Kabla ya kumshikirikisha Rais Samia hoja ya Katiba mpya, tumhoji sababu za mchakato wa awali kufia mikononi mwake na Mzee Samuel Sitta

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Tunaweza tukawa tunataka ku-push agenda tukiamini tunayetaka kumfikishia agenda hiyo ni mgeni na anahitaji vikao vyakumpitisha kwenye kile tunachokita. Naomba niwaambie we are wrong, hakuna sababu ya kikao kumfikishia ujumbe Mhe. Rais kuhusu katiba. Yeye anafahamu mwanzo mwisho wa mchakato uliopita kwa sababu alikuwa kiongozi Na. 2 kwenye Bunge la Katiba.

Nadhani tuamini kwamba kama mchakato wa awali ulifia mikononi mwake na Mzee Sita, jukumu letu la Kwanza nikumuuliza mama sababu zilizopelekea kufa kwa mchakato ule.

Tunapaswa kuhoji mchakato ule Kwanza kwa sababu, yawezekana sababu zilizopelekea kufa kwa mchakato wa awali zina nguvu Hadi Sasa. Na Kama Zina nguvu na zilimpelekea kukubaliana na kifo cha mchakato wa Katiba ya Warioba basi yeye siyo mtu sahihi kumpelekea agenda ya Katiba. Tusubiri mtu anayeweza kuamini na kukubaliana kwamba sababu za kufa kwa mcahakato wa awali hazina mashiko.

Hakuna mtu anayetaka kuendelea kutawala atakayetengeneza mazingira Bora ya watawaliwa. Atawaminya, ila tofayti yakuwaminya itatofautiana. Mama anatuminya kama wengine walivyotuminya isipokuwa yeye anatuminya kwa kisingizio cha kuboresha mfumo.

Mnaodai katiba hojini kuhusu ulipoishia mchakato wa awali. Watafteni akina Warioba mapema mzungumze nao ili jamii ielewe tulikwama wapi. Msipotumia fursa yakukwapua malighafi vichwani mwa wazee mtashangaa muda unaisha na wanaondoka na Siri ya kukwama kwa Katiba.

Mhe. Rais awe wa mwisho mkiwa mnajipanga kwenda kuzipangua hoja zilizokwamisha mchakato wa awali.
 
Aulizwe Makonda, nasikia kuna siku alimkaba Mzee Warioba kwa sababu ya Katiba! Anaweza akawa anajua siri maana mtu na akili zako kumkaba babu yako siyo jambo rahisi!

Inabidi kujitoa ufahamu kweli kweli
 
Aulizwe Makonda, nasikia kuna siku alimkaba Mzee Warioba kwa sababu ya Katiba! Anaweza akawa anajua siri maana mtu na akili zako kumkaba babu yako siyo jambo rahisi!

Inabidi kujitoa ufahamu kweli kweli
.
FB_IMG_1623017604570.jpg
 
Hivi waziri mkuu mstaafu si anapewa mlinzi.

Kwanini hakuwa shahidi kutendewa bosi wake vile
 
TOR za katiba ya Chenge zilitokea wapi? Tume ya Katiba inayofahamika ilikuwa chini ya Jaji Joseph Sinde Warioba. Sheria ilivunjwa kwa timu ya Chenge kupewa kuandika Rasimu maana ya Warioba ilikuwa kwa mujibu wa Sheria ya Bunge. Pili hata namna Kikwete alivyoongea Bungeni baada ya Warioba kuwasilisha ilikuwa uvunjaji wa Sheria.

Tatu jiulize kwa nini Dr Mvungi akiwa mjumbe wa Tume aliuliwa kiajabu ajabu.
Kwa faida yako nitakuambia leo kwa nini Rasimu ya Katiba ya Warioba ilitupwa. Kulikuwa na kifungu cha Marais kuwajibika kwa makosa yao watakayokuwa wamefanya wakiwa madarakani. Sasa Jakaya aliruhusu na alipokea fedha za Escrow kutoka kwa Harbinder Singh/ Rugemalira.

Wakati huo huo Andrew Change naye akiwa ni mnufaika wa Escrow kutoka kwa Rugemalira. Ndipo akamtonya Jakaya kuwa kama Rasimu ya Warioba itapita basi hicho kifungu cha Marais kuwajibika kwa makosa waliyofanya, basi ajiandaye kushtakiwa na kufungwa.

Ndipo Jakaya Kikwete akaelewa na kuamua kuuvuruga mchakato wa Katiba kwa kuogopa kuja kushtakiwa
 
Back
Top Bottom