Kabwe Vs. Wangwe - kisa cha mafahali wawili?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Mojawapo ya magazeti yanayotoka leo nyumbani lina kichwa cha habari "Wangwe ampinga Zitto" kuhusu kauli yake kuwa uchumi wa nchi unakua. Hii si mara ya kwanza kiongozi huyo wa Chadema kumlenga kiongozi mwenzie aidha kwa uharaka wa kuzungumza na waandishi au kutokana na sababu binafsi. Kwa wale wanaokumbuka sakata la madini kule Tarime Wangwe alikuwa ni mmoja wa watu waliopinga sana kuhamishwa wananchi na kuna wakati aliwekwa lupango. Hata hivyo wananchi wa Tanzania wengi hawakumbuki mchango wake huo na harakati zake pamoja na Lissu kuhusu madini.

Hata hivyo hapa anakuja kijana ambaye hajalipa gharama ya uanaharakati na anaanza kuvuna matunda ya kazi za kina Wangwe kwa kuonekana ndiyo "mtetezi wa wananchi". Kwa Zitto kuendelea kutajwa tajwa haimsaidii sana Wangwe.

Wote wawili bila ya shaka ni watu wanaojiamini sana, wako huru kimawazo, wasio tayari kushauriwa na kusikiliza mashauri hayo. Sitashangaa wote wawili ndani ya Chadema wameanza kuwa "maverick politicians".

Wanasiasa hawa wawili wasipoangalia watakuwa ndio chanzo cha mgogoro ndani ya CHADEMA hasa kama wataendelea kutunishiana misuli kwenye vyombo vya habari. Vinginevyo tunachoanza kushuhudia ni vita ya mafahali wawili kama ya Mrema Vs. Marando, Nyerere Vs. Kambona, n.k

Binafsi nina ushauri ufuatao kwa wote wawili:

a. Stop talking to the press each time they extend their mics to you!

b. Tafuteni wasemaji wenu rasmi siyo kila kitu mkitolee maoni "no comment" nalo ni jibu.

c. Inapobidi mzungumze mjue ninyi mnazungumzia chama chenu hakuna kitu kama "maoni binafsi" kwa kiongozi wa chama!

d. Mitazamo yenu inapogongana zungumzeni kabla hayajafika kwenye vyombo vya habari.

e. Pale mnapotofautiana kimsingi na waandishi wanataka kujua, zungumzeni pamoja na waandishi siyo huyu anasema hili akiwa madongo kuinama na mwingine anasema lile madongo kuinuka! Mnawachanganya watu!

f. Kuna vitu vingine msivitoleee maoni hadi msikilize washauri!

Vinginevyo, mtaendelea kugongana hadharani na kuthibitisha kile ambacho Watanzania wanakifahamu kwa muda mrefu, wapinzani wana migogoro ya ndani!
 
Huwa najiuliza swali moja kila mara je CCM wakishindwa wapinzani wanauwezo wa kuongoza nchi? ni mara nyingi naonaga tuu wapinzani wakijigonga kimawazo na pia kimtazamo. Bado hawajaweza kuwa na msimamo na dira moja kuongea kama wapizani au chama. Nadhani haya ni mapungufu makubwa sana kwa viongozi wa chama ambacho kinawakilisha interest za chama na wanachama na si kama mtu binafsi. I think kama ulivyosema hapo juu sometimes kukaa kimya ni jibu pia. Hivi chama kama CHADEMA hakina msemaji wa chama ambaye anakuwa anatoa kauli ya chama? Wazee jipangeni vizuri muonyeshe kuwa mna uwezo wa kuongoza watu na muwape wananchi imani kuwa mnaweza kuwaongoza. Ndio inasemekana hawa viongozi wote wana msimamo na hawashauriki. Nadhani hiyo sifa ya kutokushaurika nayo sio sifa nzuri sana. Kaeni muongee kabla ya kwenda kwenye viombo vya habari kukuza biashara za magazeti kwa tofauti zenu.

