Kabudi: Hakuna Kiongozi kama Mwalimu Nyerere

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,487
51,064



My take:
1. Nyerere katupa katiba ya Kidikteta ya mwaka 1977, Hata alivyoitengeneza, wakati wake aligoma Haki za binadamu zisiingie ndani ya hiyo katiba

2. Mwaka 1995 Nyerere alihusika kuharibu demokrasia Zanzibar na kutengeneza precedent mbaya visiwani kila baada ya Uchaguzi

3.Sera za Nyerere za Ujamaa zilituletea Umasikini wa kutisha, watu kuvaa midabwada

4. Nyerere alituondolea mfumo wa vyama vingi na kusimika mfumo wa chama kimoja

5. Nyerere aliunga mkono maasi ya Biafra, alitaka nchi ya Nigeria igawanyike wakati yeye akidai anataka umoja wa Afrika

6. Nyerere badala ya kutumia pesa za serikali kujenga shule za Sekondari yeye akataifisha za makanisa na kuacha kujenga mpya za kutosha matokeo yake shule za sekondari zikaendelea kuwa chache, na waliobahatika kuchaguliwa kuendelea na sekondari walikuwa wachache kulinganisha na wale "waliofaulu" lakini "hawakuchaguliwa

7. Nyerere ndiye aliyekuwa kinara kuongoza Kupinga wazo la Nkrumah la Afrika kuwa nchi moja immediately, matokeo yake tumeendelea kukumbatia vinchi vidogo vidogo vyenye mipaka iliyochorwa na mkoloni!, Leo hii tungepewa heshima zaidi duniani tungekuwa linchi limoja likubwa kuliko tulivyo hivi sasa.

Conclusion:
Nyerere alikuwa kiongozi mzuri wa wastani Kisiasa, alikuwa mzuri kidiplomasia na kiukombozi dhidi ya ukoloni lakini alikuwa very poor kiuchumi.
 
Nyerere alikuwa mchumi mzuri sana yeye aliamini katika uchumi wa kijamaa sio kuamini tu aliishi hivyo
Bahati mbaya wakati nchi yetu inapambana kujiweka sawa baada ya uhuru ujamaa ukawa unasambaratika

Hapo hapo mabeberu wakawa wanatuadhibu
Huku tukiwapa usaidizi wenzetu wa kusini kujikomboa
Huku vita vya uganda vikatukabili
Huku baa la njaa lilipiga

Nani angeweza kustahimili?

Nyerere ni mtakatifu
 
4. Nyerere alituondolea mfumo wa vyama vingi na kusimika mfumo wa chama kimoja

Mfumo wa vyama vingi usingekuwa na faida yeyote ile kwa sababu wananchi Wengi hawakujua kusoma na kuandika Wengi walikuwa wajinga

Nakuhakikishia vyama vingi vingeleta maafa katika Nchi kama Ndani ya chama kimoja wasaliti walikuwa Wengi
Vyama vingi vingesababisha wachumia tumbo waiuze nchi kama sahivi baadhi ya wanasiasa wanavyojaribu kifanya
 
7. Nyerere ndiye aliyekuwa kinara kuongoza Kupinga wazo la Nkrumah la Afrika kuwa nchi moja, matokeo yake tumeendelea kukumbatia vinchi vidogo vidogo vyenye mipaka iliyochorwa na mkoloni!, Leo hii tungepewa heshima zaidi duniani tungekuwa linchi limoja likubwa kuliko tulivyo hivi sasa.


Mkuu, katika point zote ulizoeleza kuhusu Nyerere, hiyo point No, 7 sio kweli kabisa.

Nkrumah na Nyerere katika muungano wa Afrika walikuwa kitu kimoja kabisa, tofauti kati yao ilikuwa ni juu ya namna gani muungano huo utekelezwe. Mmoja (nadhani Nrumah), alitaka muungano uwe wa moja kwa moja, yaani nchi zote ziungane kwa maramoja chini ya kiongozi mmoja, (hapa inasemwa Yeye Nkrumah alikuwa anajipigia upatu ili awe Rais wa kwanza wa Afrika iliyoungana), kwa upande wake Nyerere alitaka kwanza Afrika iungane kupitia kanda (Regions), yaani kanda za kusini, Magharibi, Mashariki, kaskazini, kusini na kati na baadaye hizo kanda ziungane kuleta Afrika iliyoungana kikanda, Hiyo ndiyo tofauti iliyokuwepo baina yao na si vinginevyo.
 
