Kabla ya kufikiria harusi, weka haya akilini!

Harusi ni ya wawili,shida ya wengi aim ya kufanya sherehe kwa maharusi wengi

Tamaa ya mazawadi na vitu watakavyopewa,yani wengi hutaka Harusi(sherehe) kama kupata mtaji wa Kununulia mahitaji

ya kuanzia kama Kabati,fridge,vitanda,nk nk yani zile asset kubwa kubwa

Watu wanagharamika kualika watu wengi ili COST irudi na FAIDA juuu

Harusi imekua kama Biashara siku hizi
Na huu ndio ukweli wengi ukiwauliza atakwambia anataka apate vyombo & vitu mbalimbali vya kuanzia maisha...ni uboya uboya!
 
In light of this
Naomba nishare na nyie kitabu kizuri sana kwa watarajiwa

Jina:Things I Wish i'd Known Before We Got Married
Mwandishi: Gary Chapman


Nimeshindwa kuattach ila atakaeweza atuwekee
Nadhani hii ndo elimu ya msingi ya watu kuipata kabla ya kuingia kwenye hii taasisi
 

Attachments

  • Things I Wish I’d Known Before We Got Married ( PDFDrive.com ).pdf
    1.2 MB · Views: 9
Mwanaume pambama wewe....maisha ni kitu gani haya bana....kujibanabana...tafuta hela fanya harusi, andaa sherehe watu wafurahi, wale, wanywe....sherehe ya harusi ndo sehemu ambayo unakutanisha ndugu wa pande zote mbili kwa wakati mmoja..watu watajuana hapa....ndo maana wanatambulishana...Acheni kulialia vijana na kujifanya mnajua sana budget na kupanga maisha....
Andaa sherehe ,,chakula, maji etc..kwa ajili ya sherehe ya ndoa yako...na Mungu atawabariki na atawarudishia....
Kuandaa harusi ndo kipimo cha kwanza cha mwanaume halisi....ni kipimo cha jinsi alivyo na ushirikiano na jamii na watu wanaomzunguka..
Mbona mtoa mada kasema hapo juu kama umejaaliwa kipato ama una marafiki wasio na pesa ya mawazo si mbaya kufanya sherehe kubwa tunachokikataa wengi wetu ni mtu kuanza kusumbua ilhali starehe ni yake mm nilifanya sherehe simpo tu kulingana na bajeti yangu sitaraji mtu kuja kunisumbua eti anaoa nimchangie sababu mimi sikuchangiwa na yeyote ukiwa na uwezo fanya ndugu ndio matumizi ya pesa tena mi nitakuona wa ajabu hela ipo halafu unajibana bana?
 
Ndoa Ina thamani zaidi ya sherehe lakini hii haimzuii mtu kufanya sherehe kubwa.
Kila mtu yupo na interest zake ..kuna wengine wanapenda sherehe,Kuna wengine hawapendi.
Cha muhimu watu wafanye wanavyotaka.
Hujakatazwa ndugu ila uwezo unao? au una kampani ya maana? Tunachokataa watu usumbufu mnaandaa bajeti ya Sherehe milioni 5 bwana harusi una 170,000 tu mfukoni si u*##@nge huu?
 
Mwanaume pambama wewe....maisha ni kitu gani haya bana....kujibanabana...tafuta hela fanya harusi, andaa sherehe watu wafurahi, wale, wanywe....sherehe ya harusi ndo sehemu ambayo unakutanisha ndugu wa pande zote mbili kwa wakati mmoja..watu watajuana hapa....ndo maana wanatambulishana...Acheni kulialia vijana na kujifanya mnajua sana budget na kupanga maisha....
Andaa sherehe ,,chakula, maji etc..kwa ajili ya sherehe ya ndoa yako...na Mungu atawabariki na atawarudishia....
Kuandaa harusi ndo kipimo cha kwanza cha mwanaume halisi....ni kipimo cha jinsi alivyo na ushirikiano na jamii na watu wanaomzunguka..
Hizo hela ugharamie wewe mwenyewe, usichangishe hata wana kamati.

