migomo ya vyuo
Member
- Jun 14, 2011
- 58
- 18
Awali ya yote niwapeni pole ndugu jamaa na marafiki pamoja na wana CCM kwa kuondokewa na kada wao mkongwe ndugu Costantine Mushi aliyefariki jana baada ya kugongwa na gari.mzee wetu huyu atazikwa kijiji cha Shiri Njoro siku ya Alhamisi. aliwahi kutumikia CCM kwa muda mrefu kama katibu wa tawi na mpaka kifo chake alikuwa katibu wa tawi la shiri njoro. habari hizi zimethibitishwa na kada maarufu waCHADEMA wakati akiwa kwenye harakati za kuhamasisha watu wachangie mchango wa kununua jeneza ambapo kada huyu kijana wa chadema aliyewahi kugombea udiwani ambae pia ni katibu wa mbunge jimbo la hai amefanikisha zoezi hili kwa asilimia mia moja huku alipoulizwa umetoka wapi kukusanya Michango ya mtu wa CCm alijibu kwa kifupii Kwenye siasa hakunaadui wa kudumu na hili ni jambo lakijamii zaidi sii la kisiasa.