Mkuu, katika point zote ulizoeleza kuhusu Nyerere, hiyo point No, 7 sio kweli kabisa.

Nkrumah na Nyerere katika muungano wa Afrika walikuwa kitu kimoja kabisa, tofauti kati yao ilikuwa ni juu ya namna gani muungano huo utekelezwe. Mmoja (nadhani Nrumah), alitaka muungano uwe wa moja kwa moja, yaani nchi zote ziungane kwa maramoja chini ya kiongozi mmoja, (hapa inasemwa Yeye Nkrumah alikuwa anajipigia upatu ili awe Rais wa kwanza wa Afrika iliyoungana), kwa upande wake Nyerere alitaka kwanza Afrika iungane kupitia kanda (Regions), yaani kanda za kusini, Magharibi, Mashariki, kaskazini, kusini na kati na baadaye hizo kanda ziungane kuleta Afrika iliyoungana kikanda, Hiyo ndiyo tofauti iliyokuwepo baina yao na si vinginevyo.

Hicho unachoona kama njia mbadala ya Nyerere kuunganisha Afrika badala ya ile ya Nkrumah, ndiyo sababu kubwa haswaa hatujaweza kuungana mpaka leo, na kwa sasa hivi imeshakuwa vigumu sana Afrika kuungana tena kuwa nchi moja
Hii ya kuunganisha sehemu na sehemu mpaka muwe nchi moja, utaunganisha mara ngapi na itachukua miaka mingapi? labda 1000

Halafu kitu kingine watawala wakishaonja raha ya madaraka, na raia wakajawa na upendo wa kutisha kwa vinchi vyao vidogo vidogo siku ukiwaambia kuungana ni ngumu, mfano leo hii Waafrika ya Kusini wanachoma moto waafrika wenzao wanawaona wageni.

Lakini laiti palepale, kabla hatujajua mipaka ya nchi ni nini tungungana, nakwambia Chance ya kwamba tungekuwa Afrika iliyoungana leo ingekuwa kubwa, Na hizo nchi zilizokuwa chini ya Ukoloni akina Zimbabwe, Namibia, na nyinginezo zingepata uhuru Mapema, na sisi Watanganyika tusingebeba mzigo mkubwa zaidi wa kufinance mapambano dhidi ya huo ukoloni , tungesimama tukiwa kama linchi limoja likubwa
 
Huyo Kabudi bado anafanya siasa za karne iliyopita ndani ya karne hii. Bado anaamini katika siasa za kunyenyekea viongozi bila kuwakosoa, na anaamini wazungu ndio maadui zetu na sio tabia za viongozi wetu.
 
Huyo Kabudi bado anafanya siasa za karne iliyopita ndani ya karne hii. Bado anaamini katika siasa za kunyenyekea viongozi bila kuwakosoa, na anaamini wazungu ndio maadui zetu na sio tabia za viongozi wetu.

Anataka kuturudisha kwenye enzi za diplomasia ya "uanaharakati", badala ya diplomasia ya uchumi
Diplomasia ile ya zamani ulikuwa ukivaa suti ya cho enlai, ukitukana mabeberu kwa sauti kubwa kwa majina yote, "wanyonyaji, Mabepari, Makabaila, mabwanyenye,"

Sasa wakati ule ilikuwepo audience kutoka kwa Eastern block, wangeweza kusikiliza hivyo vibwagizo wakacheka na kufurahia

Lakini sasa hivi misamiati ya mujini ni "wawekezaji, wadau wa maendeleo, wahisani, mtaji". Kabudi asipojifunza hii diplomasia ya uchumi ataturudisha enzi za kale sana na tutapoteza

Kwa mfano, hata hii video peke yake haijakaa kidiplomasia, Mwafrika yeyote wa nchi tofauti na Tanzania mwenye kujua kiswahili na kumheshimu mwalimu akiona watu wanaanza kumpa sifa kwa kudunisha viongozi wengine wa Afrika. hawatopenda. Hayo mambo waache watu wa mataifa mengine waseme au ukiamua kusema basi ondoa Kamera zote mbaki watanzania wenyewe mpige stori
 
Huyo Kabudi bado anafanya siasa za karne iliyopita ndani ya karne hii. Bado anaamini katika siasa za kunyenyekea viongozi bila kuwakosoa, na anaamini wazungu ndio maadui zetu na sio tabia za viongozi wetu.
 
