kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 8,839
- 17,437
Kaburi jingine la umati la Wahindi Wekundu lagunduliwa Canada, ni karibu na shule ya Wamishonari wa Ulaya
Vyombo vya habari vimetangaza habari ya kugunduliwa kaburi jingine la umati lenye maiti za watoto zaidi ya 160 wa Wahindi Wekundi na wakazi asili wa Canada katika mkoa wa British Colombia.
Duru za habari zimeripoti kuwa, kaburi hilo la umati limegunduliwa karibu na shule ya zamani wa Wamishonari wa Kikatoliki katika mkoa wa British Colombia.
Habari ya kugunduliwa kaburi hilo lenye maiti za zaidi ya watoto 160 imetangazwa na watu wa kabila la wenyeji wa Canada la Penelakut.
Hadi sasa hakujatolewa habari zaidi kuhusu ugunduzi wa kaburi hilo. Habari kuhusu kashfa ya kutisha ya kugunduliwa makaburi ya maelfu ya wanafunzi wa shule za bweni zilizokuwa zikisimamiwa na Wamishonari wa Kikatoliki kutoka Ulaya huko Canada zimekuwa zikigonga vichwa vya habari katika vyombo vya kimataifa katika wiki za hivi karibuni. Habari hiyo imezusha malalamiko makubwa nchini Canada ambako kumeshuhudiwa vitendo vya kuchomwa moto makanisa katika maeneo kadhaa ya nchi hiyo.
Vilevile waandamanaji wenye hasira nchini Canada wameziangusha sanamu za wakoloni Malkia Victoria na Elizabeth wa II kwenye mji wa Winnipeg nchini huku hasira za umma zikiendelea kupanda baada ya kugunduliwa mabaki ya miili ya watoto wa wakazi asili wa nchi hiyo katika shule za bweni za makanisa.
Maelfu ya watoto wa Wahindi Wekundu waliuawa na kuzikwa katika makaburi ya umati
Tangu mwezi Mei mwaka huu hadi sasa, kumegunduliwa maeneo manne yenye makaburi ya miili ya watoto hao wa shule za bweni za huko British Colombia, Saskatchewan na Manitoba. Mabaki ya miili ya watoto wasiopungua 1148 imepatikana katika kaburi la umati na makaburi mengine kadhaa yasiyo na majina ya watoto waliozikwa ndani yake.
Ripoti ya Kamati ya Ukweli na Maridhiano ya mwaka 2015 imeonyesha kuwa, watoto wasiopungua 4,100 waliuliwa wakiwa katika shule za bweni za Wamishonari wa Kikatoliki au kutoweka.
Ripoti hiyo ilifichua unyanyasaji wa kutisha wa kimwili, ubakaji, utapiamlo na unyama mwingine uliowapata watoto wengi anokadiriwa kufikia 150,000 waliohudhuria shule hizo, ambazo zilikuwa zikiendeshwa na makanisa ya Kikristo kwa niaba ya serikali ya Ottawa.
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Francis amesema kuwa, ripoti iliyotolewa inatia uchungu lakini bado hajaomba radhi rasmi kwa niaba ya Kanisa Katoliki.
Vyombo vya habari vimetangaza habari ya kugunduliwa kaburi jingine la umati lenye maiti za watoto zaidi ya 160 wa Wahindi Wekundi na wakazi asili wa Canada katika mkoa wa British Colombia.
Duru za habari zimeripoti kuwa, kaburi hilo la umati limegunduliwa karibu na shule ya zamani wa Wamishonari wa Kikatoliki katika mkoa wa British Colombia.
Habari ya kugunduliwa kaburi hilo lenye maiti za zaidi ya watoto 160 imetangazwa na watu wa kabila la wenyeji wa Canada la Penelakut.
Hadi sasa hakujatolewa habari zaidi kuhusu ugunduzi wa kaburi hilo. Habari kuhusu kashfa ya kutisha ya kugunduliwa makaburi ya maelfu ya wanafunzi wa shule za bweni zilizokuwa zikisimamiwa na Wamishonari wa Kikatoliki kutoka Ulaya huko Canada zimekuwa zikigonga vichwa vya habari katika vyombo vya kimataifa katika wiki za hivi karibuni. Habari hiyo imezusha malalamiko makubwa nchini Canada ambako kumeshuhudiwa vitendo vya kuchomwa moto makanisa katika maeneo kadhaa ya nchi hiyo.
Vilevile waandamanaji wenye hasira nchini Canada wameziangusha sanamu za wakoloni Malkia Victoria na Elizabeth wa II kwenye mji wa Winnipeg nchini huku hasira za umma zikiendelea kupanda baada ya kugunduliwa mabaki ya miili ya watoto wa wakazi asili wa nchi hiyo katika shule za bweni za makanisa.
Maelfu ya watoto wa Wahindi Wekundu waliuawa na kuzikwa katika makaburi ya umati
Tangu mwezi Mei mwaka huu hadi sasa, kumegunduliwa maeneo manne yenye makaburi ya miili ya watoto hao wa shule za bweni za huko British Colombia, Saskatchewan na Manitoba. Mabaki ya miili ya watoto wasiopungua 1148 imepatikana katika kaburi la umati na makaburi mengine kadhaa yasiyo na majina ya watoto waliozikwa ndani yake.
Ripoti ya Kamati ya Ukweli na Maridhiano ya mwaka 2015 imeonyesha kuwa, watoto wasiopungua 4,100 waliuliwa wakiwa katika shule za bweni za Wamishonari wa Kikatoliki au kutoweka.
Ripoti hiyo ilifichua unyanyasaji wa kutisha wa kimwili, ubakaji, utapiamlo na unyama mwingine uliowapata watoto wengi anokadiriwa kufikia 150,000 waliohudhuria shule hizo, ambazo zilikuwa zikiendeshwa na makanisa ya Kikristo kwa niaba ya serikali ya Ottawa.
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Francis amesema kuwa, ripoti iliyotolewa inatia uchungu lakini bado hajaomba radhi rasmi kwa niaba ya Kanisa Katoliki.