kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 12,293
- 12,588
Duniani kote "mmachinga" ni yule mtu anaetembeza bidhaa zake kwa kutembea nazo mikononi mwao au kwenye begi la mgongoni akitafuta waliko wanunuzi. Yaani badala ya mnunuzi kufuata bidhaa (dukani), mara hii mwenye bidhaa (duka) ndiye anaemfuata mnunuzi. Wafanyabiashara wa aina hii sio kero sana na hawahitaji kupewa maeneo.
LAKINI kuna watu wanasiasa wanawaita machinga pia kimakosa. Hawa ni wale wenye bidhaa nyingi kiasi cha kushindwa kuzibeba zote mikononi au kwenye begi la mgongoni hivyo wanazipanga chini au kujenga vibanda ili kuziuzia hapohapo walipozipanga. Bidhaa hizi ni nyingi kiasi kwamba zinahitaji ulinzi dhidi ya wezi, jua na mvua. Zinahitaji eneo (space), mwanga usiku na mchana, vifaa vya kuweka taka, vyoo, sehemu ya kula ya karibu na yenye miundombinu mingine.
Hawa sio machinga bali ni watu waliostahili kufungua viduka kwenye fremu hukohuko kwenye mitaa wanakoishi mijini na vijijini kama wanavyofanya wengine ili walipe kodi ya kukadiriwa. Watu hawa ndio kero halisi kwakuwa wanahitaji nafasi ili kupanga na kuuza bidhaa zao sehemu zenye wanunuzi, hivyo kusababisha kutumia maeneo yasio rasmi. Huyu sio machinga, ni mkora tu ambae anafuata wateja kwa kunyanganya haki za watu wengine kama vile kupanga bidhaa zake eneo ambalo lina matumizi ya watu wengine, kuweka bidhaa kwenye vumbi na tope na kuhatarisha afya za wengine, na kusababisha ajali kwa watu wengine.
Serikali haipaswi kuwatafutia maeneo hawa wanaopanga chini na kujengea shelters bidhaa zao, badala yake serikali ilinde na kusimamia mipango miji yake; itoe marufuku watu kufanya biashara maeneo yasiyoruhusiwa basi. Wafanyabiashara wa hivi waende kwa maofisa biashara wa vilaya, tafara, kata na vijiji wakaelekezwe utaratibu wa kufungua biashara zao kwenye maeneo yatakayokaguliwa. Maana hawa ni watu ambao idadi yao haifahamiki, hivyo huwezi kuwatengea maeneo ikatosha. Wanatoka vijijini na mijini kila siku baada ya kumaliza darasa la saba, kidato cha nne, kidato cha sita, na vyuo.
Lazima tutoe tafsiri halisi ya nani ni machinga na nani sio machinga huko mitaani, vinginevyo ni kuwatwisha zigo wakuu wa mikoa wasiloliweza. Maeneo ya kutosha kujenga vibanda wenye badhaa nyingi watayatoa wapi? kwanini wasiende kufungua viduka mitaani sawa na wengine?
LAKINI kuna watu wanasiasa wanawaita machinga pia kimakosa. Hawa ni wale wenye bidhaa nyingi kiasi cha kushindwa kuzibeba zote mikononi au kwenye begi la mgongoni hivyo wanazipanga chini au kujenga vibanda ili kuziuzia hapohapo walipozipanga. Bidhaa hizi ni nyingi kiasi kwamba zinahitaji ulinzi dhidi ya wezi, jua na mvua. Zinahitaji eneo (space), mwanga usiku na mchana, vifaa vya kuweka taka, vyoo, sehemu ya kula ya karibu na yenye miundombinu mingine.
Hawa sio machinga bali ni watu waliostahili kufungua viduka kwenye fremu hukohuko kwenye mitaa wanakoishi mijini na vijijini kama wanavyofanya wengine ili walipe kodi ya kukadiriwa. Watu hawa ndio kero halisi kwakuwa wanahitaji nafasi ili kupanga na kuuza bidhaa zao sehemu zenye wanunuzi, hivyo kusababisha kutumia maeneo yasio rasmi. Huyu sio machinga, ni mkora tu ambae anafuata wateja kwa kunyanganya haki za watu wengine kama vile kupanga bidhaa zake eneo ambalo lina matumizi ya watu wengine, kuweka bidhaa kwenye vumbi na tope na kuhatarisha afya za wengine, na kusababisha ajali kwa watu wengine.
Serikali haipaswi kuwatafutia maeneo hawa wanaopanga chini na kujengea shelters bidhaa zao, badala yake serikali ilinde na kusimamia mipango miji yake; itoe marufuku watu kufanya biashara maeneo yasiyoruhusiwa basi. Wafanyabiashara wa hivi waende kwa maofisa biashara wa vilaya, tafara, kata na vijiji wakaelekezwe utaratibu wa kufungua biashara zao kwenye maeneo yatakayokaguliwa. Maana hawa ni watu ambao idadi yao haifahamiki, hivyo huwezi kuwatengea maeneo ikatosha. Wanatoka vijijini na mijini kila siku baada ya kumaliza darasa la saba, kidato cha nne, kidato cha sita, na vyuo.
Lazima tutoe tafsiri halisi ya nani ni machinga na nani sio machinga huko mitaani, vinginevyo ni kuwatwisha zigo wakuu wa mikoa wasiloliweza. Maeneo ya kutosha kujenga vibanda wenye badhaa nyingi watayatoa wapi? kwanini wasiende kufungua viduka mitaani sawa na wengine?