Onyesheni mmekomaa kimawazo na kimshikamano, onyesheni mnaweza kuwa strong leaders ambao mna vision na sio kukimbilia nyumba ya habari maelezo na kuongea kama mtu binafsi. Nawatakieni kila la kheri katika kupigania masilahi ya taifa hili kwa faida ya taifa na wananchi wa Tanzania na si kwa ajili ya kutafuta umaarufu kama wengi tunavyoanza kuamini.
 
Kwa kuwa wote sasa ni "vingunge" ndani ya CHADEMA, kuna haja ya kutafuta namna ya kuwafunga "talking gavana" (vidhibiti kasi ya uongeaji bila kutafakari). Wajifunze kutoka kwa CCM jinsi walivyomdhibiti Makamba!

Migogoro iko hata ndani ya CCM, lakini CCM ni wajanja kwa kuwa mambo huwa wanayamaliza ndani ya chama na hayatoki nje kirahisi. Akina Butiku walitoa mambo hadharani baada ya kuona Mwenyekiti wao amejaa kiburi, lakini kama ni msikivu mambo huwa yanaishia kwenye CC na huwezi kusikia kasheshe nzito.

Tatizo la wapinzani wakati mwingine ni kusaka ujiko kwa nguvu zote hata kama wanafuka pumba. Umaarufu wa namna hiyo ndiyo unao ua vyama vya upinzani.
 
I have a feeling, kama hili siyo swala la misrepresentation ya press, tatizo ni kwamba there is less commitment to issues than self promotion and political "goal scoring".

Ndiyo maana you have all this bickering and concern about "who gets the credit" and "who is mentioned the most in the press"

They all risk sounding bogus and infected with "Mremaism"
 
true that.. maana leo gazeti jingine linasema "Spika Amshangaa Zitto" baada ya kuandika barua yake. Sasa Wangwe afanye nini ili na yeye jina lake litajwe kwa herufi kubwa?
 
true that.. maana leo gazeti jingine linasema "Spika Amshangaa Zitto" baada ya kuandika barua yake. Sasa Wangwe afanye nini ili na yeye jina lake litajwe kwa herufi kubwa?

Mmmmmh Mwanakijiji bwana unanichekesha kweli kumbe shida ni jina litajwe kwa herufi kubwa? Kama hivyo basi kazi ipo basi mwambie akajiunge na Ze Komedi ili aweze kuwa anaonekana kwenye TV!

Eee bwana thisi people have to be serious, inabidi wawe wanakaa na kufikiria kabla ya kukurupuka. You can market urself and brand urself kwa kazi yako unayofanya. Wananchi waone matutnda ya kazi yako na si kukimbilia kwenda kwenye magazeti (Mremaism).


Inabidi Chadema warestruche chama na waweke wazi majukumu ya kila kiongozi na akiongea anaongea kama CHADEMA na si mtu binafsi.

Hii sasa inakuwa kama ngonjera.

Wangwe ampinga Zitto

2007-12-26 10:26:41
Na Simon Mhina

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Chacha Wangwe, amesema madai yaliyotolewa na Mbunge wa Chama hicho Bw. Zitto Kabwe, kwamba uchumi wa nchi unakua, hayana ukweli na kwamba sio msimamo wa chama.

Hata hivyo, Bw. Wangwe, alisema yeye binafsi na baadhi ya viongozi wa CHADEMA hawaamini hata kidogo kwamba kauli hiyo ilitolewa na Bw. Zitto.

Akizungumza na Nipashe jana, Bw. Wangwe, ambaye pia ni Mbunge wa Tarime kupitia chama hicho, alisema kama kauli hiyo ina ukweli, ni ya kusikitisha na kushangaza kwa vile inaonekana kwamba Bw. Zitto amedandia gari la CCM.

`Mimi ndio maana wakati mwingine huwa nasema, kuna sababu gani kudandia gari la CCM kwa nyuma? Gari liko wazi kama mtu umelipenda unalipanda sio kudandia dandia, utavunjika mguu bure,` alisema Bw. Wangwe.

Mwanasiasa huyo alisema kwa vyovyote kama kauli hiyo ni kweli, Bw. Zitto, amejichongea sana kwa wananchi wake wa Kigoma Kaskazini ambao wameathiriwa kwa kisiasi kikubwa na mfumuko wa bei.