Mtu akiishatangulia mbele ya haki, akumbukwe kwa mema na mazuri yake na sio kwa mabaya na madhaifu yake.

Nyerere was a human being and not a saint, ndio maana wakati wa kuondoka alisema "kufanya kosa sii Kosa, kosa kurudia kosa" na akaomba msamaha kwa makosa yote ya utatawala wake, tukamsamehe na sisi Wakristu Wakatoliki tumemuanzishia mchakato wa kumtangaza Mwenye Heri ambayo ni hatua moja kabla hajatangazwa kuwa Mtakatifu.

Please usituharibie mchakato wetu.
P
 
Mtu akiishatangulia mbele ya haki, akumbukwe kwa mema na mazuri yake na sio kwa mabaya na madhaifu yake.

Nyerere was a human being and not a saint, ndio maana wakati wa kuondoka alisema "kufanya kosa sii Kosa, kosa kurudia kosa" na akaomba msamaha kwa makosa yote ya utatawala wake, tukamsamehe na sisi Wakristu Wakatoliki tumemuanzishia mchakato wa kumtangaza Mwenye Heri ambayo ni hatua moja kabla hajatangazwa kuwa Mtakatifu.

Please usituharibie mchakato wetu.
P
Kwa lipi zaidi?
 
hata Yesu ambae ni binaadam kwao ni Mungu.
Yesu ni Mungu ila alichukua tuu mwili wa kibinadamu.

Binadamu wote huumbwa baada ya lile tendo la kutunga mimba kati ya baba na mama. Mimba ya Yesu haikutokana na lile tendo, mama wa Yesu, Bikira Maria alipata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, bila kufanyika lile tendo, akiwa na bikira yake, mimba ya Yesu ikaingizwa tumboni mwake na akazaliwa kama mwanadamu.

Faiza sasa wewe ni Bibi, naomba wewe na sisi wana jf wenzangu wote tuepuke religious sentiments za lugha za maudhi kukashifu dini na imani za watu wengine hata kama wewe huamini, hili la kuita watu makafiri ni lugha ya maudhi.

Tuwe na Religious Tolerance kuheshimu dini na imani za watu wengine, maadam sisi Wakristu kwa imani yetu Yesu ni Mungu, hata kama kwa imani yako ni binaadam, please tolerate and keep it to yourself bila kutu kashif. Please!.

P
 
Yesu ni Mungu ila alichukua tuu mwili wa kibinadamu.

Binadamu wote huumbwa baada ya lile tendo la kutunga mimba kati ya baba na mama. Mimba ya Yesu haikutokana na lile tendo, mama wa Yesu, Bikira Maria alipata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, bila kufanyika lile tendo, akiwa na bikira yake, mimba ya Yesu ikaingizwa tumboni mwake na akazaliwa kama mwanadamu.

Faiza sasa wewe ni Bibi, naomba wewe na sisi wana jf wenzangu wote tuepuke religious sentiments za lugha za maudhi kukashifu dini na imani za watu wengine hata kama wewe huamini, hili la kuita watu makafiri ni lugha ya maudhi.

P
Yesu wapi anasema "Mimi Mungu"?

Mwinjilisti aliuliza...

KAFIRI NI NANI?

Swali:
Naitwa mwinjilisti Onesmo, Kwanini nyie waislamu mnatuita sisi wakristo makafiri?

Jibu:
Nashkuru kwa swali lako.

