Kabla ya kumrarua Lissu, tumwambie Rais Magufuli ukweli

Nianze na maandiko matakatifu Yohana 8:32 Tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.

Watanzania wenzangu tuna tatizo kubwa sana katika nchi yetu, ambalo sasa limekuwa ugonjwa sugu, Woga unaozaa dhambi ya UNAFIKI. Kiwango hiki cha unafiki tulichofikia ni kibaya sana ambacho kinasababisha kuambiwa ole wenu ninyi watanzania mnaopindisha kweli kwa kumwogopa JPM. Hii ni laana kufikia kiwango hiki, tunajua wazi kuwa utawala wa awamu ya tano unaongoza nchi kwa kuvunja katiba na sheria za nchi.

Kuna watu wengi wanaosema kuwa JPM anachapa kazi na kutetea raslimali za nchi, hii siyo sababu ya kuvunja sheria na kukandamiza uhuru wa watu kutoa mawazo na vyama kufanya matakwa yao

Sasa tumwambie JPM ukweli.
1-Hatawali nchi kwa kufutuata katiba na sheria za nchi. Ni kifungu gani cha katiba kinachozuia vyama vya siasa visifanye mikutano ya hadhara hadi 2020?

2-Anatumia theocracy kwenye nchi ambayo imekubaliana na mfumo wa democracy hii ni hatari anataka akiamua kitu watu wote waseme ndio. Anayetakiwa atawale kwa theocracy ni Mungu peke yake.

3-Anapandikiza chuki kati ya watanzania, kati ya vyama vya siasa, kati ya makabila na pia kati ya kanda na kanda. Watu wanajitahidi kutetea lakini ukweli wanaujua kuwa nchi inakoelekea siko

4-Amekuwa mara kwa mara akitamka maneno ya kuchochea vyombo vya dola kutumia nguvu dhidi ya raia wasio na silaha, na huku akijizungushia ulinzi mkali kama walivyo marais waovu duniani.

5-Amekuwa akiwashambulia wale wanaopinga hadharani hata kuwaita majina mabaya kama wasaliti, wapinga maendeleo na wasiokuwa wazalendo, huku akijihami kwa kuwakamata wale wote wanakusudia kumjibu.

6-Amekuwa na tabia ya wafalme wenye kiburi kama Nebukadneza, Farao na Herode waliotaka kusifiwa tu, na kuwatesa na kuwaua wale wote walijitahidi kuwakosoa.

7-Anawalazimisha watu waamini kuwa yeye tu ndiye mwenye uwezo na mzalendo wa kweli katika nchi ya Tanzania.

8-Anafikiri neno lake ndio katiba na sheria halali ya kuongoza nchi.

Lazima Aambiwe ukweli kwanza kabla ya kukimbilia kumrarua Lissu
Ahsante kaka mkubwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duuuh,Mungu tushushie rais Malaikaa,rais ambae ataongoza hadi familia zetuu,maana sio kwa povu kiasi hikii!!

Sent using Jamii Forums mobile app


Nani kakwambia Rais anaongoza? huyu tuliyenaye anatawala maana anayeongoza hawezi kusema hawezi kushauriwa kwa kuwa hakushauriwa kuchukua fomu. Musa alishauri na baba yae mkwe ambaye alikuwa kuhani wa Mungu
 
Nani kakwambia Rais anaongoza? huyu tuliyenaye anatawala maana anayeongoza hawezi kusema hawezi kushauriwa kwa kuwa hakushauriwa kuchukua fomu. Musa alishauri na baba yae mkwe ambaye alikuwa kuhani wa Mungu
Hivi kumbee,bas inabidi tujue kwamba vitu/watu hatufanani,na wakat wewe unaona sio,kuna wengine hata kama ni wachache wanaona ndio,NDIVYO TULIVYO WANADAMU.

bichwa baya
 
Hivi kumbee,bas inabidi tujue kwamba vitu/watu hatufanani,na wakat wewe unaona sio,kuna wengine hata kama ni wachache wanaona ndio,NDIVYO TULIVYO WANADAMU.

bichwa baya

Hizo tofauti zetu ndio maana tulikubaliana tuwe na katiba ili itusaidie kutusimamia, ila yeye hataki kuitii
 
Hizo tofauti zetu ndio maana tulikubaliana tuwe na katiba ili itusaidie kutusimamia, ila yeye hataki kuitii
Hii ni desturi yetu,hakuna alie tayari kuwajibika kwa maslahi ya mtu mwingine.japo leo hii ananyooshewa vidole,lkn imekua ni jambo la kujirudia rudia,sio yeye tuu,wapo wengi wamepita,na bado watakuja wengine.

bichwa baya
 
Kiongozi umeongea ukweli 100% watz wangi ni wachumia tumbo tu mtu analinda kibarua chake kwa kuwa mnafki wengi wanaogopa kusema ukweli kwa kuhofia kufukuzwa kazi anabaki kutetea ujinga japo ukweli anaujua tz wanafki sana namuunga mkono lisu kwa kumchana ukweli ukabila,ukanda,undungu inakera sana
 
Nianze na maandiko matakatifu Yohana 8:32 Tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.