Alisema lengo la CHADEMA ni kuweka serikali mbadala ya kuongoza Tanzania na ili kufanikisha lengo hilo, lazima chama hicho kiwe na mawazo, falsafa na dira mbadala.

``Sasa utawekaje serikali mbadala kama huna sera mbadala?`` alihoji.

Mwanasiasa huyo alisema bado uchumi wa Tanzania uko chini na pengine kinachokuwa ni biasra na mapato ya wakubwa.
Alisema shilingi ya Tanzani inashuka thamani kila kukicha, huku zile za nchi jirani za Kenya na Uganda zikikua.

Bw. Wangwe alisema anashangazwa na msimamo wa Zitto, kushabikia ukuaji wa uchumi wa Tanzania ambao upo kwenye majedwali na takwimu.

``Uchumi wa Tanzania umekuwa kwenye takwimu tu, lakini si katika uhalisi. Sasa kama uchumi umekuwa mbona mfumuko wa bei ni kila siku?`` Alihoji.

Bw. Wangwe, alisema kwa mujibu wa sera za CHADEMA sekta ya kilimo ambayo imetelekezwa na CCM ndio njia pekee ya kuinua uchumi wa nchini.

Alisema uchumi wetu utaendelea kudidimia kwa vile serikali imeshindwa kukitengenezea kilimo sera nzuri na kuwaenzi wakulima kwa pembejeo.

Alisema hata miundombinu mibovu iliyopo, imewafanya wananchi wanaolima kienyeji kukosa pa kupeleka mazao yao.
Alisema kilimo kinaenda sambamba na viwanda, lakini serikali imeua viwanda vyote na kulifanya Taifa kuwa tegemezi katika bidhaa.

``Ndio maana Tanzania ni dampo la bidhaa feki, sisi ni jalala la kila bidhaa isiyo na viwango. Haya ni matokeo ya serikali kutotilia mkazo wa ujenzi wa viwanda,`` alisema.

Alisema badala ya serikali kuzipa kipaumbele sekta zitakazowainua wananchi wake, vigogo wamekazania migodi, kwa vile wanapata maslahi.

Alisema kwenye migodi wananchi waliokuwa wamejiajiri wamefukuzwa na hao wanaoitwa wawekezaji, ambao hulipa fedha kidogo kuliko mali wanayopata.

``Kwa hiyo nawaeleza watanzania kwamba uchumi haujakuwa na huo ndio msimamo wa CHADEMA.

Watu wenyewe ni mashahidi jinsi wanavyotaabika na maisha... Kama Zitto kasema hivyo, basi ana lake jambo, na huo ni msimamo wake binafsi,``alisisitiza.
http://www.ippmedia.com/ipp/nipashe/2007/12/26/105044.html
 
Wangwe as I see him ni mtu wa kutaka umaarufu tu na kutambulika,
ni kweli alifungwa kwa ajili ya kugombana na wezi wa madini kule Tarime,sasa mara Zitto anaingia na credit zote zinahamia kwake.But if you may recall kipindi kile Zitto anahusishwa na Amina Chifupa (RIP),alisema wazi kuwa kuna watu NDANI ya chadema hawamtaki na wanampinga sana kwani wana hofu kuwa anaweza kuwaharibia malengo yao ya kisiasa.Now was it Wangwe whom he meant or other (known to himself)?Only time will tell...
 
Umakini wa mwanasiasa ni pamoja na kutolazimisha kuwa on front page all the time.Ni lazima muelewe kuwa media can build your image and at the same time tannish your image.Matokeo ya kila wakati kuongea na media ni pamoja na kuongea pumba, kwani utalazimisha story ambazo hazina kichwa wala miguu ili mradi utoke.Umaarufu hautafutwi ila unakuja tu.Mr Wangwe na Zitto lazima mjue athari za kutofautiana katika kila jambo na kukimbilia kwenye vyombo vya habari.Kwa tabia hii mliyonayo ya kwenda kupingana katika vyombo vya habari mnajenga uadui ambao madhara yake yatakuwa kwa chama kizima.
 
