilizotumika kuiweka ccm ikulu mwaka 2005 zitasemwa na kuandikwa waziwazi.

Nawashauri ccm wafungue kesi hii dhidi ya Mbowe kama wana ubavu
 
Pendekezo lako ni zuri. Ila mimi nilikuwa nadhani kuna listi ndeeefu ya viongozi ambao wanastahili kuhojiwa kwanza kabla hatujakimbilia kumhoji Mheshimiwa Mbowe. Mimi nilikuwa nafikiri wahojiwe kwanza;

1. Benjamin Mkapa - Kwa kuingia dili chafu (kiwira etc) akiwa ikulu, kinyume na maadili ya uongozi.

2. Mkurugenzi wa TAKUKURU - Kwa kukiri hadharani kwamba RICHMOND ni safi, kitu ambacho baadaye kiligundulika kuwa si kweli.

3. JK - (a) Kwa kutotekeleza ahadi yake ya "Maisha Bora kwa wote" aliyoitoa mwaka 2005, ambayo tumekuja shtukia kuwa alikuwa akiielekeza ahadi hiyo kwa washkaji wake wote (Maisha Bora kwa washkaji wote) na kwa bahati mbaya na sisi wananchi wa kawaida tukafikiria na sisi tumo humo ushkajini, kitu ambacho with time tumekuja ku-prove kuwa ni flat wrong.

( b) Kwa kutoifanyia kazi mpaka leo hii listi ya wauza unga aliyopewa na Amina Chifupa (RIP) pamoja na mikwara yote ya kutaka watu wampelekee majina.

(c) Kwa kutotumia executive power aliyonayo kumweka kifungoni Rais aliyemtangulia licha ya kuwa na vielelezo vyote kwamba alikiuka maadili ya uongozi akiwa Rais wa Jamhuri ya wadanganyika

( d ) Kwa kutowachukulia hatua watendaji wakuu wa serikali (wengine bado wamo madarakani) walioshirikiana na Balali (RIP) katika deals chafu za kuwaongezea wadanganyika umaskini

(e) .............

4. etc etc ...

Kuna wengi sana wa kuwahoji kabla hatujamfikia Mbowe. Kuna maswali mengi sana ambayo wadanganyika tunajiuliza na hatupati majibu yake ambayo niliowataja hapo juu na wengine niliowasahau wangeweza kutupatia kabla hatujamfikiria Mheshimiwa Mbowe.

Wakishahojiwa hao kwanza then ndio ulete rasmi pendekezo la kutaka kumhoji Mbowe. Ama wewe unaonaje ndugu Kada?
 
Nakupongeza kada mpinzani kwa hoja yako namimi. Nakuunga mkonokwamba Mbowe ahojiwe na wala sio swala la kumchukia huyo ni kiongozi wa chama kikubwa cha siasa.

Hivyo kauli yake una ushawishi mkubwa mbele ya wanachama wake na wananchi kwa ujumla. Ili kukomesha kauli hizo kwa maana yeye anawatambua wauwaji wa viongozi hao aisaidie polisi kwa kuwataja wauwaji hao ili waweze kukamatwa na kufikishwa kwenye mbele ya sheria nakupongeza sana.

Mafisadi wakubwa kwa udogo wanajitokeza taratibu, Kada endeleza hii thread ili mafisadi wote hapa JF wajulikane.

Ipole, kama ccm mna ubavu mfungulieni Mbowe kesi kwenye hili muone yatakayotokea. Ufisadi una mwisho wake na nyie ccm mwisho wenu umekaribia.
 
Status
Not open for further replies.
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom