Uchaguzi 2020 Kachero Mbobevu Bernard Membe atua nchini, adai ukata umepelekea kusuasua kwa Kampeni za Vyama vya Upinzani nchini

mwanamwana

JF-Expert Member
Aug 1, 2011
1,076
4,113
BERNARD Membe, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha ACT-Wazalendo amesema, mazingira magumu ya Siasa kwa sasa, yamesababisha marafiki na wafanyabiashara kushindwa kuwasaidia. Na kwamba, kusuasua kwa kampeni hasa vyama vya upinzani nchini, kunatokana na ukweli kwamba, wagombea wengi wana ukata kwani hawana msaada tofauti na chaguzi zilizopita.

“Mnapokuwa katika mbio za urais, unatakiwa ukae ujipange kifedha na uwe na timu za kampemi, vyama vyote vyenye wagombea, wana ukata wa fedha sababu vyanzo vyetu vinavyokubalika kisheria, wafanyabiasha wanaotoa msaada wote wamekimbia, hatuna fedha,”

“Sababu nyingine, tunazuiliwa muingiza fedha, ukitaka kuingiza ama kutoa fedha, unakataliwa. Nikiwa rais, nitaboresha mfumo wa fedha kuiondoa changamoto hiyo,”

Akielezea sababu za kushindwa kuendelea na kampeni za urais kwa mujibu wa ratiba yake, amesema waliamua kusitisha kwa kuwa baadhi ya wagombea wa ubunge na udiwani kwenye chama chake waliwekewa pingamizi.

“Kilichotokea, baada ya kuteuliwa mgombea wa urais, sisi wabunge wetu zaidi ya 40 waliwekewa pingamizi.

Sasa akili inakutaka utafute changamoto ya tatizo kwanza. Huwezi kukurupuka peke yako, unawaacha wabunge na madiwani wamewekea pingamizi,” amesema Membe.

Akizungumzia safari yake ya Dubai Membe amesema, alikwenda kwa kuwa, ni ratiba yake ya kawaida kwa maana ndani ya mwaka mmoja anapaswa kwenda mara nne kutokana na shughuli zake binafsi.

“Kuna malalamiko kwanini ameenda Dubai kipindi hiki, huwa naenda Dubai mara nne kwa mwaka, kuna kampuni mimi ni mwanachama, sasa sikwenda mara mbili sasa nimeenda, lakini pia nimekwenda kucheki afya yangu,”

Mwanahalisi
 
Aache kulia lia Kama anao mvuto aombe achangiwe na Wananchi mbona Lissu anachangiwa tajiri gani atakubali kupewa kesi ya utakatishaji pesa?

Tunapambana hivyo hivyo Kama mabadiliko yanakuja yanakuja tu hakuna wa kuyazuia.
Wameshaomba kuchangiwa tuwaunge mkono.

Screenshot_20200915-133128.png
 
Kwa kinywa chake, nazidi kumshusha thamani siku hadi siku. Bora angekua anakaa kimya.

1. Ufadhili wa wafanya biashara
Kwani ikulu kuna biashara gan ambayo itamuwezesha kulipa fadhila.kumbuka wafanya biashara hawana pesa za kuchezea hovyo !!anachotoa jua utakirudisha tu.

2. Hawaruhusiwi kuingiza fedha
Hiz ndio zile wanaficha account za nje ya nchi au ndio uadhil wa mataifa ya nje? Kama ni ufadhil, ana mpango wa kuzirudisha vp akipewa madaraka?

Kachero mbabaishaji bwana!
 
Aache kulia lia Kama anao mvuto aombe achangiwe na Wananchi mbona Lissu anachangiwa tajiri gani atakubali kupewa kesi ya utakatishaji pesa?

Tunapambana hivyo hivyo Kama mabadiliko yanakuja yanakuja tu hakuna wa kuyazuia.
Mabadiliko yepi ya kuchangishwa pesa za kampeni kitu ambacho hakijawahi kutokea Tanzania.
 
Asije akawa amerudi na mabulungutu ya fedha chafu....Financial Inteligent Unit mchunguzeni kwa umakini
 
Ok kachero mbobezi BKM tunajua upo kazini na payslip inasoma km kawaidaaaa.

Watz sio wajinga
Watanzania hawahawa waliyoletewa Fisadi(Lowassa) na wakampigia kura awe rais wao? unataka wafanye nini tena ili ndio uone kuwa ni wajinga?
 
Back
Top Bottom