They just need to be careful with the media. It is the media that promoted Mrema and it is the same media that demoted him. Sasa akili ni nywele na kila mtu ana zake.

By the way ni kweli kwamba Zitto alisema uchumi unakua, maana report zote zinaonyesha kuwa hali ya uchumi inazidi kuwa mbaya ikiwemo kukua kwa deni la taifa.
 
Wangwe anahitaji ku-back off tu, yeye kama baadhi ya viongozi wa CCM wanajaribu kudandia umaarufu wa hoja za Zitto, mbele ya wananchi, na I have a feeling kuwa huenda anatumiwa na CCM,

Reading betweeen the lines ya hizi new comments za the ishu inaonekana kuna baadhi ya "Watu" ndani ya Chadema, wameshaanza kuwa na wivu against mafanikio ya kisiasa ya kijana Zitto, unajua kuna swali mwananchi unapaswa kujiuliza WHO IS WANGWE? Na meshalifanyia nini taifa?

Kwa sababu we all know what Zitto, has done kwahili taifa letu! Tunawaomba wakuu huko Chadema, muacheni Zitto, aendeleze kazi ya kuliamsha na kuliokoa taifa letu, ambayo tayari ameshaianza na wananchi tumeiona tayari, na hata mataifa ya nje yameiona pia.

Mungu Ambariki Zitto, na Tanzania Yetu.
 
Ukisoma mawazo ya Wangwe utagundua kuwa hakupata kusoma taharifa aliyoisema Zitto. Isipokuwa ni kama alikuwa anakunywa kahawa mahala akakutana na Nipashe, kwa kukurupuka akaanza kumwaga hisia zake.

Next time inatakiwa aambiwe apate taharifa kamili kabla ya kutoa maoni yake halafu kama CHama (Sijui ametumwa na wanachadema au kila mtu ni msemaji wa Chadema?).

Zitto amesema uchumi unakua katika nyanja ya Madini na Utalii na akatoa maelezo kuwa hakuna faida inayopatikana, Kwa kifupi hakuna manufaa kwa taifa. Ukisoma kwa makini hana tofauti na kusema hakuna ukuaji wa uchumi.
 
Majuzi wangwe alipo pakaziwa na Nipashe tulionana pale G & G Hotel mjini hapa Musoma .Akawa analia lia kupakaziwa na waandishi ambao waliandika habri za yeye kuzomewa lakini wako Dar na hawakuwa kwenye mkutano huo .Mimi nilikuwepo pale Tarime na niliona Mkuu wa Wilaya anazomewa ila baadaye habari ikawa tofauti .Leo hii amesahau na anaanza kuwatumia wale wale waliomkandamiza ?

The best opetion kwao ni ku keep their mouth shut na kutafuta wasemaji wao ama wasemaji wa Chama .It is high time Chadema wajue kwamba wana watu nyuma na waache migogoro ya kiajabu .
 
Wangwe anahitaji ku-back off tu, yeye kama baadhi ya viongozi wa CCM wanajaribu kudandia umaarufu wa hoja za Zitto, mbele ya wananchi, na I have a feeling kuwa huenda anatumiwa na CCM,

Reading betweeen the lines ya hizi new comments za the ishu inaonekana kuna baadhi ya "Watu" ndani ya Chadema, wameshaanza kuwa na wivu against mafanikio ya kisiasa ya kijana Zitto, unajua kuna swali mwananchi unapaswa kujiuliza WHO IS WANGWE? Na meshalifanyia nini taifa?

Kwa sababu we all know what Zitto, has done kwahili taifa letu! Tunawaomba wakuu huko Chadema, muacheni Zitto, aendeleze kazi ya kuliamsha na kuliokoa taifa letu, ambayo tayari ameshaianza na wananchi tumeiona tayari, na hata mataifa ya nje yameiona pia.

Mungu Ambariki Zitto, na Tanzania Yetu.