Watanzania wenzangu tuna tatizo kubwa sana katika nchi yetu, ambalo sasa limekuwa ugonjwa sugu, Woga unaozaa dhambi ya UNAFIKI. Kiwango hiki cha unafiki tulichofikia ni kibaya sana ambacho kinasababisha kuambiwa ole wenu ninyi watanzania mnaopindisha kweli kwa kumwogopa JPM. Hii ni laana kufikia kiwango hiki, tunajua wazi kuwa utawala wa awamu ya tano unaongoza nchi kwa kuvunja katiba na sheria za nchi.

Kuna watu wengi wanaosema kuwa JPM anachapa kazi na kutetea raslimali za nchi, hii siyo sababu ya kuvunja sheria na kukandamiza uhuru wa watu kutoa mawazo na vyama kufanya matakwa yao

Sasa tumwambie JPM ukweli.
1-Hatawali nchi kwa kufutuata katiba na sheria za nchi. Ni kifungu gani cha katiba kinachozuia vyama vya siasa visifanye mikutano ya hadhara hadi 2020?

2-Anatumia theocracy kwenye nchi ambayo imekubaliana na mfumo wa democracy hii ni hatari anataka akiamua kitu watu wote waseme ndio. Anayetakiwa atawale kwa theocracy ni Mungu peke yake.

3-Anapandikiza chuki kati ya watanzania, kati ya vyama vya siasa, kati ya makabila na pia kati ya kanda na kanda. Watu wanajitahidi kutetea lakini ukweli wanaujua kuwa nchi inakoelekea siko

4-Amekuwa mara kwa mara akitamka maneno ya kuchochea vyombo vya dola kutumia nguvu dhidi ya raia wasio na silaha, na huku akijizungushia ulinzi mkali kama walivyo marais waovu duniani.

5-Amekuwa akiwashambulia wale wanaopinga hadharani hata kuwaita majina mabaya kama wasaliti, wapinga maendeleo na wasiokuwa wazalendo, huku akijihami kwa kuwakamata wale wote wanakusudia kumjibu.

6-Amekuwa na tabia ya wafalme wenye kiburi kama Nebukadneza, Farao na Herode waliotaka kusifiwa tu, na kuwatesa na kuwaua wale wote walijitahidi kuwakosoa.

7-Anawalazimisha watu waamini kuwa yeye tu ndiye mwenye uwezo na mzalendo wa kweli katika nchi ya Tanzania.

8-Anafikiri neno lake ndio katiba na sheria halali ya kuongoza nchi.

Lazima Aambiwe ukweli kwanza kabla ya kukimbilia kumrarua Lissu
Wasukuma tulisifika kwa upole na USHAMBA. Huyu "lahizi" katushushia heshima kwa kiwango cha juu sana. Tz hatuna "Rais" kwa sasa, ni UBABE MTUPU.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ungetumia katiba pia kumkosoa unapoona anakosea ukavirusha hapa vipengele na hayo unayomtuhumu tusome. Si unataka tukuelewe haya edit post yako, shusha nondo.

Tundu Lissu kawaona hamna msaada kwake na chama chenu eeeeh
Kavunja Ibara ya 150 (1) ya Katiba ya Tanzania. Imedhuia ukaimishaji wa madara ya Jaji, lakini sasa ni takribani miezi 7 tuna Kaimu Jaji Mkuu. Uko wapi Uhuru wa Mahakama?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hapo ni vile uonavyo wewe, naamini si sahihi. sasa unataka siasa zifanyike kipindi chote na kazi zitafanyika mda gani na ukizingatia nchi yetu bado changa maana unaowahubiria ni raia ambao walitakiwa kuwa kwenye shughuli zao za kila siku.

udikteta upi, ukiambia fanya kazi ndo udikteta kwahiyo unataka upewe tu, yaani wewe huna tofauti na walibya na leo wanahangaika tu kwa laana waliopata.

sisi mzee anafanya mabadiliko na baadae vizazi vyetu viishi kwa amani lakini bado tunaona hafanyi kazi, upendeleo wowote unaweza tokea so long as kazi inafanyika kwa Taifa basi safi kabisa, tumeona zamani labda kulikuwa hakuna ukanda lakini kulikuwa na urafiki, sioni kama ni kweli kwa lolote.
Kwani siasa sio kazi? hivi hujui kuna watu wameajiriwa kwa ajili ya kufanya siasa tu? Kama kisingizio ni kufanya kazi mbona wanaratibu maandamano ya kumpongeza rais, huo muda wa kupongeza unatoka wapi? Ukweli ni kwamba ccm ilimalizwa mwaka 2015 kwenye uchaguzi mkuu na katazo la kutofanya siasa ni kujaribu kuficha aibu ya kukataliwa.
 