Money is too important to be wasted in such manner!
 
Ubaya upo hapa
received_459675611297985.jpeg
 
Wanawake hawawez kuelewa ...
Mfano
Mi nilimweleza ishu kama uliyeisema ..
Jibu nililopewa
Linafurahisha sana ...
Acha ttu hawa wanawake hawa...
Nikaambiwa ivii
Iyoo hafla fupi itakuwaje ..na wale watyu wanaokuja kutunza zawadi itakuwaje ...
kwaiyoo yeye hatopokea zawadi ??
Aliniuliza kaswalii ...
Aahh nikabaki nafurahi tyuu
Ikabidi nami nimchokoze
Kwani zawadi zinamchango gani kweny harusi ...au umuhimu wake ni nn ??
Nikajibiwa ...
Zinafariji piah zinasaidia kunenepa
Daaa ..nilichoka sana
Ikabidi nikubali tyuu yaishee
Tuishi nao kwa akili kwa kweli...
 
bf8852f5aa6c3b1693eb3a25bbe2c43f.jpg


WENGI wakiwaza kuhusu kufunga ndoa, mawazo yao huenda moja kwa moja kwenye namna sherehe ya harusi itakavyokuwa! Anataka gari kali la maharusi, ukumbi wa gharama, vyakula vya bei mbaya, wasanii maarufu wa kutumbuiza n.k.

Ni kweli ni vema kuifanya siku hiyo maalum na ya pekee maishani kuwa yenye kumbukumbu isiyofutika! Watu wanapenda kufanya sherehe kubwa ambayo itawafurahisha watu.

Katika kufanikisha hilo, huwa kunakuwa na kamati ya maandalizi ambayo ndiyo huratibu shughuli nzima. Katika kikao cha kwanza cha kuwaita wanakamati kuwaeleza nia yako ya kutaka kuoa, ahadi huwa nyingi sana.

Huyu atasema atagharamia gari la maharusi, mwingine atasema atasimamia usafiri wa wazazi, yule atasema mapambo nk, mradi kila aliyefika kwenye shughuli hiyo ya mwanzo wa maandalizi ya harusi ametoa ahadi yake.

Hapo huwa mwanzo wa mikikimikiki ya kukusanya fedha za michango na kuweka sawa mipango ya harusi. Ni safari ambayo huwa si ya chini ya miezi mitatu. Usipokuwa makini, kabla ya ndoa, bwana harusi anaweza kukonda kutokana na changamoto za kukimbizana na maandalizi.

Mwisho wake ni nini? Sherehe ya saa nne tu ukumbini, mamilioni yanakuwa yameshakatika. Kuna ishu nyingine ambayo vijana wanaotarajia kuoa huwa hawajiandai nayo kabla.

Baadhi ya watu huwa hawakamilishi walivyoahidi, mwisho wake unajikuta shughuli imekaribia na mambo hayajakamilika. Kwa kuwa lazima mambo yaende kama yalivyopangwa, ndipo bwana harusi mtarajiwa hujikuta akiingia kwenye mzigo wa madeni!

Yaani anachukua mke, anaanza naye maisha, badala ya kuanza na kuangalia maendeleo ya familia, anaanza kulipa madeni. Wakati mwingine madeni aliyojitengenezea yanaweza kuzalisha ugomvi ndani ya ndoa hiyo changa.

CHUKUA HII

Ndoa ina thamani kubwa kuliko sherehe ya kifahari ya saa chache. Sherehe yako haitakuwa na maana ikiwa ndoa itakuwa na migogoro. Mwanaume mjanja, hufikiria zaidi kumfurahisha mkewe, kuishi maisha ya amani na kuangalia maendeleo kuliko sherehe ya kifahari kwa lengo la kuwafurahisha watu.

Kama kweli uko vizuri, una fedha za kutosha, unaweza kuandaa sherehe kubwa; au kama una marafiki wenye ushirikiano mzuri, ‘wasio na pesa za mawazo’ unaweza kufanya sherehe kubwa, muhimu usiruhusu sherehe iwe chanzo cha kukupotezea furaha baada ya kutumia fedha nyingi.