Kaka umenena, ila kwa kumbukumbu zangu, wakati tatizo la Buzwagi linaanza, Wangwe alimfuata Zitto akiwa ametumwa na Barrick Gold ili amshawishi aende kutembelea migodi ya Barrick. Zitto alitoa masharti matatu:
1-Kwanza Barrick wamuandikie kwa maandishi kumualika na asiende peke yake.
2-Pili gharama zote za safari ajigharamie mwenyewe
3-Kila kitakachofanyika kiwe public na hakuna cha kuficha.

Baada ya kupewa masharti hayo, Wangwe hajaonekana tena (kuhusu suala hilo), na hiyo ikiwa ni ishara kwamba masharti yalikua "MAGUMU".

Lakini pia kwa wanaokumbuka, wakati Zitto anapokewa na umati mkubwa wa watu pale Jangwani, Wangwe aliingia akiwa ndani ya gari la Zitto wakiwa pamoja juu, wangwe akiwa anaonyesha vidole vyake kama alama ya Chadema na Zitto akiwa anaonyesha bendera ya TAIFA. Hiyo ina maana yake. Na Wangwe aliamua kusimama katika gari hilo juu, kwa maana gani bora pengine angekua kiongozi wa upinzani bungeni, Hamad Rashid, Katibu Mkuu wa Chadema, Dr Slaa, ama hata Mwenyekiti wao, Mbowe, lakini si Wangwe kwa wakati huo ambao hakuwa hata na cheo alichonacho sasa. Lakini kwa sisi tuliokua pale Jangwani baada ya mkutano kwisha, tulimuona Wangwe akiondoka uwanjani pale kwa miguu akikanyaga matope baada ya Zitto kuondoka kutokana na kuzongwa na umati wa watu waliotaka kumsalimia. Wangwe alionekana wazi kukerwa kwa kuachwa wakati gari yake haikuwa pale uwanjani na mashabiki wake kutoka mkoani Mara walimuona akiingia kifahari sasa wanamuona anaondoka kwa miguu. Kama binadamu hilo LILIMUUMA sana na nina hakika hatosahau pamoja na kuwa HAWEZI HATA SIKU MOJA KULIWEKA WAZI. LITAMSUMBUA SAAAAANA.

Pili, katika uchaguzi, ilibainika wazi kwamba Zitto alikua akimuunga mkono Arfi, ambaye alikua mpinzani wa Wangwe, kwa hiyo kuna kila sababu kwa yeye kutofurahia nyendo za Zitto.

Lakini pia kama alivyosema Mzee ES, kisiasa Zitto anaonekana kama mtoto mdogo ambaye hajawekeza sana katika siasa lakini ameanza kuvuna kwa haraka kuliko wenzake kama Wangwe ambao wamewekeza siku nyingi ikiwa ni pamoja na kupata misukosuko ya DOLA kwa kuwekwa ndani. Zitto katika harakati za madini hampati hata kidogo Wangwe japo Wangwe harakati zake zinaishia jimboni kwake TARIME TU. Hawezi kujivunia kuwatetea wachimbaji wa Kahama na Geita. Zitto hampati hata kidogo Tundu Lissu na mwenzake Nshala na Shauri, ambao hadi leo wana kesi kwa kutetea wachimbaji wadogo na shirika lao la LEAT ndilo limefanya tafiti kibao kuhusu sekta ya madini, lakini ni Zitto anayeonekana shujaa kwa kuzungumzia Buzwagi. Hapo ndipo watu WANAUMIA SANA, ,lakini wanashindwa kujua SIASA ni mchezo wa KARATA TATU.
 
Inatakiwa Mbowe awaambie wazi hawa waheshimiwa kwamba wao sio maarufu kuliko chama na inabidi wafuate taratibu wanapoongea na waandishi wa habari.

Kama CHADEMA wanasema uchumi unaporomoka na Zitto anasema unapanda, hilo ni kosa kubwa. Vile vile kwa Wangwe, kumshambulia mbunge mwenzake wakati hata hana uhakika na alichosema Zitto ni makosa makubwa sana.

Tatizo kubwa la wabunge wetu ni kushinda Dar Es salaam badala ya kuwa kwenye majimbo yao wakishughulikia matatizo ya wananchi. Wakiwa Dar hawana la kufanya na hivyo kutumia magazeti ili waonekana kuna kitu wanafanya.