Kwani siasa sio kazi? hivi hujui kuna watu wameajiriwa kwa ajili ya kufanya siasa tu? Kama kisingizio ni kufanya kazi mbona wanaratibu maandamano ya kumpongeza rais, huo muda wa kupongeza unatoka wapi? Ukweli ni kwamba ccm ilimalizwa mwaka 2015 kwenye uchaguzi mkuu na katazo la kutofanya siasa ni kujaribu kuficha aibu ya kukataliwa.


Siku ya kusomwa ripoti ya makinikia walilazimisha watu wote waangalie, tena siku ya kazi, je hawakujua kuwa watu wanatakiwa wafanye kazi?
 
Zamani tulikuwa tunazikana na kusherekea pamoja tunajuliana hali pale penye matatizo tunaacha siasa pembeni lakini sasa hivi huyu ametufanya tuchukiane wenyewe kwa wenyewe masikini ! Tumekuwa mazuzu tunaumizana wenyewe kwa wenyewe wakati yeye yupo pembeni anatucheka tumekuwa kama tumelogwa na mganga aliekufa dawa ya kutuzindua hamna ! Tuamke watanzania wenzangu ! TUSIVUMILIE KUWA WATANZANIA BADALA YAKE TUJIVUNIE KUWA WATANZANIA

Sent using Jamii Forums mobile app
Shetan Mzee
Hivi ule mchanga Wa makanikia umesharuhusiwa kwenda au bado tunafamya uchunguzi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nianze na maandiko matakatifu Yohana 8:32 Tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.

Watanzania wenzangu tuna tatizo kubwa sana katika nchi yetu, ambalo sasa limekuwa ugonjwa sugu, Woga unaozaa dhambi ya UNAFIKI. Kiwango hiki cha unafiki tulichofikia ni kibaya sana ambacho kinasababisha kuambiwa ole wenu ninyi watanzania mnaopindisha kweli kwa kumwogopa JPM. Hii ni laana kufikia kiwango hiki, tunajua wazi kuwa utawala wa awamu ya tano unaongoza nchi kwa kuvunja katiba na sheria za nchi.

Kuna watu wengi wanaosema kuwa JPM anachapa kazi na kutetea raslimali za nchi, hii siyo sababu ya kuvunja sheria na kukandamiza uhuru wa watu kutoa mawazo na vyama kufanya matakwa yao

Sasa tumwambie JPM ukweli.
1-Hatawali nchi kwa kufutuata katiba na sheria za nchi. Ni kifungu gani cha katiba kinachozuia vyama vya siasa visifanye mikutano ya hadhara hadi 2020?

2-Anatumia theocracy kwenye nchi ambayo imekubaliana na mfumo wa democracy hii ni hatari anataka akiamua kitu watu wote waseme ndio. Anayetakiwa atawale kwa theocracy ni Mungu peke yake.

3-Anapandikiza chuki kati ya watanzania, kati ya vyama vya siasa, kati ya makabila na pia kati ya kanda na kanda. Watu wanajitahidi kutetea lakini ukweli wanaujua kuwa nchi inakoelekea siko

4-Amekuwa mara kwa mara akitamka maneno ya kuchochea vyombo vya dola kutumia nguvu dhidi ya raia wasio na silaha, na huku akijizungushia ulinzi mkali kama walivyo marais waovu duniani.

5-Amekuwa akiwashambulia wale wanaopinga hadharani hata kuwaita majina mabaya kama wasaliti, wapinga maendeleo na wasiokuwa wazalendo, huku akijihami kwa kuwakamata wale wote wanakusudia kumjibu.

6-Amekuwa na tabia ya wafalme wenye kiburi kama Nebukadneza, Farao na Herode waliotaka kusifiwa tu, na kuwatesa na kuwaua wale wote walijitahidi kuwakosoa.

7-Anawalazimisha watu waamini kuwa yeye tu ndiye mwenye uwezo na mzalendo wa kweli katika nchi ya Tanzania.

8-Anafikiri neno lake ndio katiba na sheria halali ya kuongoza nchi.

Lazima Aambiwe ukweli kwanza kabla ya kukimbilia kumrarua Lissu

Huyu we mwache tu siku ataona kiganja cha mkono kimeandika kwenye ukuta wA ikulu teke mene mene tekeli siku atakimbia na walinzi atawaacha halafu ataota ile ndoto kama ya nebukadreza
 
Back
Top Bottom