Kada wa CCM afa kwa kunywa gongo akishangilia ushindi

Mtoto wa Mkulima

JF-Expert Member
Apr 12, 2007
681
126
Wakuu hii nayo kali

Kada wa CCM afa kwa kunywa gongo akishangilia ushindi
Na Abdallah Nsabi, Maswa

FURAHA ya ushindi wa Chama cha Mapinduzi CCM kupata ushindi wa Udiwani imemtokea puani mkazi wa kata ya Nguliguli Wilayani Maswa, Lonjini Petro (54) ambaye alikunywa lita tatu za pombe aina ya gongo na kufariki dunia.


Tukio hilo lilitokea juzi katika kata hiyo baada ya kutangazwa matokeo ya ushindi wa chama hicho ndipo Petro alipokwenda nyumbani kwa Gumba Mboje na kuangiza lita tatu za gongo ili anywe afurahie ushindi huo ambao alikuwa anausubiri kwa hamu.


Polisi wilayani hapa wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa kifo cha marehemu Petro kilitokana na ulevi wa pombe haramu aina ya gongo wakati akisherehekea ushindi wa mgombea udiwani wa CCM.


Chanzo cha habari kutoka katika eneo hilo kilisema kuwa Petro aliwekeana ahadi na mtu mmoja ambaye jina lake halikuweza kupatikana kuwa iwapo chama cha CCM kingeshinda wangenunuliana pombe aina ya gongo na kunywa mpaka asubuhi.


Inadaiwa kuwa mara baada ya ushindi wa chama cha Mapinduzi CCM, marehemu aliamua kujikita katika moja ya nyumba ambayo wanafanya biashara hiyo na kisha kuanza kunywa pombe hiyo haramu hadi kukutwa na umauti papo papo.


Marehemu huyo ambaye enzi za uhai wake alikuwa kada wa chama hicho, siku hiyo alifurahi kupindukia baada ya chama chake kushinda ndipo alikwenda kunywa kinywaji hicho kufurahi ushindi wa mgombea wao.


Baada ya kumwona mwenzao amezidiwa na kinywaji hicho kutokana na kuanguka chini na kuzimia walianza kumwagia maji ya baridi huku wakimpepea lakini baada ya muda mfupi aliaga dunia.


Inadaiwa kuwa Petro alikuwa na kawaida ya kunywa pombe, lakini akuwahi kulewa kama ilivyotokea siku hiyo .


Mbunge wa Maswa, John Shibuda, alithibitisha kutokea kwa kifo hicho cha mwanachama wa CCM na kuongeza kuwa hali hiyo ilimtokea wakati akishangilia ushindi wa mgombea wa CCM.


Alisema marehemu aliaga dunia mara baada ya Msimamizi wa Uchaguzi ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri kumtangaza mgombea wa chama kwa ushindi ndipo alipoamua kupiga mayowe na kisha kuelekea katika moja ya nyumba iliyokuwa inafanya biashara hiyo na kuagiza lita tatu za gongo na kuzinywa

http://www.mwananchi.co.tz/newsre.asp?id=2625
 
Duuh! Nimekimbilia kusoma haraka haraka nikifikiria KadaMpinzani nd'o ka... samahani sana Kada, simaanishi utani, it's true nimekimbilia hii thread...

SteveD.
 
Mambo ya kinywaji kikongwe hayo........kumbe sisiemu nao hawana adabu yaani wanakunywa gongo!!??. Pole nyingi kwa familia ya Petro. Jina la bwana lihidimiwe!!.
 
Duuh! Nimekimbilia kusoma haraka haraka nikifikiria KadaMpinzani nd'o ka... samahani sana Kada, simaanishi utani, it's true nimekimbilia hii thread...

SteveD.

heheheeeee, duh hiyo kali steve-d ! umeniacha mbavu wazi, mie mzima bana !
 
Wakuu hii nayo kali

Kada wa CCM afa kwa kunywa gongo akishangilia ushindi
Na Abdallah Nsabi, Maswa

FURAHA ya ushindi wa Chama cha Mapinduzi CCM kupata ushindi wa Udiwani imemtokea puani mkazi wa kata ya Nguliguli Wilayani Maswa, Lonjini Petro (54) ambaye alikunywa lita tatu za pombe aina ya gongo na kufariki dunia.


Tukio hilo lilitokea juzi katika kata hiyo baada ya kutangazwa matokeo ya ushindi wa chama hicho ndipo Petro alipokwenda nyumbani kwa Gumba Mboje na kuangiza lita tatu za gongo ili anywe afurahie ushindi huo ambao alikuwa anausubiri kwa hamu.


Polisi wilayani hapa wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa kifo cha marehemu Petro kilitokana na ulevi wa pombe haramu aina ya gongo wakati akisherehekea ushindi wa mgombea udiwani wa CCM.


Chanzo cha habari kutoka katika eneo hilo kilisema kuwa Petro aliwekeana ahadi na mtu mmoja ambaye jina lake halikuweza kupatikana kuwa iwapo chama cha CCM kingeshinda wangenunuliana pombe aina ya gongo na kunywa mpaka asubuhi.


Inadaiwa kuwa mara baada ya ushindi wa chama cha Mapinduzi CCM, marehemu aliamua kujikita katika moja ya nyumba ambayo wanafanya biashara hiyo na kisha kuanza kunywa pombe hiyo haramu hadi kukutwa na umauti papo papo.


Marehemu huyo ambaye enzi za uhai wake alikuwa kada wa chama hicho, siku hiyo alifurahi kupindukia baada ya chama chake kushinda ndipo alikwenda kunywa kinywaji hicho kufurahi ushindi wa mgombea wao.


Baada ya kumwona mwenzao amezidiwa na kinywaji hicho kutokana na kuanguka chini na kuzimia walianza kumwagia maji ya baridi huku wakimpepea lakini baada ya muda mfupi aliaga dunia.


Inadaiwa kuwa Petro alikuwa na kawaida ya kunywa pombe, lakini akuwahi kulewa kama ilivyotokea siku hiyo .


Mbunge wa Maswa, John Shibuda, alithibitisha kutokea kwa kifo hicho cha mwanachama wa CCM na kuongeza kuwa hali hiyo ilimtokea wakati akishangilia ushindi wa mgombea wa CCM.


Alisema marehemu aliaga dunia mara baada ya Msimamizi wa Uchaguzi ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri kumtangaza mgombea wa chama kwa ushindi ndipo alipoamua kupiga mayowe na kisha kuelekea katika moja ya nyumba iliyokuwa inafanya biashara hiyo na kuagiza lita tatu za gongo na kuzinywa

http://www.mwananchi.co.tz/newsre.asp?id=2625
Posho ya gongo ukute alipewa na chama ili apige kura
 
CCM wameamua kutoa kafara kwa kutumia gongo... mpk yatokee hayo inaelekea upinzani ulikuwa mkubwa sana. Kumbe usukumani bado kuna upinzani. Yajayo yanafurahisha
 
CCM wameamua kutoa kafara kwa kutumia gongo... mpk yatokee hayo inaelekea upinzani ulikuwa mkubwa sana. Kumbe usukumani bado kuna upinzani. Yajayo yanafurahisha


Ungefuatilia ziara ya mkuu ungejua CCM ina hali gani kanda ya Ziwa, ukweli si mahali salama tena kama zamani
 
Anhaa, Kumbe Alikuwa Msukuma!!!! Oky apambane tu na mboko za Mnyaazi Mungu huko Aliko!!!
 
Back
Top Bottom