CCM wakiona weaknesses kama hizo wataanza kuzitumia mara moja.

Tumieni vyombo vya habari kueneza sera za chama na sio kwenda kujitangaza wenyewe na kutaka kuonekana kwenye TV kila siku.

Nilikuwa naamini CHADEMA ni chama makini na kwamba yale mambo ya TLP, NCCR hayawezi kutokea lakini hii migogoro midogo midogo isipokaripiwa mapema, hawa fahari wawili wataua mafaniko ya chama.

Kama ni umwamba wenu si onyesheni kwenye vikao vya CHADEMA? Huko toeni hoja za nguvu na pambaneni kimawazo lakini mkitoka hapo, mnatekeleza lile mlilokubaliana nalo.
 
Tumieni vyombo vya habari kueneza sera za chama na sio kwenda kujitangaza wenyewe na kutaka kuonekana kwenye TV kila siku.


I think this is a very important point. Na pengine vyombo vyetu vya habari vingejifunza kuripoti habari za taasisi badala ya mtu, kwa mfano badala ya kusema Zitto alisema hivi, wangesema CHADEMA wasema hivi, hii itasaidia kukuza taasisi zaidi ya watu.
 
They just need to be careful with the media. It is the media that promoted Mrema and it is the same media that demoted him. Sasa akili ni nywele na kila mtu ana zake.

By the way ni kweli kwamba Zitto alisema uchumi unakua, maana report zote zinaonyesha kuwa hali ya uchumi inazidi kuwa mbaya ikiwemo kukua kwa deni la taifa.
Kitila Mkumbo
Hakuna hata report moja so far ambayo imesema uchumi haukui, issue ni unakuwa kwa kiasi gani? na nini kinaukuza?, Zitto was right. Issue ni kwamba impact ya uchumi kukua kwa raia wa kawaida italetwa tu na kukua kwa kilimo hili JK na wachumi wengi pia wanalisema. Na wala sio madini na utalii tu! Jambo lingine ni kwamba lazima uchumi wetu ukue kwa 10% kwa miaka zaidi ya kumi mfululizo ndio umaskini uliokithiri utapungua, sasa hili ni jukumu la kila mtu kutimiza wajibu[kufanya kazi]wake hata JK akikasirika kila siku haitasaidia
 
Kaka umenena, ila kwa kumbukumbu zangu, wakati tatizo la Buzwagi linaanza, Wangwe alimfuata Zitto akiwa ametumwa na Barrick Gold ili amshawishi aende kutembelea migodi ya Barrick. Zitto alitoa masharti matatu:
1-Kwanza Barrick wamuandikie kwa maandishi kumualika na asiende peke yake.
2-Pili gharama zote za safari ajigharamie mwenyewe
3-Kila kitakachofanyika kiwe public na hakuna cha kuficha.

Baada ya kupewa masharti hayo, Wangwe hajaonekana tena (kuhusu suala hilo), na hiyo ikiwa ni ishara kwamba masharti yalikua "MAGUMU".

Kumbukumbu yangu ya Ziara ya Mh. Zitto mara baada ya kupewa adhabu na wabunge wa CCM inaonyesha kwamba hakufika Mkoani Mara ambako pia kuna migodi ya dhahabu, je, hii inaweza kuwa mojawapo ya sababu zilizosababisha Mh. Zitto asifike huko????
 
Pili, katika uchaguzi, ilibainika wazi kwamba Zitto alikua akimuunga mkono Arfi, ambaye alikua mpinzani wa Wangwe, kwa hiyo kuna kila sababu kwa yeye kutofurahia nyendo za Zitto.

Lakini hili halipaswi kuwa tatizo kwa sababu kwa vyovyote vile isingewezekana kila mtu amuunge mkono Chacha au Arfi. Lakini baada ya uchaguzi huyo aliyeshinda inakuwa basi imetoka na wala yeye mshindaji hapaswi kuanza kutunishia watu msuri. Hayo ya ziara ya mikoani na Jangwani nafikiri unachokonoa na unachokoza jambo ambalo sio muhimu sana.
 
Back
Top Bottom