MIFANO HAI

Ipo mifano ya watu wengi maarufu duniani wenye fedha zao, ambao hufanya sherehe ndogo.

Unaweza kuita kikao kidogo cha watu wako wa karibu kabisa – marafiki na jamaa mnaoshirikiana kwa shida na raha, mkaandaa hafla ya kawaida tu ya watu wasiozidi 100 (kwa mfano) na ukaweka kumbukumbu nzuri kwenye maisha yako.

Hii ni safu yetu sisi wanaume, kwa hiyo nimeongea kiume. Wanawake hata uwaeleze nini, hiki nilichokiandika hawawezi kukielewa. Nachukua time!
Alafu mwanamke aje apa aanze kupinga haya akitaka sherehe kubwa badala ya kushukuru Mungu amepata Mume na Ndoa imetimia anaanza kuwaza Sherehe za Gharama reaaly!!?

Yani mimi kwa mawazo niliyo nayo ingewezekana siku ya Kuoa Muhimu ni Kanisani tu ndoa ifungwe baada ya apo nimchukue Wife twende ata sehemu hoteli ya standard na Ndugu wachache kutoka pande zote as you said 100 ivi wanatosha tukafanya ka party kadogo maisha yakaendelea hayo mamilioni si bora wangepewa wana ndoa wakaanzie maisha!!
 
Kuna watu wanapenda sherehe halafu binafsi uwezo kugaramia hata nusu ya garama ya sherehe hawezi. Yani michango yake na familia yake na watu wake wa karibu na bado garama ya sherehe haitimii. Ndio hapo unaanza kuwapigia watu simu hata ulikua huna mawasiliano nao miaka kibao. Zaidi ya kuangaliana WhatsApp status hamna salamu.
Hahah mstari wa mwishk nimeupenda, ndugu mpo whatsapp. Mnaangaliana status tu no salam wala kutumiana video!! Watu kama hawa tuwa handle je mkuu?
 
Alafu mwanamke aje apa aanze kupinga haya akitaka sherehe kubwa badala ya kushukuru Mungu amepata Mume na Ndoa imetimia anaanza kuwaza Sherehe za Gharama reaaly!!?

Yani mimi kwa mawazo niliyo nayo ingewezekana siku ya Kuoa Muhimu ni Kanisani tu ndoa ifungwe baada ya apo nimchukue Wife twende ata sehemu hoteli ya standard na Ndugu wachache kutoka pande zote as you said 100 ivi wanatosha tukafanya ka party kadogo maisha yakaendelea hayo mamilioni si bora wangepewa wana ndoa wakaanzie maisha!!
Mimi harusi yangu ntafunga asubuhi jumuiyani ntamwita padri kwenye jumuiya itashereheshwa na wanajumiya na ndg wachache wa pande mbili. Jambo hilo nimeshamweleza ila anasema ati simpendi.!
Ukweli ni kwamba mimi nimechangia watu wengi sana ikafika mahali nikaacha.

Ukiniambia nifunge harusi ya ukumbini Mzee wangu hataudhuria (ninavyojua) sasa yanini ufanye Harusi uibue hoja za watu kukujadili kuhusu wazazi wako? Haina maana.
 
Mimi nilikuwa na sherehe ya harusi kipindi naoa kama ifuatavyo.
Baget =1000000(nilikuwa nayo)

Watu =50 mchanganuo uko Kama ifuatavyo
mchungaji na wasaidizi wake -5,
Majirani=10
Ndugu =20
Wakwe =10
Marafiki=5

Matumizi
Chakula =250000
Vinywaji=300000(bia zilikuwepo)
Mziki =150000
Mapambo =100000
Keki=50000
Mengineyo=150000
Mc (mshikaji wangu)

Watu walikula adi wakasaza bila kuchangia ata shilling moja ila walikuja na Zawadi za kutosha.

Mpaka nacomment hapa kuna shati nimevaa nilipewa kama Zawadi.
 
64 Reactions
Reply
Back
Top Bottom