Hatuwaiti hivyo kwa utashi wetu bali ni MwenyeziMungu (Allah) mwenyewe ndo kasema katika kitabu kitakatifu cha Quran 5:72-73

QURAN 5:72-73
72. Hakika wamekufuruwalio sema: Mwenyezi Mungu ni Masihi mwana wa Maryamu!
Na hali Masihi mwenyewe alisema: Enyi Wana wa Israili! Muabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wangu Mlezi na Mola wenu Mlezi. Kwani anaye mshirikisha Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu atamharimishia Pepo, na mahala pake ni Motoni. Na walio dhulumu hawatakuwa na wa kuwanusuru.
TAFSIRI:
Wenye kudai kuwa Mwenyezi Mungu yu katika Isa bin Maryam hata akawa yeye Mungu, kama wasemavyo Wakristo hii leo, hakika wamekufuru! Yeye Isa hana dhambi ya haya, kwani hakupata kudai hivyo hata mara moja. Bali yeye aliwaamrisha Wana wa Israili wamsafie imani Mwenyezi Mungu peke yake kwa kusema: Hakika Mwenyezi Mungu ndiye aliye niumba mimi na nyinyi, na ndiye anaye niendeshea mambo yangu yote, na kwamba kila mwenye kumshirikisha Mwenyezi Mungu malipo yake ni kuwa hatoingia Peponi kabisa, bali ataingia Motoni, kwa kuwa amekiuka mipaka ya Mwenyezi Mungu. Na mwenye kuvunja mipaka yake hataepuka na adhabu.(Yesu kasema: "Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja." Marko 12.28. "Mimi siwezi kufanya neno mwenyewe".Yohana 5.30 "Ninapaa kwenda kwa...Mungu wangu naye ni Mungu wenu." Yohana 20.17 )

73. Kwa hakikawamekufuru walio sema: Mwenyezi Mungu ni wa tatu wa Utatu. Hali hakuna mungu ila Mungu Mmoja.
Na ikiwa hawaachi hayo wanayo yasema, kwa yakini itawakamata adhabu chungu walewanao kufuru
TAFSIRI:
Haiwi mwenye kudai kuwa Mwenyezi Mungu ni mmoja katika Utatu, kama wadaivyo Wakristo sasa, awe anamuamini Mwenyezi Mungu.!! Na hakika iliyo thibiti ni kuwa hapana mungu ila Mwenyezi Mungu mmoja pekee. Na ikiwa hawa walio potoka hawatoacha itikadi zao potovu, wakarejea kwenye ut'iifu wa Mwenyezi Mungu, hapana budi ila itawasibu adhabu kali. (Biblia inasema kuwa ya kwanza katika Amri Kumi alizo pewa Musa ni: "Usiwe na miungu mingine ila mimi." - Kutoka 20.3. "Wewe umeonyeshwa haya, ili upate kujua ya kuwa Bwana ndiye Mungu, hapana ila yeye." - Kumbukumbu la Torati 4.35. Katika Injili ya Yohana 17.3 Yesu anamsemeza Mwenyezi Mungu: "Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli na Yesu Kristo uliyemtuma.")

Kwahiyo tunawaita makafiri kwa sababu miongoni mwenu mnamwita Yesu kuwa ni Mungu na miongoni mwenu mnasema kuwa Mungu ni wa tatu wa utatu.



My take: Kama unaudhika kuitwa kafiri usikufuru.
 
Tumshukuru Mungu kwa kutupatia Nyerere
Bila Yeye Tanzania isingekuapo

Tushukuru Mungu saaaana kwani sasa tunaye Mwl Nyerere II, Rais Dr Magufuli!!! Kama siyo yeye ungekuta ukanda wote wa Pwani ya Tanzania Bara bandari ya Bagamoyo kama makao makuu umechukukuliwa na China/Oman. Kumbuka baada ya waliokabidhiwa nchi na Mwl Nyerere kufisidi viwanda, mashirika ya umma na kujigawia nyumba zote za serikali na mashirika ya umma wakaenda kwenye hatua nyingine ya kuuza nchi(kwa mkataba wa miaka zaidi ya mia! Wajerumani walitawala kwa miaka 40, Waingereza miaka 30 lakini China/Oman walikuwa wamepewa kwa miaka 99 + 33 ila mzalendo Magufuli kaokoa jahazi! Long live Rais Dr Magufuli. Kudos!
 
Back
Top Bottom